Search This Blog

KITABU - 4

 





    Simulizi : Kitabu

    Sehemu Ya Nne (4)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yeye na familia yake walipokua kule serengeti katika mbuga za wanyama kabla hawajaingia kwenda kutalii alikukutana na binti mmoja wa kiafrika,wakati wanazipiga hatua kuingia ndani ya gari ili kuelekea kutazama wanyama alidondosha hati ya kusafiria(International passport ) binti yule wa kiafrika aliokota hati hiyo akapaza sauti akasema"hey is this your passport?"(hii ni hati yako ya kusafiria?) alipogeuka alimuona binti wa kiafrika akiwa amenyosha mkono wake huku akishikilia hati hiyo, aliacha kuingia ndani ya gari na kuamua kukimbia kumfuata binti huyo wa kiafrika pale alipokua amesimama.Yule binti wa kiafrika alimkabidhi passport hiyo, yeye akasema""thanks my friend(asante rafiki) kisha akavua mkufu aliokua kauvaa shingoni mwake na kumkabidhi binti huyo wa kiafrika, alitabasamu kisha akazipiga hatua kurudi kule lilipokuwepo gari



    *************



    Baada ya kukumbuka hayo aliweza kutambua kuwa huo ndio ule mkufu wake aliemkabidhi yule binti wa kiafrika ,,,akajisemea moyoni"bila shaka huyu ndie yule binti alieokota passport yangu na kunikabidhi .....aliamua kuacha kumdhuru latifa akazipiga hatua kurudi nyuma kisha akarudi nyuma kisha akatoweka kimiujiza.

    latifa aliogopa hakuamini kama kiumbe huyo angemuacha hai macho yalimtoka na mapigo yake ya moyo yalikua yakipiga kwa kasi ya ajabu ,akatazama huku na kule alipoona kiumbe huyo ametoweka latifa alikichukua kitabu akatimua mbio akaufuata mlango na kutoka nje alikimbia bila kujua ni wapi anakoelekea.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ************



    Upande mwingine alionekana chery akiwa ndani ya kile chumba chenye mwanga hafifu wa rangi nyekundu huku machozi yakimtoka na kusema""ee Mungu nisaidie nitoke humu, maisha yangu yakuwa kama mfungwa kosa langu ni nini? chery aliyaongea maneno hayo huku akilia kwa uchungu...alitazama majeraha yaliyokuwa mikononi na miguuni mwake kwenye zile sehemu alizokuwa amefungwa minyororo....



    ***********



    upande mwingine alionekana Latiffa akitimua mbio kuelekea kituo cha polisi ili aombe msaada..

    alipofika aliwaelezea polisi kile alichokiona safarii hii walianza kupata wasiwasi kwa sababu nguo za latifa zilionekana kua na damu ,damu hiyo ilimimwagikia baada ya yule kiumbe kumnyanyua sebo na kukielekezea kichwa chake kwenye feni iliyokua inazinguka kwa kasi ikachinja shingo.

    Askari mmoja aliekua na cheo aliwaamuru maaskari watatu waongozane na latifa mpaka kwenye nyumba ya sebo , wakatoka nje haraka wakaingia kwenye gari na kuanza safari ya kuelekea kwa sebo ,,wakiwa njiani latifa alikifu.nua kitabu mpaka sehemu ya nane ili aone tukio linalofuata hadithi ilisimulia tukio la mauaji ya kutisha yaliyofanyika kwenye kituo kimoja cha polisi....alionekana kiumbe wa ajabu kuvamia na kuuwa askari wote waliokuwa zamu siku hiyo...latifa alistuka macho yakamtoka..akasema kwa sauti ya juu,"" simamisha gari...

    yule askari aliyekuwa akiendesha gari aliamua kupunguza mwendo wa gari hatimae gari likasimama.....latifa akasema""embu waambie askari wote waliopo kituoni waondoke muda huu...watauwawa...

    wale maaskari waliokuwemo ndani ya gari walistahajabu walihisi latifa kachanganyikiwa baada ya kushuhudia tukio la mauwaji.....baada ya sekunde kadhaa kupita ilisikika radio call ya kwenye gari ikitoa taarifa kuwa kituo cha polisi cha Temeke usalama wa taifa...kimevamiwa na kiumbe wa ajabu na kuuwa polisi wote waliokuwemo kituoni humo....wale maaskari walistuka wakaanza kumuogopa latifa...wakafungua milango ua gari na kutimua mbio kuelekea kusikojulikana huku wakimuacha latifa ndani ya gari.........latifa alihisi kuchanganyikiwa....akakifunua kitabu haraka ili aone nini kitatokea tena.....alipoanza kusoma hadithi sehemu ya tisa....latifa alipiga kelele.....hadithi ilisimulia mauwaji ya kutisha watu walivamiwa na kiumbe wa ajabu wakiwa hospitali....na kuuwa hakufanikiwa hata mtu mmoja kutoka hai katika hospitali hiyo kubwa

    (ya rufaa) latifa akakumbuka kuwa mama yake mzazi ni daktari wa Muhimbili...huenda tukio hilo likafanyika hospital hiyo....

    kabla hajamaliza kusoma hadithi hiyo...ghafla simu yake iliita..alipoitazama aliona ni mama yake anampigia.....alipoipokea alisikia sauti za watu wakipiga kelele ghafla simu ikakatwa...



    Latifa aliogapa sana akafungua mlango wa gari na kutoka nje..akafungua mlango wa mbele na kuingia uoande wa dereva akaliwasha gari la polisi...akaliondosha kwa kasi mpaka Muhimbili, alipofika aliona watu wakikimbia huku na kule..kila mmoja alioita njia yake....akatoka nje ya gari na kuanza kutimua mbio kuelekea ndani ya hospital..hata walinzi waliokuwa getini walitimua mbio wakalitelekeza geti likiwa wazi...watu walimshangaa latifa kumuina anaingia ndani ya hospitali wakati wenyewe kanakimbia kutoka ndani ya hospitali..ili kuoa maisha yao....latifa alikutana na maiti nyingi....zikiwa hazina vichwa, nyingine zikiwa zimetobolewa tumboni na kutolewa utumbo...latifa aliingiwa na wasiwasi juu ya mama yake...lakini akajipa moyo akazidi kusonga ndani zaidi kunako hospitali hiyo....



    kwa mbali aliona kundi la watu wakiwemo manesi na badaktari pamoja na wagonjwa wakitimua mbio....miongoni mwa kunfi hilo alikuwemo mama yake..ghafla kiumbe ye akajitokeza na kuanza kufanya mauwaji ya kikatiri akauwa wote akabakia mama yake latifa pekee akiwa hai...kiumbe yule akaanza kumfuata mama latifa..CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mama latifa akaanza kutimua mbio....yule kiumbe alipogeuza shingo yake aliona kunamgonjwa ndani ya wodi..mgonjwa huyo alikuwa anapumua kwa msaada wa mashine maalumu ya hewa safi(oxygen machine) akazipiga hatua kuingia ndani ya wodi hiyo alipomkaribia mgonjwa aliyekuwa amelala kitandani...akamvunja mguu mmoja..mgonjwa yule alihisi maumivu makali sana....kisha kiumbe yule akaunyofoa mguu huo...akamvunja mguu wa pili na kuunyofoa...kisha akazipiga hatua mpaka dirishani akavunja kioo akachukua kipande cha kioo kilichokuwa na ncha kali akarudi mpaka kwenye kitanda alichokuwa amelazwa mgonjwa yule...akanjanyua mkono wake na kumchoma shingoni kwa kutumia kioo hicho kisha akakiacha hapohapo shingoni mgonjwa yule alitapatapa kupigania pumzi kwa sekunde kadhaa akaiaga dunia....



    ******************



    upande mwingine alionekana mama latifa akitimua mbio...huwezi amini pamoja na umri mkubwa aliokuwa nao mama latifa,alikimbia kwa kasi kama binti wa miaka ishirini...ghafla yule kiumbe akajitokeza mbele yake.....akamkamata shingini na kumnyanyua juu..alipotaka kumtoboa tumbo...ikasikika sauti ya latifa""hey muache mama yangu tafadhali nakuimba usimdhuru.!!

    kiumbe yule akageuza shingo yake alipomuona latifa akamuachia mama latifa...kisha kiumbe huyo akatoweka kimiujiza.. ....

    latifa akakimbia mpaka pale alipokuwa amedondoka mama yake...wakati huoama latifa alikuwa akitokwa na haja ndogo mfululizo....akanyanyua mama yake na kuondoka nae..... wakati huo ukimya ulitawala hospital hiyo..haikusikika sauti ya kitu chochote..hapakuwa na mtu hata mmoja....



    walipotoka nje ya hospotal hiyo...latifa alistahajabu kuina maaskari wameizunguka hospital hiyo....huku wameshikilia siraha kuelekea upande walipokuwepo latifa na mama yake.....askari walipogundua kuwa ni binadamu wa kawaida wakashusha siraha zao...kisha wakaingia upande wa ndani ya hospotal ili kumtafuta muiwaji..



    ***************

    mama latifa pamoja na latifa walikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani...walipofika latifa akamsimulia mama yake kuhusu hadithi ya kitabu cha chery...mama latifa alistahajabu sana..akaomba asome kitabu hicho alikisoma kuanzia sehemu ya kwanza mpaya sehemu ya nane....alistahajabu kuina matukio yaliyoandikwa ndani ya kitabu ndio yaliyotokea na mengine yanaendelea kutokea.......alipoanza kuisoma sehemu ya tisa macho yalimtoka akaogopa sana hadithi ilielezea mtu mmoja aliyekuwa uwezo wa kipekee mtu huyo anaitwa JABU...

    jabu alitengeneza mtego wa kunasa vitu visivyo onekana(invisible) hadithi ilieleza kuwa baada ya kiumbe hiyo wa ajabu kugundua kuwa kuna mtu ambaye ametengeneza mtego ambao ungeweza kumnasa....alichukia sana kiumbe huyo akaamua kumtafuta jabu..



    *************



    upande mwingine hadithi ilisimulia kuwa siku hiyo jabu aliamua kwenda kufanya majaribio ya mtego huo kwa kuutega angani..kwa hiyo vitu au kitu chochoye ambacho kilikuwa na uhai bila kujionesha mbele za macho ya binadamu basi kitanaswa na kuvutwa upande wa juu kuelekea angani na kuingia ndani ya mtego huo......wakati jabu akiwa njiani kwenda kuutega mtego huo.....

    wakati huo huo yule kiumbe alikuwa yupo njiani kuelekea kwa jabu.... jabu akiwa njiani wakakutana uso kwa uso.....jabu alikuwa na uwezo wa kuona viumbe wasionekana kwenye macho ya binadamu wa kawaida.........ghafla kiumbe yule aliruka na kutua juu ya gari la jabu...



    Jabu akaliendesha gari kwa kasi,akakanyaga breki..gari likasimama ghafla na kumtusha kiumbe yule mbele akadondoka chini.....kisha jabu akachukua ule mtego na kuuanda harakaharaka...

    yule kiumbe alipo ona hivyo akatimua mbio na kutoweka kimiujiza......wakati jabu anatahamaki

    ghafla kiumbe yule alijitokeza na kumuuwa jabu..



    mama latifa alistuka akakifunika kitabu hicho wazo likamjia kuwa kuna mjomba wake aliyekuwa anaishi bukoba.....alikuwa ni fundi wa kutengeneza miatambo mbalimbali kwa kubuni yeye mwenuewe....akachukua simu yake na kumpigia mjomba wake....wakati huo latifa alikuwa akimshangaa mama yake...alijiuliza mama yake anampigia nani simu!!je kaona nini kwenye hadithi ya kitabu cha chery???



    simu ikapokelewa...kisha mama latifa akauliza hata bila kumsalimia mjomba wake""upo wapi ???

    mjomba akajibu,"nipo bukoboba najiandaa kuufanyia majaribio mtambo wangu mpya ambao unauwezo wa kunasa vitu vilivyo na uhai visivyoonekana....mama latifa akasema kwa sauti kubwa"" usiende mjomba utakufa...mjomba wake akacheka na kusema "kwa nini unasema hivyo mpwa wangu???

    mama latifa akajibu kunakiumbe anayeuwa watu kikatiri atakuangamiza,nakusihi usiende......ghafla simu ikakata....



    ****************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    upande mwingine alionekana mjomba wake mama latifa...akiuingiza mtambo ule ndani ya gari lake na kuianza safari ya kwenda kuufanyia majaribio......alipofika eneo aliloona kuwa ameona litafaa kwa kuutega ule mtego..alishuka kutoka ndani ya gari nakuushusha mtambo ule.....akachimba shimo refu kiasi kisha akauweka mtego ule ndani ya lile shimo.....akauwasha...ikatokea mionzi iliyoelekea upande wa juu (angani) mionzi hiyo haikuonekana kirahisi mpaka uwe na lenzi maalumu ya kuweza kuiona mionzi ile.....kisha akafukia shimo lile..... mionzi hiyo alisambaa angani kwote.....alipohakikisha ameutega vyema mtego huo akaingia ndani ya gari na kurudi nyumbani kwake...

    akiwa njiani akatoa rimoti maalumu ya kuuruhusu mtambo huo ili ufanye kazi...kabla hajabonyeza kitufe kwenye rimoti hiyo.....ghafla kiumbe yule akajitokeza na kutua juu ya gari lake.....akatoboa upande wa juu na kunyofoa kutoka ndani ya gari na kumrusha upande wa nje.akadondoka na kuvunjika kiuno...kiumbe yule akamfuta ili amuuwe...kumbe alipodondoka rimoti ikamponyoka na kudondokea kando yake.....alipogeuza shingo yake..aliiona rimoti ile akajivuta akaichukua rimoti ile..

    kiumbe yule akamrukia na kumtoboa tumbo...

    wakati anapigania kuivuta pumzi ya mwisho akabonyeza kitufe cha rimoti hiyo....ule mtambo ukaanza kufanya kazi muda huohuo...



    wakati huohuo alionekana chery akiwa ndani ya chumba kile chenye mwamga hafifu wenye rangi nyekundu...chery alinyanyuka akachukua shoka lililokuwa kando kando juu ya meza iliyokuwa na zana za kutisha....akaanza kukata minyororo ile...akafanikiwa kukata minyororo iliyokuwa imefungwa miguuni mwake....lakini alikuwa amechoka sana kwa sababu alitumia nguvu nyingi sana mpaka kuweza kukata minyororo hiyo. akawa amedondoka chini na kupoteza fahamu.....



    ************



    upande mwingine alioneka latifa na mama yake...

    mama latifa aliipiga simu ya mjomba wake lakini iliita tu bila kupokelewa.......

    latifa akakichukua kitabu haraka akafunua mpaka sehemu ya tisa akasoma hadithi.....alipofunua ukurasa wa sehemu ya kumi latifa alipiga kelele..

    hadithi ilielezea mauwaji ya kikatiri aliyofanyiwa binti mmoja aliyekuwa amefungwa ndani ya chumba....alipotazama mchoro wa picha iliyokuwa imechorwa ndani ya kitabu ilionesha binti huyo amefungwa minyororo alifanikiwa kuikata minyororo hiyo alipotaka kutoka ili akimbie kiumbe yule alijitokeza huku ameshikilia mashine maalumu ya kukatia vyuma (grender mchine)

    kisha akaiwasha na kuzipiga hatua kumfuata binti huyo aliyekata minyororo na kujaribu kutoroka....



    alipomkaribia akataka kumkata mara ghafla ule mtego wa mjomba wake mama latifa ukaanza kufanya kazi ukamnasa kiumbe yule na kumvuta mpaka kwenye lile shimo ambalo aliufukia ule mtambo uliotoa mionzi kuelekea juu ya anga..

    kiumbe yule akadondoka kando ya shimo hilo....na kisha akazungukwa na mionzi akawa yupo kati kati...hakuwa na ujanja tena....



    ******************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    upande mwingine alionekana chery akijaribu kujinasua kutoka kwenye minyororo aliyokuwa amefungwa mikononi...hatimae alifanikiwa lakini alipata maumivu makali sana...kwa sababu kipindi anavuta mikono yake,kuanzia juu ya viganja vyake ngozi ilitoka utadhani mtu anavua groves..kwa sababu minyiroro ilikuwa imekazwa vyema..



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog