Search This Blog

JICHO LA TATU - 3

 







    Simulizi : Jicho La Tatu

    Sehemu Ya Tatu (3)



    ***ilipoishia***



    wakati huohuo alionekana Mtemi akiwaamuru walinzi wake wa karibu wakamuite Vida anamaingezi nae.

    wale walinzi walipoingia chumbani kwa Vida hawakumkuta,,wakamtafuta kila kona..hawakufanikiwa kumuona vida.. wakarudi kwa Mtemi kutoa taarifa kuwa Vida hayupo..Mtemi akastuka akahisi huenda binti yake hayupo katika sehemu salama!!! akaamuru vijana wote wamtafute Vida usiku huohuo..na popote watakapomkuta...wahakikishe wanamrudisha haraka iwezekanavyo.....akasema,,"mtu yeyote atakayekutwa na binti yake...akamatwe...na kunyongwa hadharani.....

    msako ukaanza........



    ***Endelea***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Upande mwingine alionekana Michael,akiwa bado yumo ndani ya kichaka kajificha.....upepo ulikuwa ukivuma kwa kasi kutokana msitu huo ulikuwa na miti mikubwa....

    upepo huo ulisababisha baridi kali..na mbu pamoja na wadudu watambaao/siafu walimng'ata Michael lakini hakuwa na namna alivumilia.akakumbuka mafunzo na mateso kipindi amejiunga na jeshi...ghafla zikaanza kusikika ngurumo za radi.....wingu likaanza kutanda na kuzifunika mbaramwezi na nyota...giza likatanda ghafla Mvua ikaanza kunyesha....

    ilinyesha mvua kubwa kupita kiasi...



    *******************



    Upande mwingine walionekana wale maaskari sita waliobaki...wakiwa bado wamo ndani ya kile kicha walichokuwa wamejificha tangu mchana..mvua iliwanyeshea...ikiambatana na baridi kali sana..wakaanza kutetemeka......mmoja kati yao..kumbe alikuwa anasumbuliwa na kifua.....huwa kinambana na kushindwa kumpumua,,,,akipigwa na baridi kali.......ghafla akaanza kushindwa kupata pumzi...akahangaika sana..wenzake walijitagidi kumsaidia kwa kumkumbatia kwa pamoja wakamuweka katikati,,,lakibi haikusaidia...na baada ya dakika kadhaa..askari huyo alikata Roho....wale maaskari wenzake waliskitika sana wakajikuta wanadondokwa na machozi bila kutarajia,,wakabaki maaskari watano.

    mvua iliendelea kunyesha kwa kasi kubwa...walitamani ardhi ipasuke watumbukie ndani yake.....



    *************************



    Upande mwingine alionekana Vida akiwa ameketi kando ya Makala huku akimtazama kwa macho ya kimitego mitego(kimahaba) vida alishindwa kuongea na makala kutokana kila alichomwambia Makala,,,Makala alibaki kimya bila kujibu...kutokana na lugha aliyokuwa akiitumia Vida kuongea nae,,,Makala aliweza kuyaelewa maneno machache...lakini akaagundua kuwa Vida anamtamani kimapenzi....uzalendo ulimshinda Vida akaanza kumtomasa Makala....

    Makala alijizuia,,kwa sababu alikuwa anampenda sana Norega...hakuwahi kufikilia kumsaliti mkewe.



    Kumbe wakati Vida anatoka chumbani kwake kuelekea kwenye nyumba aliyokemo Makala...

    SUBI alisikia mlango wa chumba cha Vida ukifunguliwa....Subi ni mama mzazi wa Vida....akaamua kufatilia ili abaini binti yake anaenda wapi usiku huo!!! akamuona binti yake anaingia kwenye ile nyumba alipomokuwemo makala.....Subi akazipiga hatua za kunyatia...akazunguka nyuma ya nyumba hiyo...

    kutokana nyumba hiyo ilitengenezwa kwa miti.....Mama Vida aliweza kuchungulia na kuona kila kitu kilichokuwa kinaendelea mule ndani......macho yakamtoka...kumuona binti yake anamlazimisha Makala kufanya nae ngono....akaamua kuondoka aende akamshtaki Vida kwa Baba yake...lakini alipoingia upande wa ndani ya nyumba...akamkuta Myemi ambaye ni mumewe anafanya matambiko yake......na alishasema tangu mwanzo..kuwa kama akiwa anafanya matambiko....asiongeleshwe na mtu yeyote hata mkewe......

    Mama vida akaingia chumbani akaketi kumsubiri Mumewe amalize kufanya matambiko,,ili amueleze kile alichokiona vida anakifanya..



    ********************



    wakati huo huo kila kijana wa jamii ya wakololo alikuwa kashikilia kitani cha moto..kilichotengenezwa kwa mti,,huku upande wa juu kumefungwa kwa kuzungushiwa kamba zilizochunwa kwenye magome ya miti..na kupakwa mafuta ya wanyama...

    vijana hao wakaingia mstuni zaidi kumtafuta vida,,binti Pekee wa Mtemi...walitafuta kwa muda mrefu sana mpaka majira ya saa nane za usiku,,lakini hawakuweza kufanikiwa kumpata vida,,wala hawakuona dalili yoyote ya vida kuwepo maeneo hayo..wakaamua kurudi kule kijijini kwao,,ili wakatoe taarifa kwa Mtemi kuwa,,hawajafanikiwa kumpata vida.....wakiwa njiani wanarudi alionekana mkuu wa vijana hao wa kikololo,,,akiwa nwenye mawazo mazito,,alikuwa akitafakari neno la kumwambia MTEMI....kwa sababu Mtemi wao huwa hataki kusikia kauli ya kushindwa....endapo akitoa agizo....ni lazima litekelezwe na endapo wakishindwa kufanya walichoagizwa,,huwa anawachinja bila huruma vijana kadhaa wa kikololo......waliendelea kuzipiga hatua kurudi kule kijijini.....hatimae wakafika,,,lakini yule mkuu wa vijana hao..akasema,,"kabla sijaenda kutoa taarifa kwa Mtemi,,,itabidi tukague nyumba moja hadi nyingine..huenda Vida yupo hapa hapa kijijini....wakaanza kufanya msako kwenye nyumba moja baada ya nyingine.....walimtafuta vida bila mafanikio....mkuu wa vijana hao akapagawa....lakini hakuwa na namna ya kufanya....akazipiga hatua kuufuata mlango wa Mtemi ili akatoe taarifa....ghafla wazo likamjia akasita kutembea akageza shingo yake na kuitazama nyumba iliyo kuwa mbali kidogo na hapo alipo......akajisemea moyoni,,"hiyo nyumba hatujaikagua..yawezekana vida akawemo ndani ya nyumba hiyo....CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    pia akawaza kuwa,,huenda Makala katoroka na vida....

    akapaza sauti,,"akaongea kwa lugha yao akimaanisha waende kufanya msako kwenye ile nyumba iliyotengenezwa kwa miti,,

    nyumba hiyo ndio ile nyumba aliyokuwemo MAKALA pamoja na VIDA......





    wale vijana wa Kikololo wakatii amri ya mkuu wao,,wakazipiga hatua kuifuata nyumba hiyo.

    wakati huo huo alionekana Vida akiendelea kumpapasa Makala.,

    Makala akaongea kwa sauti ya ukali nakusihi acha hilo jambo unalotaka kulifanya Vida akastuka ingawa hakuelewa lugha aliyoitumia Makala lakini akagundua kuwa makala hataki yeye afanye jambo hilo.

    kitendo hicho kilimfanya Vida akose furaha kwa sababu mwili na hisia zake zilikua tayari kufanya ngono na Makala ,Vida akachukia akanyanyuka kwa hasira .

    Upande wa nje wa nyumba hiyo walionekana vijana wa Kikololo wakiizunguka nyumba hiyo huku wakipiga kelele za mayowe kwa lugha yao, Vida akastuka akaingiwa na hofu baada ya kujua mayowe hayo yakiashiria hali ya hatari akamtazama makala kwa macho ya mshangao!! Vida akatimua mbio huku akinyata akaingia kwenye kile chumba kingine akajificha chumba hicho kilikua na makololo mengi yakiambatana na ngozi pamoja na pembe za wanyama mbali mbali



    ******************



    Upande wa nje ya nyumba hiyo....alionekana yule mkuu wa vijana hao wa kikololo akiwaamuru vijana watatu kuingia ndani ya nyumba hiyo wafanye msako...ni kitendo cha sekunde wakafungua mlango na kuingia upande wa ndani..wakamkuta Makala.....ameketi wakaanza kuangaza angaza macho huku na kule....hawakumuona Vida!!! Makala akaanza kuingiwa na hofu...wale vijana watatu wakaingia kwenye kile chumba alichokuwemo Vida..wakaangaza angaza macho lakini hawakumuona vida...

    kijana mmoja kati ya vijana hao watatu,,akazipiga hatua kuelekea kwenye zile ngozi zilizokuwa zimepangwa.....akaangaza angaza macho lakini hakumuona Vida,,,kumbe Vida alikuwa amejificha kwenye kona ya chumba hicho na kujifunika ngozi ya chui iliyokuwa imekaushwa......

    wakati anazipiga hatua kutoka hapo...akasita akahisi kitu,,,akawaita wenzake kwa lughatq yao....akimaanisha waje wasaidiane kuzitoa ngozi hizo ili watazame huenda Vida kajificha chini ya ngozi hizo......

    wale vijana wawili wakaja haraka...wakaanza kutoa ngozi moja moja.....lakini kijana mmoja akasema kwa lugha yao akimwambia yule yule kijana aliyewaita,,akimaanisha,,"utakuwa umeona vibaya hakuna mtu hapa.....wakarudisha haraka ngozi hizo.....kwa kuzipanga.

    walipomaliza wakazipiga hatua kutoka nje ya chumba hicho.......

    Vida aliendelea kujificha lakini uzalendo ukamshinda kutokana na joto na harufu kali ya ngozi hizo za wanyama pia alianza kukosa pumzi..akakurupuka akanyanyuka huku akikohoa kwa nguvu....

    sauti ya Vida ikasikika...vyema kila mtu aliweza kusikia sauti ya vida akikohoa.....

    wakarudi haraka ndani ya chumba kile..wakamkuta Vida wakamsisitiza atoke aende kwa baba yake anamaongezi nae.....



    hawakuweza kumgusa wala kumkamata Vida..kwa sababu ni mwiko kumgusa binti wa Mtemi...isipokuwa Mwanaume atakae kuwa Mume wake.....Vida akatoka ndani ya chumba hicho,, akazipiga hatua kuelekea kwa baba yake huku akilindwa kwaulinzi mkali......



    Yule mkuu wa vijana hao akaingia ndani ya nyumba hiyo akamfuata Makala..akamtazama kwa macho ya huruma kisha akamuingelesha makala kwa lugha yao akimaanisha,,"Nasikitika sana kwa sababu unamasaa machache ya kuishi,,,alipomaliza kuongea hivyo akaondoka zake akimuacha Makala bado kaketi..lakini kitu kilichomshangaza zaidi Makala,,,alipomuona mkuu wa vijana wa kikololo akifunga mlango huo kwa nje.......Makala alistuka akajaribu kukumbuka Hayo maneno yanamaana gani? kwa sababu alishawahi kusoma historia ya jamii hiyo katika kitabu...hivyo alikuwa anaelewa baadhi ya maneno ua lugha hiyo.....ghafla akastuka akanyanyuka haraka..baada ya kukumbuka maana ya manenk hayo kwa kiswahili..macho yakamtoka akaingiwa na hofu kubwa kupita kiasi,,mapigo yake ya moyo yakaanza kupiga kwa kasi huku jasho linamtoka...akajisemea moyoni,,"Inamaana nitakufa!!!!????

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *****************



    upande mwingine alionekana Subi(mke wa Mtemi)

    akijilaza kwenye kitanda kilichotengenezwa kwa miti kikiwa kimetandikwa kwa manyoya mengi ya ndege....na upande wa juu zikatandikwa ngozi mbili za mnyama simba.. Subi alikuwa akisubiri mumewe amalize kufanya matambiko ili amueze kile alichokuwa anakifanya binti yake wa pekee..

    akajikuta amepitiwa na usingizi akasinzia kabisa bila kuongea chochote na mumewe..(Mtemi)



    wakati huo alionekana Vida akiingia ndani ya nyumba...akamkuta baba yake(Mtemi) ameketi kwenye kiti baada ya kumaliza kufanya matambiko....Mtemi akasema,,kwa lugha yao akimaanisha,,"ulikuwa wapi?Binti yangu kipenzi!

    nilikuwa na wasiwasi huenda umepatwa na jambo baya....kabla Mtemi hajamaliza kuingea,,akaja yule mkuu wa vijana wa kikololo..akatoa heshma kwa Mtemi kisha akasema,"tumemkuta kwenye ile nyumba tuliyomuhifadhi yule mtu tuliemkuta kule mstuni....

    Mtemi akakasirika sana,,,akajisemea moyoni...yani huyu mwanaharamu anathubutu kumgusa binti yangu....hii ni Fedhea!! akaongea kwa ukali kwa kusema,,"nenda kamfunge kamba...na awekewe ulinzi wa kutosha ili asije akatoroka.....na itakapofika kesho asubuhi Anyongwe hadharani mlaka kufa ....



    ****************



    upande mwingine kule mstuni alionekana Joshi akizipiga hatua za kikakamavu usiku huohuo akisonga mbele zaidi....aliweza kuona vyema kutokana na lile jicho la chui alilolipachika kwenye jicho baada ya kulilinyofoa.. jicho lake....

    kwa sasa akawa na uwezo mkubwa wa kuona vizuri hata akiwa mbali....

    alizidi kusonga mbele ....alitembea umbali mrefu mpaka pakakukucha.....kwa mbali akasikia kelele za watu wakiimba kwa kilugha akaamua kuelekea upande huo ambao kelele hizo zinapotokea......alipokaribia akaona watu wamekusanyika kumzunguka mtu aliyekuwa amesimama juu ya meza iliyotengenezwa kwa miti...huku kafungwa mikono yake kwa kamba. pia akamuona kijana mmoja wa kikololo akimvika kamba shingoni yule mtu aliyesimama juu ya meza hiyo...Joshi akatabasamu akazipiga hatua za haraka haraka kuwafuata watu hao....





    Alionekana yule kijana wa kikololo akiendelea kuifunga kamba balabala juu ya mti ikitokea kwenye shingo ya Makala. watu wa jamii hiyo ya wakololo walikusanyika kushudia tukio hilo huku wakiimba nyimbo kwa lugha yao, Makala akavuliwa nguo zote nakubaki uchi wa mnyama tayari kwa kunyongwa....watu hao waliendelea kuimba kwa lugha yao huku wakipiga kelele wakimsubiri mtemi aje kutoa amri Makala anyongwe..

    Ghafla ulionekana upanga mrefu uliorushwa kutokea msituni, upanga huo ulikwenda moja kwa moja mpaka kwenye shingo ya yule kijana aliyekua anamfunga kamba Makala....akandondoka chini na kupoteza maisha papo hapo .,wale watu jamii ya wakololo wakashtuka na kutazama ule upande ambao ule upanga umetokea, wakamuona mtu mrefu mwenye sura ya kutisha akizipiga hatua kuja huo upande walipo .Wakaanza kurusha mikuki huku wengine wakirusha mishale, walirusha mikuki na mishale mingi mfululizo .

    Mishale na mikuki iliingia kwenye mwili wa Joshi lakini Joshi aliichomoa na kuitupa chini pia alichomoa mikuki na kuirusha kule walipokuwepo wakololo.,



    Wakati huo huo alionekana Makala akihangaika kujinasua kutoka kwenye kitanzi akafanikiwa kukata kamba zilizofungwa mikononi mwake ,akazua kitanzi (kamba iliyokua imefungwa shingoni mwake), akaanza kutimua mbio. Kutokana na mwili wa Makala kua mnene na kitambi ,Makala alipata wakati mgumu kukimbia kwa kasi akajikuta anadondoka mara kwa mara, kwa mbali alionekana Mtemi akiwa amesimama nje ya mlango wake macho yalimtoka akastaajabu kumuona Joshi.



    ***********CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Upande mwingine kule msituni walionekana wale maaskari watano wakichimba shimo ndani ya kichaka hicho kwaajili ya kumzika mwenzao ....walipata wakati mgumu sana kutokana walikuwa hawana vifaa vya kuchimba shimo...wakaamua kuchimba kwa kitumia panga zao fupi..walizokuwa wamezifunga kwa mkanda...kwenye viuno vyao,huku wakiutoa udongo nje ya shimo hilo kwa kutumia mikono yao. iliwachukua masaa manne mfululiizo mpaka wakachimba shimo la urefu wa futi nne(4) walipomaliza wakamzika na kulifukia shimo hilo..wakatoka kwenye kichaka hicho na kuanza kutafuta njia ya kutoka kwenye msitu huo..walizipiga hatua huku macho yao yakitazama kwa tahadhari kubwa..na bunduki zao zikiwa tayari kupambana na chochote kitakachotokea mbele yao.....walitembea umbali mrefu sana..bila kupata uelekeo wa njia ya kutoka mstuni humo...wakaanza kupatwa na njaa....wakajikaza kwa kupoza njaa kwa kunywa maji yaliyokuwemo ndani ya vibuyu vyao vya plastiki....



    *******************



    Upande mwingine alionekana Michael akiwatafuta wenzake ili ahakikishe kama wapo salama..kwa sababu yeye ndio mkuu wa kikosi hicho,,,wakati huo,Michael alikuwa hajui kuwa kapoteza askari mwingine,,yeye aliamini bado wapo sita......akaendelea kuwatafuta wenzake.....aliwatafuta kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote...akaanza kuhisi njaa...akaamua kuwinda angalau mnyama ili aweze kujipatia mlo.

    haikuwa kazi ngumu kwa Michael kwa sababu alizaliwa katika familia ya Uwindaji...Baba yake alimfundisha kuwinda kwa kutumia mbinu mbali mbali za uwindaji....akachomoa upanga wake akakata Fito kadhaa (miti mwembamba sana) akachonga miti hiyo..ikatengeneza ncha kali....akachimba mashimo mafupi manne..akaichomeka miti hiyo..akachuna kamba za magome ya miti na kuifunga kwa kuivuta akafunga kamaba hizo kwenye mti mikubwa miwili..kwa kuegesha....akawa tayari katengeneza mtego wa kumnasa muama ueyote atakaye katiza eneo hilo..... akazipiga hatua na kujificha kwenye kichaka.......



    **********************



    Upande mwingine kule kwenye kijiji cha jamii ya Wakololo,,,hali ilikuwa tete...Joshi aliendelea kufanya mauwaji ya kikatiri bila huruma....

    Mtemi....alipo ona watu wake wanauwawa akaingia ndani kufanya jambo fulani......akachukua mshale akaupaka dawa maalum kwenye ncha ya mshale huo... dawa hiyo ni sumu kali sana ya kichawi,,ya mila za Wakololo.... ambayo inauwezo wa kupenya kwenye Mzimu....hata kama Mzimu huo umevaa kiwiliwili cha Binadamu .......akachukua upinde akazipiga hatua akatoka upande wa nje....



    Wakati huohuo Joshi aliendelea kuwaangamiza wale vijana wa Jamii ya wakololo...akachukua ule upanga wake kwa kuuchomoa kutoka kwenye shingo ya yule kijana alimchoma kwa kuurusha upanga huo.....akaanza kuwafyeka shingo zao vichwa vikaruka kando....Joshi aliuwa watu wengi kwa muda mchache...

    wakololo waliobaki wakaanza kutimua mbio na kutokomea mstuni..baada ya kuona mambo yamekuwa magumu.......

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mtemi alionekana akutafuta sehemu nzuri ya kujificha ili aweze kuufyatua mshale huo kutoka kunako upinde huku akiwa ametulia.......na kulenga shabaha kwa umakini mkubwa ili mshale huo uingie katikati ya kifua cha..Joshi.

    akafanikiwa kupata sehemu ya kujificha vyema...akachukua ule upinde akaweka mshale na kuuvuta vyema...akawa tayari kwa kuufyatua....lakini alikuwa akisubiri Joshi ageuke ili afyatue mshale huo kifuani mwake...

    Ghafla Joshi akageuka ili kutazama nani kabaki ili amuangamize.........

    Mtemi akavuta upinde huo kwa nguvu zake zote akauachia mshale huo............



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog