Search This Blog

NYOKA WA KUTUMWA - 3

 





    Simulizi : Nyoka Wa Kutumwa

    Sehemu Ya Tatu (3)





    ………………. Ilipoishia …………………………

    MZEE.1: Mfalme tumekuja hata tunashida ya kuzungumza na wewe.

    MFALME: kuweni huru wazee wangu mimi ninawasikiliza.

    MZEE 2: Mtukufu mfalme sisi tumekuja hapa kwa ajil ya kuongelea kuhusu hili tatizo lilokumba hiki kijiji chetu cha mbaka kwasasa.

    MFALME: Tatizo gan tena ?

    MZEE 3: kuhusu huyu nyoka ambae amekuwa akisumba sana hapa kijijini kwetu.

    MFALME: kweli huyu nyoka kwa sasa amekuwa tishio hapa kijiji kwetu ila mimi nimepata maelezo yote kuhusu huyu nyoka.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MZEE 2: Kwahiyo umeamua kufanya nini baada ya kujua kuhusu huyu nyoka.

    Mfalme kabla ajajibu mara mzee sube akafika maana alipelekewa taarifa kuhusu kikao kilichopo kwa mfalme, mfalme baada ya kumuona mzee sube alijkuta na yeye akiwa anamtete yule nyoka.

    ……………….. Endlea ……………………………………

    MFALME: KwelI huyu nyoka ni hatari sana ila hatakiwI kuwindwa maana atakuwepo hapa kwa mda tu na baadae ataondoka.

    Maneno ya mfalme yaliwashangaza sana wale wazee maana wao walitarajia kuambiwa yule nyoka atafutwe na hauawe ila mfalme alisema kinyume kabisa na mawazo yao. Ila kwa upande wa mzee sube alifurahi sana kusikia mfalme akisema vile alijua moja kwa moja kafankiwa kuteka ufahamu wa mfalme. Wale wazee waliendelea kuongea huku mzee sube akiwa anawahudumia wagonjwa.

    MZEE 1: Kwahiyo itabidi tuvumilie tu. angaliania mtukufu mfalme watu wanavyo umia ila kwa kuwa umeamua hivyo sawa sisi tumekulewa.

    Wakamuaga mfalme na kuondoka zao huku wakiwa wamesononeka kutokana na jibu ambalo alikuwa ametoa mfalme. Siku hiyo mzee sube aliendea kufanya kaz yake na hatimae akamaliza na kurudi kwao na ile siku ikawa imepta. Siku kadhaa zilipita huku watu wakiwa wanaendelea kupata tabu na nyoka aitwae yoka ambae katumwa na mzee sube kwa ajili ya kijtafutia umaharufu pale kijijini kwake. Siku moja mchana kulikuwa na vijana kama watano wakiwa wanatembea wakielekea shambani kwao ghafla mmoja wao akang'atwa na yoka. Kitendo kile kiliwakasilisha sana wale vijana wengine na ndipo wakaanza kumkimbiza Yoka huku wakiwa wameshika fimbo na wengine panga pamoja na mawe. Vijana hao walijitahidi sana kumkimbiza lakini baada ya kumkaribia ghafla yoka akaingia kwenye kichaka Fulani, wote kwa pamoja wakakizunguka hiko ili nyoka asitoke sehemu ile na kuanza kuishambulia kwa kupiga mawe pamoja na zile fimbo walizobeba. walipomaliza kufanya hivyo mmoja kati yao akaanza kukatakata kile kichaka wakiamini wamefanikiwa kumuua yoka lakini kwa bahati mbaya waliambulia patupu. Walijiuliza mda gani nyoka ametoka maana hawakutegemea kuona kile walichokiona, lakini halikupatikana jibu zaidi ya kutazamana na kusikitika kumkosa adui wao mkubwa. Wakaondoka na wakarudi mpaka kwa yule mwenzao kisha wakamchukua na kumpeleka nyumbani kwa mzee sube kwa ajili ya kumfanyia matibabu, walipokelewa vizuri ndipo mzee sube akaanza kuwauliza tatizo japokuwa alikuwa anajua alifanya hivyo ikiwa kama kuwapumbaza na wasihisi kitu chochote kuhusu yeye na yule nyoka.

    MZEE SUBE: Vijana huyu mwenzenu kapatwa na nini.

    kijana mmoja akaanza kumsmulia jinsi ilivyokuwa.

    KIJANA 1: Tulikuwa tunaenda shamban ila kwa bahati mbaya akatokea nyoka na kumbana mwenzetu, tukajitahidi kumkimbiza ili tumuuwe lakini kwa bahati aliingia kwenye kichaka na kutupotea kwa mzingra ya kutatanisha ndipo tukamchukua huyu mwenzetu na kumleta huku kwako kwa ajili ya kumfanyia matibabu.

    Mzee sube alichukia sana aliposikia wale vijana walihitaji kumuua nyoka wake, akaingia ndani kuchukua dawa na kumpatia mgonjwa, Wale vijana walifurahi sana wakitegemea kumuona mwenzao akirudi kwenye hali yake ya kawaida. Mda mfupi wakielekea majumbani kwao hali ya mwenzao ikabadilika na kuwa mbaya zaidi ya mara ya kwanza, haraka waligeuza na kurudi nyumbani kwa Sube na kumkuta akiwa amekaa na mke wake, wakamueleza jinsi hali ya mwenzao ilivyobadilika, mda huo mgonjwa alikuwa amelazwa chini huku akipwitapwita kama kuku aliepigwa jiwe kichwani au kuchinjwa. akiwa kwenye hali ya kuangaika na maumizu makali ghafla alimuona nyoka mkubwa akiingia kwenye kichaka kilichokuwa karibu na nyumba ya mzee sube. Alitamani awaambie wenzake lakini kwa kuwa alikuwa mahututi alishindwa kuongea na kubaki akimuangalia Yoka kwa hasira mda mfupi mbele akakata roho, kumbe mzee sube aliwapa dawa tofauti ya kutibu sumu ya nyoka, alifaya hivyo ikiwa kama adhabu kutokana na kitendo walichokifanya cha kutaka kumuua Yoka. Jambo hilo liliwaumiza sana wale vijana na kuwa na hasiri ya kumtafuta yule nyoka kwa hudi na uvumba bila kujua kuwa mda ule alikuwa karibu yao. Wakamchukua yule mwenzao na kwenda kumzika kisha wakaenda mpaka kwa mfalme kwa ajili ya kuomba kufanya mkutano wa kijiji kizima kwa ajli ya kupanga mipango ya kumuangamiza yule nyoka. Walipofika wakamueleza shida yao na hatimae mfalme akawakubari ndipo ikapangwa siku rasmi ya kufanyika huo mkutano. Siku hiyo ilipofika watu walikusanyika kwa wingi nyumbani kwa mfalme maana kila mtu alipata taarifa ya kuwepo kwa hiko kikao na alichoshwa na matatizo wanayoyapata kutoka kwa huyo nyoka. Mda ulipofika kikao kikaanza huku viongozi wote wa kijiji wakiwemo bila kumsahau mzee sube, Mfalme akasimama kuanzisha mkutano rasmi.

    MFALME: Ndugu wanakijiji cha mbaka tumekutana hapa kwa ajili ya kujadiri hili swala lilitupata ambalo limekuwa likitunyima raha pia limetufanya tusiishi kwa maani . Nahisi wote munajua nini tatizo lilipo hapa kijijini kwetu kwa sasa kwahiyo kuanzia sasa hivi nafungua mkutano rasmi na nani ruhusu mtu kutoa wazo pia na ruhusu mtu kupinga wazo ila kwa viongozi tu.

    Mfalme akaa chini huku watu wakiwa wanampigia makofi kutokana na kile alichokiongea, mzee mmoja akasimama na kuanza kutoa mawazo yake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MZEE: Mtukufu mfalme nina wazo moja kama litakuwa zuri naomba lifanyiwe kazi. Mimi ninaona bora huyu nyoka tumtengeneze mtego ambao utamnasa kama tulivyofanya kwa baadhi ya watutu hatari ambao walikuja hapa kijijini kwetu, hilo ndio wazo langu.

    Mzee aliposema vile watu wote walipiga makofi mpaka na mzee sube mwenyewe, zamu za viongozi kukubali au kupina ikafika, kila kiongozi aliko mbele aliongea na kulikubali lile wazo mpaka mzee sube maana alikuwa anajua hakuna awezae kumtega Yoka akafanikiwa kumpata, lakini mke wake alishangaa kuona Sube akilikubali lile wazo maana yeye alikuwa afahamu nini mume wake aliwaza. Mtu mwingine akasimama kutoa wazo lake.

    KIJANA: Mtukufu mfalme wazo langu ninaona bora ikifika usiku tuanze kumtafuta maana yeye uwa anadhuru sana usiku kuliko mchana kwahiyo inamaansha kuwa usiku ndio rahisi kumpata, hilo ndio wazo langu.

    Mzee sube baada ya kusikia vile akasimama na kuanza kuipinga lile wazo la ya yule kijana maana aliona wakifanya hivyo itakuwa rahisi sana kumkamata yoka maana huwa anaenda mbali sana na eneo lake majira ya usiku kwahiyo wanaweza kumkimbiza na hatmae wakamkamata. Baadhi ya watu walishangaa kuona mzee sube amepinga lile wazo ila mfalme aliona kawaida maana alikuwa anamsikiliza sana mzee sube.

    MFALME: Jamani wanakijiji huyu ndie tabibu wetu pia ni mzee wetu kwahiyo yeye anajua mambo mengi kuliko sisi ni vizuri endapo akisema kitu tumsikilize maana hata mimi nimeona hilo wazo sio zuri kwetu.

    Vijana wengi walisikitika kusikia mfalme akiumuunga mzee sube, ndipo kijana mmoja akasimama na kuanza kutoa wazo lake.

    KIJANA 2: Mtukufu mfalme pamoja na wanakijiji wote wazo langu naona tungepita kila sehemu kwenye kichaki tuviondoe maana tukifanya hivyo nyoka hatakuwa na sehemu ya kakaa na atakuwa anazunguka zungika na ndio itakuwa rahis kumuua.

    Wazo la huyo kijana lilipendwa na kila mtu mahara pale mpaka mfalme mwenyewe lakini ilikuwa tofauti kwa mzee sube, maana hakupiga makofi kuonyesha kuunga mkono lile wazo wala kutabasamu jambo ambalo liliwashangaza sana viongozi wenzake. Mfalme akasimama na kumpongeza lile wazo lilitolewa.

    MFALME: Kijana hongera sana kwa kutoa wazo zuri kiasi hiki nimefurahi sana na tutaanza kulifanyia kazi wazo lako ili tuone mafanikio yake.

    Mfalme akaa na kupisha viongozi wengine waonge kuhu lile wazo, kila aliesimama alilipongeza na kushauri lianze kufanyiwa kazi wazo hilo lakini ilikuwa tofauti ilipofika zamu yam zee sube kutoa maoni yake juu ya wazo lile.

    MZEE SUBE: Jaman mimi nilikuwa sijui kuwa vijana wa hiki kijiji chetu ni wajinga na wapumbavu kiasi hiki yani wanapitwa mawazo na wazee. Hivi unaonaje mtu aje nyumbani kwako kuaribu nyumba yako utamuacha kweli hata kama atakuwa na upanga lazama utajitahidi kadri uwezavyo kumzuia kufa hivyo hii ndio itakavyokuwa kwa hiyo siku mutakayo anza kuondoa hivyo vichaka . maana yule nyoka awezi kukubali kuona munaharibu nyumba yake kwahiyo ataanza kuwauma na hatimae mukapata madhara ya kujitakia.

    Watu walibaki vivywa wazi maana hawakutegemea kusikia maneno yale kutoka kwa mzee sube, Kikoa kiliendelea na mwishowe wakaamua kufanya kama alivyosema mtu wa kwanza kutoa wazo, wakachaguliwa vijana shupavu mashujaa mahodari kwenye masuara ya utegaji mitego na kuwapa kazi na hatimae kikao kikafika mwisho.Siku ya pili ilipofika wale vijana waliochaguliwa kuifanya kazi wakachukua zana zao za kutengenezea mtego na kwenda nao sehemu ambayo ilisemekana huyo nyoka kufika mara kwa mara. Walitega huo mtego kisha wakamchukua mbuzi na kumuweka ikiwa kama chambo cha kumuitia nyoka, Walipomaliza wote wakaenda kujificha kusubilia nini kitatokea, lakini matumaini makubwa ya kufankiwa yakiwa juu yao, wakaa kimya wakisikiliza kwa makini ili wasikie pindi mtego ukifyatuka. Zilipita dakika kadhaa ghafla mbuzi ambae aliwekwa kwenye mtego akaanza kulia kwa sauti ya kuashiria amepatwa na tatizo, wale vijana wakaa vizuri huku wakiwa wameshika mapanga wakisubilia kusikia mtego ukifyatuka, sekunde kadhaa mbele mtego uliskika, haraka walitoka walipojificha na kuelekea kwenye mtego wao wakiwa na mawazo ya kumkuta nyoka akiwa amenasa kwenye mtego wao. Walishangaa kukuta mtego ukiwa umefyatuka huku yule mbuzi akiendelea kula majani, wakaukagua vizuri na kukuta ukili ukiwa umenasa kwenye mtegeo, wakautoa na kuutupa pembeni na kuanza kuongelea jambo lile.

    KIJANA 1: Jamani nini kimetokea hapa maana sielewi mbona mtego umefyatuka na hakuna kitu kilichonaswa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    KIJNA 2: Hata mimi nana shangaa jambo hili, au kuna mtu ametuchezea.

    KIJNA 3: Nahisi maana tangu nianze kutega hii mitego sijawai kuona ikifyatuka nyenyewe bila kunasa kitu.

    KIJANA 4: labda kuna kitu kiligusa huu mtego . Kama vipi tutege tena alafu tukajifiche na tuangalie kama itatokea tena .

    Wakatega tena kisha wakaenda kujificha bila kujua kuwa walifanikiwa kumnasa wakiemtaka na kumtoa wenyewe kwenye mtego na kumuacha huru tena. Walipoenda kujificha tena, Yoka akarudi kwenye umbile lake ya nyoka na kurudi nyumbani kwake.



    Walikaa mda mrefu bila mafanikio yoyote na hatimae jioni ikaingia wakarudi mpaka kwa mfalme na kumpa taarifa hukusu kushindwa kwao kumpata nyoka. taarifa ile ilimuhuzunisha sana mfalme maana alitegemea mafanikio makubwa kutokana na wale watu walio wachagua kuwa hodari kwenye kazi kama zile. Lakini mmoja kati ya wale vijana aliongea kitu ambacho kiliwashangaza sana wenzake pamoja na mfalme.

    KIJANA: Lakini kuna kitu kinanishangaza kila nikitafakari, hivi ukili una uwezo wa kuufyatua ule mtego, alafu nimeshangazwa na kitu kimoja pale ambapo nilikuwa nimeuhifadhi sikuuona wakati tunatoa ule mtego.

    MFALME: Mh! Ukili sijawai kusikia ukifyatua mtego, au kuna mtu atakuwa anatuchezea mchezo hapa kijini, sasa nyie nendeni hili jambo nitalifikisha kwa wazee wa kijiji tutajua jinsi gani tufanye.

    Wale vijana wakaondoka na kurudi majumbani kwao huku kila mmoja akifikiria kuhusu ule ukili, mda mfupi mbele mfalme akaita wazee baadhi wenye cheo pale kijijini kisha akamtuma mlinzi wake mmoja aende akamuite mzee sube. Zikapita dakika kadhaa hatimae yule mlinzi akarudi akiwa ameongozana na mzee sube, mfalme alifurahi kuona vile maana alikuwa anampenda sana yule mzee bila kujua yeye ndie chanzo cha matatizo yote pale kijijini. Kikao kiaanza huku wale wazee wakiwa awajui nini wameitiwa hamala pale.

    MFALME: Wazee wangu nimewaita hapa kwa ajili ya kuwapa taarifa niliyoipata kutoka kwa wale vijana tuliowatuma kumtega nyoka, lakini kwa bahati mbaya hawakubahatika kumpata lakini kuna jambo wameniambia la kushangaza kidogo.

    Mfalme akaeleza kama alivyoambiwa na yule kijana na mwisho akawapa nafasi na wao watoe mawazo yao juu ya kile alichowaambia, ndipo mzee mmoja akaanza kuongea.

    MZEE: Mtukufu mfalme kutona na hiyo taarifa moja kwa moja inaonyesha kuna mtu anatuchezea kwahiyo hatuna budi kumtafuta mganga atakae wenza kutusaidia kututatulia hili tatizo.

    Mzee sube akamuangalia yule mzee kwa jicho Fulani la kuonyesha kuchukia kile alichokiongea lakini kwa bahati mzuri hakuna mtu ambae alimuona akiwa kwenye hiyo hali.

    MFALME: Kweli kabisa mzee wangu maana watu wamekuwa wakikichezea sana hiki kijiji chetu cha mbaka kwahiyo lazima tumtafute huyo mganga na ikiwezekana leo hii hii tumchague mganga na apewe taarifa yake ili kesho aje aianze kazi yake, Au unasemaje mzee Sebe unasemaje kuhusu wazo hili. { Aliuliza huku akimtazama mzee sube usoni na kumwachia nafasi ya kuongea }

    MZEE SUBE: Ni wazo zuri na hatuna budi kulifanya maana huyu nyoka sasa hivi amekuwa hatari na endapo tutamuacha aendelea kuzuru watu wa hiki kijiji tutajikuta wote tumepotea.

    Mfalme alifurahi sana kuona wote wamekubaliana jambo lile na ndipo akatoa nafasi ya kumpendekeza mganga ambae wao wanaona ataweza kusaidia kutokana na lile tatizo, mzee mmoja akasimama na kumtaja mganga aliehisi yeye kuwa anafaa kuifanya hiyo kazi.

    MZEE: Mtukufu mfalme kuna mganga mmoja anaitwa mzee Duba ambae tangu ujana wake amekuwa akiifanya hiyo kazi ya uganga na amesaidia watu wengi sana hapa kijijini na kwa sasa anapatika karibia na msitu wa dawa.

    Mfalme akawauliza wale wazee wengine kama kweli kile alichokisema mwenza, kila aliemuuliza aliitikia haraha lakini ilipofika zamu yam zee sube alisita kwa sekunde kadhaa kisha akakubali kuwa yule huyo mzee Duba anafaa kuifanya hiyo kazi. Baada ya wote kukubaliana mfalme akafunga ule mkutano na kuwaruhusu wale viongozi warudi majuimbani kwao ili kesho yake asubuhi wawai kufika kwa ajili ya kumpokea huyo mzee Duba maana yeye alikuwa hamfahamu. Wale wazee walipoondoka akatumwa kijana mmoja aende huko kwa huyo mganga akampe taarifa kuwa anahitajika kufika kwa mfalme kesho yake, kijana akafanya kama alivyo ambiwa akaanza safari ya kwenda huko karibu na msitu wa dawa kumfuata mganga. Sube alipofika nyumbani kwake akaingia moja kwa moja mpaka ndani bila kumwambia kitu chochote mke wake ambae kwa mda huo alikuwa amekaa nje na kumsababishia mawazo mengi, Haraka mke akainuka na kumfuata mumewe ili akajue nini tatizo mpaka awe kwenye ile hali na wakati sio kawaida yake.

    BIBI SUBE: Kulikoni mbona upo hivyo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MZEE SUBE: Mke wangu tupo kwenye wakati mgumu sana, usiku wa leo kuna kazi tunatakiwa tuifanye.

    BIBI SUBE: E ! kwani kimetokea nini huko kwa mfalme. { Aliuliza huku akiwa na uwoga }

    MZEE SUBE: Kuna mganga kachaguliwa kwa ajili ya kuja kualibu mambo yetu.

    Bibi sube aliposikia vile, akaanza kutetemeka huku akimrahumu mume wake juu ya wazo ambalo alilitoa ambalo sasa hivi limeanza kuwatia jamba jamba.

    BIBI SUBE: Heeee ! Sasa tutafanyaje si kuhumbuka huku mume wangu. Lakin mimi nilikuambia hiki tunachokifanya yatatukuta kama yaliyomkuta mzee SUI .

    MZEE SUBE: Mke wangu wala usiogope haiwezi kutokea kama kilachotokea kwa mzee sui na kila siku nakuambia kuwa mzee sui kilchofanya afe ni uzembe wake yeye pamoja na mwanae. Sasa sikiliza mganga aliechaguliwa ni yule mzee duba kwahiyo leo usiku inatakiwa twende tukapoteze uhai wake maana kama tukimuacha kweli yatatukuta kama ya mzee sui na ama.

    BIBI SUBE: Hivi kweli tutaweza kumuua yule mzee maana kaanza mda mrefu sana ile kazi na lazima katuzidi uwezo.

    MZEE SUBE: Hahahaha mke wangu unafurahisha sana. Mzee duba hawezi kufurukuta kwangu japokuwa ameanza zamani ile kazi ila mimi ni zaidi kwahiyo awezi kuzuia uchawi wetu hata siku moja.

    BIBI SUBE: Hapo sawa mume wangu maana roho yangu ilikuwa hipo juu.

    Kwa upande wa yule kijna ambae alitumwa aende kutoa taarifa kwa yule mganga kwa bahati mzuri akabahatika kumkuta yule mganga akiwa anatengeza dawa na wakati huo giza lilikuwa lishaanza kuingia. Alipokelewa vizuri sana na mzee Duba na baada ya kufahamiana akamueleza kilichompeleka pale, Mzee duba alifurahi sana kusikia amechaguliwa kuwa mganga anaetakiwa kutatua lile tatizo lililopo pale kijiji, akamuomba yule kijana ile siku walale pale alafu asubuhi na mapema waanze safari yao ya kwenda kwa mfalme. Wakati huo Duba alikuwa Hafahamu kitu chochote kinachoendelea juu yake. Masaa yalienda na hatimae mda wa kulala ukafika Duba akamuandalia yule kijana sehemu mzuri ya kupumzika, na yeye akaenda kulala sehemu yake, mda huo kwa upande wa sube na mke wao walikuwa wakijiandaa kwenda kuifanya kazi walio ikusudia kuifanya siku ile. Mda wa kazi ulipofika wakakusanya vitu vyao na kuweka kwenye ungo kisha na wao wakapanda na kusafiri mpaka nyumbani kwa Duba na kumkuta akiwa amelala fofofo. Walipofika wakamwaga unga huku wakiizunguka nyumba na mwisho wakashikana mikono na kuingia ndani kwa kutumia ukuta. Ghafla sura zao zikabadili na kuwa tofauti ambazo mtu yoyote isingekuwa rahisi kuwafahamu, Wakaanza kuimba na kucheza nyimbo zao za kichawi huku wakizunguka kitanda cha ukambaa alicholalia Duba, Walipomaliza wakamwamsha kwa mkitikisa mpaka alipozinduka kutoka usingizini. Duba alishtuka sana alipokutana uso kwa uso na wawili wale waliokuwa na sura za kutisha, akakurupuka pale kitandani na kuangukia chini. Wawili wale waliendelea kumfuata mpaka huku yeye akiwa anarudi nyuma nyuma, na mwisho akasimama na kukimbilia nje, Ghafla nje ya nyumba mulipo mwagiwa ule unga mkaanza kuwaka moto na kumfanya Duba ashindwe kuendelea kukimbilia mbali na pale. Akadondoka chini huku akitafuta wapi wale watu walipo, Ndipo sube na mke wakatokea pale pale alipokuwa ameanguka ndipo Duba akaanza kuwauliza maswali wawili wale huku kijasho kizito cha kujuta kikimtiririka.

    MGANGA: Kwani munataka nini kwangu kama kuna kitu munakiitaji niambieni mimi nitawapatia.

    Yule mganga baada ya kusema vile ndipo mzee sube akaanza kucheka kwa dharahu na kumjibu.

    MZEE SUBE: Hahahaha wewe si mganga ambae unataka ukaaribu mambo yangu. Sasa nimekuja kwa ajili ya kupambana, uwezo wako ndio utakufanya uendelee kuishi .

    Sube baada ya kujibu vile ndipo Duba akagungua kuwa ni mzee sube, maana walikuwa pamoja zamani kwenye shughuli zao za kichawi lakini baadae Duba akaacha kuloga watu na kuwa mgawa, chapokuwa nae ni mchawi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MGANGA: Nimekujua wewe sube na mimi nilijua tu lazima hipo siku utanifanyia kitu kama hiki maana umezoea kuwatesa wanakijiji. kama unataka kuniua niue tu ila endapo utaniacha nitasema ukwel kwa mfalme.

    Sube alichukia sana kusikia vile, ndipo akajibadirisha na kurudi kwenye sura yake ya kawaida na kusogea karibu na alipo Duba na kuanza kuongea.

    MZEE SUBE: Vizur sana kama umegundua mimi nani sasa kwa kuwa unajfanya jeuri basi leo ndio utakuwa mwisho wako wa kuonahuu ulimwengu, kamwe sitakuacha hai.

    MGANGA: Sawa wewe fanya utakalo lakini jua kuwa siku za mwizi ni arobaini hipo siku ukweli utajurikana tu hata kama utaniua.

    Sube akasimama akamkazia macho Duba ghafla damu zikaanza kumtoka puani mdomoni na masikioni, huku akiangaika kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata hatimae akakata roho.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog