Search This Blog

NILILALA NA MAITI 20 ILI NIOLEWE NA RAIS - 4

 



    Simulizi : Nililala Na Maiti 20 Ili Niolewe Na Rais

    Sehemu Ya Nne (4)



    “Adela! Adela!”

    Waliita kwa pamoja Sonia na Sarah. Sauti zao ziliendelea kuita uku zikijirudia midomoni mwao mara mbili mbili. Wale wachawi wao walikuwa bado wakishikilia mienge iliokuwa ikitoa moto uku wakiinua kwa juu. Walikuwa wamepoza sauti zao kupisha sauti za Sonia na Sarah. Sonia na Sarah ambao bado walikuwa wamebakiwa na mioyo miwili miwili kila mmoja mikononi mwao. Wakanirushia tena kwa mara ya pili.Wale wachawi wakaanza upya kuimba ile nyimbo niliokuwa nikiipenda.Wakashangilia!

    “Adela unatakiwa kuila hiyo mioyo yote haraka iwezekanavyo!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliongea Sonia kwa sauti ya juu. Kitendo cha kuongea tu wale mbung’o wakaiwahi tena ile mioyo iliyokuwa imerushwa na Sarah na Sonia. Wakaifakamia na kufurahia kupata kitoweo pasipo jasho. Nikainua mikono yangu nakuanza kunyang’anyana na mbung’o wenye njaa kali.Mbung’o wakatawanyika nakuniachia ile mioyo.Wakakimbilia maeneo ya kifuani mwangu kama walivyokuwa wakifanya awali. Wakazidisha kutengeneza duara kubwa katika maeneo niliokuwa nimekatwa matiti. Maumivu makali yakaanza kupenya katika mwili wangu. Nilijikuta nikiambulia kushika moyo mmoja tu uku ile mingine nikiiachia. Nikaushikilia kwa nguvu na kwa hisia zote. Nikaufinya ule moyo katika kiganja changu mpaka ukawa laini sana mithili ya maini. Nikausogeza mpaka maeneo ya mdomoni mwangu nakuutafuna. Kadri nilivyokuwa nikiutafuna ndivyo na mapafu yangu mwilini yalivyokuwa yakinitanuka. Yakazidi kutanuka nakusababisha tumbo lionekane kubwa sana. Mpasuko! Mwili wangu wote ukasambaratika kuanzia mikono tumbo mpaka kiuno na miguu vikasambaa. Adela mimi nikabakiwa kichwa peke yake uku nusu ya mwili wangu ukiwa umesambaratika juu ya tope.. Mdomo ukawa hauna tena uwezo wa kutoa sauti na kuongea zaidi ya macho yangu kuangaza mbele. Mbele kulipokuwa kumezungukwa na idadi ya kundi kubwa la wachawi wakiwa wameshikilia mienge inayowaka moto wakiongozawa na Sarah na Sonia.Akili ikaumia sana kuukosa moyo.Moyo uliokuwa ukimsaidia kwa mawazo. Moyo ambao tayari ulikuwa umeshajikusanya na viwili wili kusambaratika juu ya tope.Mchawi yeyote anaweza hata kukatwa kichwa na bado akawa anaongea kama waongeavyo binadamu wa duniani. Hiyo ni nguvu ya ajabu waliokuwa nayo wachawi wote.

    **************

    “Adela?”

    Sauti ya Sophy ikashtua ngome ya masikio yangu.Macho yangu bado yalikuwa yamefumba japo masikio yalikuwa wazi kusikia chochote. Nikatoa macho kuangaza Sophy alipo.Ubaridi mkali bado uliendelea kutawala katika shingo yangu iliokuwa imeachanishwa na kiwili wili. Lile eneo niliokuwa nimelalia tope uku mbung’o wakinitafuna halikuwepo tena mbele ya macho yangu. Kichwa changu kikawa kama kimehifadhiwa chini ya mti mkubwa. Kichwa tupu! Sikuweza kujigeuza nakutambua sauti ya Sophy ilipokuwa ikitokea.

    “Adela jamani! Pole sana Adela!”

    Sauti ya Sophy ikawa bado ikiniongelesha uku hisia za kuwa yupo maeneo ya karibu nikiwa nazo. Tahamaki! Macho yangu yakakutana uso kwa uso na Sophy. Sophy aliyekuwa mtupu kama alivyozaliwa. Akanishika kichwa changu nakukiweka kwapani.

    “Twende!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alionesha kuwa na hasira kali kwani hata macho yake hayakuwa ya kawaida. Alinishikilia kwa nguvu kwapani mwake. Shingo yangu ndio kwanza ilizidiwa na baridi kali hali ilionifanya nisikie upepo mkali ukinitoka kupitia puani, masikioni na mdomoni. Upepo mkali uliojawa na vumbi. Sikuweza kupiga hata chafya japo hisia za kupiga chafya nilikuwa nazo. Nikatamani sana nimuulize Sophy tunapoelekea lakini hali ikawa pale pale kwamba sikuwa na uwezo wa kutoa sauti zaidi ya kusikia tu. Baada ya Sophy kutembea kwa umbali kidogo masikio yangu yakaanza tena kusikia ile nyimbo niliokuwa nikiipenda ikiimbwa na wachawi kwa mbali. Ile sauti ya nyimbo ikaonekana kumkera sana Sophy. Akachukua kichwa changu nakukiweka mbele ya uso wake. Akatikisa kichwa chake kwa hasira kali alizokuwa nazo. Ule uso wake ukabadilika rangi nakuwa na sura ya yule mmama aliyenileta uku kwenye himaya hii ya wachawi wengine. Sura ya Sophy ikabadilika tena ikawa kama ya Sonia mara kama ya Sarah. Akachukua kichwa changu nakukitupa mpaka chini. Nikahisi kama napasuka kichwa. Kichwa changu kilibiringita zaidi ya mara ishirini mithili ya mpira wa miguu kisha kikagota karibia na mti mkubwa. Nikaanza kuvuja damu si damu kwani ilikuwa ni ya bluu sana. Ikaanza kunitoka kuanzia masikioni. Masikio yote mawili yakatoa damu damu za bluu mithili ya bomba litoavyo maji kwa wingi.Masikio yakashirikiana na pua katika kutoa damu damu nakupelekea mdomo kushikwa tamaa ya kutoa damu. Mdomo nao ukaanza kufurahia kutoa damu damu.Nikaachama uku nikitoa ulimi nje nakuruhusu damu damu zile zinitoke kwa nguvu zote. Nikayatoa macho ya ukali kumuangalia yule niliyedhania ni Sophy mbele yangu. Nikashuhudia akisinyaa nakuwa mdogo sana kama panya. Akakimbia!

    Zile damu damu zikaanza kujikusanya nakuweka mstari mmoja. Zikatawanyika kwa kufuata mkondo mmoja uku zikitokomea ndani ya pori zaidi. Zikakata kutoka katika sehemu zangu za masikioni,puani na mdomoni. Macho yakaanza kuangaza sehemu damu zilipokuwa zikielekea. Misukule watatu wakatokea katika ile sehemu damu ilipotokomea. Walikuwa wamebebeshana mwili wa mtu alioonekana mwanamke kutokana na kuwa na matiti kifuani mwake uku

     akiwa hana kichwa zaidi ya kubakiwa na shingo pekee. Wakasogea mpaka karibu na kichwa changu kilipo. Wakaangusha ule mwili wa yule mtu. Wakajipanga mstari kuashiria kuna mtu anatokea katikati yao.

    “Adela!”

    Sauti ya Sonia sasa ikawa imeshakaririshwa rasmi na masikio yangu. Akatokea Sonia miongoni mwao.akainama mpaka chini nakushika kichwa changu. Akatoa tabasamu pana.Akanong’ona!

    “Bado tunakupenda!”

    Akanena kwa sauti ya kimya kimya masikioni mwangu. Masikio yakatingishika mithili ya mbuzi ‘beberu’ akitaka kufanya mapenzi na mbuzi jike.Akatoa ile dawa yetu ya wachawi ya “CHAYA” inayoweza kuunga kiungo chochote cha mchawi kikiharibika ama kukatwa. Sonia akaanza kunipaka nayo shingoni mwangu uku akisugua kwa nguvu zote.Alipomaliza alionesha ishara kwa ile misukule. Misukule ikainua ule mwili wa mwanamke uliokuwa chini. Sonia akatoa tena chaya nyingine nakupakla shingo ya ule mwili nakusugua kwa nguvu zote. Kisha akachukua kichwa changu nakukiunga na ule mwili. Vikang’ang’ana!

    “Adela? Adela? Ongea basi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Abee! Unasemaje?”

    Nillijikuta naweza kutoa sauti, tena sauti tofauti na sauti yangu ya kawaida. Ilikuwa ni mchanganyiko wa sauti ya kike na ya kiume. Sauti iliyoshiba na yenye kumtetemesha mtu yeyote.Akili ikafurahia nakuanza kuutafuta moyo ndani yake ulipo.ukafanikiwa kuuona moyo nakufurahia kuwepo pamoja kwa mara nyingine.



    ******************



    Nguvu za kichawi zikanijaa upya. Mwili ukajipa ubabe wa muda kwa kujitingisha.Nikaanza kujaribu viungo vya mwili kama vina ushirikiano. Nikapiga hatua mbili mbele moja nyuma. Nikainua mikono yangu nakuikumbatia kwa hisia. Nikajikumbata! Nikaigeuza shingo yangu kumuangalia Sonia pamoja na ile misukule. Patupu! Sikuweza kumuona hata mmoja.Lile eneo nikabaki kuwa peke yangu kwa mara nyingine tena. Ile hali ya woga aikaniondoka kwa muda huu.

    “Ahhh liwalo na liwe!”

    Nikausemea moyo nakujijaza ujasiri wa hali ya juu. Ujasiri wa kupambana na chochote mbele yangu.Sikujua nilipotokea wala nilipokuwa nikielekea. Nikafuata kinjia cha pori nakuongoza. Kwa takribani hatua kama arobaini uku giza likiwa limenizunguka na macho ya kichawi yakiwa kama mwanga wa kuangaza. Sauti ya nyimbo ile ile tena ninayoipenda ikatikisa ngome ya masikio yangu. Shtukizo! Ile sauti ikaongezeka kupaa na kuwa sauti kubwa na nyingi zikiimba kwa shangwe. Nikasimama! Nikashikilia majani ya mti kwa nguvu na hisia mwilini uku nikiisikiliza ile nyimbo ikiimba. Mara ile sauti ya nyimbo ikakata tena!

    “Oiyeee he”

    “Heeeee!!”

    Sauti za wachawi wenzangu zikatokea upande wa nyumba yangu.Kila mmoja alionesha kuwa na ngozi ya binadamu wa duniani katika eneo lake la sehemu za siri. Walikuwa ni wengi sana wakinifuata kwa kunikimbilia uku mikononi mwao kila mmoja akionesha kuning’iniza mienge ya moto. Mwanga ukawa mkali sana. Sikuwa na jinsi zaidi ya kusimama nikiwaangalia wakinifuata. Wakanisogelea mpaka karibu kisha wakanizingira.Wakatangeneza duara kubwa. Nikajihisi akili ikichanganyikana na ubongo. Sikujua dhamira yao. Moyo ukabaki kuwa na maswali mengi kwani wachawi wa kambi yetu huwa hatuna mchezo wa kumsumbua mgeni kama wafanyavyo hawa. Wakatanua njia kidogo kuonesha kuna kitu kinakuja katikati yao. Akatokea mzee alioonesha kuwa na upara. Alibebwa juu juu na misukule sita uku mikononi mwake akiwa ameshikilia fimbo kubwa iliokuwa imenakshiwa vizuri kwa fuvu la binadamu. Hakuwa amevaa nguo hata moja mwilini mwake.Mtupu!

    “Ineku wane?”

    Akaita kwa sauti ya juu akimaanisha ‘mgeni wa kutoka wapi’. Wale wachawi wenzake wakabaki kimya wakinitolea macho. Akajitokeza Sonia miongoni mwao.Akamfuata yule mzee mpaka alipo. Akamnongoneza masikioni mwake.

    “Sai sonsimba”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yule mzee akatoa amri kwa lugha yetu ya kichawi akimaanisha ‘mpeni heshima yake’. nikastaajabu misukule wakimshusha yule mzee mpaka chini kabisa kisha wakaondoka. Wakabakia wale wachawi na mzee wao. Macho kodo! Upepo mkali ukatawala ghafla. Ukazunguka eneo la kwangu nilipokuwa nimesimama. Ukapuliza kwa muda mrefu ukichanganyikana na mwanga mkali. Ukakata! Pakabaki tuli. Nikaangaza tena nakushuhudia lile kundi la misukule likizingira na kupanga binadamu wa duniani .Wakawapanga chini zaidi ya kumi.

    “Adela?”

    “Mzee huyu kajuaje jina langu? Au Sonia kamwambia?”

    Yule mzee akaniita kwa sauti ya juu uku akinitazama kwa mkazo. Nikabaki nikiulizana na moyo bila kupata jibu.

    “Habari zako ninazo.hizo hapo chini ni maiti za kiume. Maiti ambazo zilipata ajali.Ajali ambayo sisi ndio wasababishi. Unachotakiwa iyvo ivyo ukiwa uchi anza kuzinyonya nakuzikalia kila mmoja katika sehemu zake za siri haraka iwezekanavyo.”

    Nikajihisi kusisimka kwa mwili.Tamaa! Ile hali ya kufanya mapenzi na maiti ikaushtua sana moyo wangu. Nikafurahi sana uku nikaangalia ule umati wa wachawi uliokuwa umenizunguka. Kila mmoja akawa ameshikilia moyo mkononi mwake uku akitetemesha mdomo mithili ya mtu aliyetoka kuoga maji ya baridi sana katikia eneo lenye ubaridi. Wakawa kimya kunitazama nitakachofanya.Nikaanza kufanya kama nilivyoambiwa na mkuu wao. Nikaanza kulala nazo kuanzia maiti moja mpaka nyingine. Maiti zilikuwa na ladha tofauti kidogo na hata sehemu za siri zilikuwa zina uchachu sana. Kadri nilivyokuwa nazinyonya ndivyo na ladha ilivyokuwa ikibadilika katika mdomo wangu. Kunakipindi nilijihisi kutapika lakini nikakumbuka kuwa ni mwiko kwa mchawi yeyote kutapika katika mazingira yoeyote. Nikakumbuka sheria ambazo nilishapewa juu ya machawi atakayetapika na adhabu yake ya kutolewa ulimi na kuwa kama misukule. Nikajikaza nakumalizia kuzinyonya zote. Nilipomaliza nikaanza kuikalia kila mmoja nikiikatikia kidogo kidogo. Hofu! Nilipomaliza kuikatikia tu maiti ya mwisho. Manyunyu yakaanza kudondoka mpaka chini kuashiria mvua inataka kuja.Ngurumo za mianga ya radi zikapenya katika mboni ya macho ya kichawi. Kila mmoja akaanza kutawanyika akikimbia pasipokueleweka.Mvua ikaanza kunyesha. Mvua kubwa ile ya mawe.Nikainuka namimi kutaka kuondoka lakini nikajihisi miguu mizito kutembea. Nikainua mguu wa kulia ukainuka lakini nyayo zikabaki. Nikainua na wa kushoto napo ukaacha nyayo katika ardhi. Maumivu makali yakanijia mwilini. Nikajikuta eneo lote nikibakia na zile maiti ambazo nilitoka kuzinyonya na kuzilala.Maiti zile zikaanza kuinuka moja baada ya nyingine. Kila zikiinuka zilikuwa zikiweweseka nakuanguka tena uku nyingine zikijikaza mithili ya mazombi. Zililowana sana kiasi cha kuinuka zikiwa na tope tope jepesi. zikaanza kunifuta mpaka karibu zikitaka kuning’ang’ania mwili wangu.

    “Niacheni ukoooo!!!”

    Nilitoa sauti ya ukali lakini haikusaidia kitu kwani ndio kama nilihamsha na maiti nyingine pale chini. Zikanizunguka nakuniweka kati.Wakanikumbatia kwa wote huku mvua ikiendelea kunitandika mfululizo.Hawakuwa na sauti ya kuongea zaidi ya kutoa sura ya kikatili. Sura ya kumfanya mtu yeyote aweze kuogofya.Wakaanza kunishambulia kwa kunitafuna tafuna. Nikajihisi mwili kunyumbulika kama ilivyokuwa awali. Nikadondoka mpaka chini nakupoteza fahamu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *******

    “Adela?”

    Nilishtuka nakujikuta nipo chini nimelala katika mazingira ambayo sikuayelewa. Nilikuwa ndani ya maji mengi sana mfano wa bahari. Ilikuwa ni kama dunia nyingine, kila mmoja alikuwa amenizunguka huku sura zao zikioneshwa kuwa na tabasamu la haja!

    “Wewe nani?”

    Nikauliza kwa ukali kidogo. Nikamuuliza yule dada aliyekuwa ameniita jina langu.

    “Naitwa Diana! Nipo paomoja nawe, kwanza hongera!”

    Nilijiangalia mara mbili mbili kwanini napewa hongera. Nikawaangalia na wale watu walioonesha kuwa tofauti sana kwani walikuwa wamevaa mavazi mazuri sana tofauti na wachawi wote niliowahi kuwaona. Walikuwa ni wasichana tupu. Shingoni na mikononi mwao kulijawa na dhahabu za kung’aa. Meno yao yalikuwa ya rangi ya silva.Yakimetameta!

    “Hongera ya nini?”

    Nikang’aka kwa utuli!

    “Adela? Umefanikiwa kuwa na vigezo vyote vya kuweza kuolewa na Rais. Na kwa sasa Rais yupo ikulu anakusubiri kufunga ndoa nakuwa rasmi mke wake kuanzia leo kwa muda wa miezi miwili”

    “Kweli?”

    Sikutaka kabisa kichwa changu kiamini yasemayo na Diana. Nikayafumba macho. Halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi haraka nakukumbuka kuwa kuna mtu niliambiwa anaitwa Diana ambaye alishawahi kuolewa na Raisi yeye ndiye atakayeniambia kila kitu jinsi ya kufika mpaka kwa Rais. Nilijikuta nikiushukuru moyo kwa uvumilivu ulioonesha nakuniongoza mpaka nilipofika. Zile ndoto zangu za kuolewa na Rais zikawa zimeshakubaliana na akili yangu. Nikainuka nakumkumbatia Diana. Diana akanishika mkono nakuniongoza ndani ya maji kuelekea uko ikulu kwa ajili ya kufunga ndoa.



    ******************************************

    **** Adela atafanikiwa kufunga Ndoa na Rais? Na ni Rais yupi huyo? Kundi la kichawi la kina Sophy wanajua hilo? Na itakuwaje kama wakijua?

    **** Nini hatma ya Adela baada ya misukosuko yote hiyo? Tatizo la umeme linafanya simulizi hii iwe inachelewa kufika muda muafaka. Tuvumiliane kwa hilo ukiona inachelewa kutoka kama ilivyopangwa. Soon Tanesco wataelewa tu!

    ***** Simulizi hii iko katika hatua za kuhamishiwa katika kitabu chake ‘kijarida’ ambacho hutotaka kukiweka chini ukianza kukisoma. Kaa mkao wa kukisoma Tanzania yote kitapatikana.

    **** Simulizi hii ni ya kweli na mambo yaliopo ni ya kweli kwa wachawi hakuna hata kimoja kilichobuniwa. Najua lazima kuna baadhi ya wachawi watakuwa wameiona simulizi hii ama kuambiwa na watu. Ni kwamba Adela ameahidi kuwaumbua wachawi wote na njia zao zinazotumika ili watu wa duniani wajue. Kwa pamoja tunaupinga uchawi

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog