Search This Blog

JICHO LA TATU - 2

 







    Simulizi : Jicho La Tatu

    Sehemu Ya Pili (2)



    ***ilipoishia***

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Joshi akazipiga hatua kadhaa akaangaza angaza macho huku na kule..akamuona yule askari mwingine akiwa anajinasua kwenye kichaka kilichokuwa na miba..aliingia kwenye kichaka hicho bila kujua kuwa kilikuwa na miba mirefu...

    wakati akiendelea kujinasua...Joshi akamkaribia na kumfyeka kichwa kikaruka kando...akabaki kasimama kama sanamu..huku akiwa bado kanasa kwenye kichaka hicho chenye miba...

    Joshi akatoka eneo hilo akasonga mbele zaidi....kwa mbali akaona kuna hema lililotengenezwa kama nyumba..akaamua kulifuata hema hilo.....



    ***Endelea***



    kule ndani ya Hema alionekana Makala,,akitafuta sehemu iliyojificha ajihifadhi ,,endapo kama mtu akiingia humo ndani asionekane kwa urahisi....aliamua kujificha kwa sababu ndani ya msitu huo,,Tayari kuna hali ya hatari.....na wenzake watano tayari wameuwawa na Joshi jitu katiri...

    mapigo yake ya moyo yalipiga kwa kasi kutokana na hofu kubwa iliyokuwa imetanda juu yake....ghafla akasikia vishindo vizito vya miguu!!! akaogopa sana akahisi labda ni mnyama Tembo anatembea upande wa nje!! macho yakamtoka hofu ikazidi kuongezeka...akachungulia lakini hakuweza kuona upande wa nje,,

    vishindo havikusikika tena,,,,ukimya ukatawala...

    Pasipo kutarajia,, Joshi akaingia ndani ya hema hilo...akaangazaangaza macho..hakuona mtu yeyote......akazipiga hatua kadhaa kuingia ndani zaidi....kutokana na urefu aliokuwanao ilimlazimu kuina ili atoshe kuenea ndani ya hema hilo......katika kuangaza angaza...akajikuta amekitazama kioo kikubwa kiasi kilichokuwemo ndani ua hema hilo...akakisogelea kioo hicho...akaonekana kukitazama kioo kwa dakika kama mbili hivi,mfululizo....Joshi alichukia, akakasirika sana baada ya kuona uso wake ulivyojeruhiwa na chui...kumbe alitobolewa jicho na kucha za chui yule...........

    Joshi akachukua upanga wake akauingiza ndani ya jicho hilo lililotobolewa akalinyofoa jicho na kulitupa chini,,,,akapiga kelele kwa hasira,,na maumivu ya hali ya juu...

    kelele hizo zilitoa mngurumo wa kutisha.....na kwa sababu ukimya ulitawala ndani ya msitu huo....kelele za Joshi,,,zilisikika maili nyingi....

    zikasababisha ndege warukao,,,kuruka kutoka kwenye matawi ya miti na kutokomea angani,,,pia wanyama wakatimua mbio na kutokomea ndani zaidi ya msitu huo....



    **************************



    Joshi akaanza kuvuruga vuruga vitu vilivyokuwemo ndani ua hema hilo...kwa kuvitupa chini...akanyanyua kiti kilichotengenezwa kwa mbao akakirusha upande mwingine...

    kumbe ndio ule ule upande alipokuwa amejificha Makala...kiti kile kilikwenda moja kwa moja mpaka kwenye mgongo wa Makala....

    Makala akahisi maumivu makali sana nusu anyanyuke hapi alipo..akajikaza kiume.....



    Upande mwingine liliinekana gari likipita ndani ya msitu huo,,,,gari hilo lilikuwa limebeba maaskari wa kulinda wanyama pori....kumbe maaskari hao,,waliletwa ili wale maaskari waliokuwa wakilinda siku ya jana......leo watolewe wakapumzike.....wakiwa njiani kuelekea kule lilipokuwepo Hema....wakastka kukuta kuna gari limetobolewa magurudumu!!!! wakaamua kulisogelea garo hilo,,wakastahajabu kukuta teki ta kuhifadhia mafuta limeng'olewa na kutupwa pembeni,,kumbe gari hilo ndio lile gari alilokujanalo Makala pamoja na wafanyakazi wenzake humo mstuni kwa ajili ya utafiti.....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mmoja kati ya maaskari hao akasema,,"kutakuwa na tatizo!! kwa nini hili gari limetobolewa magurudumu na limetelekezwa hapa???

    wakaweka siraha zao tayari kwa mapambano...wakaingia ndani ya gari lao na kusonga mbele kuelekea kwenye hema.......kabla hawajafika mbali wakaona maiti ya askari mmoja amekatwa shingo....huku kichwa chake kikiwa kando kabisa!!! wakastuka....dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo akaliendesha kwa kasi ili wawahi kuangalia kama maaskari wengine wapo salama kule kwenye hema!!! ghafla wakakutana na maiti nyingine ya mtu kakatwa shingo...

    kumbe maiti hiyo ni ya mmoja kati ya wale wafanyakazi waliikuja na Makala....

    maaskari wakaanza kuingiwa na hofu.....askari mmoja akasema,,"aisee geuza gari turudi tukatoe taarifa,, yule dereva akasema,," tutarudi vipi!!! je? wale maaskari wenzetu itakuaje?? unamaanisha tuwaache huku mstuni????

    wacha tukawachukue....dereva huyo alitasema maneni hayo huku akizidi kuzipanga gia,wakaanza

    kulikaribia hema.....walipotazama kwa mbali..wakaona kuna mtu akitikea ndani ya hema huku kavalia joho refu jeusi...likiwa limefunika upande wa kichwani mpaka usoni....huku kashikilia upanga mrefu wenye ncha kali.....yule dereva akasimamisha gari haraka,,ili watazame mtu huyo anataka kufanya nini....

    Joshi akanyanyua usi wake ukutazama ule upande ambao lilikuwepo gari la maaskari wa kulinda wanyama pori.....akaanza kuzipiga hatua kulifuata gari hilo.....akaingeza kasi ya kutembea hatimae akaamua kukimbia huku akiwafuata wale maaskari....

    yule dereva akaingiwa na hofu..akaamua kuliwasha gari ili wakimbie...alipojaribu kuzunfusha ufunguo gari halikuwaka...akajaribu tena na tena,, lakini bado gari hilo halikuwaka...akasema,,"gari imeflot mafuta yanarudi kwenye kabreta...wale maaskari wakachanganyikiwa baada ya kusikia hivyo!!!wakaamua kupiga simu makao makuu waletewe msaada...kabla hawajamaliza kutoa taarifamtandao ukawa unakatakata...hivyo hawakusikilizana vizuri..



    walipoangaza macho yao kumtazama mtu huyo kafika wapi..wakastuka!!! hawakumuona tena....wakiwa bado wanatahamaki...ghafla alionekana Joshi akitokea kwenye kichaka kilichokuwa karibu kabisa na gari hilo...........walipojaribu kufyatua risasi kumlenga Joshi..tayari walikuwa wameshachelewa..Joshi aliwafyeka shingo zao kwa kutumia upanga wake... .wakafa papohapo,,,kumbe wakati wanapiga simu mtandao ukakata.... hawakukuta simu ile ilibaki hewani ikisikika kule makao makuu..



    Kule ndani ya Hema,,alionekana Makala....akinyanyuka kutokea ile sehemu aliyokuwa amejificha,,akazipiga hatua za tahadhari...kuufuata mlango ili achungulie upande wa nje,,wakati huo mapigo yake ya moyo yalikiwa yakipiga kwa kasi,,huku jasho linamtiririka kama kamwagiwa maji....alipochungulia upande wa nje,,kwa mbali akaona kuna gari limesimama...akafurahi,,akajua atapata msaada wa kutoka kwenye msitu huo.....akaangaza macho yake kwa kutazama huku na kule,,hakuona dalili yoyote ya mtu kuonekana eneo hilo...akatoka ndani ya hema akazipiga hatua za haraka haraka huku akitazama kushoto kulia......alipolikaribia lile gari,,akastuka kuona watu wamo ndani ya gari hilo,,,akatazama kwa umakini akagudua watu hao..walikuwa hawana vichwa...vilionekana viwiliwili tu.....hofu ikatanda juu yake....akatimua mbio kulifuata gari hilo akafungua mlango wa upande wa dereva akamvuta yule askari aliyekuwa dereva wa gari hilo na kumtoa nje...akaingia ndani ya gari hilo akafunga mlango...akazungusha ufunguo ili gari liwake....lakini gari halikuwaka....macho yakamtoka....akaamua kufungua mlango kutoka nje....akaingia uvunguni, mwa gari hilo kwa ajili ya kujificha...



    ***********************



    Upande mwingine kule makao makuu,,alionekana askari anayehusika na mawasiliano ya moja kwa moja na maaskari wakiwa huko porini kwa ajili ya kulinda wanyama, akajaribu kufanya mawasiliano kwenye ile simu iliyopigwa kutokea kule msituni



    Makala alisikia mlio wa simu ikiita ndani ya gari hilo, kutokana na hofu kubwa aliyokua nayo hakuthubutu kutoka chini ya uvungu kuipokea ile simu..... simu iliita mpka ikakata na baaada ya sekunde kadhaa simu ikaita tena!!lakini Makala aliiacha hivyo hivyo ikiita, wazo likamjia akajiona yeye ni mjinga akajisemea moyoni,,"wacha nipokee simu hii huenda nikaweza kupata msaada..akanyanyuka haraka kutoka uvunguni mwa gari akafungua mlango wa gari akaangaza macho yake ndani ya gari hilo,, akafanikiwa kuiona simu,,alipotaka kuipokea simu ikakata

    kumbe tayari alikua amekwisha chelewa!!! akajarbu kuipigia hiyo namba...lakini simu ikamwambia kuwa hakuna salio la kutosha kuweza kupiga simu hiyo....akaamua kuichukua simu hiyo akaiweka mfukoni mwake..akarudi chini ya uvungu wa gari.......akajificha.

    baada ya dakika tano simu ikaita tena...akaitoa mfukoni haraka,,alipobofya kitufe cha kupokelea..simu ilikuwa imeishiwa umeme(charg) ikazimika,,Makala akajutia kwa kusema,,"USIPO ZIBA NYUFA UTAJENGA UKUTA..sasa wacha nijenge ukuta.....mimi ni mjinga kiasi gani,,,kwa nini mwanzo sikupokea simu ilipokuwa ikiita!!!

    ghafla akasikia vishindo vizito vya mtu akitembia..

    akastuka..hofu ikazidi kuongezeka....akasikia gari linatikiswa....akafumba macho....ili asishuhudie akiuwawa.... alipofumbua macho ghafla akaona gari linavurutwa....akaamua kulishikilia kwa nguvuzake zote...

    kumbe Josgi alirudi na kulivuruta gari hilo aende akalifiche kwenye vichaka vilivyokuwa mstuni humo,,kama kunamtu anayetaka kutoroka,,basi atoke mstuni humo kwa kutumia akili zake mwenyewe,,..Makala aliendelea kushikilia kwanguvu...vyuma vilivyokuwa chini ya gari hilo...

    Joshi alilivuruta gari hilo umbali mrefu sana....kwa mbali akaona kuna korongo kubwa,,akatabasamu....akazipiga hatua za haraka haraka huku akilivuruta gari hilo akalitupe kule chini ya korongo.....Makala alipotazama ni wapi Joshi anaelekea,,akaona Joshi anaelekea kwenye korongo lililokuwa na mteremko mkali...akastuka macho yakamtoka.....akajilaumu kwanini asingebaki palepale lilipokuwa limesimama gari....



    *************************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    upande mwingine kule makao makuu...alionekana mkuu anayehusika na kitengi cha wanyama pori...akiamuru....askari waende kwenye msitu UNGEBO kuwaokoa maaskari waliokuwemo ndani ya msitu huo........

    akamteuwa MICHAEL awe kamanda mkuu aongoze kikosi kitakachokwenda msitu UNGEBO..

    zikaruka ndege mbili..zilizokuwa na maaskari watatu kila ndege moja...kuelekea msitu Ungebo

    Michael na maaskari saba wakaingia ndani ya gari na kuianza safari ya kuelekea msitu Ungebo..



    ***********************



    kule mstuni,,Joshi alionekana akiendelea kuliviruta gari akakaribia kabisa kwenye korongo...Ghafla akasikia mngurumo wa ndege....akanyanyua shingo yake kutazama angani.....

    wakati huo huo..kule angani..alionekana askari mmoja..akiwa ameshikilia Darubini(BINOCOLUS)

    Akitazama upande wa chini kwa kupitia darubini hiyo..akastuka kumuona mtu mrefu anavuruta gari..alipotazama kwa umakini..akaona viwiliwili vya maaskari vikiwa havina vichwa..ndani ya gari hilo....akazungusha (ZOOM)darubini ili kumuona yule mtu ni wa aina gani..ananguvu gani za kulivuta gari zito aina ya JEEP!!!akastuka kuona mtu huyo...hana sura...usowake ulionekana kama nyama mbichi......akasema,,"WEKA SHABAHA,, SHAMBULIA....bila kupoteza muda Rubani wa mdege hiyo ya kijeshi..aliweka shabaha akaanza kumshambulia Joshi kwa kubonyeza kitufe cha kufyatulia risasi mfululizo....

    risasi hizo zilitoka nyingi nyingi kama mvua....

    Risasi hizo ziliingia kila mahali kwenye mwili wa Joshi....akaamua kuliachia gari na kutimua mbio akatokomea mstuni...hapo ndipo walipoamsha hasira za Joshi!!! alikasirika sana......akaanza kung'oa miti kwa hasira huku akipiga kelele zilizotoa mngurumo mkubwa wa kutisha....akachukua mti mkubwa alioung'oa akauvunja katikati..akaurusha angani kuilenga ile ndege iliyokuwa ikimshambulia.....mti huo uligonga pembeni ya ndege...na kung'oa injini moja ya ndige hiyo..ikapoleza uelekeo na kudondoka kuelekea chini kwenye korongo ikaripuka.....wakati huo Makala alikuwa bado yupo kule chini ya gari....akitetemeka kwa uwoga...haja kubwa na ndogo zilimtoka mfululizo......



    *****************



    Upande mwingine alionekana Michael akiwa pamoja na maaskari saba(7) wakianza kuingia ndani ya msitu huo.... wakasikia sauti ya mripuko mkubwa!!!!....wakati bado wanataamaki..ghafla kuna mti mkubwa uliong'olewa ukarushwa na kutua mbele ya gari lao njia ikaziba na mti huo....



    Michael pamoja na wale maaskari saba..wakastuka...wakashuka kutoka ndani ya gari haraka....wakaweka sawa bunduki zao..tayari kupambana na chochote kitakachotokea mbele yao...Michael akasema,,"Hakuna kurudi nyuma tusonge mbele kuhakikisha tunawaokoa maaskari waliokuwemo kwenye msitu huu..SAWA??

    wale maaskari saba hawakuwa na budi kutii amri ya kamanda mkuu wa kikosi hicho.....wakaanza kuzipiga hatua kusonga ndani zaidi ya msitu huo...

    walizipiga hatua kwa tahadhari...huku wakiwa katika mstari mmoja..

    walitembea mwendo wa lisaa lizima,,lakini hawakufanikiwa kumpata askari hata mmoja...wakazidi kusonga mbele zaidi.....wakatokezea kwenye lile Hema....wakalifuata na kuimgia ndani ya Hema hilo kwa tahadhari huku maaskari watatu wamebaki nje..kwa ajili ya kulinda usalama...

    miongoni mwa wale maaskari wanne(4) alikuwemo kamanda mkuu Michael...wakaona vitu vimevurugika huku matone ya damu yakiwa yamedondoka chini...wakastuka!!! Michael akasema kunatatizo ndani ya msitu huu..akafanya ishara ya kuondoka,,kisha wakatoka nje huku bunduki zao wameziwaeka tayari kwa kupambana. wakasonga mbele....



    ***********************



    Upande mwingine alionekana Makala akiwa bado yupo kule chini ya gari...akatazama pande zote..akaona ukimya umetawala..akaamua kutoka chini ya uvungu wa gari hilo..na kuanza kutimua mbio..wakati anakimbia akatereza na kuanza kuserereka kuelekea chini ya korongo....alijigonga kwenye mawe mpaka akafika chini kabisa ya korongo hilo akajingonga kwenye jiwe upande wa kichwani akapoteza fahamu......

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *********************



    Upande mwingine walionekana watu wanaoishi mstuni...watu hao walikuwa wametoboa masikio yao na kuweka vipande vikubwa vya miti...yakaonekana kuvutika na kuwa marefu...walikuwa wameshikiria mikuki ikiambatana na upinde mishale....watu hao walijulikana kwa jina la jamii ya WAKOLOLO...walikuwa wamevalia ngozi za nyani!!! kufunika sehemu zao za siri...kwenye jamii hiyo..hakuwahi kukanyaga binadamu wa kawaida na akatoka akiwa hai katika ardi hiyo...watu hao waliishi kwa kula matunda na wanyama pori....

    siku ya leo wawionekana vijana shupavu wa jamii hiyo ya WAKOLOLO wenye umri wa kuanzia miaka kumi na minane na kuendelea...wakizipiga hatua kwenda kutafuta kitoweo.....kutokana na ukame mkali..wanyama walilazimika kwenda mbali kutafuta majani mabichi pamoja na maji...hivyo jamii ile walipata vitoweo kwa tabu..walikuwa wakitembea maili nyingi kwenda kutafuta vitoweo..



    ************************



    Upande mwingine alionekana Joshi akizidi kusonga mbele zaidi kuingia ndani kabisa ya msitu huo huku kashikilia upanga wake mrefu...akiwa anatembea akakutana uso kwa uso na mnyama chui..Joshi akapandwa na hasira akakumbuka kapoteza jicho lake kwa kuraruriwa na chui...akarusha upanga wake..ukaenda moja kwa moja mpaka ubavuni mwa chi huyo...chui akalia kwa sauti kali....kutokana na maumivu makali aliyoyapata..akatimua mbio huku upanga huo ukining'inia huku sehemu ya upanga huo ikiwa ndani ya ubavu wa chui huyo...alikimbia lakini hakufika mbali akadondoka chini...Joshi akamfuata,,alipomkaribia akauchomoa upanga huo..akazamisha vidole vyake kwenye jicho moja la chui huyo akalinyofoa jicho...na kulipachika katika lile sehemu iliyokuwa wazi ya jicho lake moja...kisha akachana kipande cha nguo yake akajifunga kichwani kuizungu sehemu ya paji la uso mpaka jichoni...akazipiga hatua na kusonga mbele zaidi.....



    **************************



    upande mwingine alioneka Michael akiwa na wale maaskari saba(7) wakizidi kusonga mbele huku macho yao yakitazama kwa tahadhari kubwa...wakakutana na Fisi wengi kiasi wakiwa wamezunguka wakionekana wanakula....wakawastua wale fisi kwa kuponda jiwe,,,lile eneo ambalo fisi hao walikuwa wamelizunguka,,

    wale fisi wakatimua mbio na kutokomea mstuni...

    Wakastuka kuona maiti ya askari ikiwa haina kichwa ndiyo ilikuwa chakula cha fisi hao....wakasikitika sana pia hofu ikaanza kuwaingia wakaanza kuwa makini zaidi...wakati bado wakiwa wanaitazama maiti hiyo.......kunaupanga ukarushwa kutokea kwenye kichaka..upanga huo ulikwenda moja kwa moja mpaka kifuani mwa askari mmoja.....akapoteza maisha papohapo hata bila kuvuta pumzi.....

    wale maaskari wengine sita wakatimua mbio wakamuacha Michael akiwa kasimama..



    *****************



    Upande mwingine,,alionekana Makala...akiwa bado yupo pale chini alipodondoka na kupoteza fahamu......yale matukio ya mauwaji ya wafanyakazi wezake yalizunguka katika ubongo wake!! ghafla akizinduka akapata fahamu,,hakutazama kushoto wala kulia...alinyanyuka na kutimua mbio....akapanda korongo kuelekea upande wa juu..na baada ya nusu saa alifanikiwa kutoka ndani ya korongo hilo....akaanza kutimua mbio....kabla hajafika mbali akakutana uso kwa uso na wale watu jamii ya WAKOLOLO. wakiwa wameshikilia mikuki,,wengine wakiwa na upinde na mishale......

    watu wale wakamtazama Makala kisha wakaanza kuwasiliana kwa lugha yao......wakati huo Makala alibaki kasimama akitafakari nini cha kufanya...mara ghafla watu wale wakaanza kumfuata huku wakipiga lele na kuongea lugha yao.......Makala akaingiwa na hofu kubwa akaanza kutimua mbio ghafla akajikwaa na kudondoka chini...........





    akanyanyuka haraka akaendelea kutimua mbio....

    akaonekana mtu mmoja wa jamii ya WAKOLOLO..akiweka mshale kwenye upinde..akauvuta...ghafla ikasikika sauti ya mkuu wa vijana hao akiongea kwa lugha yao,,akimaanisha,,"Muache hawezi kukimbia na kufika mbali...wengine piteni upande huu,,na wengine piteni upande mwingine...mumzunguke...

    lile kundi la vijana wa jamii ya wakololo wakatii amri ya mkuu wao,,wakatimua mbio huku kila mmoja akipita njia yake....kwenda kumnasa Makala..



    *******************



    upande mwingine,,kule alipokuwa amesimama kamanda Michael...alistshajabu kumuona Joshi akija upande wake huku akizipiga hatua za kikakamavu...Michael akaanza kumshamburia kwa kufyatua risasi kuelekea upende ambao joshi alikuwepo!! akashangaa risasi zilingia kwenye mwili wa Joshi lakini bado akaendelea kumfuata..

    Michael akaona mambo yamekuwa magumu akaamua kutimua mbio na kutokomea mstuni..

    Joshi akaendelea kuzipiga hatua mpaka pale alipokuwepo yule askari aliyechomwa na upanga..

    alipomkaribia akachumua ule upanga...kwenye mwili wa askari huyo...

    akazipiga hatua kwenda kumnasa Michael pamoja na wale maaskari waliokuwa wamekimbia na kutokomea mstuni humo.....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***********************



    wakati huo huo walionekana wale maaskari wakiendelea kutimua mbio ili kunusuru uhai wao..

    wakaona kichaka kikubwa kilichozungukwa na miti mingi iliyo ota kwa karibukaribu...wakaamua kuingia ndani ya kichaka hicho na kujificha...



    Upande mwingine alionekana Kamanda Michael akititua mbio....akaamua kupanda juu ya mti akatazama huku na kule huenda akaona njia ya kutoka ndani ya msitu huo.....alipotazama kwa mbali aliliona lile gari walilokuja nalo mstuni humo..akakumbuka kuwa,,ndani ya gari hilo walibeba silaha nzito za kivita....akashuka haraka kutoka juu ya mti akatimua mbio kulifuata gari hilo....baada ya dakika kadhaa alifanikiwa kulifikia gari hilo akafungua mlango akachukua silaha maalumu kwa kutungulia ndenge angani...ROCKET RANGER(RPG) akaweka kombora moja ndani yake pia akabeba kombora jingine akaliweka ndani ya begi..

    wakati huo alionekana Joshi akija upande huo huo...safari hii Joshi aliongeza kasi ya kutembea....



    *******************



    upande mwingine alionekana Makala akiendelea kutimua mbio.....ghafla wale wakololo wakajitokeza mbele yake wakamuweka katikati yao......Makala akapagawa.....akajiuliza nini cha kufanya...

    akaonekana yule mkuu wa vijana hao..akizioiga hatua kumfuata makala,,,lipomkaribia akaongea lugha ya Kikololo,,,Makala aliweza kuelewa baadhi ya maneno yaliyotamkwa..kwa sababu Makala alikuwa akisoma vitabu kudadisi na kutaka kujua makabila pamoja na jadi zao....akajibu kwa kuongea Lugha yao!!! yule mkuu wa vijana hao wa wakololo akastuka akamtazama Makala kwa macho ya msisitizo....akanyoosha mkono wake juu akiwafanyia ishara wenzake,,wasimdhuru Makala...wale wakololo wengine wakastahajabu....lakini hawakuwa na budi kutii amri ya mkuu wao....wakamchukua Makala kumpeleka kwenye kijiji cha Wakololo.....Makala akaanza kuingiwa na imani kiasi...akajipa moyo kuwa yupo katika mikono salamaa.....wakololo

    walipofika kwenye kijiji chao wakampeleka Makala moja kwa moja mpaka kwa MTEMI wa jamii hiyo..

    yule mkuu wa vijana akaanza kuongea na Mtemi kwa lugha yao....mtemi akanyanyuka nakumtazama Makala kwa umakini huku akimzunguka..........akaamuru Makala apelekwe kwenye nyumba iliyotengenezwa kwa miti awekwe humo.....



    ************************



    upande mwingine alionekana Michael akizipiga hatua za tahadhari...kumuwinda Joshi huku akiwa amebeba begani ile silaha maalumu ya kutungulia ndege(RPG) alimuwinda Joshi lakini hakufanikiwa kumpata....hatimae usiku ukaingia....



    upande mwingine walionekana wale maaskari sita waliobaki hai miongoni mwa wale maaskari saba aliokujanoa Michael....maaskari hao waliendelea kujificha ndani ya kichaka hicho tangu mchana....



    **************************



    Upande mwingine,,kule kwenye kijiji cha Wakololo alionekana Makala ameketi kwenye ngozi ya simba,,iliyokaushwa ndani ya ile nyumba iliyotengenezwa kwa miti...

    kwa mbali alionekana mwanamke mmoja akizipiga hatua,,huku akiangaza angaza macho yake huku na kule...

    mwanamke huyo aitwae,,,VIDA kumbe ni bimti wa pekee wa MTEMI wa Wakololo,,,,mwanamke huyo aliinekana kuvutiwa kimapenzi na Makala Tangu alipomuona mchana akiletwa na vijana wa jamii hiyo ya wakololo....

    mwanamke huyo alizipiga hatua akafungua mlango wa nyumba aliyokuwemo Makala...

    Makala akastuka kumuona mwanamke ameingia ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa na vyumba viwili..vilivyotenganishw.....Vida alikuwa kavalia ngozi ya nyani iliyokuwa imefunika sehemu zake za siri huku makalio yakiwa wazi pamoja na matiti..akamsogelea Makala...



    wakati huohuo alionekana Mtemi akiwaamuru walinzi wake wa karibu wakamuite Vida anamaingezi nae.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wale walinzi walipoingia chumbani kwa Vida hawakumkuta,,wakamtafuta kila kona..hawakufanikiwa kumuona vida.. wakarudi kwa Mtemi kutoa taarifa kuwa Vida hayupo..Mtemi akastuka akahisi huenda binti yake hayupo katika sehemu salama!!! akaamuru vijana wote wamtafute Vida usiku huohuo..na popote watakapomkuta...wahakikishe wanamrudisha haraka iwezekanavyo.....akasema,,"mtu yeyote atakayekutwa na binti yake...akamatwe...na kunyongwa hadharani.....

    msako ukaanza..........



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog