Search This Blog

MWANAFUNZI MCHAWI - 2

 







    Simulizi : Mwanafunzi Mchawi

    Sehemu Ya Pili (2)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Eddy vipi unataka kujiua" Jackson alisema kwa mshtuko huku akimnyang'anya kinguvu vidonge vile.

    "Acha nife tu!" Alisema Eddy kwa unyonge.

    "Huwezi kufa, na huwezi amini Eddy nimempigia simu mama yako nimemwambia una matatizo aje kukuchukua!"

    "What! Sitaki Mimi! Sipendi kiherehere chako Jack! Umemwambia nini?"

    Eddy alifoka kwa hasira.

    "Hebu tulia bro! Mimi sijamwambia bays lolote, nimemwambia una matatizo ambayo hutaki walimu wajue, na sio muda anakuja!"

    "Umenikera sana ujue, sitaki kwenda home! Bora ningekunywa dawa zangu mapema kabla haujafanya huo ujinga wako.. Sio siri kaka umeniboa kinazi!"

    Alizidi kufoka Eddy.

    "Eddy haupo sawa.. Jack usimsikilize huyu sio kosa lake! " alisema Zawadi.

    "Nani hayupo sawa unamaana nina kichaa sio? Nyie wote mabwege tu.. Siwaelewi wala nini.." Eddy alikuwa kama mwenda wazimu, Jack na Zawadi walitulia kimya tu.

    "Nawaharibia sasa hivi mjue! Niondokeeni hapa.. Poteeni maboya nyie..!"



    Jackson na Zawadi walitulia kimya tu, ghafla meseji iliingia kwenye simu ya Jackson. Ingawa simu zilikuwa haziruhusiwi shuleni pale ila alikuwa na simu ya kimagendo.

    "Nimefika hapa shule mwanangu!"



    Ilikuwa ni meseji kutoka kwa mama yake Eddy kwani alikuwa amewasiliana na patron ambaye alikuwa anafahamiana nae vizuri hivyo waliyamaliza.



    Hazikupita hata dakika kumi Eddy alikuja kuchukuliwa bwenini. Alikuwa na hali mbaya sana kwani alikuwa kama mwenda wazimu.



    Mama take alipoletewa kijana wake hakuamini.

    "Eddy mwanangu wakufanya nini? Wamekupa kichaa?" Alisema mwanamama yule mrembo.

    "Siendi kokote mie, siendi na mtu!" Eddy alikataa kuondoka . Ikabidi wambebe kinguvu na kumsweka kwenye gari ya mama yake.

    "Mungu wangu mtoto mwenyewe mmoja huyu kama roho.. Mungu wangu wee!"

    Alilia Mama Eddy.

    ****



    Doreen alisikia taarifa za kuondoka kwa Eddy, roho ilimuuma ila hakuwa na jinsi alijifanya kuhuzunika na wenzake kumbe yeye ndiye aliyefanya kila kitu.



    Alitamani kuondoka mapema kabla siri zake hazijafichuka lakini alikuwa amebakiwa na kazi moja kubwa sana. Alitakiwa achukue titi moja la msichana mrembo sana shuleni pale ili akamilishe kazi yake.



    Alijiuliza sana achukue titi la nani bado ulikuwa mtihani kwake. Akajilaumu kwanini hakuchukua titi la Dorice kwani ingekuwa kazi rahisi kwake.



    " Nilizembea sana! Sasa nifanyaje?" Alijiuliza Doreen.

    Baada ya kuumiza kichwa kwa muda mrefu hatimaye alipata jibu. Picha ya msichana mzuri aitwaye Nadia Joseph ilimjia kichwani. Alikuwa in msichana mzuri sana kwa sura, umbo mpaka tabia.



    "Wow! Atanifaa sana! Na vile vititi anavyovibust vile.. !" Doreen alitabasamu akijua tayari kazi imeisha. Ushindi ni wake. Alifurahia sana kumfanyia mwenzie ukatili.



    Kilichobaki ilikuwa ni kusuka mipango ili mambo yake yaende sawa.Aliinuka kitini na kumfuata Nadia Joseph darasani, alimkuta binti yule mwenye sura ya upole na werevu akiwa ametulia kimya kwenye dawati lake akiendelea kujisomea.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Mambo mrembo!"

    "Poa.. Habari yako?"

    "Salama.. Nimekuja kupiga stori na were, vipi upon tayari?"

    "Karibu.." Alisema Nadia Joseph huku akimkazia macho Doreen.

    "OK!"



    Wakati Doreen akikakaa, Nadia alihisi kitu.. Tens kitu kibaya sana! Machale yakamcheza kwa kasi sana akajua hakuna usalama wowote kwa Doreen. Haraka sana akaamua kuchukua hatua.......



    .DORICE alimtazama malkia yule kwa woga huku fimbo ile ya dhahabu ikiwa kifuani mwake. Alihisi kifo chake kipo njiani lakini akajipa moyo wa imani kuwa hawezi kufa kwani hakutenda kosa lolote. Malkia Yule alicheka kicheko kikali cha kutisha.



    "Dorice wewe in mchawi sio?" Alisema Malkia yule huku akiwa na sura ya kutisha sana.

    "Mimi sio mchawi!" Alijibu Dorice kwa kutetemeka.

    "Mbona ulipovamiwa na chatu pale njiani uliongea maneno ya kichawi?"





    "Ndio niliyaongea lakini mimi so mchawi, maneno hayo nilifundishwa na babu yangu ambaye ni mganga!" Dorice alishikwa na woga kupita kiasi.

    "Hahah Dorice... Kuwa mkweli?"

    "Kweli kabisa.. Mimi si mchawi.. Tafadhali naomba mniruhusu niende!" Alisema Dorice huku akilia.

    "Unaenda wapi?"

    "Naenda Singida kwa babu yangu!"



    Aliomba Dorice akiwa amepiga magoti huku akilia kwa hofu.

    "Huwezi kwenda Dorice... Sahau kuhusu kuondoka hapa!" Alisema malkia yule kisha akamwamrisha mlinzi wake amwondoe pale Dorice ampeleke sehemu nyingine.

    Mlinzi alitii agizo la malkia akamtoa Dorice pale na kumpeleka eneo lingine.



    Kilikuwa kama chumba kidogo chenye mwanga hafifu lakini kilikuwa na mapambo mengi sana ya dhahabu. Kilipendeza sana na kilivutia macho kupita kiasi, Dorice alibaki anashangaa.Aliingizwa chumbani mle bila kuambiwa kitu chochote na mlango ukafungwa. Akabaki peke yake.



    Hofu ilimzidia sana alitetemeka kama MTU aliyekumbwa na baridi Kali sana, hakupata fursa ya kutazama kitu chochote ndani ya chumba kile akabaki ameinama huku akilia. Alijuta kutoroka shule kwaajili ya Doreen, aliona heri angebaki tu kuliko kuchukuliwa na viumbe wale wa ajabu.



    Ghafla akiwa katika dimbwi zito la mawazo alishtuliwa na sauti nzito ya kiume ikimwita jina lake."Dorice" Dorice alishtuka sana kwani alipoingizwa mle hakukuwa na mtu yeyote wala hakusikia mlango ukifunguliwa.Aliinua kichwa na kumtazama aliyemwita.



    "Usiogope Dorice.. Naitwa Mansoor, ni mtoto wa Malkia.." Alijitambulisha mwanaume Huyo mwenye sura nzuri ajabu, alinukia marashi mazuri sana yasioisha hamu kuyanusa. Dorice alishangazwa na uzuri wa kiumbe yule mwenye umbo tofauti na viumbe wengine aliowaona kwenye eneo lile. Kwa haraka alimkadiria kuwa na umri wa miaka kama 21 au 22.



    "Dorice! Nimeshangazwa sana na uzuri wako uliojaaliwa.. Ama kweli umeumbika! Karibu kwenye himaya yetu!" Alisema kijana yule aliyejitambulisha kwa jina la Mansoor huku akitabasamu na kumpa mkono Dorice. Dorice alibaki ameduwaa kwa mshangao.

    ****

    Eddy alikuwa bado ana hali mbaya iliyomliza sana mama yake kwani Hakuwa na mtoto mwingine yeyote zaidi ya Eddy. Kila Mara alimtazama Mwanaye kisha akatikisa kichwa kwa majonzi. Kwa wakati huo baba yake Eddy alikuwa hayupo nyumbani, alikuwa yupo Dubai kwaajili ya buashara zake.



    "Eddy mwanangu una nini?"

    "Sina tatizo mama! Naomba nirudi shule..!" Alisema Eddy huku akilia.

    "Huna tatizo wakati una tatizo kubwa? Eddy mwanangu nakufahamu vizuri, hebu niambie una tatizo gani?"

    "Sina tatizo... Naomba chakula!"

    "Nakupa ila naomba uniambie..!"

    "Nitakuambia mama ila ngoja baba arudi!"



    Mama Eddy hakuishiwa maswali kwa mwanaye, alitamani ajue anasumbuliwa na nini lakini jitihada zake ziligonga mwamba. Eddy hakuwa tayari kumweleza chochote.



    Mama Eddy alimwandalia chakula akipendacho mwanaye. Wali na samaki aina ya Sato vilikuwa tayari vipo mezani vikimsubiri Eddy avishughulikie. Eddy alikitazama chakula kile kisha akaachia sonyo Kali.



    "Mama! Hivyo ndio nini? Ntakulaje chakula kina harufu kama nini? Huoni hao funza walivyojaa humo au ndio chakula chenu siku hizi?"

    Alisema Eddy akiwa amekunja sura kama amekula ndimu iliyooza.



    "Funza? Funza wako wapi?" Mama Eddy alishangaa kwani chakula kile ndio kwanza alitoka kupika mda ule.

    "Funza hao! Huoni wanavyotembea tembea humo kwenye bakuli? Mama toaaaa..!" Alisema Eddy kwa sauti.

    "Mmh! Mwanangu we umerogwa.. Sio Bure..!" Alisema mama Eddy huku akiondoa chakula kile mezani.

    "Eddy kweli umeona funza?"

    "Ndio kwani we hujaziona?" Eddy Alisisitiza na kuzidi kumshangaza mama yake.



    Mama Eddy alizidi kuchanganyikiwa, akachukua simu na kumtafuta baba yake Eddy.

    "Hebu achana na hizo biashara baba Eddy! Mtoto ana hali mbaya sana!" Alisema mama Eddy kwa msisitizo.

    "Kwani ananini?"

    "We njoo mume wangu, uje haraka sana!"

    "Mh! Leo nakata tiketi ya ndege nakuja!"

    Mama Eddy alikata simu kwani alikuwa amempigia mumewe kupitia mtandao wa IMO.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kesho yake baba Eddy aliwasili nchini na kufika nyumbani kwake haraka.

    Alipomtazama Eddy hakuona kama ana tatizo sana. Aliona yupo kwaida na alishindwa kuelewa ni kwanini mkewe alichanganyikiwa kiasi cha kumfanya aache biashara zake na kurudi nyumbani.



    "Wanawake bhana mbona Eddy mzima kabisa?"

    "Mzima? Amerogwa huyu mume wangu tangu.. afike Jana hajala kitu anasema eti anaona funza?"

    "Eti nini? Mbona sielewi? Hujazoea utani wa Eddy mke wangu!?" Baba Eddy alichukulia kimasihara suala la Eddy. Ikabidi wamkalishe chini na kumuuliza vizuri kilichomsibu kijana wao.



    Sikh hiyo Eddy alikuwa mpole kupita kiasi, ni kama vile akili zilirudi kichwani mwake.

    "Baba! Mama! Hapa nilipo sio MTU tena, siwezi kuishi tena kwani nikiishi sitakuwa mkamilifu.. Bora nife!"

    Maneno hayo ya Eddy yalikuwa kama upanga kwani yalichoma mioyo ya wazazi wake na kuiachana katikati huku damu zikichuruzika bila kikomo.



    "Eti nini Eddy!"

    "Bora nife!" Aliridia Eddy

    "Kwasababu gani? Tumekukosea nini? Kuna kitu hatujakupa?"baba Eddy alichanganyikiwa na kuinuka sofani kama amechomwa na mwiba.

    "Wazazi wangu! Nimefanywa vibaya na binadamu katili, nimechukuliwa.. .. Ah.. Nime..!" Eddy aliangua kilio na kushindwa kuendelea kuongea.

    "Sema tu.. Umechukuliwa pesa? Au umebiwa vitu vyote sema tu.."





    ****

    "Doreen unataka nini kwangu?" Aliuliza Nadia Joseph.

    "Sitaki kitu.. Nataka tupige stori..."

    "Stori zipi za kutaka kuniwangia mchana kweupeee?"

    Maneno ya Nadia yalimshtua sana Doreen, hakutaka kuamini kama Nadia amejua lengo lake alistaajabu kidogo lakini hakutaka kushindwa.





    "Doreen unataka kuniwangia? Usitake kunijaribu nitakuaibisha!" Alisema Nadia kwa sauti ndogo iliyosikika vizuri.



    Doreen bado hakumuamini akajiweka sawa, akataka atumie ufundi na nguvu za uchawi wake ili amtulize kimya Nadia. Akaachia kombora lake la kichawi lakini....



    ..EDDY hakuwa na jinsi kwani aliona hana sababu yoyote ya kuwaficha wazazi wake juu ya tatizo lake.Aliamua kuwaambia ukweli Ili kama kuna uwezekano wa kumsaidia basi wamsaidie. Kwa kilio cha kwikwi kilichoonesha huzuni kuu iliyotawala moyo wake, Eddy alifungua kinywa na kusema ukweli.



    "Sehemu zangu za siri... Zimepotea.. Sielewi zilikoenda!" Maneno ya Eddy yaliibua sura mpya kwa wazazi wake. Walishtuka mshtuko ambao haukuwahi kuwatokea maishani. "Ati nini? Hebu rudia tena..!" Mr.Alloyce hakuamini maneno ya mwanaye. Mama yake Eddy hakueweza hata kufumbua kinywa chake kwani alikuwa amechanganyikiwa kupita maelezo.



    "Ndio hivyo baba yangu.. Sina raha ya kuwa hai..!" Eddy alizidi kulia pindi alipozungumza maneno hayo.



    Kiukweli kisa kile kiliwakata maini wazazi wa Eddy. Walihisi kuishiwa nguvu kabisa mwilini, walibaki kimya wakiwa wameinamisha vichwa vyao. Huzuni iliyochanganyika na mshangao ndiyo iliyotawala katika jumba lile la kifahari la Mr.Alloyce. Zilipita dakika tano kukiwa na ukimya wa kuogofya. Hatimaye Mr.Alloyce alivunja ukimya ule kwa kumdadisi mwanaye kwa maswali.



    "Kuna mtu ulimkosea?"

    "Hapana baba!" Alijibu Eddy.

    "Sasa ilikuwaje mwanangu?" Mr.Alloyce aliuliza kwa sauti ya upole sana.

    "Sijamkosea mtu ila kuna binti anaitwa Doreen..!" Eddy alitaka kusimulia jinsi ilivyokuwa lakini baada tu ya kutaja jina la Doreen hakuweza kuendelea kuzungumza kwani alipigwa Kofi moja zito, likamyumnisha pale kitini, kichwa kikamzunguka akahisi kama radi imempiga. Alipiga ukelele uliowashtua wazazi wake na kufanya wahamaki.



    "Eddy nini?"Mr.Alloyce aliuliza kwa mshangao kwani alimuona Mwanaye akidondoka kitini bila kujua kinachoendelea.



    Wakazidi kuchanganyikiwa sana, wakamsogelea Eddy na kumwinua lakini Eddy hakuwa na habari, alikuwa kama mzoga ambao unapelekwapelekwa kokote bila kutoa ushirikiano. Hali hiyo ilimtisha sana mama Eddy, akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikali.



    *******

    Dorice aliendelea kumshangaa Mansoor bila kutia neno lolote, ingawa moyoni alibaki kumsifia kwa uzuri alionao mwanakaka yule bila shaka hakuna mwanamke ambaye kwa hali ya kawaida asingevutiwa nae. Yote hayo yalibaki moyoni mwa Dorice na asingeweza kusema lolote kwa kijana yule.



    "Dorice mbona upo kimya wala hutaki kunijibu lolote.. Hata salamu?" Alisema Mansoor huku akiachia tabasamu mwanana.

    "Mh! Umesemaje?" Dorice akajifanya hakusikia lolote.

    "Ina maana hukunisikia kabisa..?"

    "Ndio"

    "Inawezekana kweli.. Maana unaonekana una mawazo mengi.. Unawaza nini?" Mansoor alimsogelea kwa ukaribu zaidi Dorice na kuketi.

    "Nataka kurudi nyumbani!"

    "Unataka kurudi? Kwasababu gani?"

    "Siwezi kukaa huku! Nataka nirudi nyumbani!" Alisema Dorice huku machozi yakimlengalenga.

    "Dorice! Utarudi vipi wakati mama yangu ameniambia amenitafutia mke? Nataraji kufunga ndoa nawewe hivi karibuni.." Maneno hayo ya Mansoor yalimshtua Sana Dorice akatoa macho kwa mshangao.



    "Unasemaje wewe?" Dorice aliuvua woga akajikuta ameropoka kwa hasira.

    "Sikiliza Dorice.. Kwa muda mrefu sana nilikuwa natafuta mke, sikumpata. Nilitamani sana kuoa binadamu ili niishi nae, na kwakuwa mama yangu ananipenda amenitafutia wewe na ninakupenda. Nataka nikuoe..!"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Toka hapa.. Usinisogelee... " Alifoka Dorice na kumsukuma Mansoor.

    Mansoor alihuzunika sana kwa kitendo alichofanyiwa na Dorice, akatikisa kichwa na kupiga hatua za taratibu kisha akatoweka ghafla machoni kwa Dorice. Dorice alishtuka sana akabaki ametumbua macho tu.



    "Mungu wangu nisaidie niondoke huku, mkosi gani huu? Nitafanywa vibaya na viumbe hawa sijui majini... Bila shaka ni majini! Niolewe na jini? Siwezi Mimi...!" Alizidi kuwaza Dorice huku kijasho chembamba kikimtoka kwa kasi.



    Ghafla mlango wa chumba alichokuwamo Dorice ukafunguka ghafla, Dorice alishtuka sana kukutana na sura ya malkia akiwa na hasira kupita maelezo.



    "Dorice binadamu! Ungekuwa umeuwawa masaa mengi yaliyopita.. Lakini kutokana na mapenzi ya mwanangu Mansoor kwako ndio maana upo hai mpaka sasa.. Ni kitu gani kinakupa jeuri ya kumtesa mwanangu wa pekee?" Malkia alizungumza kwa sauti Kali iliyoambatana na radi. Alionekana mwenye hasira sana.



    Dorice aliogopa sana wala hakuthubutu hata kunyanyua kinywa chake akabaki kimya huku akitetemeka.

    "Dorice! Una machaguo mawili tu! Chagua moja... KUOLEWA NA MANSOOR AU KIFO!"

    Alisema malkia yule kwa ukali, Hofu ikamzidia Dorice.



    ********

    Doreen alipoathubutu kutumia uchawi wake kumdhuru Nadia Joseph, ghafla akakumbana na kichomi kikali sana ubavuni mwake. Akahisi maumivu makali yaliyomfanya apige kelele sana zilizowashtua darasa zima. Wanafunzi wote wakamgeukia yeye lakini kwa kukwepa aibu akajifanya kujinyoosha akiwa bado anaugulia maumivu yale makali. Baada ya hapo wanafunzi wale wakaendelea na shughuli zao.



    "Doreen.. Nakupa onyo, acha kuwachezea wenzio! Unajivunia uchawi lakini Mimi nina MUNGU.. Hunitishi kwa lolote maana niliyenaye ni mkuu kuliko nguvu zote.. Nimemwomba Mungu anioneshe MTU anayevuruga shule nashukuru sasa amenionesha! Achana na Uchawi!" Alisema Nadia kwa ujasiri sana ingawa aliongea kwa sauti ndogo ili asisikike sana.



    Doreen aliumbuka sana, akaondoka bila kuaga.

    Kengele iligongwa wanafunzi wote walitakiwa waende mstarini. Baada ya mkusanyiko wa wanafunzi wote alisimama mwalimu mmoja kwaajili ya matangazo muhimu.



    "Kuuna taarifa za kusikitisha sana! Kiufupi ni kwamba Mwalimu Mkuu msaidizi na mwalimu wa taaluma hatuko nao tena. Wameaga dunia Leo asubuhi.. Pia kuhusu mwalimu John kuna sintofamu imetokea kiufupi ni kwamba hajafa bado yuko hai..." Wanafunzi walisikitishwa sana na taarifa zile ila walipigwa butwaa kuhusu mwalimu John kwani walikwisha tangaziwa kuwa amefariki lakini iweje waambiwe yuko hai? Walishindwa kuelewa.



    Baada ya mwalimu kutoa matangazo aliondoka zake pale mstarini. Ndipo Nadia Joseph alipoomba nafasi ya kuzungumza na akapewa.



    "Jamani wanafunzi wenzangu, hali hapa shule ni mbaya sana... Acheni masikhara hebu fanyeni maombi ya kweli! Mkisali kwa uaminifu MUNGU atajibu tu... Msichukulie mazoea tafadhali..." Aliposema hivyo kuna wanafunzi waliguna lakini Nadia hakujali hilo akaendelea.



    "Sasa hivi wanataka titi la msichana.. Usipokua makini unaweza ukachukuliwa lako..!" Nadia aliposema hivyo, alimwona Doreen kwa mbali akiwa amenuna sana huku akimtazama Nadia utadhani anataka kummeza.

    Wanafunzi wote wakataharuki, walianza kuogopa sana.

    Nadia akaondoka pale mbele kisha wanafunzi wote wakatawanyishwa.



    Doreen alikuwa na hasira za kuua MTU. Alimchukia Nadia kupita kawaida, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana...





    MWALIMU John alijishangaa kupita kiasi kwani miguu yake yote miwili ilikuwa imeoza vibaya. Alikuwa hahisi maumivu yoyote hapo kabla lakini pindi alipojitizama tu alianza kuhisi maumivu makali sana. Punde funza wakaanza kutoka mguuni. Akabaki anajiuliza nini kimetokea bila kujua sababu.



    Mkewe na baadhi ya ndugu zake walibaki kimya, wakimtazama Mwalimu John kwa woga.







    "Mke wangu bado unaniogopa? Hunionei hata huruma mumeo? Ama kweli mapenzi yapo kwenye raha tu!" Alisema Mwalimu John kwa huzuni iliyochochea huruma nyingi machoni mwa mkewe. Taratibu akaanza kumsogelea mumewe lakini kuna ndugu yake mmoja akata kakumzuia.







    "Niache! Nampenda mume wangu ingawa yupo kwenye hali hiyo.." Alisema mke wa mwalimu John huku akimsogelea mumewe kisha akamkumbatia kwa mapenzi mazito, bila kujali hali aliyokuwa nayo mumewe.







    "Nakupenda mume wangu.. Nashukuru umeurudia uhai ili tuendelee kuwa pamoja" alisema mwanamke yule huku machozi yakimchuruzika.







    "Nakupenda sana mke wangu, nilikuwa nakuwazia sana hali ambayo ungeikabili kama ningekufa.."



    "Sijui ningemweleza nini mwanao aliyeko tumboni mwangu!" Walizungumza yote hayo wakiwa bado wamekumbatiana. Maneno ya mke wa Mwalimu John yalimfariji sana John, akahisi kwamba kweli amerudi duniani.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ndugu walibaki wametumbua macho wakiwatazama wawili wale, hawakuwa na la nyongeza zaidi ya kumkaribisha mwalimu John ambaye hakuweza hata kutembea kutokana na maumivu ya miguu. Funza walizidi kuongezeka miguuni.







    "Mke wangu naumwa sana hii miguu, sijui kama itapoa!"



    "Usijali itapona tu mume wangu.. Ila naomba unieleze kila kitu kilichokutokea..!" Alisema mke wa mwalimu John huku akimwinua taratibu mumewe pale chini alipokuwa ameketi.



    Mwalimu John alilalama sana kutokana na maumivu Yale lakini ikabidi ajikaze mpaka walipoingia ndani.



    "Mke wangu Leyla.. Kweli nimeamini unanipenda!"



    Leyla akatabasamu na kumbusu mumewe kisha akasema



    "Nakupenda sana mume wangu hebu nisimulie imekuwaje..!"



    "Ni stori ndefu sana mke wangu..lakini ngoja nikusimulie mbele ya hawa ndugu zangu wote..!"



    Wote sebuleni pale walitulia kimya kusikiliza kisa cha ajabu kilichompata Mwalimu John. Lakini cha ajabu Mwalimu John alipotaka kusimulia tu..





    *******



    Wazazi wa Eddy walichanganyikiwa sana wakahisi mtoto wao mpendwa tayari amefariki dunia. Wakazidi kumtikisatikisa huku mama yake akiushusha mchozi kama maji, ndipo wakagundua Eddy hajafa ila amepoteza fahamu. Kofi alilopigwa halikuwa la mchezo, lilikuwa kama radi ingawa wazazi wake hawakujua kitu.



    Na hiyo ilikuwa ni kazi ya mzimu unaomsaidia Doreen.





    Mr.Alloyce alitumia nguvu zake zote kumpepea Eddy mpaka alipozinduka. Alikuwa amevimba USO mzima jambo lililowashtua wazazi wake. Wakatazamana kwa nyuso zilizojaa viulizo bila kujua majibu ya uhakika.



    "Eddy" Mr.Alloyce aliita.



    "Naam!" Eddy aliitikia kwa sauti ya chini.



    "Vipi?"



    "Nimepigwa!"



    "Umepigwa? Umepigwa na nani?"



    "Sijui!"



    Yote yaliyomtokea Eddy yalibaki kuwa viulizo kwa wazazi wake, yaliibua fumbo ambalo lilikuwa gumu sana kulitatua.



    "Baba Eddy"



    "Sema mke wangu..!"



    "Mi naona twende kwa mganga tu!"



    "Wapi?"



    "Tanga kwa mganga Tembo wa Bahari.. Umewahi kumsikia?"



    "Mmh! Hapana..!"



    "Nasikia ni kiboko sana kwani hata Mama Zuwena aliwahi kwenda akasaidiwa!"



    Mama Eddy aliamua kumshauri mumewe waende kwa mganga wa kienyeji anaepatikana Pangani Tanga. Mganga Hugo alifahamika kwa jina la Tembo wa Bahari kwani alisifika kwa kutatua matatizo yaliyoshindikana lakini Mr.Alloyce alisitasita kuhusu suala hilo.



    "Waganga siwaamini mke wangu..!"



    "We unafikiri tutafanyaje sasa! Kama hutaki niachie kila kitu Mimi nitahangaika na mwanangu..!" Mama Eddy alilivalia njuga suala lile hatimaye Mr.Alloyce akaingia laini na kumkubalia mkewe.



    "Sawa tutaenda!"



    "Twende kesho!"



    "Haina shida"





    Walikubaliana kuianza safari yao siku ya kesho yake.





    Siku ile hawakumsumbua Eddy kwa swali lolote lile, usiku aliingia kulala akiwa bado hana raha kabisa huku akiisubiri siku ya kesho yake ili waende kwa mganga.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    Eddy alipojilaza kitandani tu, usingizi mzito ukampitia. Ghafla akamuona Doreen ndotoni akija na kisu kikali sana kinachowaka moto. Eddy aliogopa sana akatamani kuamka lakini akashindwa.



    "Eddy ukithubutu kusema lolote kuhusu Mimi utakiona cha moto... Kubwa zaidi ukithubutu kwenda kwa mganga hiki kisu ni halali hapo kifuani pako.. Utakufa!"



    Ilisikika sauti ya Doreen ikiongea kwa msisitizo sana huku ikijirudiarudia.





    "Mamaaaa!" Eddy alishtuka usingizini na kumwona mama aliyekuwa amelala chumbani kwake ili kujua maendeleo ya Eddy kila wakati.



    "Vipi mwanangu?" Mama Eddy alishuka kitandani na kukisogelea kitanda cha Eddy.



    "Ndoto mama.. Naogopa!"



    "Pole mwanangu.. Usiogope tupo wote humu..! Alisema mama Eddy lakini Eddy bado aliogopa.





    Usiku ule ulikuwa mrefu sana kwa Eddy kwani alikumbana na vitisho Vinci kutoka kwa Doreen. Kulipokucha Eddy aliona ahueni kidogo ili aachane na mauza uza ya usiku.





    Majira ya SAA kumi na mbili na nusu asubuhi wazazi wa Eddy walikuwa tayari wamejiaandaa. Wakamwamsha Eddy ili anywe chai kisha waanze safari, cha ajabu Eddy aligoma kuondoka.



    "Siwezi kwenda kwa mganga! Siendi!"



    "Huendi?" Mama Eddy alishtuka



    "Siendi mama! Hata kwa greda!"



    "Kwanini?"



    "Sitaki!"



    Eddy aligoma kabisa kuondoka lakini mama yake alimlazimisha na kumweka kwenye gari akisaidiana na baba yake. Safari ikaanza.





    ********



    Doreen aliamua kusubiri usiku uingie ili amfuate Nadia na kumfanyia uchawi wake ili aondoke na ziwa.





    Usiku ulipoingia Doreen alikuwa akijipanga kwa kuita mizimu yake yote ili imwongezee nguvu. Alikuwa amejitenga peke yake kwenye kichaka huku akijpakapaka madawa yake ili aongeze nguvu zake za kichawi. Akainuka akiwa uchi huku akijiaminisha kuwa sasa yù kamili. Akatamka maneno yake ya kichawi akatoweka eneo lile..



    Muda huo ilikuwa ni saa name usiku.





    Akaenda moja kwa moja mpaka bwenini kwa Nadia na kukifikia kitanda chake, mh! Alichokutana nacho hakuamini.. Moto ilikizingira kitanda kizima na hakumuona Nadia Joseph alipo. Akaamua kukisogele kitanda kile taratibu lakini ghafla akapigwa dhoti Kali na kudondoka chini puuuh! Kama mzigo. Na kila alipojaribu kuinuka alishindwa.. Hofu ikamjia akajua tayari amekamatwa kwenye mtego....





    DORICE alikuwa akiyatafakari maneno ya malkia wa himaya aliyokuwepo kwa wakati ule. Alikuwa haelewi afanye nini na achague lipi kati ya kifo au kuolewa na jini. Alijikuta yupo kwenye wakati mgumu sana mpaka akajuta kutoroka shuleni. Alimlaani sana Doreen kwani ndiye chanzo cha matatizo yote. Alijikuta analia bila kujua msaada wake utatoka wapi.



    Akiwa katika wimbi la mawazo alishtushwa na harufu Kali ya marashi iliyomfanya azinduke na kumtazama mgeni wake. Alipoinua kichwa chake alikutana tabasamu mwanana kutoka kwenye sura nzuri ya upole ya kijana Mansoor.



    "Nakupenda Dorice.. Olewa na Mimi!" Alisema mansoor kwa sauti tamu iliyojaa huba. Lakini sauti na maneno hayo habvikuwa kitu kwa Dorice, aliachia sonyo Kali iliyodhihirisha chuki kuu dhidi ya Mansoor.



    "Kama kuniua niueni! Siwezi kuolewa nawewe!" Dorice alisema maneno hayo kwa ujasiri sana bila kujali jambo hilo lingeonekanaje kwa Mansoor.

    Mansoor alihuzunika sana, akatikisa kichwa kama ilivyokuwa kawaida yake . Akashindwa kuyazuia machozi ya damu machoni mwake lakini Dorice hakujali hilo.

    "Dorice! Kwanini haunipendi? Au kwa sababu Mimi sio binadamu mwenzio?" Aliongea Mansoor kwa huzuni sana lakini Dorice hakujibu kitu.



    "Tafadhali niambie Dorice... Nikufanyie nini ili uamini kuwa nakupenda?" Aliuliza mansoor kwa sauti ya upole.

    "Utanifanyia?"

    "Ndio Dorice!"

    "Naomba unirudishe duniani..."

    "Nikikurudisha sasa nitakuoaje? Siwezi ishi mbali nawewe!"

    "Umesema utanifanyia nikuombacho.. Umeniahidi!"

    "Ndio ila hilo suala gumu... Kwanini hunipendi?"CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nampenda mtu mwingine.. Na ndie aliyenifanya nipate matatizo haya yote.." Dorice alisema maneno hayo huku machozi yakimlengalenga kwani kila alipomkumbuka Eddy alidondosha chozi na hakutaka kuamini kama Kweli Eddy amemwacha na yupo na Doreen.

    "Unampenda nani?"

    "Nampenda mtu anaitwa Eddy, siko tayari kimkosa nataka nipiganie penzi langu... Samahani sana Mansoor... Wewe ni mzuri ila sins hisia na wewe kabisa!" Dorice alijikuta akiropoka maneno hayo yote ili kufikisha hisia zake kwa Mansoor. Maneno Yale yaliugusa vyema moyo wa Mansoor, alihuzunika sana ila ilibidi akubaliane na ukweli.

    "Nashukuru kwa kuwa mkweli Dorice.. Nakupenda sana ila siwezi kukulazimisha unipende... Hakutakuwa na mapenzi hapo.. . Naumia sana ila inabidi nizielewe hisia zako!" Alisema Mansoor kwa sauti iliyojaa masikitiko makubwa sana ila hakuwa na jinsi. Mansoor alikuwa ni mini mstaarabu kupita kiasi ingawa mama take alikuwa katili tena mwenye roho mbaya sana.



    "Umenielewa Mansoor?!"

    "Ndio.. Nimekuelewa sana! Ila nisimulie ilikuwaje?"

    Dorice alifuta machozi na kutabasamu kidogo ingawa bado alikuwa na maumivu ya mapenzi kwa Eddy. Akajua ule ni msaada wa kwanza kwake kwenye eneo lile, akaamua kumsimulia kila kitu kama ilivyokuwa kati ya yeye na Eddy na kisa cha kutoroka.



    Mansoor alihuzunika sana, akamwonea huruma sana Dorice.

    "Binadamu wabaya sana..!"alisema Mansoor.

    "Inaniuma sana! Nampenda sana Eddy..!"!



    Mansoor alichukua kitu kama kioo, akakitazama kwa muda kisha kikamletea picha ya Doreen.

    "Mh! Huyu Doreen.. Ni mtu mbaya sana .. In mtu hatari kupita kawaida..!"



    Alisema Mansoor kwa mshtuko huku akimtazama Dorice. Dorice alikuwa haelewi chochote akabaki akishangaa tu.

    "Doreen ni mchawi sana.. Na kuna kitu anatafuta! Amemharibu sana Eddy... Eddy yupo kwenye wakati mbaya na muda wowote anammaliza..!"



    Maneno ya Mansoor yalimshtua Dorice

    "Amemfanyaje? Nisaidie kumwokoa Eddy tafadhali..!"

    "Mama hatanikubalia ila inabidi nikusaidie Dorice.. Yote ni kwasababu nakupenda.. Nitakusaidia usijali!"

    Alisema Mansoor.

    "Nitafurahi sana ukinisaidia Mansoor!"

    "Usijali.. Ila mama ni kikwazo..!"

    "Jitahidi Mansoor!"

    Dorice alichanganyikiwa sana baada ya kusikia kuwa Eddy atauliwa muda wowote na Doreen, ilibidi azidi kumsihi Mansoor aweze kumsaidia kwa namna yoyote ile kwani alitambua uwezo mkubwa aliokuwa nao jini yule mstaarabu.



    ******

    Doreen alibaki pale chini kwa muda mrefu sana akishindwa kutoka mle ndani.

    Alihangaika sana mpaka kijasho kikaanza kumtoka kwani aliziona kabisa dalili za kufamwa, aliwaza aibu ambayo ingemkuta hakujua afanyaje.



    Akiwa katika harakati hizo za kutaka kuondoka akahisi moto mkali ukimpitia, akapiga kelele za maumivu huku akigalagala pale chini. Chumba kizima kilikuwa kimya sana kwani wanafunzi wote walikuwa wamelala fofofo na hakuna aliyeweza kusikia kilio kile.



    Doreen aliteseka sana na tangy aanze uchawi hakuwahi kukumbana na hali ile.



    Aliona uchawi sasa ni wa mateso, kwani maumivu aliyokuwa anayapata hayana mfano.



    Doreen alijitahidi kufanya kila awezalo ili aweze kutoka ndani ya bweni lile lakini halo ikazidi kuwa mbaya. Ghafla akasikia mtu akikohoa akajua mwisho wake umefika. Akaanza kuropoka maneno yake ya uchawi ili aweze kutoka hatimaye akafanikiwa. Ikawa ahueni yake ingawa mwili wote ulikuwa unamuuma vibaya sana.



    Alifika kwenye kichaka ambacho aliacha vitu vyake, akajibwaga kama mzigo huku akiugulia maumivu. Aligalagala pale chini kwa muda wa SAA zima hatimaye maumivu yakapungua. Akaamua kurudi bwenini kulala.



    Alinyatanyata mpaka alipokifika kitanda chake. Alilala huku akimfikiria Nadia.



    "Mh! Huyu mtu si wa mchezo dah!" Alijisemea Doreen kimoyomoyo, kwa maumivu aliyoyapata hakuweza hata kuinuka kitandani.

    " Nitafanyaje Mimi? Siku zimeisha sana sasa lakini bado kitu kimoja tu, titi la msichana mzuri! Nitapataje sasa?" Alijiuliza Doreen bila kupata majibu.

    "Enhe! Inabidi nifanye kitu.. Nimtumie MTU..!" Doreen alipata wazo kuwa inabidi amtumie mtu ili kupata titi hilo ili akamilishe mambo aliyoyahitaji. Lakini asingeweza kufanya kwa usiku ule kwani alikuwa hoi bin taabani.



    Usingizi ukampitia kidogo na kwakuwa ilikuwa SAA kumi na nusu hakulala sana kengele ya kuamka ikamshtua.

    Kulikuwa tayari kumekucha. Doreen alikuwa hana nguvu kabisa mwilini na mwili wake ulikuwa bado unamuuma hivyo akashindwa kwenda darasani kwa madai kuwa alikuwa mgonjwa. Ila moyoni alimwogopa sana Nadia na hakutamani hata kumwona kwani alimuonea aibu.



    Wanafunzi wote walienda darasani isipokuwa Dorice, alibaki bwenini na alitaka kuitumia nafasi ile vizuri ili amtumie mtu kutafuta titi la msichana mzuri wa kuvutia.



    ******

    Wazazi wa Eddy walishika njia kutokea mkoani Iringa kuelekea pangani Tanga.

    Walikuwa na matumaini mazito ya kumpata mganga mashuhuri aitwaye Tembo wa Bahari.

    Hawakua na wasiwasi wowote juu ya mganga huyo kwani tayari walikuwa wamezisikia sifa zake kuwa yupo vizuri sana katika suala la matibabu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Eddy alikuwa ametulia kimya ndani ya gari lile ambalo dereva alikuwa ni Mr.Alloyce.

    Kila Mara aliyakumbuka maneno ya Doreen kuwa endapo watafika kwa mganga basi uhai wake utakuwa umefikia kikomo. Kuna wakati aliyapuuzia mawazo hayo lakini wakati mwingine alihisi yana ukweli ndani yake, kama Doreen aliweza kumtoa sehemu zake nyeti atashindwa kumuua? Alijiuliza Eddy.

    Ukimya ulitawala ndani ya gari lakini kelele nyingi zilitawala kichwani mwa Eddy kwani mawazo yalikuwa hayakauki kichwani mwake

    "Mama!" eddy aliita.

    "Sema mwanangu..!"

    "Nina njaa!"

    "Ngoja nikupe chakula..!"

    Mama Eddy alichukua hotpot na kumtolea mapaja ya kuku yaliyokaushwa vizuri pamoja na chipsi mayai zilizoshikana vizuri.

    "Chukua ule.."

    "Sawa! Ila nipe chakula!"

    "Mh! Chakula hicho!"

    "Hicho siwezi kula maana kina uchafu..!"

    Alisema Eddy maneno yaliyomchanganya sana mama yake kwani kila alipotazama chakula kilikuwa kizuri tu.

    "Hakuna uchafu..!"

    "Upo!"

    Eddy alisisitiza na Mara hiyo akaanza kuhisi kichefuchefu.

    "Mama simamisheni gari nataka nikatapike nje.."alisema Eddy. Kwa haraka Mr.Alloyce alisimamisha gari wakamtoa nje Eddy ili akatapike.

    Eneo like lilikuwa na miti mingi kwani lilikuwa pori. Eddy aliwatazama wazazi wake, kisha akasogea kando kidogo.

    Akawatazama tena kwa jicho la wizi , akajiweka sawa kisha bila wazazi wake kutarajia akatimua mbio Kali kuelekea porini.

    Wazazi wake wakapigwa butwaa sana wakashindwa wafanye nini wakabaki wamezubaa huku wakitazama kwa mshangao. Eddy alikuwa tayari amewapotea machoni mwao kwani mbio alizokuwa akikimbia zilikuwa za MWENDOKASI.....



    ..DOREEN alikuwa bado hana hali nzuri kiafya, mwili wake ulikuwa hauna nguvu kabisa kwani ile adhabu aliyoipata usiku ilimwadhibu haswa. Alijikuta anamwogopa Nadia kupita kiasi, moyoni mwake alikiri kuwa kweli Nadia Joseph alikuwa Mchamungu kweli.



    Wakati huo akiwa bado yupo kitandani akiugulia maumivu, Doreen alifikiria jinsi ya kuweza kupata titi la msichana mrembo ili akamilishe kazi yake aliyotumwa kuifanya. Siku zilikuwa zimeisha sana lakini alijipa moyo kuwa ameshamaliza kazi kwani kupata titi aliona kama kazi rahisi tu ingawa ilishaanza kupata vikwazo.



    Doreen alishuka kitandani kwake. Akavua nguo zote kisha akasogelea begi lake na kuchukua shanga nyeusi akaivaa shingoni mwake.



    Na kwakuwa alikuwa peke take chumbani mle Doreen alifanya mambo yake bila woga. Akachukua kichupa kimoja kidogo kwenye begi lake halafu akamimina kidogo unga unga uliokuwamo mle na kujipaka usoni kisha akapiga magoti chini na kuinamisha kichwa chake huku akitamka maneno Fulani.



    Ghafla karatasi ambayo ilifanya mauaji ya walimu ofisini ikamjia mkononi make.Ikumbukwe kuwa karatasi ile ilichukuliwa na mwalimu Jason ambapo kulikuwa na maandishi yaliyomuonya kuwa asimpe mtu mwingine, hivyo Mwalimu Jason aliamua kukimbia nayo na alikuwa akikaa Nayo kwa siku zote zile.



    Doreen alitabasamu baada ya kuitazama karatasi ile, akaishika vizuri kwa mikono miwili kisha akasema "NENDA KWA MWALIMU JASON! MWAMBIE ANILETEE TITI LA MSICHANA MREMBO! NAKUAMINI!" alisema Doreen kisha akaiachia karatasi ile, ikapaa hewani na ikapotea.



    Doreen alifurahi sana akajua tayari amekwisha maliza kazi yake. Akiwa bado ameketi pale chini akiendelea na mambo yake mengine ghafla mlango wa bweni lake ukagongwa halafu akakumbuka kuwa hakuubana mlango ule vizuri kwa komeo Doreen alishtuka sana kwani alikuwa mtupu na alikuwa na maunga unga usoni. Akahisi fumanizi la uchawi tayari limemfikia.



    ********

    Mansoor alikubali kumsaidia Dorice ili kumwokoa Eddy lakini bado moyo wake ulimuuma sana. Hakuwa radhi kumwacha binti yule kirahisi pasina kumuoa ilhali moyo wake ulizimia kwa mapenzi kwa mrembo yule. Mansoor alimpenda sana Dorice hivyo akajiona bwege sana kumwacha msichana yule aondoke kwenye himaya yao wakati moyo unamhitaji.



    "Mwanamke anahitaji kubembelezwa! Nikimbembeleza sana anaweza kunikubali.... Yawezekana anamuogopa mama yangu kutokana na vitisho alivyompa... Mhh nitajaribu tena bahati yangu kwani moyo wangu hautakuwa na amani kabisa nikimuacha Dorice!" Aliwaza Mansoor akiwa ametulia peke yake kando ya Maua mazuri yanayotoa harufu ya kuvutia. Aliwaza sana juu ya kumpata Dorice lakini bado hakuona njia sahihi ambayo ingekubalika haraka zaidi ya kumshawishi tu huba na kumbembeleza kwa mahaba.



    Akiwa katika wingu hilo zito la mawazo Mansoor alishtushwa na upepo mkali. Akajua moja kwa moja mama yake alikuwa njiani kwani upepo ule zilikuwa in hatua za Malkia. Punde si punde malkia akatia timu na kuketi kando ya Mansoor.



    "Vipi mwanangu? Mbona unasononeka sana kiasi cha kuondoa amani ya moyo wangu?"

    "Hakuna tatizo mama!" Alijibu Mansoor huku akijaribu kuachia tabasamu.

    "Unanificha Mansoor.. Au yule binadamu asiyejaa hata kiganjani bado anakusumbua?"

    "Hapana mama.. Hana tatizo lolote na anaonesha moyo wa kunipenda!" Ilibidi Mansoor amdanganye mama yake kwani alijua madhara ambayo angemfanyia Dorice kama angemweleza ukweli.

    "Kweli?" Malkia alifurahi.

    "Kweli mama yangu.. Malkia mtukufu..!" Alitabasamu Mansoor ingawa moyoni aliumia.

    "Vizuri sana... Nadhani furaha yako itarejea sasa!"

    "Ndio mama wala usiwe na wasiwasi!"

    Malkia aliondoka zake akiwa ameghairi lengo lake la kumwangamiza Dorice. Kwani alipanga kuondosha uhai wake endapo angekataa kumpenda Mansoor.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mansoor alimfuata Dorice kwenye chumba alichokuwa anaishi. Aliingia chumbani mle akiwa amemletea zawadi ya maua mazuri yanayonukia vizuri sana. Alipoingia tu, akasikia sauti ya kilio kutoka kwa Dorice. Mansoor akashtuka kidogo kisha akamsogelea taratibu Dorice.



    "Unalia mini Dori?"

    "Nataka nirudi nyumbani... Wazazi wangu watakuwa wananitafuta sana..!"

    "Usilie Dorice...!"

    "Siwezi kuzuia maumivu yangu juu ya wazazi wangu Mansoor... Pia namfikiria mpenzi wangu..!"

    "Nyamaza Dorice.. Nitakusaidia kwa yote hayo... Hebu nitazame!" Mansoor alimkazia macho Dorice kisha akamkabidhi Maua aliyokuwa ameyashika.

    "Yanini..?"

    "Usijali.. We pokea tu.."

    Dorice aliyapokea maua Yale huku akisitasita sana. Baada ya kuyapokea mansoor alitabasamu sana.

    "Asante kwa kupokea zawadi yangu Dorice... Nakupenda sana!" Dorice hakujibu kitu zaidi ya kumshangaa Mansoor.

    "Nataka nikusaidie... Upo tayari..?"

    "Nipo tayari Mansoor tafadhali.."

    "Sawa Dorice.. Kabla sijakusaidia nahitaji unisaidie kitu.."

    "Kitu gani!?" Dorice alishtuka sana.

    "Nataka uolewe na Mimi.. Tafadhali Dorice... Nitakusaidia kwa lolote utakalo ukikubali kuolewa na Mimi..!"

    "Mansoor! Nilishakwambia nampenda Eddy..."



    "Ukikubali kuolewa na Mimi nitakusaidia kumpata Huyo Eddy na nitakuruhusu uendelee Naye... Nakuomba Dorice! Ilidhishe nafsi yangu!" Alisema Mansoor huku akipiga magoti.



    *******

    Mwalimu Jason alikuwa akisumbuliwa sana na karatasi lile alilolichukua ofisini baada ya kifo cha Mwalimu Mbeshi. Halikutakiwa kuonekana na MTU yeyote wala kuguswa na maji.



    Lilikuwa likimchanganya sana kichwa kwani kila siku lilikuwa likibadili ujumbe na kuandika masharti mapya.Siku hiyo asubuhi mwalimu Jason kutokana na kutokwenda kazini aliamka asubuhi na mapema ili afue nguo zake.



    Alikusanya nguo chafu zote na kuziweka kwenye beseni la kufulia lenye maji na sabuni. Na alikuwa na uhakika kabisa kuwa karatasi halikuwa kwenye nguo zile. Akaanza kufua nguo zake kwa umakini ili azitakatishe ndipo alipogundua kuwa suruali yenye karatasi lile la maajabu ipo ndani ya beseni la maji.



    Kengele ya hatari ikagonga kwa kasi moyoni mwake, akaipoa suruali ile huku mapigo yake ya moyo yakimpiga kwa kasi.



    Akaanza kutafuta karatasi lile kwenye mifuko ya suruali ile. Hofu ikamzidia maradufu baada ya kutafuta kila mfuko na kulikosa karatasi lile.



    Mwalimu Jason alichanganyikiwa sana, ikambidi aanze kupekua suruali zake zote na kutafuta vizuri karatasi lile alikuwa akiliita karatasi la kifo kwani kila mara lilikuwa likimuonya kuwa akikosea sharti basi lazima afe.



    Mwalimu Jason alipekuwa kila suruali aliyokuwa ameiloweka kwenye maji lakini bado hakuona karatasi akazidi kuchanganyikiwa.



    Alizitupa chini nguo zote kisha akaingia ndani na kuanza kupekua kwenye kila suruali lakini bado hakuona karatasi lile. Mwalimu Jason alipigwa na butwaa. Kijasho chembamba kikaanza kumtoka kila kona ya mwili wake. Akajitupa kitandani na kuanza kulia kwa woga. Alijua tayari kifo kiko mbele yake si muda mrefu.



    Ghafla simu yake ikaita na kwakuwa alikuwa kwenye kilio hakuweza kupokea simu. Akaicha tu bila hata kuingalia.



    Lakini kwa bahati njema aliona karatasi ikiwa pembeni ya mto wake wa kulalalia. Mwalimu Jason alifurahi kisha akaichukua karatasi ile na kusoma ujumbe mpya ulioandikwa hivi "MSICHANA YEYOTE ATAKAYELALIA KITANDA HIKI.. UNATAKIWA UMKATE TITI LAKE LA KUSHOTO HARAKA IWEZEKANAVYO. LASIVYO UHAI WAKO UTAFIKIA KIKOMO!"



    Mwalimu Jason akatumbua macho kwa mshangao. Akarudia kusoma ujumbe ule mara mbilimbili lakini hakuna kilichobadilika. Akahisi mwili wake unaishiwa nguvu kabisa kwani Siku ile alikuwa na miadi na mpenzi wake. Alijiuliza atafanya nini hakuwa na la kufanya.Simu take ikaita tena akaitazama ilikuwa ni namba ya mpenzi wake. Akapokea.



    "Baby mbona hukupokea simu?"

    "Ulipiga?" Jason alijifanya kama hajui lolote kama simu ilipigwa.

    "Kwani hukuona? Ok.. Nipo njiani nakuja!"

    "Eeeh!" Jason alishtuka sana.

    "Vipi mbona unashtuka?"

    "Ah..una.. Naomba usije home Leo.. Kama vipi tukutane Hotelini.."

    "Hivi Jason una akili timamu wewe? Hapo kwako kuna nini? Au una MTU mwingine?"

    "Sina MTU mwingine baby.. Ila.." Jason alitamani kujitetea ila hakuweza kufanya hivyo.

    "Nitoke Dar kuja Iringa kwaajili yako halafu uniletee hizo habari zako.. Kwani tulikubaliana nini?" Msichana yule alimjia juu mwalimu Jason

    "Usipaniki baby basi.. Hotelini ni kuzuri pia..!"

    "Kama una michepuko yako basi tutajua..!"

    Msichana yule akakata simu.



    Mwalimu Jason alijiona ana mtihani mkubwa sana. Aliwaza na kuwazua lakini bado hakupata jibu. Majira ya SAA Kumi na nusu jioni mlango uligongwa. Mwalimu Jason alienda kufungua akakutana USO kwa uso na sura ya Judith ambaye ni mpenzi wake akiwa amenuna sana.



    Mwalimu Jason hakuwa na la kufanya zaidi ya kumkaribisha Judith ndani.Waliposalimiana tu Judith akaingia chumbani kwa mwalimu Jason ili akaweke mizigo yake.Lakini kila alipomtazama Mwalimu Jason, hakuwa na furaha hata kidogo.



    "Mbona hujanifurahia?"CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliuliza Judith

    "Nipo kawaida.. !" Alijibu mwalimu Jason.

    "Ok basi ngoja nikapumzike kidogo maana nimechoka kweli..!" Alisema Judith huku akipiga hatua kuelekea kitandani...



    . MANSOOR alimtazama Dorice kwa jicho la kiulizo lililomtaka azungumze chochote lakini Dorice hakusema neno zaidi ya kuangua kilio cha huzuni baada ya kukosa msaada kwa Mansoor. Dorice alilia sana kwani alijua kurudi tena duniani sasa ni ndoto.



    "Mansoor naomba unisaidie!" Dorice alipiga magoti akamsihi Mansoor aweze kumsaidia ili arudi kwao pia amsaidie kumwokoa Eddy ili furaha ya penzi lake irudi.



    "Dorice! Naweza kukusaidia kwa yote hayo... Ila inabidi ukubali kuolewa na Mimi maana bila hivyo mama yangu hatonielewa...!" Mansoor alisisitiza.

    "Siwezi kuolewa na wewe..!"



    "Kwanini? Au kwa vile Mimi sio binadamu mwenzio? Jua nakupenda na nitakuruhusu kuendelea na Eddy.. Nielewe Dorice!" Mansoor alizidi kumweka Dorice katika wakati mgumu sana. Kwani kiukweli Dorice aliuhitaji msaada wa Mansoor ila masharti yake yalikuwa kikwazo sana. Dorice alishindwa kung'amua juu ya mtihani ule mzito. Alijua fika wazazi wake wataumia sana endapo wakijua kuwa Hayupo duniani, aliyafikiria maumivu ambayo mama yake angeyapata kama yeye angepotelea kule kwenye ulimwengu wa majini.



    "Sijui nimkubali halafu akinirudisha duniani nimkatae?" Dorice Alizidi kuwa na utitiri wa mawazo kichwani mwake. Ghafla akashtushwa na sauti nzuri ya mahaba ya Mansoor akizidi kumshawishi kuwa amkubalie ili aweze kumsaidia kutatua matatizo yake.



    "Dorice! Nifanye nifurahi tafadhali.. Nilipendwa na wengi ambao si chaguo langu.. Nasikitika chaguo langu linakuwa mwiba moyoni mwangu! Kwanini lakini?"



    Dorice alivuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu, huku akiwa ameinamisha kichwa chake. Taratibu akanyanyua kichwa chake na kumtazama Mansoor. Macho yake yalistaajabu uzuri wa asili aliokuwa nao kijana yule. Hata kama majini ni wazuri lakini Mansoor alizidi kipimo, kuanzia macho yake, pua yake na midomo mizuri ya kupendeza sana.



    "Nimekubali Mansoor! Ila kabla ya yote naomba uniahidi kama utanisaidia!" Alisema Dorice kwa sauti iliyotulia sana. Maneno hayo yalifungua ukurasa mpya moyoni kwa Mansoor, alifurahi kupita kiasi akamkumbatia kwa nguvu Dorice.



    "Nakuahidi kukusaidia Dorice!" Alisema Mansoor akiwa amemkumbatia Dorice.

    Walikumbatiana kwa muda kisha wakaachiana. Mansoor akamtazama Dorice huku akitabasamu.

    "Nataka uvae vizuri nikupeleke kwa mama yangu muda huu!"

    "Nitavaa nini? Sina nguo!"



    Alisema Dorice kwa woga huku moyo wake ukimsuta kwa kumsaliti Eddy kwani alikwisha muahidi kuwa hatokuwa na mwanaume mwingine yeyote zaidi yake."lakini ni kwa sababu yake..!" Alijipa Jibu Dorice.



    "Unapenda nguo gani?" Aliuliza Mansoor.

    "Nguo yoyote itakayonifaa!" Alijibu Dorice.

    Mansoor alinyoosha mkono juu ghafla ukatokea mfuko mmoja wenye ukubwa kiasi kisha akamkabidhi Dorice. Dorice aliogopa sana, akasita kupokea.



    "Usiogope.. Chukua!"Dorice akapokea mfuko ule japo kwa woga kisha akaufungua ili atazame kilichomo. Akapigwa na bumbuwazi.

    *****

    Eddy aliwaacha wazazi wake barabarani pale wakiwa hawaelewi la kufanya. Walibaki wanatazamana kwa muda wa dakika tano nzima bila kusema neno lolote. Kila mmoja alionekana kutoelewa kilichotokea.



    "Mr. Alloyce.. Tutakuwa wazembe tena wajinga... Mtoto ameondoka tumesimama tu kama milingoti hapa!" Alisema mama Eddy.



    "Tufanyeje mke wangu?"

    "Tumfuate!"

    "Tutamfuata wapi sasa?"

    "Kokote, kwani we hujaona alikokimbilia?"

    "Dah! Tuna mtihani mzito!"



    Ilibidi waingie msituni na kuanza kumsaka Eddy. Walimtafuta kila kichaka lakini hawakuona hata dalili za uwepo wa kijana wao. Jua liliwawakia huku wakizidi kumtafuta Eddy lakini bado hawakuona hata dalili za kumpata.



    "Hili tatizo la kimwendokasi dah!" Alisema baba Eddy.

    "Inabidi tulitatue kimwendokasi!"alijibu mama Eddy akiwa ameshika mkono kiunoni. Anahema kupita kiasi kutokana na uchovu aliokuwa nao.

    "Mke wangu!"

    "Abee.."

    "Mimi naona turudi tu nyumbani hapa tutafanya kazi bure!" Alishauri Mr.Alloyce

    "Nilishasema wewe humpendi mwanangu.. Turudi nyumbani halafu?"



    Mama Eddy alimjia juu mumewe, akaona kama hana mapenzi wala uchungu kwa mwanae lakini baba Eddy alikuwa sahihi kabisa kwani mpaka pale walipofikia wasingeweza kumpata Eddy. Walikuwa wamechoka sana, pia wasingeweza kusonga mbele zaidi kutokana na ukubwa wa msitu waliokuwamo.



    "Sikiliza mke wangu.. Nataka turudi tutafute njia sahihi ya kumtafuta mtoto hapa tunazidi kupoteza muda!" Kwa shingo upande mama Eddy aliamua kusikiliza ushauri wa mumewe. Wakatembea umbali mrefu sana mpaka walipolifikia gari lao.

    Walipofika kwenye ile gari, kengele ya hatari iligonga mioyoni mwao wakatazamana kwa mshangao lakini hawakuwa na la kufanya kwani gari yao ilikuwa ikiteketea kwa moto mkali utadhani imemwagiwa petroli.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nini hiki?" Walijiuliza kwa pamoja bila kupata jibu la haraka. Ilibidi wasogee kwa ukaribu ili wahakikishe wakionacho. Ni kweli gari yao ilikuwa ikiwaka moto, na alikuwa hatua za mwisho kiasi kwamba hata wangezima moto ule bado gari yao isingesalimika.



    "Haya maajabu!"

    "Tena maajabu haswaaa ya ulimwengu..!"

    Wakiwa bado wanaendelea kushangaa ajali ile ya moto kwenye gari ile, ghafla moto ukazima kama vile umezimwa kwa maji halafu gari ikatoweka machoni mwao.

    Waliogopa kupita kiasi wakajikuta wanatimua mbio bila kutazamana.



    Walikimbia sana wakiifuata barabara, kwa bahati mbaya mama Eddy alijikwaa na kuanguka chini kama gunia. Damu nyingi zikaanza kumtoka mguuni. Akapiga kelele Kali za maumivu, zilizokatisha mbio za Mr.Alloyce. akageuka nyuma na kumwona mkewe akivuja damu nyingi sana. Akarudi haraka.



    "Vipi mke wangu?"

    "Nime..nimeumia Mme..wangu..!" Mama Eddy aliongea kwa shida sana kwani alipata maumivu makali sana.

    Walikuwa hawana hata mia mbovu mifukoni mwao kwani pesa zote waliziacha kwenye gari ambalo limepotea kimaajabu.

    "Mke wangu" aliita baba Eddy baada ya kuona mkewe anakoroma isivyokawaida.

    "Mama Eddy..!!!!!!"

    *****

    Mwalimu John alikuwa bado anatokwa na funza mguuni, alitaka kuieleza familia take juu ya kile kilichompata lakini pindi alipotaka kuiambia familia yake juu ya mkasa ule mzito ghafla akapigwa Kofi zito lililomrusha kama shoti ya umeme kutoka juu ya kiti mpaka chini. Alipiga yowe Kali lililowashangaza watu wote sebuleni pale. Waliogopa sana.



    Leyla mke wa Mwalimu John alimsogelea mumewe na kumwangalia kama yupo salama ghafla akapigwa na mshangao ulioambatana na furaha kwani miguu ya mwalimu John ilirudi katika hali ya kawaida na haikuwa na funza tena.

    "Mume wangu!" Aliita Leyla kwa Furaha, lakini John aliendelea kulalamika pale chini kwani Kofi alilopigwa lilikuwa zito kuzidi uzito wa mwili wake lakini hakujua limetoka wapi.



    "Jamani.. Njoo muone maajabu..!"

    Alisema Leyla akiwaambia ndugu wengine wa mumewe.Wote walimsogelea na kushangaa kilichotokea, wakakiri kwamba kweli dunia ina maajabu tena yanayotisha na kuogopesha.



    Mwalimu John aligalagala pale chini kwa muda wa kama robo saa kisha taratibu akainuka. Alipotazama miguu yake aliifurahia sana kwani ilikuwa imerudi kwenye hali yake ya kawaida. Akainuka pale chini na kumkumbatia kwa furaha. Lakini cha ajabu kila alipotaka kuzungumza chochote..



    *****

    Doreen alibaki ametulia kimya pindi mlango unagongwa. Aliona anachofanya ni ujinga ni heri ainuke avae nguo kabla hajafumwa. Alipoinuka tu mlango ulifunguliwa. Doreen alishtuka sana kwani alikuwa yupo uchi wa mnyama na alikuwa amevaa shanga huku usoni amejipaka maungaunga na kumfanya awe na mwonekano wa kutisha.



    Madamu Amina akiwa ameambatana na nesi wa shule walishtuka sana kukmkuta Doreen akiwa vile. Walitazamana kwa mshangao kisha wakamtazama Doreen kwa hofu.



    "Doreen unafanya nini?" Aliuliza Madam Amina kwa woga ingawa alikikaza tu. Doreen alibaki kimya tu bila kujibu chochote. Macho ya Madam Amina yalitua moja kwa moja kwenye kile kichupa cha dawa kilichokuwa pale chini tena kilikuwa kimefungwa kijitambaa kidogo cha kaniki kwa juu. Kiliwatisha sana.



    "Doreen! Unafanya nini? Mbona hujibu?" Alisema nesi kwani walikuwa wamefikishiwa taarifa kuwa Doreen ni mgonjwa ndio maana amebaki bwenini.



    .MAMA Eddy aliendelea kukoroma kwa nguvu pale chini na kuzidi kumchanganya sana mumewe Mr.Alloyce. Mwanaume yule alichanganyikiwa haswa na kujikuta akiangusha chozi lake kwa uchungu kwani alishindwa kuielewa hali ya mkewe. Alimuita Mara kadhaa lakini Mama Eddy aliendelea kukoroma tu bila kujibu neno.



    Mr.Alloyce akazidi kuchanganyikiwa sana bila kuelewa afanye nini na kwa wakati ule hakukuwa na msaada wowote katika eneo lile. Akachukua simu yake na kuitafuta namba ya rafiki yake haraka kisha akapiga lakini alipopiga tu akakutana na maandishi haya " Emergency call only" ndipo akagundua kuwa sehemu aliyokuwapo haikuwa na mtandao, akazidi kuogopa huku huzuni ya kupotelewa na mkewe ikimvaa kwa kasi ya ajabu. Kwa muda wote huo hakuna gari yoyote ilipita eneo lile.



    "Na..na..nakufa..nakufa mume ..wangu.." Ilisikika sauti ya mama Eddy.Sauti ile ya mama Eddy ilikuwa kama mwiba mchongoma uliopenya katikati ya moyo wa Baba Eddy. Hakuamini kile alichokisikia kwa mkewe akahisi ilikuwa ndoto tu isiyokuwa na ukweli wowote.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog