Search This Blog

JICHO LA TATU - 1

 







    IMEANDIKWA NA : YOZZ PIANO MAYA



    *********************************************************************************





    Simulizi : Jicho La Tatu

    Sehemu Ya Kwanza (1)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hahahahahaha mimi sidanganyi nakwambia ukweli kabisa...unajua usiku wa jana sijalala kabisa..niliota ndoto..ikawa inajirudia rudi kama mara tatu hivi..

    Sauti hiyo ilisikika ikitokea ndani ya chumba katika nyumba ya Kijana aitwae MAKALA..alikuwa akimsimulia mkewe kuhusu ndoto ya kutisha aliyoiota usiku wa jana.....mke wa Makala alifahamika kwa jina la NOREGA...

    Makala akasema,,"kama umemaliza kufunga nywele zako zima taa tulale,sasahivi ni saa sita kasorobo...Norega akafanya kama alivyoagizwa na mumewe..akazipiga hatua kadhaa kuifuata swichi iliyokuwa ukutani karibu na mlango wa kuingilia chumbani humo...akazima taa akapanda kitandani wakaanza kuutafuta usingizi....



    ***************

    Upande mwingine ilionekana Nyumba moja ikiwa imejitenga peke yake....jirani wa karibu na nyumba hiyo alikuwa umbali mrefu kama kilomita sita hivi kutoka kwenye nyumba hiyo iliyojitenga peke yake alionekana mwanaume mmoja wa makamo akichimba shimo usiku huhuo wa saa sita. nje ya nyumba hiyo....mwanaume huyo alifahamika kwa jina la JOSHI....aliendelea kuchimba shimo takribani kama masaa mawili mfululizo....aliopohakikisha kachimba shimo lenye urefu aliokuwa amekusudia,,akatoka ndani ya shimo hilo na kuzipiga hatua kuingia ndani kwake......na baada ya dakika tatu hivi...akatoka huku amebeba maiti ya binadamu...akazipiga hatua kulifuata lile shimo alilolichimba akadumbukiza maiti hiyo ndani ya shimo,,akaanza kufukia kwa kutumia koleo....

    ilipofika saa kumi za usiku,,alimaliza kufukia shimo hilo...kisha akamwaga mbegu za za mchicha..ili paonekane kama ni bustani ya mbogamboga.....



    kisha akaingia ndani ya nyumba yake..akafunga mlango...ndani ya nyumba hiyo palionekana kutisha kutokana na makorokoro kuwa mengi yamewekwa bila mpangilio...nyumba hiyo ni kubwa sana ilikuwa na vyumba Tisa...akazipiga hatua akaingia kwenye chumba kimojawapo..akawasha taa...kikaonekana kiti cha mbao kikiwa na kamba...pia chumba hicho kilijaa zana kutisha..... alizitumia katika shughuri zake ambazo hazifahamiki mpaka muda huu...Joshi hakuwahi kuwa na rafiki tangu utotowake mpaka uri huo alionao sasa....ni baada ya wazazi wake kuuwawa na mtu asiyejulikana...wazazi wa Joshi waliuwawa akiwa na umri wa miaka saba..alishuhudia mauwaji hayo..akiwa amejificha chini ya meza iliyokuwa sebuleni...

    yule mtu katiri aliyefanya mauwaji hayo...alipokuwa anatoka nje ya nyumba ya kina Joshi...akatereza kwenye vigae kutokana alikuwa amekanyaga Damu zilizokuwa zimetapakaa chini akadondoka na kuangukia kisogo akupoteza fahamu....Joshi alipo ona muuwaji huyo kadondoka,,akajua amekufa...akaatoka pale alipokuwa amejificha chini ya meza akaanza kulia huku akitazama maiti ua Baba yake pamoja na Mama yake...waliuwawa kwa kuchinjwa shingo na kukatwakatwa mapanga mwili mzima...CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Joshi akazipiga hatua kwa hofu kubwa..akamsogelea yule muuwaji....akamtazama usoni akaina kovu kubwa la mda mrefu lililokuwa kwenye shavu la kushoto mwa muuwaji huyo...akahisi kuwa amekufa....akazipiga hatua akarudi ndani.....baada ya sekunde kadhaa..muuwaji alizinduka akapata fahamu..Joshi alipomuona ananyanyuka akajificha haraka,,chini ua meza....yule muuwaji akajishika kisogo huku akiugulia maumivu...akazipiga hatua na kuondoka zake,akatokomea kusikojulikana....



    ****************



    Joshi alijificha hapo masaa mengi kiasi...alipo ona kuna hali ya itulivu akatoka chini ya meza,,akakumbuka baba yake alimfundisha kuwa endapo akiona kunahatari..au siku nyumba ikiwaka moto alafu wazazi wake hawapo nyumbani basi apigege simu ya mezani kwenda namba 112..kisha ataje namba ya nyumba yao ambayo ni S/0043......joshi alikariri maneno hayo ya baba yake sikunyingi....

    akachukua simu ya mama yake haraka,,akapiga namba hizo za Dharura 112..simu ikapokelewa kwenye kituo cha polisi..Joshi akaelezea tukio zima,,pia akatoa anuani ya nyumba..baada ya dakika kadhaa maaskari walikuja mpaka kwenye nyumba hiyo....wakachukua maiti zile mbili na kuzipeleka mochwari...kutokana zilikuwa zinamajeraha makubwa ya kukatwa na mapanga..ililazimika wazikwe siku hiyo hiyo ili maiti hizo zisiharibike na kutoa harufu....

    taratibu za mazishi zikafanyika...wakazika...

    Shangazi wa Joshi ambaue ni mdogo wa mwisho wa baba yake Joshi..alichukua jukumu la kuishi na kumlea Joshi katika nyumba hiyo....Jishi aliendelea kukua kadri miaka ilivyozidi kwenda..

    alipotimiza umri wa miaka ishirini na tatu....shangazi yake ambaye alikuwa mlezi wake alifariki dunia.....

    kutokana alikuwa tayari kafikisha umri wa kujitegemea Joshi aliamua kuishi mwenyewe ndani ya nyumba hiyo.....akiwa peke yake..



    ********BAADA YA MIAKA TISA KUPITA********



    Joshi alitimiza umri wa miaka therathini na mbili(32)alikuwa anafanya kazi ya kupasua kuni anazikusanya..zikiwa nyingi anaziuza kwa pamoja....siku moja akiwa mjini kwenye matembezi alimuona mtu..akamfananisha..mtu huyo alionekana kuwa mzee kiasi..

    Joshi akamsogelea mzee huyo akamtazama kwa makini..akaona lile kovu shavuni mwa mzee huyo.

    akakumbuka kuwa huyu ndiye muuwaji aliyewauwa wazazi wake..akaamua kumfatilia mzee huyo mpaka anapokwenda..akagundua nyumba anayoisgi mzee huyo....akamteka na kumpeleka nyumbani kwake..kwenye ile nyumba waliyokuwa wakiishi wazaziwake..yule mzee alistuka kuona anapelekwa kwenye nyumba hiyo..akakumbuka kuwa miaka 25 iliyopita,,alifanya mauwaji kwenye nyumba hiyo...aliamua kumuuwa baba Joshi pamoja na mkewe....kwa sabavu walikuwa wanamdai pesa nyingi baada ya kuuziwa nyumba na baba yake Joshi...aliwauwa ili asilipe deni hilo...

    Joshi akamtesa mzee huyo kwa mateso makali sana mpaka akafa...

    kumbe ile maiti aliyoizika Joshi ilikuwa ni maiti ya mzee huyo aliyewauwa wazazi wa Joshi..



    ********BAADA YA MWAKA MMOJA KUPITA*****



    Mzimu wa mzee huyo ukafufuka na kuanza kufanya mauwaji ya kikatiri na yenye kutisha..

    Siku moja majira ya usiku wa saa saba..ule mzimu ulionekana ukifufuka kutoka kwenye ile bustani ya mbogamboga alizozipanda Joshi....





    mzimu huo ukanyanyuka na kuzipiga hatua..mpaka kwenye mlango wa nyumba ya Joshi...ukaingia ndani...wakati huo Joshi alikuwa amelala...ghafla akaota ndoto kuwa yule mzee muuwaji..aliyewauwa wazazi wake,,amefufuka na kumfuata huku ameshikilia upanga mrefu uliokuwa na mpini mrefu kama wa jembe la kulimia......Joshi akastuka kutoka usingizini..akakurupuka kitandani..akawasha taa..akachungulia dirishani kutazana kule nje alipomzika yule mzee na kupanda bustani ya mbogamboga....ili aone kama pamefukuliwa...lakini hakuweza kuona vizuri kutokana na giza totoro kutanda upande wa nje...akazipiga hatua akafungua mlango na kutoka nje...akaelekea kwenye ile bustani ya mbogamboga...alipofika..hakuona kitu chochote zaidi ya mbogamboga..zikiwa vilevile kama anavyoziona kila siku.....akaamua kurudi ndani..akafunga mlango na kuufuata mlango wa chumbani kwake..alipoufungua alistuka sana kumuona yule mzee aliyemzika..yumo ndani ya chumba chake!!!macho yakamtoka Joshi,,akajisemea moyoni,,"inamaana ile ndoto niliyotoka kuiota dakika chache zilizopita ilikuwa ni ya kweli!!!?.....Joshi alibaki amesimama kama sanamu akistahajabu....wakati huo akili zilikuwa zimemruka....

    alipotahamaki...akataka kutimua mbio....mzimu wa yule babu ukamvaa ukaingia ndani ya kiwiliwili cha Joshi....

    ni kitendo cha sekunde,,akili ya Joshi ikaanza kubadilika,,akaingiwa na Roho ya ukatiri wa hali ya juu!!!..akili ya Joshi ikawa inaongozwa na ule mzimu.....akazipiga hatua za kikakamavu..huku uso wake ukionekana kuwa na msisitizo wa kufanya jambo fulani....akafungua mlango wa chumba kingine,,alichokitumia kama stoo ya kuhifadhi zana zake za kupasulia kuni,,,akachukua nyundo kubwa..akaitazama kwa umakini..akairudisha,,akachukua,,shoka akazipiga hatua kadhaa..akasita.akarudi akaiweka chini shoka hiyo...akachukua upanga mrefu uliokuwa na mpini mrefu..akaunyanyua upanga huo huku akiutazama kwa hisia kali,,akauramba kwa ulimi wake.......kwa mara ya kwanza Joshi akatabasamu..kwa sekunde mbili kisha akarudi katika uso wa msisitizo wa kutenda jambo fulani,,

    akazipiga hatua na kutoka nje ua nyumba yake huku akiuwacha mlango wazi!!!!

    akazipiga hatua za kikakamavu akatokomea kusikojulikana..........



    ***********************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Asubuhi palipokucha alionekana Makala akiwa nyumbani kwake akijiandaa kwenda kazini...mke wake Norega alimuandalia chai,,Makala alipomaliza kuvaa nguo..akatoka chumbani na kuelekea sebuleni,,akanywa cha haraka haraka huku akiongea na mkewe.....akasema,,"Leo nimechelewa kuamka alafu ile ndoto niliyoiota juzi imejirudia tena....nimeota wafanyakazi wenzangu smwatano wameuwawa kikatiri na mtu aisiyefahamika.....

    Norega akasema,,"hiyo ni ndoto tu mume wangu..

    baada ya dakika kumi Makala alimaliza kunywa chai,,akamuaga mkewe kwa kumbusu shavuni..akatoka nje na kuingia ndani ya gari lake..akaliwasha..na kuianza safari ya kuelekea kazini......

    Makala alikuwa anafanya kazi katika shirika la kiserikari la HIFADHI YA MISITU NA UWOTO WA ASILI...

    Alipofika kazini..akaingia moja kwa moja mpaka ndani ya ofisi yake...baada ya dakika tatu kupita..alikuja sekretari wake akamletea barua ikitokea MAKAO MAKUU...alipoifungua barua hiyo,,ilikuwa ikisema kuwa,,siku ya leo anatakiwa aende kwenye msitu UNGEBO uliopo ndani ya Mbuga ya wanyama ya SAADANI iliyopo hapahapa jijini dar es salaam....

    safari hiyo ilikuwa ni ya kwenda kuchunguza mmea unaosadikika kuota ndani ya msitu huo..matawi ya mmea huo yalikuwa ni sumu...ilibainika baada ya kukutwa baadhi ya wanyama wamekufa na walipofanyiwa uchunguzi ikajulikana kuwa wamekula matawi ya mmea huo usiojulikana.....

    Makala akaamuru wafanyakazi watano aongozane nao kuelekea kwenye msitu UNGEBO..



    ********************



    upande mwingine alionekana joshi,,akiwa barabarani akizipiga hatua za kikakamavu huku lile panga lake refu likiwa limetapakaa Damu iliyoganda.....kwa mbali akaona nyumba,,akaamua kuifuata nyumba hiyo,,akaingia ndani bila kupiga hodi...akamkuta bibi kizee hajiwezi..akiwa amelala ndani ya nyumba hiyo...Joshi akamchinja na kuondoka zake....akasonga mbele zaidi,akatokezea kwenye pori,akasita kutembea akaangaza angaza macho yake huku na kule,,akatabasamu kwa mara ya pili,, akazipiga hatua kuingia ndani ya pori hilo...akasonga mbele zaidi,,akatokezea kwenye msitu UNGEBO akaonekana kufurahia mazingira ya msitu huo..akatabasamu mara ya tatu....



    ************************



    Upande mwingine kule kazini kwa Makala alionekana akiingia ndani ua gari..yeye pamoja na wafanyakazi watano..jumla wakawa sita...akaliwasha gari na safari ya kuelekea Msitu UNGEBO ikaanza.....

    baada ya lisaa limoja walifika kwenye mbuga ya wamyama ya SAADANI..wakasonga mbele zaidi na kuingia ndani kabisa ya mbuga hiyo.....Makala alizidi kuzipanga gia hatimae wakatokezea kwenye msitu UNGEBO,,wakaingia ndani ya kabisa katikati ya msitu huo....Makala akalisimamisha gari..kisha wakashuka kutoka ndani ya gari...wakachukua vifaa vya kufanyia utafiti wa mimea...wakajigawa katika makundi mawili...Makala na wafanyakazi wawili wakaelekea upande mwingine..

    na wale wafanyakazi watatu wakaelekea upande mwingine..ili kazi iwe rahisi kuliko kuwa eneo moja wote sita.......

    kazi ikaanza wakazipiga hatua kuingia ndani zaidi ya msitu huo......wakati Makala na wenzake wawili wakiendelea kuutafuta mmea huo...Makala akastuka,,akasita kutembea...akasema,,"tazama kule!! wale wenzake wawili walipotazama wakaona mtu kalala chini akiwa amekatwa shingo.....wakaisogelea maiti ile..Makala akasema,,"mtu huyu kauwawa muda mchache uliopita si unaona damu bado mbichi!!!!?

    wakaanza kuingiwa na hofu wakaamua kutimua mbio kurudi kule lilipokuwepo gari walilokujanalo.....

    walipofika eneo hilo..wakastahajabu kutokulikuta gari lao....hofu ikaongezeka..wakaanza kutimua mbio bila kujua ni wapi wanaelekea.......mara ghafla Makala akawazuia wenzake wasiendelee kukimbia akawavuta mpaka kwenye kichaka akawafanyia ishara kwamba wakae kimya,,kisha akasema kwa sauti ya chini chini,,""TAZAMA KULE...walipotazama wakastuka..wakataka kutimua mbio..Makala akawazuia......





    Akasema,,"msijaribu kupiga kelele,mkifanya hivyo tumekwisha,,huyu mtu anaonekana hana nia nzuri....

    Joshi akazipiga hatua kuelekea upande mwingine.huku kashikilia upanga mrefu....Makala alipo ona Joshi kaondoka eneo hilo...akasema,,"tukimbieni...kabla hajamaliza kuongea hivyo...wale wenzake watatu,wakaanza kutimua mbio,,,walikimbia bila kujua ni wapi wanaelekea....



    ******************



    upande mwingine walionekana wale wafanyakazi watatu..wakiendelea kufanya utafiti...wenyewe hawakuweza kufahamu chochote kwa sababu hawakuona ile maiti..wala hawakumuona Joshi...

    waliendelea kufanya utafiti upande huo,,,lakini kila mmoja alipita njia yake...

    akaonekana Joshi akizipiga hatua, akakutana uso kwa uso na mmoja kati ya wafanyakazi hao.....yule mfanyakazi hakujali akaendelea kufanya utafiti,,kwa kuweka kile kipimo maalu cha kuchunguza mimea.....hakujua kuwa kwa sasa Joshi hakuwa katika akili uake ya kawaida,, akamsalimia Joshi,,"habari yako

    Joshi hakujibu kitu,akabaki amesimama kikakamavu..yule mfanyakazi alipo ona Joshi hajibu salamu yake akaamua kuendelea na utafiti...akastuka kumuona Joshi akizipiga hatua kumfuata,,,alipotahamaki Joshi alikuwa amemkaribia jirani kabisa...akamfyeka shingo kwa kutumia ule upanga mrefu...kichwa kikaruka kando..damu zikaruka...mfanyakazi huyo akatapatapa na kudondoka chini akafa papohapo.

    Joshi akazipiga hatua kadhaa akamuona mfanyakazi mwingine....akamfuata na kumfyeka shingo....yule mfanyakazi aliyebaki kati ya wale watatu..aliona kitendo hicho cha mauwaji ya kikatiri alichofanyiwa mwenzake.....akaamua kutupa kile kifaa cha kufanyia utafiti akatimua mbio....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ************************



    upande mwingine alionekana Makala pamoja na wenzake wawili wakitimua mbio itadhani wanashindana mbio kwenye mashindano ya mbio za mita mia.....walikimbia wakajikuta wametokeze..ule upande ambao wale wenzao watatu walikuwepo huko...wakastuka kukuta maiti ya mfanyakazi mwenzao ikiwa haina kichwa..wakaingiwa na hofu..wakatimua mbio,,ghafla Makala akajikwa akadondoka chini,,kumbe hapo alipoangukia..ilikuwepo maiti ya yule mfanyakazi wa pili....Makala akaogopa sana.akanyanyuka na kuendelea kutimua mbio...

    sasa hivi hakuwaona wenzake walikuwa wameshatokomea mstuni humo,,,walimuacha hatua nyingi kiasi wakati yeye alijikwa na kudondoka...wenyewe waliendelea kusonga mbele.....



    *********************



    upande mwingine, alionekana yule mfanyakazi mmoja aliyeshuhudia mwenzake akichinjwa kikatiri...akikimbia bila uelekeo...huku akiangaza angaza macho yake huku na kule.....akasikia matawi yakitoa mlio kama kunamtu anakimbia kumfatilia akageuka nyuma huku akikimbia kwa kasi ya ajabu,,,huenda Joshi anamkimbiza kwa nyuma....lakini hakuona kitu chochote zaidi ya miti....alipogeuka kutazama mbele anakoelekea ghafla akajikuta kajichomeka kwenye mti uliokuwa umechongoka,,ukatoboa tumbo na kutokezea mgongoni..akafa papohapo....wakabaki watu watatu.Makala pamoja na wenzake wawili



    **********************



    upande mwingine walionekana wale wawili wakitimua mbio,,,walitamani watoke ndani ya msitu huo lakini ni kilomita nyingi kutoka mstuni mpaka kuifikia barabara kuu....wakati wanakimbia wakaamua kuingia kwenye kichaka kwa lengo la kujificha,,

    mmoja wao akagusa mzinga wa nyuki..akautingisha nyuki wakatoka na kuanza kuwashambulia,,wakakurupuka kichakani humo na kukimbia huku wakipiga mayowe ya kelele za maumivu....

    kelele hizo zilimfanya Joshi,agundue ni wapi walipo akazipiga hatua kuzifuata kelele hizo....wakakutana uso kwa uso...wakabaki wamesimama huku nyuso zao zimevimba manundu manundu..kwa sababu wameumwa na nyuki...wakati wanatahamaki..Joshi akawafuata..wakaanza kutimua mbio kurudi walipotoka....Joshi akarusha upanga..kama mtu anayerusha mkuki...upanga huo ulikwenda moja kwa moja mpaka mgongoni mwa mfanyakazi mmoja..akadondoka chini...yule mfanyakazi mwingine alipo ona mwenzake kanaswa akaongeza kasi ya kukimbia...

    Joshi akazipiga hatua za haraka haraka,,mpaka pale alipokuwa amedondoka yule mfanyakazi..akauchomoa upanga wake...kutoka mgongoni mwa mfanyakazi huyo..kisha akamchinja.....na kuondoka zake..



    ***********************



    upande mwingine alionekana Makala akiendelea kutimua mbio huku macho yamemtoka..akaamua kupanda juu ya mti,,ili kujificha kwa usalama zaidi.

    alipofika juu ya mti...akatazama upande wa chini,,akastuka kumuona Joshi akizipiga hatua kuja upande huo!!! akakumbatia mti huku akitetemeka kwa hofu...Joshi alipoukaribia mti huo..akasita kutembea akaangaza angazaacho yake huku na kule,,hakuona mtu.....akakasirika sana,,,akajiuliza,,mtu huyu kakimbilia wapi???

    wakati huo mapigo ya moyo ya Makala yalikuwa yakipiga kwa kasi,,huku akipumua kwa kubana pumzi ili Joshi asisikie sauti ya Muhemo...

    Makala akahisi kadondokewa na tone la maji..akainua shingo yakeili atazama ni nini hicho kimemdondokea begani..akastuka kumuona CHUI akiwa kwenye mti huo hou....alipotazama upande wa chini ili ajirushe..akaina bado Joshi kasimama

    wala hana dalili ya kuondoka hapo alipo...





    akafumba macho akajikaza kiume huku akimuomba Mungu....amnusuru na majanga hayo.

    yule mnyama Chui akaona Damu kwenye ule upanga wa Joshi...na kwa jinsi Joshi alivyokuwa ametapakaa Damu kwenye nguo zake...Chui huyo akajitosa kwa kuruka kutoka juu ya mti akatua kichwani mwa Joshi...kutokana na uzito wa chui huyo...Joshi alidondoka chini....

    Makala,,akaweza kupata upenyo wa kujirusha kutoka juu ya mti mpaka chini akaanza kutimua mbio na kutokomea mstuni,,bila kujua ni wapi anakoelekea........

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Joshi akaanza kupambana na Chui..akafanikiwa kuchoma na upanda tumboni,, utumbi ukamwagika..chui akatapatapa mpaka akafa....Joshi akanyanyuka,,lakini uso wake ulikuwa umejeruhiwa vibaya kwa makucha ya chui yule.....ngozi ya usoni ikabanduka yote..na kubaki nyama ya ndani ya ngozi..huku akitokwa na damu..

    Joshi alihisi maumivu makali sana...akapiga kelele huku amenyanyua upanga wake juu....kwa hasira...



    *******************



    upande mwingine alionekana yele mfanyakazi mmoja kati ya wale wawili waliokuwa na Makala,

    alitimua mbio bila kugeuka nyuma....akatokezea kwenye sehemu yenye majani marefu kiasi,..akaona simba watatu wakiwa wamejilaza,,,Simba hao walionekana kuwa na njaa kali....

    Yule mfanyakazi akasita kukimbia,,,hofu ikazidi kuongezeka,,akaamua kirudi alipotoka kule ndani ya msitu...alikimbia kwa kasi zaidi kabla Simba hawajamuona........akatokezea ile sehemu alipouwawa yule chui.....akastuka akasimama ghafl,,,kutokana alikuwa anakimbia kwa kasi na kile kitendo cha kisimama ghafla..akadondoka chini na kuserereka mpaka pale alipokuwepo chui yule aliye uwawa.....akanyanyuka haraka huku akimtazama yule chui kwa mshangao....

    wakati huohuo wakaonekana maaskari wa kulinda wanyama pori..wakija upande huohuo....wakamuona yule mfanyakazi akiwa kasimama anamtazama chui huyo....maaskari walipo ona chui ameuwawa,,wakahisi kuwa mfanyakazi huyo ndiye aliyuuwa chui huyo kwa lengo la kumchuna ngizi,,,

    mmoja kati ya maaskari hao,akapaza sauti,,"TULIA HIVYO HIVYO HAPO ULIPO..

    yule mfanyakazi akaamua kutimua mbio bila kutazama ni nani anayesema maneno hayo....wale maaskari..wakaamua kufatua risasi wakijua kuwa mtu huyo ni jangiri...risasi moja ilimpata kichwani yule mfanyakazi akapoteza maisha papohapo..



    **********************



    Upande mwingine alionekana,,Makala akiendelea kutimua mbio,,kwa mbali akaona kuna HEMA limetengenezwa kama nyumba...akaamua kulifuata ili kuomba msaada...alipofika akaita kwa kusema,,"Hodi jamani...hakuona dalili yoyote ya mtu kutoka nje....akazipiga hatua kuusogelea mlango wa kuingilia ulikuwa wazi...mlango huo ulikuwa wa kufunga kwa zipu....akaingia ndani ya hema hilo.....hakukuta mtu,,akaangaza angaza macho akaona kuna kofia ya askari wa kulinda wanyama pori.....akagundua kuwa hema hilo ni kwa ni maalumu kwa ajili ya maaskari wa porini..

    akaamua kujihifadhi humo,,kwa usalama wa maisha yake....



    ************************



    upande mwingine,,walionekana wale maaskari pori,wakachukua kamba wakamfunga miguu ya mbele na ya nyuma....wakapitisha mti mrefu kiasi kati ya miguu ya mbe pamoja na miguu ya nyuma...wakimbeba yule chui wakaanza safari yakuelekea kule kwenye hema.....

    wakiwa njiani kuelekea huko.....wakakutana uso kwa uso na Joshi,,wakastuka kumuona mtu akiwa hana ngozi usoni,,huku ameshikilia upanga mrefu ukiwa umetapakaa damu...

    wakasita kutembea,,mmoja kati ya maaskari hao akauliza,,"umepatwa na nini?? mbona umeumia kiasi hicho?

    Joshi hakujibu kitu akabaki kimya,huku akiwatazama maaskari wale...sura yake ilionekana kutisha sana.....akazipiga hatua kuwafuata,,akanyanyua upanga wake juu...

    wale maaskari wakadhani Joshi anafanya mzaha..

    na walipo ona haongei kitu...wakaamua kuendelea na safari yao...ghafla wakaona damu inaruka na kuwamwagikia,,,wakageuka nyuma haraka.....wakaona mwenzao anadondoka chini huku chingo yake ikiwa haina kichwa....wakamtupa chui waliokuwa wamembeba...wakaweka sawa.. bunduki zao,,, tayari kwa kumshambulia Joshi..kabla hawajaanza kifyatua risasi..Joshi akanyanyua upanga na kufyeka shingo ya askari mwingine.....kichwa kikaruka kando akafa papohapo......wakaanza kufyatua risasi mfululizo kuelekea kwenye mwili wa Joshi risasi ziliingia mwilini kwa joshi,..lakiniJoshi akawa anazitema risasi hizo kwa kupitia mdomoni mwake zikawa zinadondoka chini..wale maaskari wawili waliokuwa wanafyatua risasihizo..wakaona huyo sio binadamu wa kawaida wakaamua kutupa bunduki zao wakatimua mbio,,kila mmoja akapita njia yake.....



    Joshi hakuwakimbiza akazipiga hatua kusonga mbele hukohuko walipoelekea maaskari hao...baada ya kutembea hatua kadhaa akasita kuendelea kutembea katazama huku na kule...akaamua kupita upande mwingine ili awanase kwa urahisi.....

    baada ya muda wa dakika kumi kupita...akakutana uso kwa uso na mmoja kati ya wale maaskari wawili waliokuwa wakikimbia.....akamkamata akamchoma na upanga kwenye jicho..upanga huo ukatokezea kisogoni,,,kisha akauchomoa upanga huo kwa kuuvuta...askari huyo akadondoka chini na kupoteza maisha....CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Joshi akazipiga hatua kadhaa akaangaza angaza macho huku na kule..akamuona yule askari mwingine akiwa anajinasua kwenye kichaka kilichokuwa na miba..aliingia kwenye kichaka hicho bila kujua kuwa kilikuwa na miba mirefu...

    wakati akiendelea kujinasua...Joshi akamkaribia na kumfyeka kichwa kikaruka kando...akabaki kasimama kama sanamu..huku akiwa bado kanasa kwenye kichaka hicho chenye miba...

    Joshi akatoka eneo hilo akasonga mbele zaidi....kwa mbali akaona kuna hema lililotengenezwa kama nyumba..akaamua kulifuata hema hilo.....



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog