Search This Blog

MWANAFUNZI MCHAWI - 1

 





    IMEANDIKWA NA : ENEA FAIDY



    *********************************************************************************



    Simulizi : Mwanafunzi Mchawi

    Sehemu Ya Kwanza (1)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni majira ya saa moja jioni ambapo mkuu wa while ya Mabango alikuwa ofisini kwake akiwa amechanganyikiwa sana kwani hali ya shule hiyo ilizidi kutisha sana hasa baada ya kutokea kwa vifo vya wanafunzi kumi na tano mfululizo ndani ya wiki moja tu. Tena vifo vya ghafla tu.



    Mkuu wa shule mama Dayana Mbeshi alikuwa kwenye wakati mgumu sana kubaini chanzo cha tatizo lakini bado hakupata majibu.Mara ghafla mlango wa ofisi ukagongwa, akaingia mwalimu wa malezi wa shule hiyo akiwa na USO wa huzuni sana hali iliyomshtua sana mkuu wa shule



    "vipi kulikoni?"

    "hali mbaya mkuu.. wanafunzi wawili wamefariki tena bwenini" mwalimu wa malezi alizungumza kwa huzuni iliyochanganyika na hofu.

    "what? mmh! sio bure.. kuna kitu hapa..!" alisikika mwalimu Mbeshi huku akiinamisha kichwa chake chini na kukiegemeza kwenye kiganja chake.



    ******

    Wanafunzi wengi walionekana kuwa na hofu sana baada ya vifo visivotarajiwa kuzidi kutokea katika shule yao. Kila MTU aliwaza sana juu ya vifo vile huku kila mmoja akihisi zamu yake IPO karibu. Nyuso za huzuni ndizo zilizotawala kwa wanafunzi wote si wa kike wala wa kiume. Hakuna aliyetamani kulala wala kukaa mbali na kundi la watu kwani hofu iliwajaa mioyoni mwao, hawakuweza hata kusoma.



    Lakini hali ilikuwa tofauti sana kwa binti Doreen ambaye alikuwa na wiki tu toka ahamie shuleni hapo. Alionekana kutoogopa chochote wala kuguswa na misiba ya wanafunzi wenzake. Kila Mara alionekana akiwa na furaha, hali hii iliwatisha wanafunzi wenzake na kuwafanya wawe na maswali mengi juu yake.



    Doreen alikuwa msichana mrembo, sura yake nyembamba iliyopambwa na macho makubwa legevu, kope ndefu nyeusi tii, pua nyembamba iliyochongoka vyema na midomo mizuri yenye mvuto wa aina yake vilimfanya awe tishio kila kona kwani alikuwa ni mzuri kupindukia lakini Tabia ilikuwa tofauti na uzuri wake.



    Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke take nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na Giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....



    DOREEN aliendelea kuongea maneno aliyoyajua mwenyewe akiwa bado yupo uchi wa mnyama nyuma ya bweni alilokuwa anaishi.



    Ghafla kipande kidogo cha karatasi nyeupe kikashuka mikononi mwake bila kuonekana kilikotokea. Doreen alicheka kwa sauti Kali ya kutisha sana kisha akalikazia macho karatasi lile, matone ya damu yaliangukia kwenye karatasi lile kutoka kwenye macho yaliyotisha sana ya Doreen kwani yalikuwa na rangi nyeusi halafu yakawa na umbile kama macho ya paka.



    "Nenda mpaka ofisi ya mkuu wa shule ukamalize kazi." alisema Doreen akiwa amelinyanyua karatasi like kwa mkono wake wa kushoto. Karatasi likatoweka mkononi mwake na kupepea kwa nguvu kama vile limerushwa na upepo mkali.



    Doreen alipomaliza kazi hiyo akasimama vizuri kama mwanajeshi aliyejipanga kwaajili ya gwaride kisha akainamisha kichwa chake chini akapotea eneo lile.



    **********

    Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata Mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.



    Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.

    "unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"

    "Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.

    "siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu anayeua wenzake naye IPO Siku yake tu!"

    "Najua baby Ila hali inatisha"

    "Tuzidi kuomba Mungu mpenzi wangu kila unalofanya muombe Mungu."

    "Nakupenda "

    "Nakupenda pia"



    Wakati Eddy na Dorice wakiendelea kuzungumza maneno hayo, Doreen alikuwa nyuma ya mti waliosimama hivyo alisikia kila kitu.



    Roho ilimuuma sana kwani tangu alipohamia shuleni hapo alitokea kumpenda sana Eddy na alitamani awe mpenzi wake kwani ndio chaguo la moyo wake lakini Dorice alikuwa kikwazo. .



    Suala hilo lilimuumiza Doreen ndani kwa ndani. Akainuka pale kwenye mti na kupita katikati yao, akamwita Dorice pembeni.

    "Dorice.. mimi nawahi kulala Ila kesho unione!"

    "nikuone?"

    "ndio kwani hujaelewa?" alijibu Doreen kwa ukali jambo lililomwachia maswali mengi Dorice. Lakini Doreen hakujali kitu akaondoka zake Ila moyoni alipanga jambo zito la kumfanyia Dorice siku ya kesho yake.



    *********

    Ilikuwa asubuhi tulivu sana majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi ambapo mwalimu Dayana Mbeshi aliwahi ofisini kwake kama ilivyokuwa kawaida yake.



    Majengo ya ofisi yalimkaribisha kwa shangwe naye akaitikia ukaribisho huo kwa kufungua ofisi yake kisha akasogeza mapazia ya dirishani ili kuruhusu mwangaza wa jua changa uweze kupenyeza vizuri.



    Baada ya kukamilisha yote hayo Madam Mbeshi akasogeza kiti chake karibu na meza kisha akaketi halafu akaanza kusogeza vitu vilivyokuwepo mezani pale lakini ghafla akakutana na karatasi chafuchafu mezani kwake lakini ilikuwa na maandishi.



    Akashtuka kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri. Mwalimu Mbeshi hakutaka kuamini kile alichokiona, akataharuki kwa hofu na mshangao..



    .Mwalimu Mbeshi aliposoma ujumbe ule kutoka kwenye ile karatasi chafuchafu alizidi kuchanganyikiwa sana, mapigo ya moyo yalimwenda kasi kama gari iliyokata breki ikiwa mlimani. akarudia tena na tena ujumbe ule uliosomeka "POLE SANA MWALIMU KWA MASWAHIBU YALIYOKUKUTA SHULENI KWAKO.. MIMI DOREEN MBWANA NIMEFANYA YOTE HAYO! PIA MUDA WA KIFO CHAKO U KARIBU KWANI UMESOMA UJUMBE WA MWANAFUNZI MCHAWI"



    Jasho jembamba lilimtiririka mwanamama yule bila kuelewa afanye nini. Akataka kulitupa chini karatasi lile lakini ghafla akaona karatasi lile limebadilika ghafla, sio karatasi tena bali kitu kama ngozi ya binadamu iliyooza sana huku ikitoa harufu mbaya ikiwa imeambatana na funza wengi wakitembea tembea.



    Madam Mbeshi alihisi kinyaa sana huku woga ukiwa umemtawala kupita kiasi kwani katika maisha yake hakuwahi kushuhudia mauzauza ya namna ile hats Mara moja. Alitamani akimbie lakini miguu ilikuwa imeganda kama msumari kwenye sumaku.



    Mbeshi alihangaika sana na wale funza mkononi mwake kwani walizidi kumpanda mwilini kwa kasi na kumtia ghasia. Machozi yalimtoka mwalimu mbeshi lakini kila tone lililodondoka lilikuwa damu.



    Hofu ikamzidia sana, hakuwa na tumaini la kusalimika tena kwani kwa hatua aliyofikia ilitisha sana. Na yote hayo yalisababishwa na binti Doreen Mbwana.



    Ghafla mlango wa ofisi ya mwalimu Mbeshi uligongwa lakini Mbeshi hakuwa hata na uwezo wa kuzungumza chochote. Mlango uligongwa sana lakini Mbeshi hakuweza kuufungua ingawa alitamani yule aliyegonga mlango aingie ili iwe ahueni kwake lakini ilishindikana.



    Kila aliponyanyua kinywa ulimi ulikuwa mzito na hakuweza kuzungumza chochote ikambidi atulie kimya akiugulia mateso yake yalimzonga ndani ya muda mfupi tu.



    "Masikini Mimi inamaana ndo nakufa? masikini familia yangu ambayo Mimi ndio tegemezi! ee Mungu nisaidie!" aliwaza Mbeshi huku machozi ya damu yakizidi kutiririka.



    *******

    Walimu hawakujua lolote linaloendelea ofisini kwa mkuu wa shule hivyo waliendelea na ratiba za shule kama kawaida.

    Wanafunzi walienda mstarini, wakajipanga vizuri kwa mistari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha NNE.



    Mwalimu John ambaye alikuwa zamu kwa wiki ile alikuwa amesimama mbele kwaajili ya matangazo lakini ghafla akasikia wanafunzi wachache wakimzomea.



    Moyo wake ukamlipuka akautazama msitu ule wa watu lakini macho yake yakatua moja kwa moja kwa wanafunzi wa kidato cha NNE, akamwona Dorice na nyuma yake alikuwa amesimama Doreen akiwa anacheka sana kwa sauti ya dharau na kiburi. Hasira za mwalimu John zikampanda akaumanisha meno yake kwa ghadhabu



    "Doreen! hebu njoo mbele haraka sana!" alisema mwalimu John kwa sauti kali iliyojaa ghadhabu lakini bila aibu Doreen aliachia sonyo Kali iliyowafanya wanafunzi wote wamgeukie yeye na kumwangalia kwa mshangao.

    "We mtoto! unanisonya Mimi? una adabu kweli?"

    "Kwanini nisikudharau wakati we mwenyewe umejidharau?" alisema Doreen kwa kujiamini sana.

    "Ati nini?"alishangaa mwalim John kwani hakutegemea kama Doreen angekuwa jeuri kiasi kile.

    "We unavokuja kazini hivo unategemea nini?"

    "Vipi" alishtuka Mwalimu John.

    "Unakuja kazini bila kuvaa suruali ili iweje!?"

    "Una wazimu wewe nani hajavaa suruali?"



    "Jiangalie huko chini kama umevaa suruali;" alisema Doreen na kumfanya Mwalimu John ajiangalie vizuri akagundua kweli alikuwa hajavaa suruali.



    Alishtuka kupita kiasi wanafunzi wote wakamtazama Mwalimu John kwa mshangao kwani kweli alikuwa hajavaa suruali. Baadhi ya wanafunzi walicheka, lakini baadhi walimhuzunikia wakiamini kuna mchezo kachezewa na si bure.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mwalimu John akakimbia mstarini pale Kama mwendawazimu na kwenda ofisini lakini kila alipojaribu kuvuta kumbukumbu zake alikumbuka kuwa alipotoka nyumbani alikuwa amevaa suruali tena suruali yake mpya ya kadeti.



    "Sasa imeenda wapi?? mnh hapana kuna MTU kanichezea lazima nimweendee Malawi hata Nigeria ntafika Ila siwezi kumwacha" aliwaza Mwalimu John na wakati huo waiimu wenzake waliamua kwenda nyumbani na kumletea suruali nyingine ili aweze kuondoka Nayo.



    ********

    Baada ya wanafunzi kuingia darasani kwao. Doreen aliamua kumuita Dorice nje kwani alikuwa na mazungumzo nae mazito sana.Dorice alionekana kuogopa kwani wito ule haukuwa wa kawaida, akasimama kwa hofu akimtazama Doreen



    "vipi mbona unaogopa, unaogopa nini?" alisema Doreen.

    "siogopi kitu!"alijibu Dorice

    "basi nisogelee"

    Dorice akamsogelea Doreen kwa hatua chache.

    "Jana ulikuwa na nani pale kwenye mti usiku?" aliuliza Doreen huku akiuchezesha mguu wake wa kulia chini na mkono mmoja akiwa kaushika kiunoni.

    "hukuniona au?" aliuliza Dorice kwa mshangao.

    "jibu swali!"

    "OK! nilikuwa na Eddy"

    "nani yako Eddy?"

    "Doreen unanitisha ujue?"

    "kha! nakutisha nina mapembe hapa? nijibu swali langu"

    "Eddy mpenzi wangu!"

    "nimekupata sasa... tangu lini Eddy mpenzi wako hujui kama ni mume wangu mtarajiwa?"

    "Ati nini....... Eddy ni. .."



    DORICE alishtuka sana kusikia Eddy ni mume mtarajiwa wa Doreen hakutaka kuyaamini maneno ya Doreen hata kidogo.

    "hivi we Doreen umechanganyikiwa au upo timamu?" Dorice aliropoka kwa hasira.



    " nikuulize wewe, hivi upo timamu au mwendawazimu unavomng'ang'ania mpenzi wangu Eddy? mpaka watu wanakushangaa! inaniuma sana Dorice usione nimekukaushia!" Alisema Doreen kwa msisitizo wa hali ya juu. Maneno ambayo yalizidi kumuumiza Dorice mpaka machozi yakaanza kumlengalenga machoni mwake. Alimtazama Doreen kwa hasira huku akiumanisha meno yake kwa ghadhabu, moyoni alitamani kumuadhibu vikali Doreen kwa kutaka kulitia DOA penzi lake na Eddy lakini hakuwa na uwezo huo.



    "Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako! sitaki kuamini kama rafiki yangu kipenzi Leo unageuka adui yangu!"alisema Dorice huku akipiga hatua na kutaka kuondoka mbele ya mbaya wake. Lakini ghafla Doreen akamvuta shati na kumrudisha pale alipokuwa amesimama.



    "we vipi? hebu niache niondoke?"

    "nitakuachaje sasa wakati unaniharibia penzi langu na Eddy?" alisema Doreen kwa kujiamini sana huku akibetua midomo yake kwa dharau utadhani Eddy ni mpenzi wake kweli kumbe hakuna lolote ni tamaa na wivu vinavyomsumbua.



    "umefanikiwa kuniumiza moyo wangu Doreen mpaka najuta kukufahamu.... haya Fanya lolote utakalo tena ili kunyang'anya haki yangu ya mapenzi... do it!" alisema Dorice kwa kwikwi kwani alishindwa kuzuia kilio chake kutokana na maumivu makali aliyoyapata moyoni mwake kwani maneno ya Doreen yalikuwa kama mkuki wenye sumu katikati ya moyo wake.



    "hata Mimi najuta kukutana na mwanaharamu wewe, Kwa usalama wako achana na Eddy... sijui unanielewa?"



    Dorice hakusema chochote zaidi ya kumkazia macho ya hasira Doreen, bila kujua kuwa kutazamana na Doreen kwa wakati ule ilikuwa ni kujikaanga kwa mafuta yake mwenyewe kwani Doreen aliitumia nafasi ile vizuri sana.



    Alijibadilisha macho yakawa ya kutisha sana kisha kila alipomtazama Dorice machoni alimhamishia vitu Fulani visivyoeleweka, kisha baada ya hapo Doreen alimsogelea Dorice na kumzodoa lakini haikuwa kumzodoa kwa kawaida Bali alimpaka vitu kama kamasi USO mzima na kumfanya Dorice atie kinyaa sana bila yeye mwenyewe kujitambua.



    "hebu niondokee hapa mpuuzi wewe na ushukuru Mungu sijakufanya kitu kibaya" alisema Doreen baada ya kuhakikisha amekamilisha kazi yake aliyokusudia kwani sio siri Doreen alipania kumpata Eddy kwa vyovyote vile.



    Dorice alitembea taratibu na kumfuata Eddy darasani huku akiendelea kulia.



    **********

    Walimu wote walikuwa hawaelewi mambo yanayoendelea shuleni pale, kwani kila siku liliibuka jipya. Suala la mwalimu John kuvuliwa suruali kwa mazingira ya kutatanisha lilizidi kuwapa maswali mengi walimu wa while ya sekondari mabango mpaka wakaogopa hata kuingia madarasani, kwani walihisi wanaweza kudhalilishwa kama ilivyomtokea mwalimu John.



    Mbali na suala hilo pia suala la mkuu wa shule kujifungia ofisini liliwapa mtihani mkubwa kwani haikuwa kawaida yake.

    "jamani nimeenda ofisi ya mkuu wa shule karibia Mara tatu nimegonga sana lakini hakutoa jibu hata nilipojaribu kusukuma mlango inaonekana amefunga kwa ndani!" alisema makamu mkuu wa shule baada ya kuingia staff.

    "hata Mimi nimeenda pale ofisini lakini palikuwa kimya sana ingawa mlango unaonekana umefunguliwa kwa nje... nimepiga simu haipokelewi" alisema mtaaluma.

    kiukweli iliibuka sintofahamu miongoni mwa walimu wote waliingiwa na hofu kubwa.

    " mmh! hii sio kawaida ya mkuu kabisa inabidi tufanye jambo"

    "Mimi naona tuvunje mlango tu" alipendekeza mwalimu wa nidhamu.



    walimu wote walikubaliana kuvunja mlango wa ofisi ya mkuu wa shule. wakaebda moja kwa moja mpaka ofisini kwa mkuu na kuvunja mlango kisha wakaingia.. walichokutana nacho kila MTU hakuamini , walibaki midomo wazi huku machozi yakiwadondoka kama chemichemi katikati ya mlima.



    Mwili wa mwalimu Mbeshi ulikuwa umeoza vibaya sana funza walitapakaa kila mahali wakisindikizwa na harufu mbaya iliyojaa ofisini mle. hakuwa mbeshi tena mwanamama aliyejipenda na kunukia marashi muda wote Bali jina lilibadilika na kuwa maiti.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Walimu walitulia kimya kwa muda wa dakika mbili nzima Vila kusema chochote lakini macho ya makamu mkuu wa shule yalitua mpaka mezani kwa mbeshi ambapo aliona karatasi ndogo nyeupe yenye ujumbe. Akaisogelea na kuichukua, kisha akaanza kuisoma. Ghafla alishtuka sana baada ya kusoma ujumbe ule "UNAFATA WEWE ULIYESOMA KARATASI HII."



    Makamu yule kwa woga na hamaki akaropoka " Mimi sijasoma chochote... tusisingiziane hapa!" alisema huku akificha macho yake na kumkabidhi mtaaluma karatasi ile kwani walimu wote hawakujua kilichotokea hivyo wakatamani wasome ujumbe uliokuwemo mle.



    ********

    Dorice alimtuma MTU amwitie Eddy darasani lakini mwanafunzi yule akakataa. hivyo Doreen aliamua kwenda mwenyewe darasani mle.



    Darasa lilikuwa limetulia kimya sana, Dorice akafungua mlango na kuingia lakini ghafla alipoingia wanafunzi wote darasani mle wakacheka kicheko kikali sana kilichomtia hofu sana Dorice. lakini akajikaza kisabuni licha ya kwamba alijua wanamcheka yeye, akamsogelea Eddy na kumtaka watoke nje lakini Dorice aligundua mabadiliko makubwa sana kwa Eddy Ila hakuuliza chochote wakatoka nje. wanafunzi wakacheka tena kwa dharau kitendo kilichomuumiza sana Dorice.



    "hivi we demu unajisoma??" alisema Eddy kwa ukali. maneno hayo yalimshtua sana Dorice.

    "Eddy! sijakuelewa!"

    " unajisoma kweli? hivi kwanza unajua majamaa wanakucheka kwa sababu gani?" maneno ya Eddy yalimfanya Dorice ataharuki.....



    ...DORICE alimtazama Eddy kwa mshangao wa hali ya juu kwani tangu walipoanza mahusiano hakuwahi kumuona akiwa na chuki dhidi yake kwa kiasi kile. Dorice alikosa ujasiri wa kuzungumza chochote kwa wakati ule kwani alihisi viungo vyake vyote vinakosa nguvu. Akabaki ameduwaa kama zuzu mbele ya Eddy.

    "we Dorice nimekuuliza unajua wanakucheka nini darasani?" aliuliza Eddy kwa ukali.

    "Sijui" alijibu Dorice kwa huzuni

    " Sasa kama hujui wanakucheka jinsi ulivyomchafu, hebu jiangalie hizo kamasi ulizojipaka kama mtoto asiyejua hata kutembea, pili hiyo yako chafu, na tatu...." kabla Eddy hajamaliza Dorice alishtuka sana kusikia vile kwani alipofika darasani asubuhi alikuwa msafi kama ilivyokuwa kawaida yake.

    "Eddy umesemaje?!" aliuliza Dorice kwa mshangao. Na wakati huo Doreen alikuwa alikuwa amejificha nyuma ya darasa karibu na waliposimama akina Dorice, na aliweza kusikia kila kitu kinachozungumzwa. Alisikiliza kwa umakini sana huku akiyafurahia majibu ya Eddy Kwa Dorice.

    " Hujanisikia? tena ukome kunifuatilia, usahau kama nilishakuwa mpenzi wako , unifute akilini mwako, sikupendi?" alisema Eddy akiwa amenuna kama aliyekula ndimu.

    "unasemaje Eddy! hebu rudia nisikie"

    "Sikutaki , sikupendi na sikuhitaji!" alisema Eddy huku akiondoka

    "Eddy! Eddy! nimekukosea nini mpenzi wangu?"

    "Achana na Mimi Dorice! huna hadhi ya kuwa na mimi , demu mwenyewe huna hata mvuto!" alisema Eddy na kusonya. Kisha akaenda zake darasani.

    Alimwacha Dorice kwenye bahari ya simanzi na machozi yasiyoweza kuzuilika. Alilia kwa uchungu kama MTU aliyefiwa na MTU muhimu, lakini kilio hicho cha Dorice kilikuwa shangwe na furaha kwa Doreen. Alijiona kama mshindi kwa kufanikiwa kulivuruga penzi la Eddy na Dorice bila hata huruma kwani wawili hao walipendana sana na walikuwa na malengo makubwa katika maisha ikiwa ni pamoja na kufunga ndoa pindi watakapotimiza malengo yao.



    Doreen alicheka kwa dharau kisha akaondoka zake na kwenda darasani, ambapo alimfuata Eddy pale alipokuwa amekaa.

    Eddy alimkaribisha Doreen kwa tabasamu mwanana na macho ya matamanio.

    "Mambo Eddy handsome" alisema Doreen kwa sauti ya utulivu iliyomkuna vyema Eddy hadi akakosa ujasiri wa kuongea.

    "Eddy mbona huitikii salam yangu?"

    "Niko poa... vipi wewe mtoto mzuri"

    "mh! nani mzuri Eddy?" Doreen alijifanya kuona aibu. Na kwakuwa darasa lilikuwa na kelele nyingi walipata mwanya wa kuzungumza zaidi.

    "mzuri wewe hapo mtoto wa kitanga!"

    "Acha hizo Eddy! mzuri no Dorice!"

    "Eh! usinitajie huo uchafu"

    "mh! uchafu tena? "

    "ndio... Doreen bora umekuja hapa kukaa.. nina kitu muhimu sana nataka nikwambie"

    "mh! kitu gani Eddy?" aliuliza Doreen huku akirembua jicho lake kubwa zuri kwa madaha.



    ***

    Karatasi lile lenye ujumbe mzito lilitua mikononi mwa mtaaluma wa shule, kwa haraka macho yake yalitua kwenye maandishi yaliyoandikwa kwenye karatasi ile lakini maandishi yalikuwa tofauti na yale aliyoyasoma makamu mkuu wa shule, yalisomeka hivi "TOENI HUO MZOGA LA SIVYO MTAISHA"

    Mwalimu yule wa taaluma aliogopa sana akashindwa kuongea akampasia karatasi mwalimu wa nidhamu lakini alipochukua tu ujumbe ulibadilika ukasomeka hivi "WEWE UTAMFUATA MAKAMU WA SHULE MAANA ULINITESA"



    "ati nin? nilikutesa wapi Mimi? hata sio Mimi ujumbe haunihusu!" mwalimu wa nidhamu aliongea kwa kuchanganyikiwa na kwa hofu kubwa. Akampasia karatasi mwalimu mwingine lakini pindi anapompa mwalimu yule karatasi ujumbe ulibadilika tena "MNANISUMBUA! UKIMPA MWINGINE UJUMBE HUU UNAKUFA MUDA HUU.. NA UKINIWEKA CHINI UTAONA CHA MTEMA KUNI"

    Mwalimu yule aliyefahamika kwa jina la mwalimu Jason alivuta pumzi ndefu sana huku mapigo ya moyo yakibadili mwendokasi na kwenda haraka sana. Akabaki ameshikilia karatasi lile mkononi mwake bila kuelewa cha kufanya .

    WAlimu waliokuwa wanasubiri kusoma karatasi lile walimfokea mwalimu Jason kwa kuendelea kulishikilia karatasi lile kabla ya wao kulisoma.

    "we vipi tupe na sisi tusome!"

    "shukuru hamjasoma"

    "Nini? usituzingue tupe hilo karatasi tusome bhana"

    walimu walizidi kung'ang'ania karatasi lile lakini mwalimu Jason hakuwa tayari kuwapa ili kulinda uhai wake. Mwalimu Jasoni akaangalia upenyo ili aweze kutoka ofisini mle kisha akatoka mbio akiwa ameshikilia karatasi lake.



    Mwalimu wa taaluma akaangalia pale chini ulipokuwepo mzoga wa Mbeshi akaona jinsi funza wallivyokuwa wakitapakaa kwa kasi.

    "Jamani tumtoeni huyu tutakufa wote"alisema mtaaluma.

    wakati huo makamu mkuu wa shule alikuwa akitokwa na haja ndogo kutokana na hofu ya kifo kama alivyoambiwa kwenye ujumbe.



    ***



    Mwalimu John alionekana mwenye sana pindi aliporudi nyumbani kutokana na kitendo cha kudhalilika shuleni. Mkewe aliingia sebuleni na kumsogelea mwalimu John

    "mume wangu vipi?"

    "kwani vipi mke wangu?"

    "nakuona hauna raha kulikoni?"

    "nipo sawa... Ila... nina safari..!"

    "kha! safari ya wapi tena mume wangu?"

    "Naenda Malawi... Leo!"

    "Malawi? kufanya nini mume wangu?"

    "usijali kuna kazi muhimu naenda kufanya.."

    "mbona ghafla sana? halafu mbona umevaa suruali ambayo si yako? au umefumaniwa?"

    Aliuliza mke wa mwalimu john huku akimkagua mume wake kwa kupitisha macho kuanzia juu had I chin... ...



    Doreen alizidi kujilegeza sana kwa Eddy ili amteke kimawazo na kiakili sawasawa. Alirembua macho kama aliyekula kungu huku akimtazama Eddy.. Hakika kwa urembo aliokuwa nao Doreen na vituko alivofanya alizidi kuziteka hisia za Eddy haswa. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mtoto wa kiume alijikuta anaishiwa pozi, uvumilivu ukamshinda akajikuta anakohoa kidogo ili asafishe koo na kuweza kusema la moyoni.



    "Eddy!" Doreen aliita kwa sauti ya mvuto sana.

    "Naam"

    "niambie basi.."

    "ah!.. Doreen kama nilivosema awali wewe in mzuri sana hivyo basi .... nataka uwe mpenzi wangu.. please! naomba unielewe!" Eddy aliongea kwa sauti ya chini ili majirani wasiweze kusikia.

    "Eddy! we ni shemeji yangu siwezi kumsaliti rafiki yangu Dorice!" Doreen alijifanya kukataa ingawa moyoni mwake alifurahia ushindi wa kumpata Eddy ilhali warembo wore shuleni pale waliikosa nafasi ile isipokuwa Dorice.

    "Doreen! plz naomba nikubalie nakupenda sana "

    "Na Dorice je?"

    "habari za Dorice achana nazo me nimeachana nae, nakupenda wewe"

    "mi sitaki Eddy!" sauti aliyoitoa Doreen ilionesha kabisa alikuwa anataka Ila alivunga tu.

    "Nikubalie Dori.. nakupenda Doreen.. usinitese!" Eddy alisema huku machozi yakimlengalenga kwani hakutaka kumkosa Doreen. Ama kweli dawa za Doreen alizotafuna kabla ya kumfuata Eddy zilifanya kazi vizuri sana.

    "Okey! nakubali kuwa na wewe!"

    "Oh my God kweli Doreen unanipenda? asante sana!" Eddy aliachia tabasamu mwanana na alitamani hata kumkumbatia Ila aliogopa kufanya vile kwani walikuwa darasani.

    "Nakupenda Eddy Ila kuna sharti moja muhimu inabidi ufate ili uwe na Mimi..."

    "sharti gani tena?" Eddy alishtuka

    "upo tayari?"

    "ehm.. ah ndio coz I love u.. ntafanya"

    "good.. nafurahi sana"

    "Niambie basi mpenzi.." alisema Eddy akitabasamu.

    "usijali nitakuambia baadae..."

    Alisema Doreen huku akiinuka kitini na kuondoka zake. Eddy alikuwa na furaha sana hakuweza hata kusoma zaidi ya kumfikiria Doreen na kila Mara aliachia tabasamu.



    Ilikuwa ni mchana majira ya SAA nane na nusu ambapo kengele iligongwa katika shule ya sekondari Mabango ambapo iliwaataarifu wanafunzi wote kuwa muda wa vipindi umekwisha na ni muda wa kupata chakula cha mchana.



    Lakini haikuwa hivyo kwani wanafunzi walitakiwa waende mstarini ambapo Habari za kusikitisha sana zilipenya mioyoni mwa wanafunzi wote wa shule ile.



    "Mkuu wa shule mama Dayana Mbeshi ameaga dunia Leo asubuhi kwa kifo cha ghafla kilichompata ofisini kwake..pia walimu wawili wana hali mbaya na wamefikishwa hospitalini kwa matibabu!" ilikuwa sauti ya masikitiko sana kutoka kwa Mwalimu Gallus iliyoonesha simanzi nzito sana aliyokuwa nayo.



    Mwalimu huyo alishusha pumzi ndefu sana na kuendelea " Maombi yenu in muhimu sana kwa walimu wenu ambao wapo hospitali... na..." mwalimu Gallus alishindwa kuendelea kuzungumza kwani machozi yalikosa adabu yakashuka kwa kasi hivyo akaamua kuondoka eneo lile.



    Wanafunzi wote waliondoka lakini mwishoni alibaki Eddy alitembea taratibu huku picha ya msichana katili anayejifanya mwema, Doreen ikizidi kumjia akilini mwake na kumfanya aisahau kabisa njaa aliokuwa nayo. Njia nzima alkuwa akizungumza peke yake kama mwehu mpaka alipofika bwenini.



    "Ah Doreen! ni msichana mzuri sana! siamini kama amekuwa wangu..!" Aliwaza Eddy huku akiachia tabasamu kisha akabadili nguo na kujitupa kitandani.



    Alionekana kutoguswa kabisa na msiba wa mwalimu mkuu kwani tayari alikuwa amechanganyikiwa na Doreen. Hakumkumbuka tena Dorice ambaye kila Mara alimuahidi kutomsaliti kwa namna yoyote.



    *******

    Dorice alikuwa amekaa kitandani kwake huku machozi yakitiririka mashavuni mwake. Weupe wa ngozi ya USO wake ulibadilika na kuwa mwekundu kutokana na kulia kwa muda mrefu, hakuamini kama Eddy angemtenda kiasi kiasi kwani siku zote aliamini Eddy ndiye MTU pekee wa kumuamini, aliamini kama Eddy ndio furaha pekee ya moyo wake iweje Leo amtupe kama taka ya msafiri ndani ya basi pale airushapo kupitia dirisha bila kujua itakapotua? Alimuona Eddy kama mnyama katili asiyekuwa na moyo wa utu.



    Marafiki zake Dorice walizidi kumbembeleza atulie bila mafanikio yoyote.



    "Kwa alichonifanyia Doreen, siwezi kumwacha kilahisi tu... lazima nimfanyie kitu..." Alijiapiza Dorice



    " Ni lazima atajuta mpaka kifo chake... hatokaa anisahau kwa ntakachomfanyia.. lazima aelewe kuwa Mimi ni Dorice mtoto wa Kinyaturu sinyang'anywi tonge mdomoni kwa urahisi!" Alizidi kujiapiza Dorice akiwa amejifunika blanket mpaka usoni. Lakini baada ya muda mfupi Dorice aliinuka kitandani pale na kujifuta machozi kisha akapiga hatua za haraka kuelekea nje.



    ********

    Mke wa Mwalimu John amuijia Juu Mumewe akitaka kujua suruali ile imetoka wapi. Lakini mwalimu John hakutaka kuweka wazi kile kilichomkumba shuleni.. alitaka iwe siri yake mpaka atakapofanikiwa kwenda Malawi kutafuta waganga wakumroga aliyemfanyia uchuro.



    "John! umefumaniwa huko sio?" alifoka mke wa John

    "usipaniki mke wangu tulia.. sijafumaniwa mim!" alijitetea mwalimu John bila mafanikio na wakati huo tayari mkewe alishaanza kumtandika makofi mumewe na alipoona haitoshi akanyanyua upawa na kumtandika nao Mwalimu John kichwani.



    Ghafla John akanyong'onyea na kutulia kimya kitini bila kutikisika..

    "John! John!" aliita mke wa mwlm John bila mafanikio John hakuweza kuitikia.

    "Mime wangu... John wangu" alizidi kuita lakinu John alikuwa kimya, mkewe alichanganyikiwa sana.......



    ...MWALIMU JOHN alikuwa kimya pale kitini akiwa hana fahamu yoyote, mkewe akazidi kuchanganyikiwa sana kwani alihisi tayari mumewe ameaga dunia.



    "Jamani mume wangu amka bado nakupenda! Nisamehe Mimi John wangu!" Alizidi kulia mke wa mwalimu John kwa huzuni na majuto makali. Alijiona mjinga sana kwa kujichukulia maamuzi mkononi bila hata kumdadisi vizuri.



    Simanzi ilimtanda mwanamke yule bila kujua la kufanya, machozi yalichuruzika kama mito miwili usoni kwake kwani ndio kwanza ndoa yao ilikuwa changa kabisa tangu waoane miezi mitano iliyopita sasa iweje John aage mapema kiasi hicho? Mkewe aliufikiria upweke ambao angekabiliana nao Siku za usoni. Huzuni ikamzidia.



    Mwalimu John akiwa bado ameyafumba macho yake akahisi yumo kwenye usingizi mzito sana lakini alikisikia vyema kilio cha mkewe.



    Alitamani aamke ili amtulize mkewe lakini mwili ulikuwa kama umegandishwa na sumaku. Hakuweza hata kutikisika, ghafla akahisi upepo mkali sana ndani ya nyumba yake alipotazama ukutani akakutana na sura ya kutisha sana.



    Huku ikifuka moshi mdomoni, macho mekundu kama damu na kichwani yalichomoza mapembe mawili marefu. John aliogogopa sana kwani tangu azaliwe hakuwahi kukutana na kiumbe wa ajabu na wakutisha namna ile. Alitamani azinduke usingizini lakini hakuweza, hivyo alibaki akitetemeka.



    Ghafla kiumbe yule akabadilika na kuwa sura ya msichana mrembo sana. Mwalimu John akabaki kinywa wazi akistaajabu ya Mussa. Alipotazama vizuri aligundua ni Doreen , akashtuka sana.Doreen alimtazama mwalimu John kwa dharau sana kisha akaachia kicheko kikali sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Mimi ni Doreen Mbwana! Daima usinichezee maana sichezewi kirahisi.. Unataka kuniendea Malawi we? Hahahahah umechelewa sana John, nina nguvu kuliko unavofikiria"



    Doreen akamsogelea John, na kutoa kucha zake ndefu nyembamba kama msumari kisha akamgusa mdomo John."Umeniita Nimekuja! Sasa utaipata fresh...! Hahahahahahahhh" alisema Doreen kisha akatoweka . John alihema kwa nguvu sana huku woga ukiwa umemtawala kupita kiasi kwani maneno ya Doreen yalimtisha.



    Mke wa Mwalimu John alizidi kulia baada ya kuona mumewe haamki kwa muda mrefu. Kelele Za kilio chake ziliwafikia majirani ambao walikuja kwa wingi kushuhudia kilichotokea. Bila hodi majirani hao walitiririka kama utitiri nyumbani kwa mwalimu John.

    "Kuna nini jirani?" Aliuliza Mzee mmoja aliyejulikana kama Makorokocho.

    "Hata sielewi mume wangu kapatwa na nini jamani...sielewi mimi" mke wa John alizidisha kilio.

    "Kwani imekuaje?"

    "Msogelee umwangalie maana mimi sielewi.. Namwita haamki.."

    "Mh!" Aliguna Mzee Makorokocho huku akimsogelea mwalimu John.

    Akamtikisatikisa John akamwita lakini John hakuitika, Ingawa John alisikia kila kitu kinachoendelea ila hakuweza kuamka.

    "Mh! Mama pole sana huyu tayari ametangulia mbele za haki..."

    "Ati mini?"

    "Ndo ivo mama chamsingi tuwapigie ndugu zake simu, taratibu za mazishi zifanywe!"

    "Hapana! Mume wangu hajafa! Iweje John afe mbele yangu.. Aaah we Mungu we!!" Mke wa Mwalimu John alilia kwa uchungu sana.



    Ndugu wa mwalimu John wakapigiwa simu kupewa taarifa za msiba, taratibu za mazishi zikaanza kufanywa.



    *******

    Dorice alipotoka bwenini kwao akaongoza moja kwa moja mpaka bweni la Mapambano ambalo ndilo alilokuwa akiishi Eddy, alitembea kama mwendawazimu mpaka alipotia timu katika bweni hill bila kujali ni bweni la wavulana pekee. Dorice aliongoza mpaka kitanda cha Eddy ambapo alimkuta Eddy akiwa na wenzake watatu. Na alikuwa akiwasimulia juu ya uhusiano wake mpya na Doreen.



    "Habari zenu" alisalimia Dorice akiwa amevimba kama kiboko aliyekasirishwa. Eddy hakujibu isipokuwa wale rafiki sake.

    "Umefuata nini hapa we mpuuzi?"

    "Nimekufuata wewe nataka nijue kama unanipenda mimi au Doreen?"

    "Hivi we mwanamke unawazimu we? Nikupende wewe kama nani? Doreen ndo mpenzi wangu, nampenda sana."

    "Kweli!?"

    "Ndio tena niondokee hapa, unanitia kinyaa!" Eddy alimsukuma Dorice kwanguvu Dorice akaanguka chini na kujigongesha kichwa kwenye kitanda.

    "Eddy usifanye ivo bhana utamuumiza mwenzio" alisema rafiki mmoja wa Eddy kwani alimuonea huruma sana Dorice.

    "Achana nae mpumbavu huyo"

    "Lakini kumbuka mlikotoka"

    "Achana na mimi kama unampenda si umchukue!"

    Maneno Yale yaliziidi kumuumiza Dorice, aliinuka pale chini akajifuta vumbi maana bweni lilikuwa na vumbi kupita kiasi.

    "Sawa Eddy! Daima kumbuka sio kila king'aacho ni dhahabu... Utanikumbuka!" Alisema Dorice kwa huzuni na kutoka.



    "Akukumbuke nani wewe? We boya tu huna lolote" Eddy aliropoka maneno hayo huku akiwashangaza rafiki zake kwani daima hawakujua kama Eddy angemchukia Dorice kiasi kile kutokana na mapenzi yao yalivokuwa.



    "Ama kweli watu wanabadilika..!" Alisema rafiki take Eddy na kuondoka zake.



    Dorice aliondoka zake mpaka bwenini kwao, akachukua begi lake dogo na kuweka vitu vyake muhimu. Isipokuwa nguo za shule na madaftari, baada ya kupaki vizuri akachukua kanga akaivaa baada ya kutoa nguo kisha akaenda bafuni kuoga.



    Alipooga na kujiandaa vizuri alikaa kitandani kwake huku kila Mara akitazama SAA yake ya mkononi ambayo alipewa na Eddy enzi za mapenzi yao. Ilikuwa SAA nzuri ya Dhahabu."Ikifika SAA kumi na mbili jioni lazima nitoroke ... Siwezi kubaki hapa!" Aliwaza Dorice akiwa kitandani kwake.



    Muda huchelewa sana pale unapousubiri ndivyo ilivokuwa kwa Dorice. Muda ulichelewa lakini ukafika, kigiza kilipoanza tu akachukua begi lake na kutoka bwenini. Hakuvaa nguo za shule hivyo haikuwa rahisi kugundua kama ni mwanafunzi wa pale. Taratibu akazipiga hatua ili atoroke shuleni pale.



    Licha ya kwamba alisumbuliwa na maswali ya wanafunzi wenzake ila hakujali ingawa aliwapa majibu ya uongo yanayoridhisha.



    Shule ya mabango ilikuwa imezingirwa na miti mingi hivyo akapita katikati ya miti hiyo ili asioneakane kirahisi. Alipokuwa anaendelea kutembea ghafla akaona kitu mbele yake akashtuka.



    ********

    Jioni ile tulivu Eddy na Doreen walikutana kwenye mti mmoja mzuri na tulivu. Walikuwa wamekumbatiana kimahaba huku wakipeana denda za kutosha.



    "Baby nakupenda sana" alisema Eddy

    "Nakupenda pia ila..."

    "Ila nini mpenzi?"

    "Sharti la kuwa na mimi ni kwamba hutuwezi kufanya mapenzi..." Alisema Doreen.

    " eh! Kwanini?"

    "Tukifanya hivyo kuna kitu kitatokea kwako?"

    "Mh Doreen! Mbona sikuelewi, tutaishije kama wapenzi?"

    "Nivumilie tu... Ila bado nina bikra"

    "Nataka niitoe bikra yako Doreen please!"

    " huwezi kufanya mapenzi na mimi, pia kuna sharti lingine mbali na hilo..."

    "Bby hapa siwezi kuwa na wewe bila kufanya mapenzi, siwezi! Halafu pia siwezi kukuacha au huniamini?"

    Alisema Eddy akiwa amezidiwa na hamu ya mapenzi na ilikuwa kazi ngumu sana kwake kujizuia....





    MIPANGO YA MAZISHI kumzika mwalimu John ilikuwa tayari imekamilika, ndugu walikuwa tayari wamewasili kwa majonzi. Huzuni iliwatawala sana kwani mwalimu John alikuwa ndiye tegemezi la familia yote kwa ujumla. Kelele za vilio zilitawala mtaa mzima aliokuwa akiishi mwalimu John, kila MTU alisema lake juu ya msiba ule lakini ukweli haukujulikana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Make wa mwalimu John alipoteza fahamu kila Mara huku akijutia tendon alilomfanyia mumewe kwa kumpiga na upawa kichwani .Lakini alijiahidi kutomwambia mtu yoyote akihofia kukamatwa kwa kosa la mauaji. Nyuso za watu wote zilitia huruma sana kwa kuondokewa na mwalimu John kipenzi cha watu wengi.



    Walimu kutoka shule ya sekondari Mabango walikuwepo pale msibani wakimuaga mwalimu mwenzao.



    Jeneza la gharama lilitengenezwa, mwili wa mwalimu John ukawekwa ndani ya jeneza. Make wa mwalimu John alikuwa haamini kama mume wake ndo anapelekwa kuzikwa.. Aliachia yowe Kali lililowashtua wote pale msibani "Rudi mume wangu.. Rudi mpenzi wangu usife..." Alilia mke wa John.



    Wazazi wake walikuwa wakigalagala chini kama wehu,hawakujali vumbi lililokuwa limetapakaa ardhini kutokana jua Kali la kiangazi.



    Hatimaye Jeneza lililokuwa limebeba mwili wa marehemu John likaingizwa kwenye gari kwaajili ya kupelekwa makaburini huku likisindikizwa na nyimbo za huzuni zinazopigwa misibani. Watu wote wakaelekea makaburini kwani magari ya kutosha yalikuwa yamekodiwa.



    Mwalimu John alikuwa ndani ya Jeneza akilia kwa sauti ili Atolewe kwani alikuwa hajafa. Lakini hakuna MTU yeyote aliyesikia kilio cha Mwalimu John wala kuhisi, " Inamaana wananizika mzimamzima?" Alijiuliza mwalimu John huku moyo wake ukiwa umezimia kwa mile akionacho.



    "Haiwezekani nizikwe mzima mzima! Hapana" alisema Mwalimu John huku akijaribu kujiinua lakini mwili wake ulikuwa bado mzito kama vile umegandishwa na barafu. Akiwa ndani ya jeneza hilo akasikia kicheko kikali sana kutoka kwa Doreen.



    "Doreen nisamehe tafadhali" alijitetea Mwalimu John.

    Machozi yalizidi kumtoka kwa kasi sana , ndipo alipokumbuka kosa lake kwa Doreen.



    Zilikuwa ni wiki mbili tangu Doreen ahamie shule ya Mabango, kutokana na uzuri na utanashati wa mwalimu John. doreen alivutiwa nae sana hivyo akaamua kumwambia ukweli mwalimu wake kuwa anampenda na anahitaji kuwa naye kimapenzi. Mwalimu John alimtazama binti yule kwa jeuri na dharau kisha akamjibu " We mtoto ni mpumbavu sana! Umezunguka kote huko ukaona uniletee umalaya wako hapa? Mbwa koko wewe hebu niondokee hapa!"

    "Mwalimu John hunitaki? Unanitusi? Sasa nitakuonyesha kazi!" Alisema Doreen kwa kujiamini sana kisha akaondoka zake

    .

    Wakati Mwalimu John akiendelea na kumbukumbu hizo ghafla akahisi jeneza lake linanyanyuliwa Tayari kwa kumuweka kaburini...



    *********

    Dorice alipokuwa akitembea ghafla akazungukwa na chatu mkubwa sana kila upande. Dorice alishtuka sana, mapigo yake ya moyo yakamwenda kasi sana akiwa haelewi la kufanya.



    Kutokana na woga Dorice aliangusha chini mkoba aliokuwa ameubeba lakini ghafla akakumbuka kitu. Akaokota mkoba wake kwa ujasiri sana kama vile hakumjali chatu yule kisha akatamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe. Ghafla bin vuu chatu yule akatoweka kimuujiza, Dorice akaendelea na safari yake.



    Alitembea mwendo wa kama dakika tano hatimaye akafanikiwa kuiacha mipaka ya shule, akaingia barabara kuu ya kokoto ambayo ilizingirwa na miti kila upande. Akaendelea kupiga hatua moja baada ya nyingine kuelekea alikokusudia.



    Safari ilikuwa ndefu sana na Giza likazidi kuiteka dunia ingawa mbalamwezi ikawa taa kwa msichana yule mwenye kujiamini.



    Dorice alitembea taratibu baada ya kuchoka kutokana na mwendo mrefu hatimaye akafika kwenye kijito kidogo kilichotawaliwa na ukimya wa ajabu. Hakukiwa na sauti ya vyura wala wadudu palikuwa kimya mno. Dorice akavuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu sana kisha akaketi pembeni ya kijito kile kimya.



    Alikaa karibia robo SAA nzima akiwa ameinamisha kichwa chake ghafla akasikia kishindo kizito ambacho kilimshtua mawazoni.

    *********

    Eddy aliendelea kumng'ang'aniza Doreen wafanye mapenzi lakini Doreen aliendelea na msimamo wake ule ule kuwa hawezi kufanya mapenzi.

    "Doreen tafadhali mpenzi...!"

    "Siwezi Eddy!"

    "Hapana Doreen, kama ni hivyo niruhusu niwe na msichana mwingine!"

    "Kwa hilo usije kuthubutu maana utahatarisha uhai wako?"

    " kivipi?"

    "Elewa hivo"

    Eddy alishtuka kidogo lakini akaachana na mawazo hayo akaendelea kumbembeleza Doreen. Doreen aliendelea kukataa Katakata ingawa nayeye pia alitamani kufanya mapenzi na Eddy ila kuna kitu alikumbuka kikamtia hofu, akazidi kumkatalia.

    Uvumilivu ulimshinda kabisa Eddy akajikuta anamtoa Sketi Doreen huku nae akishusha suruali yake. Akambwaga chini Doreen na kutaka kufanya nae mapenzi, kabla hajafanya chochote Eddy aliachia yowe Kali sana....





    ..VIJANA wanne wenye nguvu walinyanyua jeneza alililokuwamo Mwalimu John kisha taratibu walipiga hatua kuelekea kwenye nyumba yenye pembe NNE na kina kirefu kiasi aliyotengenezewa mwalimu John.



    Sauti za vilio zilizidi kutia simanzi katika eneo lile LA makaburini. Nyimbo za huzuni zilitawala eneo hill huku kila mmoja akisikitika moyoni mwake.



    Ndani ya jeneza hilo mwalimu John alikuwa akihangaika sana kuwaita vijana wale ili wasimzike lakini katu hakusikika. Alizidi kupiga kelele za kuomba msaada lakini ikabaki kuwa kazi bure. Sauti iliyojaa huzuni kuu ya mkewe Monalisa ilizidi kupenya vyema masikioni mwake, hali hii ilzidi kumtia simanzi mwalimu huyo ambaye sasa alikuwa amekata tamaa ya kuishi tena.



    "Daah Doreen hafai" alijisemea mwalimu John huku machozi yakimtiririka kwa kasi kwani bado alikuwa haamini kama kweli anazikwa akiwa mzima.Vijana wale walilishusha jeneza like lenye mapambo ya kupendeza ndani ya kaburi kisha wakatulia kidogo ili mchungaji atupie neno LA mwisho.



    Mchungaji alichukua udongo kidogo na kusogelea vyema kwenye shimo alilowekwa mwalimu John."Uliumbwa kwa mavumbi hakika utarudi mavumbini, Bwana alitoa Bwana ametwaa jina LA Bwana lihimidiwe... " Mchungaji aliyasema maneno hayo kwa huzuni kisha akaumwaga kaburini udongo ule aliokuwa ameushika mkononi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mwalimu John aliyasikia vyema maneno hayo yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wenye sumu. Hakika mwalimu John alikiri kuwa kweli duniani kuna watu na viatu, Doreen alikuwa kiatu chakavu kisichofaa kuvaliwa hata na kichaa.



    Vijana walishika vyema sepetu zao ili waanze kutupa udongo kaburini na kumzika mwalimu John lakini kabla hawajaanza kutupa udongo, kilizuka kimbunga kikali cha ghafla kilichofanya watu wapoteane. Jeneza likafunuka ghafla mwalimu John akainuka kutoka kwenye jeneza.



    ********

    Eddy aliachia yowe Kali sana ambalo lilijirudia Mara kadhaa. Yowe hill lilitokana na maumivu makali sana aliyoyapata kwenye sehemu zake za siri. Maumivu yalikuwa makali sana hivyo alianguka chini na kupoteza fahamu.

    Wakati wote huo Doreen alikuwa amebadilika sura na kuwa sura kama sura ya paka. Kucha zilimtoka kama za chui anayekabiliana na hatari. Kichwa chake kilikuwa na mapembe marefu. Hivyo akawa na umbile la kutisha sana ambalo hakuna kiumbe wa kawaida angeweza kustahimili kumtazama hata kwa nusu sekunde.



    Licha ya kwamba Doreen alikuwa kwenye umbile lile la kutisha lakini alionekana mnyonge sana. Machozi ya damu yalikuwa yakimshuka taratibu kwenye macho yake. Alimsogelea Eddy na kukaa karibu yake huku akimgusa taratibu mwilini mwake.



    "Eddy mpenzi wangu nakupenda sana.. Nisamehe kwa kilichotokea.. Halikuwa kusudio langu hata kidogo, ila umelazimisha... Nakupenda sana na ninakuahidi kukupenda maisha yangu yote...!" Alisikika Doreen akiongea kwa huzuni ila sauti yake ilikuwa ilikuwa nzito ya kutisha iliyoambatana na mwangwi mkali. Doreen alizidi kulia kwa huzuni sana na taratibu sura yake ilianza kujirudi. Akawa Doreen yule aliyezoeleka.



    Machozi yakawa hayamkauki kwa kitendo alichomfanyia Eddy mwanaume ampendaye sana.Doreen akampandisha Eddy suruali kisha akatulia kimya akimsubiri azinduke.



    Lilipita SAA zima ndipo Eddy akapiga chafya ya kwanza.. Doreen alimtazama Eddy kwa huzuni na huruma nyingi lakini Eddy hakufumbua macho. Baada ya robo SAA Eddy akapiga chafya mbili mfululizo kisha akayafumbua macho taratibu lakini hakuweza kuona chochote kutokana na Giza Nene lililozingira kila upande, Eddy akaogopa akataka kukimbia lakini mwili wake ulikuwa mchovu sana kama MTU aliyefanya kazi ngumu kupita kiasi. Akajishangaa sana .



    "Eddy mpenzi. ." sauti ya Doreen ilimshtua Eddy na kumfanya ajue kuwa hayupo peke yake. Eddy akageuka na kumwona Doreen kwa mbali kwani Giza lilimzuia asionekane sana .Kumbukumbu zikamrudia Eddy kichwani akaikumbuka ile sura ya kutisha ya Doreen aliyomwona nayo kabla ya kupoteza fahamu.



    "Toka! Usiniguse! Ushindweee.. !" Aliropoka Eddy huku akikikimbia bila kuelewa nguvu zimetoka wapi .

    "Eddy!" Aliita Doreen lakini Eddy alikuwa tayari amekimbia.

    "Oh! Shiit!" Alisema Doreen bila kuelewa la kufanya.Akasimama kwa muda kisha akaamua kuondoka zake eneo lile.



    Eddy alifika bwenini kwao akakuta mlango umefungwa kwani wenzake walikuwa darasani kwa vipindi vya usiku(prep. Time). Eddy alisonya kwa hasira akiwa ameuegamia mlango huku kashika kufuli.



    Ghafla wazo likamjia aliamua kwenda mlango wa dharula na kuingia bwenini. Woga ulimjaa ila hakuweza kwenda darasani aliamua kulala na kujifunika blanketi gubigubi.Usingizi ukampitia mpaka asubuhi.

    "Eddy vipi mbona umelala sana, Jana ulikula mzigo kwa kasi nini?"

    Alitania Jackson rafiki kipenzi wa Eddy baada ya kumwamsha.

    "Vipi kumekucha" alisema Eddy kwa sauti ya nyono.

    " hahah Eddy Yale mambo hayataki papara, hebu amka bhana! "



    Jackson alicheka kisha akamfunua blanket Eddy.Eddy alijivutavuta kisha akaamka na kwenda bafuni kuoga .Alipofika bafuni aliwakuta wanafunzi wenzake wengi wakioga. Bila wasiwasi wowote Eddy alivua nguo zake na kuanza kuoga. Ghafla wanafunzi wenzake wakabaki kumshangaa Eddy, wakaanza kukonyezana kisha wote wakaanza kumtazama Eddy kwa wizi.

    Eddy hakujua lolote akaendelea kuoga kwa kujiachia sana.

    Wanafunzi hao wambeya hawakukomea hapo Bali walitoka nje na kuwaita wenzao ambao pia wakaingia bafuni mle wakijifanya kunawa nyuso zao kumbe walizuga tu, lengo kuu ilikuwa kumtazama Eddy.



    *********



    Dorice alishtushwa na kishindo kile pale mtoni. Akageuka kutazama nyuma , hakuamini macho yake kwani alimwona MTU mrefu sana akiwa amesimama nyuma yake. Dorice aliogopa sana akatetemeka.



    "Unafanya mini hapa?" Like jitu refu lilimuuliza Dorice kwa ukali.

    "Napumzika.. Nim..nimechoka" Dorice alijibu kwa kutetemeka.

    "Umetoka wapi na unaenda wapi?"

    "Nimetoka Mabango.. Naenda mjini..!"

    "Hahahahah kwanini ukae hapa? Hii ardhi yetu.. Na muda huu ni sherehe yetu umetusumbua... Hivyo utakuwa kitoweo chetu.." Lilisema jitu lile. Dorice alitetemeka kupita kiasi, jitu lile likamsogelea Na kumshika mkono kisha wakatoweka...





    .EDDY aliendelea kuoga bila kujua kuna watu wanapiga chabo mle bafuni. Alijua wanafunzi wale wanamtazama kwa wema tu au labda wanautazama uzuri wake aliojaaliwa na Mwenyezi Mungu ambao daima unawachanganya mabinti na hata wanawake watu wazima ambao kuna wakati walimrubuni kwa kumpa vitu vya thamani ili awakubalie lakini bado hawakumpata kijana yule kutoka kwenye familia ya kitajiri ya Mr.Alloyce.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Eddy aliendelea kuoga kwa kujiamini mpaka alipofikisha mkono kwenye maeneo yake nyeti. Ghafla alishtuka sana kama vile amepigwa shoti ya umeme, macho yalimtoka kama MTU aliyekutana na simba USO kwa USO porini.



    Eddy hakuamini alichokihisi, akaamua kuyapeleka macho yake moja kwa moja mpaka kwenye bustani yake muhimu. Akagundua kuwa sehemu zake za siri hazipo. Bado Eddy hakuamini akachukua maji kwenye kiganja chake cha mkono na kuyasafisha vizuri kwani alihisi hayaoni vizuri. Jibu likabaki moja tu Sehemu zake nyeti hazikuwepo.



    "What! Mbona sielewi!" Eddy alichanganyikiwa kupita kiasi. Akachukua suruali yake na kuivaa kwa wizi ili watu wasimwone lakini alikuwa tayari amechelewa kwani alikuwa tayari ameshaonwa na watu wengi tu.



    Bila hata kujiosha povu la sabuni alilokuwa amejipaka mwilini, Eddy alikimbia na kuingia bwenini. Akajibwaga kitandani kwa Jackson rafiki yake bila kujali kuwa sabuni iliyoko mwilini mwake ilichafua shuka.



    "Eddy! Vipi mshkaji!" Aliuliza Jackson huku akimalizia kuvaa sare zake za shule.

    " Nakufa Jack... Nakufa Mimi...."

    " Unakufa? Mbona sikuelewi Eddy?" Jackson alikuwa haelewi chochote kinachoendelea kuhusu Eddy ingawa taarifa zilikuwa zimesambaa kwa wanafunzi wengi wa kiume.

    " Eddy! Niambie umepatwa na nini? Unaniacha njia panda.."

    " Jack... Nakufa... Siwezi kuishi... Nakufa..." Eddy alizidi kulia kama mtoto mdogo aliyenyimwa maziwa kwa muda mrefu. Akili yake haikufikiria kingine zaidi ya kujiua, asingeweza kuistahimil aibu ambayo ilimjia kwa kasi bila hata kupiga hodi.

    "Jack..Dunia hadaa ulimwengu shujaa.. Jack me nakufa.. Waambie wazazi wangu..Nilipenda visivyopendeka ila sio kwa matakwa yangu naamini ni shetani tu.."

    Maneno hayo yaliibua simanzi nzito kwa Jackson, machozi yalimzidi nguvu hivyo yakashuka kwa kasi machoni kwa Jackson.

    "Hapana Eddy huwezi kufa, hebu niambie tatizo..!"

    "Hata nikikwambia huwezi kunisaidia Jack.. Huwezi amini natamani kuwa hata nyuki wa mashineni kwa sasa!"

    " una maana gani!"

    "Mimi sio mwanaume tena... Unafikiri nitaificha vipi aibu hii? Bora nife.. Nikapumzike na wafu wenzangu.."

    "Eddy! Sio mwanaume tena kivipi?"

    "Uume wangu haupo!" Eddy aliposema hayo akashindwa kujizuia kulia kwa sauti. Hivyo akalia kwa sauti Kali iliyosikika bweni zima. Kwa bahati nzuri wanafunzi karibia wote walikuwa wameondoka ili wawahi mstarini.

    Jackson alitazama SAA yake ya mkononi ilikuwa tayari SAA mbili kasoro.

    " Eddy! Nitarudi sasa hivi ngoja nikakuombee ruhusa kuwa unaumwa, ila please usifanye lolote. Niahidi!"



    Eddy aliitikia kwa kichwa kuwa hatofanya lolote, Jackson akatoka huku akiwa na wasiwasi sana.Eddy aliona dunia inamwelemea na ni vigumu kukabiliana nayo. Machozi hayakuacha kumtiririka kila sekunde. Akili yake ikaanza kukumbuka mambo mengi, ndipo alipoupata ukweli kuwa Doreen ndiye aliyemfanyia ukatili ule Jana usiku.



    Akili ya Eddy ikawa kama imefunguliwa kutoka kwenye kifungo kikali. Akamkumbuka Dorice wake, msichana ampendaye sana kuliko mwingine yeyote ila akakumbuka kuwa alishamsaliti na kumdhalilisha mbele za watu.



    "U wapi Dorice mpenzi wangu! Dorice nisamehe ! Dorice haikuwa akili yangu! Nakupenda Dorice! Ingawa nakufa ila naomba unisamehe sana.... Doreen ni shetani! Hafai hata kidogo..!" Eddy alilia mpaka kamasi zilimtoka. Kichwa kikamgonga kutokana na kulia kwa muda mrefu.



    Eddy aliinuka kitandani pale na kwenda moja kwa moja kwenye begi lake. Akachukua kijidaftari kidogo, akachana karatasi ndogo. Kisha akachukua kalamu akaanza kuandika ujumbe huku machozi yakililowanisha karatasi lile .



    " Dorice mpenzi, nisamehe kwa yote yaliyotokea Nakupenda sana. Halikuwa kusudio langu mpaka sasa sielewi ilitokeaje. Mpaka kaburini, kumbuka upendo wangu, ujue kwamba Nakupenda! Nakufa mpenzi ila bado nakupenda!"



    Eddy alimaliza kuandika ujumbe huo wa kusikitisha kisha akalikunja karatasi lile na kuliweka kitandani.Eddy alishusha suruali na kujiangalia tens sehemu zake za siri ili ahakikishe kama ni kweli. Ndio ilikuwa kweli kabisa wala so ndoto. Kilio cha Eddy kikaongezeka alishindwa kuvumilia akaona ni heri ajiondoe duniani mapema.



    Eddy alifungua begi lake na kuchukua vidonge vingi alivyokuwa akivitumia kwa maumivu ya tumbo, akatafuta vidonge aina nyingine akavichanganya kwa pamoja. Lengo lake ilikuwa avitumie kama sumu ili aondokane na adha zinazomkàbili duniani. Akachukua maji yaliyokuwa kwenye kopo akalisogeza karibu. Akasali sala ya mwisho ili apokelewe vyema na malaika wa huko aendako.



    *****

    Doreen alikuwa darasani asubuhi ile. Alikuwa amekaa konani akiwa ametulia tuli huku madaftari yake mawili yakiwa yamefunuliwa kana kwamba alikuwa akiyasoma. Lakini tangu alipoyafunua madaftari Yale yalibaki hivyohivyo kwani Doreen alikuwa hayasomi ila aliyafunua kwaajili ya kuzuga tu. Mawazo yake yalikuwa yalikuwa mbali sana.



    "Inabidi ulete uume wa mwanaume umpendaye, akiwa taabani na hamu ya mapenzi, pale anapotaka kufanya mapenzi nawewe ndipo uchukue uume wake! Umeelewa!" Maneno hayo yalijirudia kichwani mwa Doreen na kumfanya ashtuke kidogo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Moyo ulimuuma sana Doreen kwa kumfanyia ukatili ule Eddy, alijiona yeye sio binadamu kabisa kwani hana roho ya ubinadamu. Huruma ilimshika sana, alimhurumia Eddy.



    "Ataishije.. Daah! Najichukia sana kwa nilichokifanya.. Nampenda sana Eddy!" Aliwaza Doreen mpaka machozi yalimlengalenga machoni. Hakuwahi kumhurumia MTU yeyote duniani kama alivyomhurumia Eddy. Alijiona mkosaji sana kwa MTU asiye na hatia.



    Licha ya yote hayo lakini Doreen hakuwa na jinsi. Ilibidi afanye vile ili atimize lengo lake lililomleta katika shule ya Mabango. Alikuwa tayari amefikia robo tatu ya kile alichotumwa. Ilibidi amalizie robo iliyobaki ya kusudio lake ndipo aibuke kinara katika ufalme ambao hauonekani kwa macho ya kawaida. Ushindi ulikuwa wake mpaka pale alipofikia.



    Doreen aliwaza mambo mengi sana lakini wazo kuu lilibakia Kwa Eddy, alitamani kujua Eddy anaendeleaje kwa wakati ule lakini hakuwa tayari kumtembelea Eddy kwani aliona kama akuwa kero kubwa kwa kijana yule na ataibua chuki.

    " masikini Eddy! Ila sina jinsi..!"



    ****

    Dorice alikuwa amepelekwa kwenye utawala wa viumbe wa ajabu ambao hakuwahi kuwaona hata Siku moja. Sura na maumbo yao yalikuwa ya kutisha sana. Alijawa na woga sana, alitetemeka kama vile ampepigwa na baridi Kali. Hakuweza kuwatoroka kwani hata njia alikuwa haijui, hakuelewa amefikafikaje eneo lile. Alizidi kumwomba Mungu amsaidie na amwepushe na mabaya.



    "Salam Malkia!" Alisalimia kiumbe yule aliyeambatana na Dorice kwa heshima na adabu.

    Mwanamke mrembo mwenye dhahabu mwili mzima na mavazi ya kung' aa mwlini mwake akiwa ameketi kwenye kiti kizuri cha dhahabu alimwitikia kiumbe yule.

    "Salam! Naona umefanya Nazi nzuri sana Leo!"

    "Ndio malkia!"

    "Vizuri sana, mtumishi wangu!"

    Dorice alikuwa ametulia kimya akisubiri kitakachomtokea.

    "Binadamu hawa jeuri sana...!"

    Alisema malkia yule huku akiinua fimbo yake ya dhahabu na kumnyooshea Dorice.

    Dorice aliogopa sana alijua kifo chake sasa kimewadia.

    Malkia yule aliinyoosha fimbo ile ikatua moja kwa moja kwenye kifua cha Dorice.

    Malkia yule akaituliza fimbo ile kwa muda wa dakika kama tano. Kisha akaachia kicheko kikali sana cha kutisha.. Doreen alizidi kupata hofu.............



    ..Jeneza la mwalimu John lilikuwa tayari limefunuka, Mwalimu John aliinuka ndani ya Jeneza na kusimama wima cha kwanza alichofanya ilikuwa ni kunyanyua kinywa chake na kumuita mkewe mpenzi kwani ndiye aliyekuwa akimfikiria kila sekunde. " Mke wanguuuuu... Niko hai..usilie" Mwalimu John alisema kwa sauti kuu, huku furaha ikiwa imefurika moyoni mwake kwani hakuamini kama kweli ameurudia uhai.



    Akiwa katika furaha hiyo isiyo na kikomo mwalimu John akatahamaki sana baada ya kuona umati wote uliokuwa ukiomboleza kwaajili yake ukikimbia. Watu walikimbia kwa fujo huku hofu ikiwa imewatamalaki. Cha ajabu hata mke wa Mwalimu John pia alikimbia kama swala anayekabiliana na mnyama mkali.



    Hakuna aliyesalia kwenye eneo lile, vumbi lilitimka na kuwaaga waombolezaji wote ambao mpaka wakati ule hakuna aliyejua kilichotokea. "Maajabu haya! Maiti kafufuka? Kweli dunia IPO ukingoni" alisikika mwanamume mmoja ambaye alikuwa amejikwaa mguu baada ya kukimbia kwa muda mrefu.Alihema kwa nguvu huku akizitafuta nguvu zingine za kukimbilia. Ghafla akahisi kuna Mtu kasimama nyuma yake



    " Vipi kuna mini kwani?" Ilisikika sauti ile ambayo ilipenya vyema masikioni mwa mwanaume yule. Akageuka kutazama anayeuliza, Mwanaume yule alitetemeka sana baada ya kukutana USO kwa uso na Mwalimu John. Akainuka haraka na kuziendeleza mbio zake.



    Mwalimu John alikuwa haelewi ni kwanini watu wote wanakimbia, na yeye akaingiwa na hofu akaanza kukimbia akijua labda kuna jambo la hatari linakuja. Alizipiga mbio kuelekea nyumbani kwake ili akajihifadhi haraka iwezekanavyo.



    Mwalimu John alipofika mtaani kwao, kila MTU alikimbilia ndani na kujifungia. Ndipo alipozidisha juhudi na kuongeza mwendokasi akidhani hatari inamkaribia. Mwalimu John alifika nyumbani kwake, alipofika getini ghafla geti likafungwa. Akastaajabu sana kwani hakufikiria kuwa mkewe badala ya kumpokea kwa shamrashamra alimfungia mlango.



    " Nifungulie mke wangu!" Alisema Mwalimu John huku akipigapiga mlango, na kwakuwa mlango haukufungwa vyema ukajifungua. Mwalimu John aliingia ndani huku akihema sana.

    "Mamaaaaa!"

    Zilisikika kelele ndani ya nyumba ya Mwalimu John, ndugu wote walipiga kelele.

    "mke wangu! Hunitaki!?" Mwalimu John aliuliza kwa sauti ya kutia huruma, huku akimsogelea mkewe.

    "Ushindweee!" Mkewe alifoka.

    "Mke wangu nishindwe Mimi? Leo unaniambia nishindwe kwani Mimi pepo?" Mwalimu John alizidi kutia huruma.

    Aliinamisha kichwa chini, kwa bahati macho yakatua mwilini mwake. Mwalimu John alishtuka kupita kiasi, akajiogopa na akatamani kujikimbia.

    "Nooooooooo!"

    *****

    Eddy alikuwa yupo kwenye wakati mgumu sana , alishindwa kujua lipi ni sahihi kichwani mwake kati ya kifo au kuishi kwa aibu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Alikuwa bado ameshikilia vidonge huku machozi yakimchuruzika kama bombs machoni mwake. Alilia kwa uchungu huku akimlaani sana Doreen, alimuona kama mnyama aliyekuja kuupoteza uhai wake. Alimchukia kuliko kitu kingine chochote lakini tayari alikuwa amechelewa.



    "I wapi thamani yangu? Edd mie ninaetegemewa na wazazi wangu! Siwezi kuishi tena.. Bora nife tu kuliko kuishi kwa fedheha hapa duniani!" Mawazo hayo yalipita taratibu kichwani mwa Eddy. Hatimaye kichwa chake kikafanya maamuzi akaamua kujiua.



    Kabla hajatupia lundo la vidonge vile kinywani, mlango ulifunguka. Hatua za miguu kulekea aliko Eddy zilimshtua. Jakson akiambatana na Zawadi walifika pale alipo Eddy, walishtuka sana kukuta vidonge vingi vikiwa mkononi mwa Eddy.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog