Search This Blog

MWANAFUNZI MCHAWI - 3

 







    Simulizi : Mwanafunzi Mchawi

    Sehemu Ya Tatu (3)



    "Usife mke wangu.. Usife mpenzi wangu!" Aliropoka Mr.Alloyce lakini tayari alikuwa amechelewa sana kwani mkewe alikuwa tayari amekata roho.



    "Mke wangu! Mke wangu!" Baba Eddy alijaribu kumuita mkewe lakini tayari alikuwa ameaga dunia. Simanzi ilimjaa Mr. Alloyce alijkuta Analia kama mtoto mdogo huku akijigaragaza chini kama mwendawazimu. Alilia kwa uchungu sana kwani alimpenda mkewe kwa dhati na hakuwa tayari kumpoteza. Alikuwa ndiye ndugu yake pekee aliyesalia kwani Mr.Alloyce hakuwa na kaka, Dada wala wazazi.



    Wakati akiwa ameushikilia mwili wa mkewe ghafla akajikuta hajashika chochote mkononi mwake zaidi ya gauni alilokuwa amevaa mkewe, ndilo pekee lililombakia mkononi. Akashtuka sana, akajaribu kupepesapepesa macho huku na kule ili aone mkewe ameenda wapi lakini hakumuona. Mr. Alloyce akainuka pale chini haraka na kuanza kutimua mbio kwani alishaona hali si shwari.



    Alikimbia kwa muda mrefu bila kujijua anakimbiaje mpaka pale fahamu zake halisi zilipomrudia ndipo akasimama kidogo na kupumzika. Alihema kwa nguvu huku akiwa amejibwaga chini ghafla akasikia mlio mkali ukimjia nyuma yake. Mr.Alloyce akainuka chini na kuanza kukimbia tena lakini akiwa katika mbio hizo akapata ufahamu tens akasikiliza tena ule mlio akagundua ni mlio wa honi ya gari.



    Akaamua kusimama ili aombe msaada. Baada ya muda ya sekunde kadhaa basis la abiria likitokea Dar es salaam lilikaribia mahali alipo Mr.Alloyce ndipo alipoanza kupunga mkono ili aombe msaada.



    Dereva wa basi lile alikuwa mwelewa sana, akasimamisha gari na kumsaidia Mr. Alloyce aliyekuwa akihema sana. Mr.Alloyce alishukuru sana akaingia ndani ya basi.



    "Vipi mbona umeshika gauni hilo mkononi?" Aliuliza kondakta baada ya kumkagua kwa macho Mr.Alloyce

    "We acha tu.." Alijibu Mr. Alloyce huku akihema sana.

    "Isije ikawa umeua huko halafu sisi tumekusaidia hapa...!" Alisema kondakta.

    Mr. Alloyce alikataa kwa kichwa tu kwani hakuweza hata kujibu kutokana na maswahibu yaliyomkuta.

    "Haya.. Unashuka wapi?"CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Naenda Ipogoro Iringa!" Alisema Alloyce na kuinamisha kichwa huku akilia.

    ******

    Doreen alishindwa la kufanya mbele ya mwalimu wake pamoja na Matron alibaki ameduwaa tu lakini cha ajabu hakuonesha aibu yoyote. Alijikausha kimya tu akiwatazama.Mwalimu Amina na Matron walomsogelea Doreen kwa woga.



    "Unaumwa nini?" Aliuliza Matron

    "Kichwa!"

    "Pole! Nakuletea dawa!" Alisema matron kwa sauti ya upole sana.

    "Asante" alijibu Doree kwa sauti ya chini kidogo ila kwa kujiamini sana.

    Matron na Madam Amina walitoka. Doreen aliinuka pale chini na kuvaa nguo zake kisha akajifuta madawa yake usoni.

    "Huku ni kudhalilika sana ingawa nimejikaza kisabuni, duh!" Aliwaza Doreen huku akirudisha vitu kwenye sanduku lake.



    Matron na madame walibaki na maswali mengi sana vichwani mwao. Kila mmoja alijiuliza kivyake lakini uvumilivu ukawashinda. Wakajikuta wameanza kuulizana ili wasaidiane kupata majibu wakati huo wakielekea kwenye dispensari ya shule kuchukua dawa.



    "Hivi we umemuelewa yule mtoto?" Aliuliza matron kwa sauti ya chini.

    "Mh! Nikajua we umemwelewa.. Sijamwelewa! Lakini nimepata jibu la kitu kimoja..." Alisema madam Amina huku akipunguza sauti na kumsogelea vizuri matron.

    "Nini tena?"

    "Nilisikia kuwa huyu binti ni mchawi na ndiye aliyesababisha majanga yote haya hapa shule na niliongea na afisa elimu kuhusu hilo.."

    "Mh! Afisa elimu hataelewa maana kama ujuavyo serikali haiamini uchawi!"Alisema matron.



    "Nilizongea nae kiutu tu.. Na Leo nimpata picha ya huyu mtoto kwenye simu..!"alisema madam Amina huku akifungua picha kwenye simu na kumuonesha Matron. Ilikuwa ni picha iliyomwonesha Doreen jinsi alivokuwa kule chumbani. Matron alishtuka kidogo kwa ujasiri aliokuwa nao madam Amina mpaka akampiga picha Doreen.



    "Nimeamua nimpige hii picha kama uthibitisho... Nimempiga kwa uangalifu sana ... " alisema madam Amina huku akimpigia simu Afisa elimu ili afike shuleni pale na waweze kumfukuza shule Doreen kama walivyokubaliana na Afisa Elimu.



    "Sasa mna vithibitisho?"

    "Hapa hakuna kutumia serikali la sivyo tutaisha... Huyu afisa elimu tumeongea mengi ambayo huwezi kuelewa..!"

    Alisema Madam Amina kwa kujiamini sana kisha matron akachukua dawa za kutuliza maumivu na kuelekea bwenini kwa Doreen. Njiani alikuwa akimpigia simu Afisa elimu lakini hakupatikana.



    Walifika bwenini ili wamkabidhi Doreen dawa. Lakini walichokikuta wakabaki wanatazama kwa mshangao wa hali ya juu.

    *****CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mwalimu Jason alitamani amzuie mpenzi wake Judith asilale kitandani kwake lakini hakuweza. Judith alikuwa tayari amejilaza kitandani kwa Jason.



    "Judith ndo tabia gani?"

    "Ipi? "

    "Umefika hata hajaongea chochote unalala? Kwanini?"

    "Kama huna muda na Mimi nifanyaje?"

    "Uvofanya sio bhana! Inuka basi njoo sebuleni.."

    "Sitaki!"



    Sijui ni shetani gani aliyempitia Judith siku ile maana alikuwa king'ang'anizi wa mambo kuliko kawaida. Licha ya mwalimu Jason kumkatalia kulala kitandani pale lakini Judith hakumwelewa hata kidogo.



    Mwalimu Jason alibaki kimya huku malumbanoakali yakiendelea kichwani mwake. Alikuwa haelewi aamue nini kati ya kifo chake au kukata titi la Judith. Alikuwa na mapenzi ya dhati sana kwa mwanamke yule lakini Leo hii shetani alitaka aingilie kati kuvuruga penzi lao. Mwalimu Jason alikaa chini machozi yakimbubujika. Judith aligundua kuwa mpenzi wake alikuwa Analia moyo wake ukashtuka kwani daima hakupenda kuona mpenzi wake akiwa katika halo ya huzuni.

    Akainuka kitandani na kumfuata Jason pale alipokuwa ameketi.



    "Baby! Mbona unalia?" Aliuliza Judith kwa sauti ya mahaba yenye kubembeleza. Lakini Jason hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kulia.



    "Nisamehr mpenzi nilikuwa nakutania tu.. Kwani hujazoea utani wangu baby?" Masikini Judith alianza kujitetea akidhani amemkosea mpenzi wake bila kujua kuwa uhai wake ulikuwa hatarini sana. Jason hakujibu kitu, akaendelea kulia tu na kumfanya Judith ajisikie vibaya sana na kuhisi kuwa alimkosea mno Jason. Judith akaendelea kuomba msamaha lakini ilikuwa kazi bure.



    "Hujanikosea!" Jason aliamua kimjibu Judith. Na wakati huo kuna sauti aliyoisikia masikioni mwake ikimwambia"Chukua titi haraka!" Jason akaongeza kilio.



    Sauti ile ilizidi kumsisitiza mpaka akajikuta anainuka na kutoka chumbani mle. Judith alibaki kajiinamia akijiuliza mini kimemkumba mpenzi wake. Ghafla akainua kichwa ns kumuons Jason akimjia huku ameshika kisu kikali sana.



    "Vipi baby?" Aliuliza Judith kwa mshangao.

    "Nakupenda sana.. Ila...inanilazimu!' Alisema mwalimu Jason huku akimsogelea Judith. Judith alitoa macho kwa hofu..



    ..DORICE alipozitazama zile nguo zilikuwa ni nguo nzuri sana za kuvutia. Kulikuwa na gauni moja refu linaloacha wazi mikono lenye rangi ya dhahabu inayong'aa sana. Kulikuwa na viatu virefu vinavyoelekeana na rangi ya gauni kidogo, ushungi wenye rangi ya gauni, mkufu wa dhahabu pamoja na hereni.

    Dorice alivishangaa vitu vile kwa mshangao wakati huo Mansoor alikuwa akiachia tabasamu mwanana pembeni yake.

    "Vaa Dorice!" Ilisikika sauti ya Mansoor ndipo Dorice alipopata nafasi ya kumtazama tena Mansoor. Akapigwa na bumbuwazi baada ya kuona mansoor amevalia nguo tofauti na alizokuwa amevaa mwanzo, alionekana kama mwanaume wa kihindi pale anapofunga ndoa kwa mavazi yake. Dorice alimshangaa sana Mansoor, woga kiasi ukamvaa moyoni mwake kisha akaanza kuzivaa nguo zile alizopewa na Mansoor.

    Pindi anapozivaa nguo zile Mansoor alikuwa tayari ameshatoweka eneo lile.Doricealipovaa nguo zile, alibadilika sana. Alionekana mrembo mno kwa jinsi alivyopendeza. Ukimtazama kwa haraka utadhani msichana kutoka India kumbe ni mnyaturu wa Singida.

    Alijitazama kupitia kioo kilichokuwa mbele yake, akajikiri kwamba kweli Mungu hakumkosea katika uumbaji ila alitumia ufundi wa hali ya juu katika kukamilisha sura na umbile lake.

    Bada ya kumaliza kuvaa, Mansoor alitokea tena palepale alipokuwa amesimama mwanzo. Alimshtua sana Dorice lakini tayari alikuwa ameshaanza kumzoea Mansoor hivyo hakuogopa sana.

    "Umependeza sana Malkia wangu.. Kwa jinsi ulivyositamani hata uende Duniani.. Nahisi wivu sana.." Alisema mansoor huku akimtazama mrembo yule kama waridi likiwa bustanini wakati wa jua la asubuhi.

    "Uliniahidi nini?" Aliuliza Dorice kwa hamaki."Usijali... Nitakupeleka duniani kama nilivokuahidi ila nimekuambia tu hisia zangu... Kama unanipenda kweli ni heri ubaki na mimi huku huku kwetu!" Alisema Mansoor kwa sauti ya upole sana. Dorice hakijibu kitu. Wakaondoka pale na kwenda moja kwa moja kwa malkia.

    Malkia alifurahi sana kuona kijana wake ameambatana na mtu ampendae. Radi tatu mfululizo zilipigwa ili kudhihirisha furaha aliyokuwa nayo malkia. Mansoor alitabasam akiwa amemshika mkono mkewe mtarajiwa.

    "Harusi ya mwanangu Mansoor... Iwe ya furaha sana kwani amepata kile alichokuwa anahitaji.." Alisena malkia kwa sauti kali. Dorice alimtazama Mansoor kwa woga.

    "Usiogope malkia wangu.. Na kuanzia Leo nitakuita Aisha..!"

    "Aisha! Kwanini?" Alihamaki Dorice.

    "Ukiwa mke wangu huwezi kuitwa Dorice.." Alisema Mansoor.

    Wakati Dorice akiendelea kushangaa ghafla upepo mkali ukapigwa, halafu kwa muda huohuo walijikuta wapo eneo lingine lililojaa watu wengi ambao Dorice hakuwaelewa elewa kwa jinsi walivyokuwa.

    ********

    Majira ya SAA moja jioni Mr. Alloyce alikuwa amewasili nyumbani kwake. Kichwa kilijaa mawazo tele ambayo hakujua yataisha vipi kwani matatizo aliyokuwa nayo yalikuwa nimazito kuzidi kilo mia za Mawe. Njia nzima aliwaza na kuwazua lakini bado alijiona yupo kwenye msitu mkubwa wa matatizo ambao hakujua atapenya vipi ili kuepukana nao.

    Kila Mara sura ya mkewe mpenzi ilimjia kichwani mwake hakuamini kama kweli amempoteza katika mazingira ambayo ilikuwa vigumu kuyaelewa. Alimfikiria mwanawe Eddy ambaye mpaka Dakika ile hakujua angeanzia wapi kumtafuta ilhali hajui alikoelekea!. Kichwa kilimgonga sana kwa mawazo.

    Alifika getini kwake na kumkuta mlinzi wake ambaye alimfungulia. Bila hata ya salamu Mr.Alloyce alipita getini pale na kuelekea ndani lakini alishtushwa sana kuona taa zinawaka ndani pia alisikia sauti kubwa ya muziki. Mr.Alloyce alisitisha mwendo wake kidogo. Akamgeukia mlinzi.

    "We Seba nani yupo ndani?"

    "Atakuwa Eddy Huyo.."

    "Eddy! Eddy gani?" Mr. Alloyce alishtuka sana.

    "Kwani kuna Eddy wangapi hapa Mzee..!" Alijibu Mlinzi Seba kwa masihara kwani alikuwa niMTU wa masihara sana.

    "Sipo kwenye utani ujue Seba.. Nani yupo ndani?.." Aliuliza kwa hasira mr. Alloyce kwani alihisi Seba anamtania.

    "Eddy Mzee.." Alijibu mlinzi.

    Mr.Alloyce alihisi kama nguvu zikimpungua mwilini mwake kwani alikuwa haamini yanayotokea kwenye maisha yake. Alijkuta anapatwa na woga ghafla.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "We Seba hebu twende wote ndani..!" Seba hakusita aliamua kumsindikiza bosi wake. Lakini moyoni mwake alikuwa na maswali mengi kwa nini bosi iweje arudi peke yake tena kwa mguu bila gari?. Alijiuliza ila hakuthubutu kunyanyua mdomo wake kuuliza chochote kwani alishaona hali ya bosi wake siku ile haikuwa nzuri.

    Walifika mlangoni na kukuta mlango ukiwa wazi ilhali waliondoka na funguo. Suala like lilizidi kumchanganya Mr.Alloyce.

    "Hebu niitie Huyo Eddy kwanza!" Alisema Mr.Alloyce kwani alikuwa anaogopa kuingia ndani ila hakujionesha kwa Seba kuwa alikuwa na hofu.

    "Eddy!" Aliita Seba.

    "Naaam!" Sauti kutoka ndani ilisikika.

    "Muite aje nje.. Haiwezekani afungue mziki kama disco humu.." Alisema Mr Alloyce kwa kujivungisha tu kwani bado alikuwa haamini kama Kweli Eddy yupo nyumbani.

    "Njoo huku we bwana mdogo.." Alisema Seba. Punde tu, Eddy alitoka nje na kumkuta baba yake. Mr.Alloyce alishtuka sana akahisi yupo ndotoni lakini ilokuwa sio ndoto Bali kweli. Machozi ya furaha yalimtoka, kwani hakutaraji kama angemkuta mwanaye akiwa yuko hai.

    "Daddy! Karibu ndani!" Alisema Eddy kwa uchangamfu sana.

    "Asante! Seba waweza kwenda..!" Alisema Mr.Alloyce huku wakiingia ndani na mwanae. Mr.Alloyce alishindwa kuizuia furaha yake, alijikuta anamkumbatia mwanaye kwa nguvu huku chozi likimdondoka.

    "Eddy mwanangu umefika SAA ngapi?"

    "Nilikuja toka mchana..!"

    "Kwanini ulitutoroka?"

    "Niliwatoroka wapi?" Aliuliza Eddy kwa mshangao, swali hilo lilimshangaza sana Mr.Alloyce. Ila hakutaka kuendekeza zaidi mada ile akijua kuwa inaweza sababisha mambo mengine.

    "Umekula nini?" Aliamua kubadilisha mada Mr.Alloyce.

    "Nilipika ugali na samaki zilizokuwemo kwenye jokofu."

    "Ulikula ee..?"

    "Ndio"

    Mr.Alloyce alishangaa sana kusikia vile kwani hakutegemea kama Eddy angekula chakula kwani siku zote alikuwa akikataa chakula akidai ni kichafu. "Leo amekula?" Alijiuliza Mr.Alloyce ama kweli Mungu ametenda.

    Mr. Alloyce pia alimshangaa sana mwanaye kwa uchangamfu aliokuwa nao siku ile, alikuwa na furaha ambayo Hakuwahi kumwona akiwa nayo tangu apate matatizo yake. Mr.Alloyce alifurahi ingawa alijiuliza sana imekuwaje?. Baada ya wote kuketi kwenye viti kwa ukimya mzito, ndipo Eddy alipoamua kuvunja ukimya kwa kumtupia swali baba yake. Swali lililoibua simanzi moyoni mwa Mr.Alloyce.

    "Mama yuko wapi?"

    Swali hilo liliibua machozi kwa Mr. Alloyce, alishindwa amwambie nini mwanaye.

    "Daddy mbona unalia kulikoni?" Aliuliza Eddy kwa mshangao.

    "Eddy... Mama yako amefariki... Sielewi ntafanyaje... Sielewi ntawaambianini ndugu zake mpaka wanielewee.. Sielewi..!"

    "Amefariki? Kivipi?" Eddy alishtuka sana.

    "Amefariki baada ya wewe kutoroka..!"

    "Kwani Mimi nimewatoroka wapi?"

    "Eddy umesahau au..? "

    *********

    Mwalimu Amina na Matron walibaki wakishangaana tu kwani walipoingia bwenini alikokuwa amelala Doreen. Hawakumkuta mtu yeyote ila walikaribishwa na harufu kali ya haja kubwa.

    Walipotazama chini kulikuwa na hali mbaya sana kwani kinyesi kilikuwa kimetandazwa chini kwa mafungu kama matano. Walikunja sura zao kwa kinyaa hawakutaka hata kuingia bwenini mle.

    "Doreen!" Aliita Madam Amina kwa sauti lakini hakujibiwa. Alienda hadi chooni kumwangalia lakini hakuwepo.Madam Amina aliamua kwenda madarasani kumtafuta lakini ilikuwa kazi Bure kwani huko pia hakuwepo.

    "Dunia ina mambo..!" Alisema Madam Amina. Matron alibaki anashangaa tu huku anatikisa kichwa kwa masikitiko.

    "Ila tusije tukauliwa na sisi...!" Alisema Matron.

    "Hakuna kitu kama hicho..!"

    " mbona unajiamini sana? Una nini mwenzetu?"

    "Mungu tu ndo nilienae ananifanya nijiamini sana..!"

    "Mh Haya.. Nimeamini kweli huyu mtoto nimchawi haswa.. Kweli amejisaidia bwenini namna ile?.. Sasa sijui ameenda wapi.."Alisema matron.

    "Bora tu aondoke ili shule ibaki na Amani tu..!" Alisema Madam Amina.

    Kiukweli aliwashangaza sana. Ila bado hawakujua binti yule ameenda wapi.

    *********

    Mwalimu Jason alikuwa ameshikilia kisu kile chenye makaliili atimizesharti alilopewa kwenye karatasi lile la ajabu. Machozu yalimchuruzika sana, alilia kwa uchungu ulioje.

    "Judith... Nakupenda... Ila sina budi kufanya hili...!" Alisema mwalimu Jason huku akitamani kusitisha jambo analotaka kufanya lakini alishindwa kutokana na nguvu za Giza zilizokuwa zikimshinikisha kufanya vile. Alimuonea huruma sana Judith, msichana ambaye alimpenda kwa dhati na kuahidi kufunga naye ndoa. Alimtazama Judith kwa simanzi, judith alikuwa akilia sana huku haja ndogo ikimshuka taratibu miguuni mwake. Alitetemeka kwa hofu sana akijuta kwanini alienda kumtembelea Jason.

    "Nataka titi lako.."

    "Jason kweli we umekuwa katili namna hiyo.. Kwanin lakini Jason.. Nimekosa nini .." Alilalamika Judith machozi yakimchuruzika mashavuni mwake alikuwa mwekundu kama pilipili iliyoiva.

    "Kwa sababu hiyo.. Bora nife Mimi Judith.. Maana nina mawili tu ya kuchagua. ." Jason aliposema hivyo tu akakiinua kisu na kukishusha kwa kasi mpaka kifuani kwake. Kikazama taratibu huku Judith akimshuhudia jinsi Jason anavyojiua..Akataka kupiga kelele lakini akajiziba mdomo kwa hofu na mshangao...



    .EDDY aliumia sana kwa taarifa zile za kifo cha mama yake. Hakutaka kuamini kama kweli mama yake hatakuwa pamoja nao tena. Machozi yalimbubujika kwa kasi huku akimwita mama take kana kwamba alikuwa karibu yake.



    Mr.Alloyce alishindwa kuvumilia, alijikuta akiungana na mwanaye kulia. Walilia sana mpaka machozi yaliwakauka, Mr Alloyce alichukua leso yake na kujifuta machozi yake kisha akachukua simu ili awajulishe ndugu na marafiki kuhusu kifo cha mkewe.



    Moyo wake ulisita sita sana kwani aliwaza ni jinsi gani ndugu wangeupokea msiba ule wa ghafla bila hata maiti.

    "Eddy watanielewaje shemeji zangu? Umesababisha yote haya mwanangu, lakini siwezi kukulaumu!" Alisema Mr Alloyce huku machozi yakimlengalenga.

    "Nisamehe dady kwa kuwa chanzo cha matatizo yote!" Alisema Eddy na kuendelea kulia.



    Lakini hawakuwa na jinsi ya kufanya kwani tayari maji yalikwisha mwagika na ilikuwa vigumu sana kuzoleka. Ilibidi wakubaliane na kilichotokea ingawa kishingo upande sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mr Alloyce alitafuta namba kwenye simu yake, MTU wa kwanza kumpata alikuwa shemeji yake aishiye jijini Dar ( Dada wa mama Eddy). Simu iliita kisha ikapokelewa, kwa kutetemeka na woga Mr Alloyce akaanzisha mazungumzo.



    "Halloo Shem"

    "Niambie Shem wake mie.. Kwema huko?" Alisema shemeji take Alloyce kwa uchangamfu sana kama ilivyokuwa kawaida yake. Hakuijua msiba mzito uliokuwa moyoni mwa Mr.Alloyce.

    "Huku sio kwema Shem..!" Aliens Mr Alloyce.

    "Sio kwema kuna nini?" Alishtuka.

    "Sio kwema naomba kesho mfike nyumbani kwangu tafadhali.."

    "Kuna nini shemeji? Naomba niambie tu.. Nini kimetokea?"

    "Utajua kila kitu kesho..!"

    "Hapana..niambie Leo.. Au MPE mama Eddy simu niongee nae..!" Maneno hayo yalimkata maini Baba Eddy hakuelewa ajibu nini akabaki kimya kwa sekunde chache akitafakari cha kujibu lakini ghafla akasikia sauti Kali ya Eddy ikimwita."Daaaaaaaaady!"



    Mr Alloyce alishtuka sana kwani Eddy alikuwa ametoka sebuleni pale dakika chache zilizopita wakati yeye akiongea na simu. Hofu ikamkamata ghafla na kumfanya Mr Alloyce atupe simu sofani na kuelekea sauti ya Eddy inakotokea. Eddy aliita tena "Daaaaaaaady!" Mara hii sauti ile iliambatana na mwangwi mkali uliozidi kumtisha Mr Alloyce.



    Alitoka sebuleni na kwenda koridoni lakini hakumuona Eddy. Akasikia sauti ikitokea chooni, alikimbia haraka na kwenda chooni lakini hakumuona, ghafla sauti ya Eddy ikasikika tena ikitokea chumbani kwa Eddy ilibidi amfuate haraka lakini cha kusikitisha Mr Alloyce hakumkuta Eddy ila alikuta damu nyingi zikiwa sakafuni. Alishtuka sana.



    *****

    Doreen aliamua kuondoka katika shule ya mabango kwani mambo yake yalikwishaanza kuharibika hivyo aliona heri aondoke zake kabla mambo makubwa hayajampata. Na yote hiyo ilitokana na maombi makali aliyokuwa akiyafanya Nadia Joseph ili kuinusuru shule yake kwa majanga yanayoikumba kila kukicha. Aliamua kujitesa kwa kufunga kila siku ili mradi tu shule yao ikomboke na irudi katika mstari ulionyooka.



    Hakika Sikio la Mungu si zito ili lisisikie, Mungu alisikia maombi ya Nadia ndio maana alianza kuharibu mambo ya Doreen taratibu.Doreen alimchukia sana Nadia, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana ili alipize kisasi



    "Ipo siku yake... Nitamwadhibu huyu mshe** kwa alichonifanyia... Nimeondoka kwasababu yake... Ila hata ipite miaka kumi ntampata tu!" Alijisemea Doreen na kusonya. Wakati huo akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa mwalimu Jason kwani alipajua vizuri sana.



    Alitembea kwa haraka kwa mwendo wa nusu SAA nzima hatimaye akawasili ndani ya nyumba ya Mwalimu Jason ili akatazame kinachoendelea.



    Aliongia mdani na kukutana na ukimya mzito. Kwa ujasiri na kujiamini sana Doreen aliingia chumbani kwa Mwalimu Jason na kukuta harufu Kali ya damu na mwili wa mwalimu Jason.



    Kwa wakati huo Judith alikuwa tayari amechapa lapa ili kuiepuka kesi ya mauaji ambayo ingemkabili. Na kama angekuwepo ndani mle basi ingekuwa nyama ya Doreen kwani angetumia vizuri nafasi ile kupata titi la Judith.



    Doreen aliutazama mwili wa Jason kisha akaachia sonyo Kali. Akakisogelea kitanda na kutafuta karatasi lake, akalikuta chini ya mto. Akachukua na kulitia kwenye mkoba wake kisha akaondoka zake.



    Akashika njia kuelekea kituo cha mabasi cha mkoani Iringa ili atafute gari liendalo mkoani Mbeya aende huko.Alipokuwa njiani alitazama pesa aliyokuwa nayo alishtuka kidogo kwani ilikuwa ni shilingi elfu moja tu ambayo haitoshi kwa lolote. Akawaza kwa sekunde kadhaa jinsi ya kufanya akapata jibu kisha akaendelea na safari yake.Alipofika mbele kidogo aliona duka kubwa limeandikwa Sanga Mini Market akaingia mle.



    "Karibu! " sauti ya mwanaume mwenye duka ilimkaribisha.

    "Asante! Nataka pop corn moja!"

    "OK.. Ya 500 au 1000?."

    "Nipe ya 500.." Alisema Doreen na alijua kabisa ana shilingi elfu moja. Lakini kuna kitu alitaka kufanya, alitaka kuiba pesa kwa kutumia ile shilingi elfu moja yake.



    Mzee yule alitoa popcorn na kumkabidhi Doreen.Doreen alichukua shilingi elfu moja kwenye mkoba wake na kumpa Muuza duka. Muuza duka alipokea akataka kumrudishia chenji lakini ghafla akasita.



    "We mtoto unanichezea? Hebu rudisha hizo popcorn... Shika hela yako.. Mpuuzi mkubwa wewe unataka kuniletea wanga wako hapa?" Alifoka muuza duka yule kwa jazba kwani alipoipokea hela ile akaugundua mchezo mzima wa Doreen aliotaka kuifanya. Doreen alishtuka, akaona aibu.



    "Kwani vipi baba?" Alisema Doreen kwa upole kwani uligundua Mzee yule in kiboko zaidi yake.

    "Wewe mtoto ntakuumbua hapa? Toka zako...." Mzee yule aliitupa chini hela Doreen na kumnyang'anya kwa nguvu ile popcorn.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Unafikiri tunauza kizembe? Wachezee huko huko hii namba tasa sio shufwa..!" Alisema Mzee yule Doreen akiwa anaondoka.Doreen aliona aibu sana lakini hakukata tamaa kwani alijua tu atapata mtu ambaye hana zindiko lolote.



    Uzuri wake uliwachanganya wengi sana kwani kila alipopita alikuwa akitazamwa kama nyota ya alfajiri huku wengine wakimpigia miruzi na wengine wakijaribu kumwita majina wanayoyajua wenyewe ili tu wabahatishe jina lake. Ni kweli Doreen alikuwa mzuri kupindukia, aling'aa kama m balamwezi ila tabia zake za ndani zilitisha zilokuwa mbaya kama Israel mtoa roho.



    Alitembea taratibu na kuingia kwenye mgahawa mmoja wa vyakula. Aliketi kisha akaagiza chipsi kavu za shilingi mia saba.



    "Sahani moja elfu moja?"

    "Samahani Dada nina mia saba tu nisaidie.. Nimetoka mbali na nina njaa sana..!" Alisema Doreen kwa upole sana ambapo aliweza kumshawishi kirahisi muuzaji, akamkubalia kwa kumuonea huruma.



    Watu walikuwa wengi mhahawani mle, Doreen alijiinamia chini tu akisubiri aletewe chipsi zake. Kwa muoneakano wa haraka ilikuwa vigumu sana kubaini tabia za Doreen kwani alionekana mpole na mkarimu sana.



    Chipsi sake zikaletwa, ilibidi atoe hela na arudishiwe chenji yake. Chenji ambayo ilikuwa tofauti na kiwango kinachostahili.

    *****

    Ulimi wa Mwalimu John ulikuwa mzito kutamka neno lolote. Kila akijaribu kusema chochote maneno yalikuwa hayaeleweki ndipo mkewe akabaini kuwa tayari mumewe amekuwa bubu. Roho ilimuuma sana kwani mumewe asingeweza kufanya kazi tena. Wataishi vipi mjini bila kazi? Aliwaza mkewe.



    Lakini licha ya kuumia moyo ila alimshukuru Mungu kwa uhai alioachiwa mumewe. Siku zikaendelea kusonga.Ilikuwa saa mbili usiku nyumbani kwa mwalimu John.Ukimya ulitawala sebuleni pale kwani ndugu wote walikuwa wameenda majumbani mwao hivyo walibaki wawili tu, ghafla mlango uligongwa.



    "Karibu! " alikaribisha Leyla mke wa mwalimu John. Bila kutegemea aliingia Judith, kwani alikuwa akipafahamu vizuri nyumbani kwa mwalimu John. Na hii ilitokana na ukaribu waliokuwa nao mwalimu John na Jason, hivyo mwalimu Jason alimtambulisha Judith kama mkewe mtarajiwa.



    "Karibu.." Alimkaribisha Leyla.

    "Asante.. Za hapa!"

    "Nzuri kiasi.. Umefika lini?"

    "Tangu juzi.." Alisema Judith lakini alionekana mwenye hofu na mawazo mengi.

    "Karibu.. Ulikuwa kwa Jason?"



    Swali like liliibua kumbukumbu ya tukio aliloshuhudia kwa mpenzi wake. Machozi yalimshuka kwa kasi, lakini alishangaa sana kwanini tangu amefika Mwalimu John hajasema lolote.



    "Hamjasikia chochote kuhusu Jason?"

    "Ndio.. Kwani kuna nini?" Alishtuka sana Leyla.

    "Ni stori ndefu sana ila mwalimu Jason alijiua!"

    "Ati nini?"

    "Ndio.. Inaniuma sana... Alitaka kuniua Mimi lakini akabadili msimamo na kusema bora ajiue yeye.." Aliendelea Julia Judith

    "Kwanini?"

    "Alisema ana sharti la.." Kabla Judith hajaendelea....





    MR ALOYCE alichanganyikiwa sana baada ya kukuta damu ikiwa imetapakaa sakafuni chumbani kwa mwanaye. Alipigwa na butwaa huku hofu ya kuondokewa na mwanae ikiwa imemvaa ghafla.



    "Eeeddy!" Alijikuta anaita kwa sauti Kali ili kama Eddy yupo mbali asikie na aitikie wito ule ambao ungemwondolea wasiwasi Mr Alloyce. Lakini wito ule haukuitikiwa na mtu yoyote zaidi ya ukimya uliokuwa umetawala ndani ya jumba lile la kifahari.



    Mr Alloyce alijaribu kuita tena na tena lakini bado hakuitikiwa. Simanzi ikamjaa tele, akajua tayari amepata pigo lingine zito kabla hata kidonda cha mwanzo hakijapona kwani ndio kwanza kilikuwa kibichi.



    "We Mungu wangu nimekukosea nini Mimi mbona unaniadhibu hivi? Nihurumie uikomboe familia yangu" alilia mr Alloyce akiwa amejibwaga sakafuni kwenye korido ya kuelekea sebuleni. Machozu yalimchuruzika kama mvua huku yakiteremka kama vijito kuelekea kwenye marumaru za rangi ya maziwa zilizochanganyika na weupe.



    "We Mungu nitaishi vipi Mimi na upweke huu? Sina mke, sina mtoto?" Alilalamika kwa majonzi mr Alloyce. Aliwaza mengi sana yaliyozidisha simanzi yake moyoni, moyo wake ukajawa na maumivu makali sana kama mtu aliyechomwa na mkuki wa moto katikati ya moyo wake.



    "Bora na Mimi nife kuliko kubaki kwenye hali kama hii...!" Aliwaza Mr Alloyce kisha akainuka pale sakafuni na kuelekea chumbani kwake. Aliingia chumbani na kuwasha taa, kisha akaisogelea droo ya dressing table akaifungua na kuanza kupekuapekua vitu.



    Alipekua kwa muda kisha akapata karasi ya ranging ya kaki akafunua kwa umakini kisha akazikuta dawa alizozihitaji. Kulikuwa na vidonge Vingi sana ndani ya pakiti ile kaki, akavibeba na kuirudisha droo kama ilivyokuwa akatoka kuelekea sebuleni.



    Alifika sebuleni na kuliendea jokofu ili achukue pombe Kali anywe pamoja na vile vidonge ili aondokane na ulimwengu huu wa mateso ambao alihisi umemtenga baada ya kumtenganisha na wapendwa wake. Akiwa anafungua jokofu na kichukua chupa moja ya konyagi ghafla alishtuka sana.



    *****

    Dorice aliyastaajabu mazingira aliyopelekwa kwani palikuwa na viumbe wengi wa ajabu ambao yeye hakuwahi kuwaona hats siku moja.



    Ulikuwa kama ukumbi mkubwa sana uliotawaliwa na viumbe wale wa ajabu, alipopiga jicho mbele ya ukumbi ule aliona viti viwili vyenye rangi ya shaba vikiwa vimetengwa peke yake. Alimtazama Mansoor kwa sura ya maswali lakini Mansoor hakuzungumza neno lolote zaidi ya kumshika mkono Dorice na kuongozana nae mpaka kwenye vile viti. Walipovifikia tu, ghafla akatokea kiumbe mmoja wa kutisha sana kwani alikuwa na macho kama ya bundi, meno marefu yaliyochongoka na kucha ndefu za miguuni na mikononi. Mwili wake ulitawaliwa na manyoya na kila alipozungumza kinywa chake kilitema moshi mweusi. Doreen aliogopa sana, akajikuta anamsogelea Mansoor kwa hofu.



    "Usiogope Mpenzi... Huyu ni mfungishaji ndoa!" Mansoor alimtoa hofu Dorice. Dorice alibaki kimya huku moyo wake ukibaki na woga wa hali ya juu.



    "Leo ndio ile siku tuliyoisubiri kwa hamu sana, hatimaye kijana wetu mtoto wa mtukufu malkia amepata mwenza wake wa maisha!" Alisema kiumbe yule wa kutisha. Radi Kali zilipigwa ishara ya kufurahia kile kinachozungumzwa.

    "Bi Aisha utakuwa mke halali wa Mansoor... Kwa kuivaa Pete hii ambayo hutakiwi kuivua maisha yako yote." Alisema kiumbe yule huku akimkabidhi Mansoor Pete nzuri sana ya dhahabu, iling'aa kupita kawaida.



    "Nakupenda sana, nakuoa leo, naahidi kukulinda Siku zote kama mke wangu. Tafadhali sana usije ukaivua Pete hii hats Mara moja!" Alisema Mansoor na kumvisha Pete Dorice. Dorice alikuwa anaogopa sana, machozi yalimlengalenga machoni kwani hakuamini kama kweli anaolewa na jini.Ndoa ilifungwa na Dorice alipewa onto la kutoivua Pete yake ya ndoa hata Mara moja.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *****

    Doreen alimkabidhi pesa ile muuz mgahawa kisha akaendelea kula chipsi zake kwa haraka sana utadhani anakimbizwa na polisi, hata kabla ya kumaliza akaziacha mezani pale na kumfuata yule mama muuzaji kisha akamdai chenji.



    Mwanamama yule alitoa shilingi mia tatu kwenye pochi ndogo aliyokuwa akihifadhi pesa kisha akamkabidhi Doreen. Lakini cha ajabu baada ya kumkabidhi tu Doreen pesa zile, kitita cha pesa zote alizouza siku ile zikaenda kwa Doreen bila yeye mwenyewe kujua. Zilikuwa kama elfu sitini na tatu halafu yeye akabakiwa na shilingi mia tatu.



    Doreen alipozichukua pesa zile akapiga hatua kubwakubwa kuelekea kituo cha mabadi kwani tayari alikuwa amepata nauli na pesa ya kutumia njiani kuelekea mkoani Mbeya.



    Yule mama aliendelea na shughuli zake kama kawaida, alimhudumia mteja mmoja kisha mteja yule alimpa shilingi elfu kumi na akahitaji chenji. Bila wasiwasi mwanamke yule aliiendea pochi yake na kutaka kuchukua hela lakini alipoishika tu pochi ile akahisi kitu, maana pochi ilikuwa nyepesi kuliko kawaida. Alishtuka kidogo kisha akaifungua. Hakutaka kuamini macho yake kwa alichokiona.



    "Hela zangu!!!!!!" Aliongea kwa mshtuko mkali kisha wote wakamtazama mama yule .

    "Hela zaaangu mieee!" Alianza kushusha kilio huku akizitafuta huku na kule lakini hakuziona.

    "Fety wapi hela zangu?" Mama yule alimuuliza mfanya kazi wake.

    "Hela? Si uliziweka humo?"

    "Ndio mbona sizioni sasa? Sema tu kama umechukua! Hakuna mwingine ni we we Fety..!' Mama yule alilia huku akimkunja mfanyakazi wake akihisi ndiye aliyemwibia.

    "Mama tangu lini nimekuibia?"

    "Nani angechukua!? Nani nakuuliza?" Mama yule aliongea kwa hasira sana.

    "Sio Mimi mama unanionea Bure..!"

    "Na utanilipa shenzi wewe..!" Alizidi kumkunja.

    "Labda umemzidishia yule mteja aliyeondoka?"

    "Tutamfata kama si yeye utanikoma..!" Aliongea kwa hasira sana mama yule kwani mtaji wote alikuwa amechukua pesa za mkopo. Hivyo alichanganyikiwa sana.

    Waliamua kumfuatilia Doreen kule alikoenda. ...



    .MR ALLOYCE alishtuka sana baada ya kusikia kishindo kalikali nyuma yake. Aliachia chupa ya konyagi kisha akageuka haraka kutazama nini kinaendelea nyuma yake. Hakuamini kumuona mwanaye akiwa amejibwaga chini kama gunia la viazi. Alikuwa anathema kupita maelezo.



    "Eddy!" Mr Aloyce aliita kwa mshangao mkubwa. Lakini Eddy hakuitikia zaidi ya kuendelea kuhema kwa nguvu.Mr Alloyce alitupa chini vidonge alivyokuwa amevishika, akamwinamia Mwanaye na kumgusa kifuani ili kusikiliza mapigo ya moyo. Aligundua kuwa mwanaye ni mzima alimsgukuru Mungu. Killed home hang a za Mr Alloyce ni kwamba pindi anarudi sebuleni pale, hakukuta mtu yeyote na wala hakusikia mtu akifungua mlango.



    "Ba...ba..!" Aliita Eddy kwa shida sana.

    "Sema mwanangu...Mimi hapa" aliitikia Mr Aloyce.

    "Usife. .!"

    "Sifi nani kasema Mimi nakufa? Vipi lakini uko sawa?" Aliuliza mr Alloyce akiwa na hofu sana, alihofia kumpoteza mwanaye kipenzi. Eddy aliitikia kwa kichwa tu akimhakikishia baba yake kuwa yuko sawa.



    Mr Alloyce aliendelea kumkagua Mwanaye kila sehemu akidhani labda ana majeraha kwani damu alizozikuta chumbani kwa Eddy zilimtisha Sana. Lakini alipomtazama mwanaye akagundua hana jeraha lolote mwilini mwake, hivyo maswali mengi yalijitokeza akilini mwake. Alijihoji maswali mengi lakini hakuwa na majibu yake.



    "Baba... Mama anateseka sana!" Eddy aliongea sauti ndogo ya kujivuta sana akiwa bado amelala pale sakafuni.

    "Anateseka wapi?" Mr Alloyce alishtuka sana.

    "Alikuja hapa.. Anateseka sana na yote kwa sababu yangu...!" Alisema Eddy kwa huzuni sana huku machozi yakimlengalenga machoni.

    "Eddy! Upo sawa kweli?" Mr Alloyce alihisi Eddy hayupo sawa hivyo anaropoka tu anachojisikia.

    "Nimefanya makosa sana.. Namtesa mama yangu..."

    "Eddy usiseme hivyo.. Unamtesa na nini?"

    "Alivyotaka kunipeleka kwa mganga wameamua kumuadhibu...!"

    "Kina nani?"

    "Wachawi...!"

    "Oh My God.."



    Maneno Yale yalizidi kumchanganya Mr Alloyce, alishundwa afanyaje kwani ilikuwa ni Mara yake ya kwanza maishani mwake kukumbana na mauzauza ya namna ile. Mara nyingi alizoea kutazama kwenye luninga tu lakini hakujua kama inaweza kumtokea kweli. Maisha yake yalikuwa machungu ndani ya muda mfupi tu kwanu matatizo aliyokuwanayo yalikuwa mazito tena yanaumiza kama gunia la misumari.

    "Baba.. Nakupenda..!"

    "Nakupenda pia mwanangu!"



    Mr Aloyce alijikuta anashusha mchozi tu kila anapomtazama mwanaye kwanu siku zote aliamini mwanaye atakuwa mtu mkubwa sana kutokana na uwezo wake darasani. Alikuwa na akili nyingi lakini Leo amekuwa mtu wa kuteseka tu. Aliwachukia wanadamu wenzake kwa ukatili wanaoufanya juu ya familia yake.



    "Baba.."

    "Naam mwanangu.."

    "Chukua hii." Eddy alimkabidhi baba yake kipande cha karatasi.Mr Aloyce alishtuka kidogo kisha akapokea karatasi like na kulikunjua ili alisome.Ujumbe uliokuwepo pale ulimshtua sana Mr Alloyce. Aliurudia tena"CHAGUA MOJA.

    EDDY APONE TATIZO LAKE, MAMA YAKE APOTEE DAIMA. AU MAMA EDDY ARUDI, EDDY ABAKI NA TATIZO LAKE"



    Mr Aloyce alibaki mdomo wazi kwa mshangao, kwani ule ulikuwa mtihani mgumu kwake."Karatasi limetoka wapi?"



    *****

    Mama muuza mgahawa alikuwa kama mwehu baada ya pesa zake kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Aliambatana na mfanyakazi wake ili wamfate Doreen. Waliifuata njia aliyoelekea Doreen na kumtazama huku na kule lakini licha ya kumfuatilia kwa muda mrefu hawakufanikiwa kumuona. Walifika mpaka kituo cha mabasi kumtafuta lakini pia hawakumuona.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Luna msichana alipita hapa, mweupe amevaa sweta jeusi na sketi ya kahawia?" Aliuliza Fetty mfanyakazi wa yule mama muuza mgahawa.

    "Ni mzuri sana?"

    "Ndio!"

    "Alipanda basi la Mbeya na limeondoka!"



    Aliwajibu kijana mmoja ambaye alionekana ni kondakta wa basi.Yule mama aliangua kilio kikali palepale kwenye kituo cha mabasi bila kujali wingi wa watu. Alilia kwa sauti Kali akiwa ameweka mikono kichwani. Watu walimshangaa mama yule wakaanza kumkusanyikia.



    "Hela zaangu.. Hela zaaangu... Nitalipa nini Mimi...!"

    "Mama twende basi..!"

    "Nataka hela zangu... Nitafanyaje hela za watu.. Hela za mkopo"



    Alilia mama yule kwa uchungu na hasira nyingi. Watu waliendelea kumshangaa pale, lakini tayari alikuwa amelizwa na binti Doreen.



    Huku mama yule akiwa analilia pesa zake, Doreen alikuwa na furaha sana kwa kupata pesa zile kwani zilimsaidia katka nauli ya kutoka Iringa kwenda Mbeya.



    Doreen hakuwa na ndugu yeyote jijini Mbeya ila aliamua kwenda Huko kwaajili ya kukamilisha kazi zake hasa hasa ikiwa kupata titi la msichana mrembo.



    Akiwa ndani ya basi, Doreen hakuweza kuzungumza na mtu yeyote. Alitulia kimya akiwa amejiinamia. Alionekana mwenye mawazo mengi sana tena mwenye huzuni kupita kiasi. Jirani yake Doreen ambaye ni mwanamama wa makamo kiasi kama miaka 40 au 45 alimuona Doreen akiwa katika hali ile. Alimwonea huruma na kuamua kumuita.



    "We binti hujambo!" Alisema mama yule lakini Doreen alibaki kimya kama vile hakusikia anavyoitwa.

    "We mdada!" Aliita na kumgusa began Doreen. Doreen aliinua kichwa na kumtazama mwanamke yule.

    "Shkamoo mama!" Doreen alimsalimia kwa heshima na adabu mwanamke yule.

    "Marhaba.. Mie naitwa Bi Carolina.. Unaitwa nani?"

    "Naitwa Doreen!"

    "Asante.. Mbona una mawazo sana? Tangu umeingia kwenye gari huna raha hata kidogo.. Una tatizo gani?" Aliuliza mwanamke yule kwa upole sana.

    "Nina matatizo makubwa sana mama?" Alisema Doreen kwa unyonge wa hali ya juu.

    "Tatizo gani?"

    "Ni hadithi ndefu sana mama angu!" Alisema Dorice safari hii machozi yalimlengalenga machoni. Maneno Yale yalivuta usikivu wa Bi Carolina. Alitamani amsikilize zaidi.



    "Mama! Acha tu.. Dunia ina mateso sana..! Sina hamu!" Doreen aliachia mchozi uliokuwa ukimlengalenga machoni. Bi Carolina alimtazama kwa huruma Doreen na kumtaka aendelee kumsimulia.



    "Mama! Iringa nilikuwa naishi na mjomba wangu, tumbo moja na mama yangu! Na alinichukua baada ya wazazi wangu kufariki, aliahidi atanisomesha lakini hakufanya hivyo.



    Alikuwa akininyanyasa, hanipi chakula, ananifanyisha kazi ngumu wakati anajua kabisa naumwa moyo, jana kanifukuza usiku wa manane akidai namchafulia hali ya hewa nyumbani kwake, sina hadhi. Nimeteseka sana, sins hata kwa kwenda!" Alisema Doreen kwa uchungu huku akilia. Simulizi yake ilimuumiza sana Bi Carolina akatamani kumsaidia Doreen.



    "Pole sana Doreen.. Kwahiyo Mbeya unaenda kwa nani?"

    "Sina ndugu huko.. Naenda tu hata kutafuta vibarua..!" Aliendelea Julia Doreen akachukua leso yake na kujifuta machozi.



    "Dash pole sana.. Kwangu naishi na mume wangu na binti yangu.. Naomba nikusaidie ukaishi kwangu.." Alisema yule mama kwa huruma sana.Doreen alifurahi sana kimoyomoyo has a alivoambiwa kuna binti anaishi pale.





    Mr Aloyce alilishikilia karatasi lile akiwa ameinamisha kichwa chake chini, mawazo yalimjaa tele kichwani mwake. Aliwaza achague lipi kati ya Yale aliyoamriwa.



    Alijiona ana mtihani mzito sana ambao alishindwa kufaulu kwa haraka. Akawaza ni heri amrudishe mkewe ili waendelee kushughulikia tatizo la mtoto wao wakiwa pamoja.



    "Namtaka mke wangu" alisema Mr Alloyce kwa sauti ya chini kisha ghafla akasikia sauti ya kicheko kikali kisha akatazama huku na kule bila kumuona mchekaji. Aliogopa kupita kiasi. Alitetemeka kama mtu aliyeshikwa na baridi Kali.



    "Umechagua vyema maana ungetaka mwanao apone.. Ungepoteza kila kitu... Mkeo yupo kule Kule alikopotelea, hajafa ila tulitaka kumfundisha adabu tu kwa kulazimisha mambo." Ilisikika sauti ile iliyoambatana na mwangwi mkali.



    Mr Alloyce alizidi kuogopa, akaangaza macho huku na kule lakini hakuona mtu. Woga ulimzidia sana baada ya karatasi alilokuwa ameshika mkononi kutoweka bila kujua limeenda wapi. Alitafuta pale sakafuni lakini hakuliona, akazidi kupigwa na butwaa. Maneno aliyoambiwa kuhusu mkewe yalizidi kujirudia kichwani mwake. Alihisi kama alikuwa akidanganywa tu, mkewe alishafariki na hawezi kurudi.



    "Mtu alishafariki, nitakaaje nae tena? Mh! Dunia ina maajabu...!" Aliwaza Mr Alloyce."Kweli nitamwona mke wangu? Sijui niende Leo? Mh sasa hivi ni usiku sana!" Mr Aloyce aliwaza na kuwazua ubongoni mwake. Aliamua kuwa na subira, asiwe na papara. Aliamua kuisubiri kesho yake asubuhi ili aende sehemu ambayo mkewe alipotelea ili akamchukue.



    Usiku ule ulikuwa mrefu sana kwa Mr Aloyce kwani hakuwa na hata lepe la usingizi, kila dakika alikuwa akiyafikiria matukio yote yaliyomtokea kwenye familia yake akahisi ndoto tu au mchezo wa kuigiza lakini ilikuwa kweli kabisa na alishuhudia kwa macho yake.



    "Eddy! Mama yako mzima, tutaenda kumfata kesho asubuhi!" Mr Aloyce aliongea.

    "Baba kweli?" Eddy alishtuka kusikia vile kwani sauti iliyokuwa ikisikika ndani mle na kumpa maelekezo Mr Alloyce, Eddy hakuisikia kabisa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kweli mwanangu!"Eddy aliachia tabasamu mwanana usoni kwake. Kwani hakika taarifa zile zilimfurahisha sana.

    "Kesho asubuhi na mapema nitamfuata kule aliko.."



    "Yuko wapi?" Kabla Mr Aloyce hajajibu swali la mwanae alishtushwa na mlio wa simu yake . simu iliita kwa sauti kutokea kwenye moja ya sofa pale sebuleni.Mr Aloyce aliinuka na kuifuata lakini alipotazama kwenye kioo alishtuka kidogo.

    *****

    Gari ilitembea kwa mwendo mrefu sana mpaka ilipofika eneo la uyole jijini Mbeya. Ndipo Bi Carolina alipoamua kuchukua simu yake na kupitisha vidole vyake laini vilivyonakshiwa kwa kucha nzuri zilizopakwa ranging nyekundu. Akatafuta namba Fulani kisha akapiga.



    "Mume wangu uko wapi? Tumefika hapa uyole sio muda mrefu tutaingia hapo Nanenane!" Alisema Bi Carolina .

    "Kwani upo na nani?" Ilisikika sauti ya upande wa pili.

    "Aah bwana .. Tupo na abiria wenzangu... Niambie uko wapi?"



    "Utanikuta Hapahapa Nanenane stendi .. Nimefika kitambo nakusubiri mke wangu!" Alisema mume wa Bi Carolina kisha simu ikakatika.



    Majira ya saa moja na nusu hivi, Bi Carolina na Doreen walikuwa tayari wamewasili katika kituo cha mabasi cha Nanenane jijini Mbeya. Bi Carolina alionesha kumjali sana Doreen kwa kumkaribisha Binti huyo jijini Mbeya .



    "Hii ndio Mbeya Doreen... Baridi hapa ndo kwake... Karibu sana"

    "Asante mama!" Aliitikia Doreen kwa sauti ya upole sana akiwa ameachia tabasamu usoni pake.



    Ghafla simu ya Bi Carolina ikaita, alipotazama ilikuwa namba ya mume wake akapokea kisha akasikiliza maelekezo . Akaelewa gari ya mumewe ilipo wakaelekea pale na kuikuta gari aina ya Prado ikiwa imepaki pembezoni mwa Barbara karibu na mango la kuingilia uwanja wa maonesho ya Nanenane.



    Tabasamu pana kutoka kwa mwanaume mfupi kiasi, mnene, mwenye rangi ya kunde likamkaribisha Bi Carolina. Lakini punde tabasamu hilo la mume wa Bi Carolina likayeyuka ghafla baada ya kuona mkewe ameambatana na mtu asiyemfahamu.



    "Mke wangu vipi?" Aliuliza mumewe huku akimtazama Doreen.

    "Kwani vipi mume wangu?"

    "Huyu nani?" Aliuliza

    "Mgeni wetu.."

    "Ndugu yako?"

    "Hapana.. Tuachane na hayo.. Tutaongea tukifika" alisema Bi Carolina.

    "Shkamoo..!" Alisalimia Doreen kwa upole sana . lakini mume wa Bi Carolina hakuitikia salamu ile.

    "Mke wangu.. Usiniletee uchuro.. Huyu wa wapi..!" Alifoka

    "Baba Pamela mume wangu.. Mbona uko hivo? Kuna ubaya gani kuja na mgeni?"



    "Hakuna tatizo kama ungenijulisha.. Kwani ni ndugu yako?"

    "Sio.. Ni mtoto tu nimeamua kumsaidia ana matatizo makubwa sana!" Alijitetea Bi Carolina lakini bado mumewe hakutaka kukubaliana nae. Hakumtaka kabisa Doreen.

    "Tupeleke nyumbani..." Aliomba Bi Carolina.

    "Ntakubeba peke yako.. Bila huyo mgeni wako.."



    "Kuwa na roho ya utu mume wangu.. Tutamwachaje huyu mtoto barabarani hapa? Si ukatili huo.

    "Nimesema simtaki mgeni wako nyumbani kwangu... Jifanye una huruma utaokota mpaka majini!" Alisema mume wa Bi Carolina kisha akafunga mlango wa gari na kuondoka zake huku akimwacha mkewe na Doreen palepale.



    Bi Carolina alibaki akishangaa kitendo cha mumewe siku ile. Alimtazama Doreen aligundua kuwa analia, tena Analia kwa uchungu sana.



    "Usilie mwanangu tutaenda hata na daladala.." Alisema Bi Carolina kwa upole.

    "Hapana mama.. Mi niache tu wewe nenda... Nisijekuharibu familia yenu bure" alisema Doreen huku akilia.

    "Siwezi kukuacha hapa Doreen, usiku sasa!" Alisema Bi Carolina.



    "Hapana mama nenda!" Alisisitiza Doreen lakini Bi Carolina alizidi kumbembeleza waondoke wote. Ghafla simu ya Bi Carolina ikaita, akapokea.

    "Mama Pamela! Ukitaka kuja na huyo mgeni wako, usifike kwangu... Ishia hukohuko..!"



    ..Baada ya kutazama kioo cha simu Mr Alloyce alishtuka kidogo baada ya kukuta namba ya shemeji yake. Aliitazama kwa muda, huku akitafakari jibu la kumpa shemeji yake kwani tayari alimtaarifu kwamba aje kesho yake asubuhi. Aliamua kupokea simu ile huku akivuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu sana.



    "Halloo Shem! mbona ulikata simu kabla hujaniambia kuna tatizo gani?" Alisema Bi Sandra Dada wa mama Eddy.

    "Ah..ah..Shem.. Usije kesho... Nimetatua ..tayari Shem!" Mr Aloyce alijikuta anapata kigugumizi cha ghafla kwani hakuwa na jibu sahihi la kumjibu shemeji yake.

    "Umetatua SAA ngapi? Mbona sikuelewi shemeji? Si umesema nije kesho?" Sandra alishangaa.

    "Ha..hapana Shem usije kwanza.. Usije!"

    "Shem sikuelewi.. Nitakuja kesho.."

    Alisikika Sandra kisha simu ikakatika.



    Usiku ulikuwa ni mrefu sana kwa familia ile ya Mr Aloyce, walikesha wakiwa sebuleni yeye na mwanae. Usingizi ulimpitia kwa dakika chache kisha akashtuka. Akatazama saa yake ya mkononi ilikuwa tayari ni Saa kumi na moja alfajiri.



    Mr Aloyce aliinuka kitini na kwenda bafuni, alioga haraka kisha akaingia chumbani na kubadili nguo.

    Hakutaka kujichelewesha sana, akarudi sebuleni na kumuaga Eddy.

    "Naondoka Eddy!"

    "Baba naogopa kubaki peke yangu!"

    "Jitahidi Mwanangu, siwezi kuondoka na wewe!"

    "Twende wote baba!"



    Eddy alizidi kumkazania baba yake lakini Mr Aloyce hakukubali hata kidogo kuondoka nae kwani alihofia misukosuko ambayo ingejitokeza wakiwa huko.

    "Baki na mlinzi basi!"

    Eddy aliinuka na kutoka na baba yake, nje kulikuwa bado hakujapambazuka vizuri hivyo kulikuwa na kigizagiza ingawa walisaidiwa na mwanga wa taa.



    Mr Aloyce alichukua gari yake nyingine na kuiwasha haraka kisha akapiga honi ili mlinzi afungue geti.

    "Bosi mbona usiku? Unaenda wapi?" Aliuliza mlinzi.

    "Hayakuhusu.. Fungua geti nitoke, baki na Eddy!"

    "Sawa bosi wangu.. Samahani kwa maswali!" Alisema mlinzi kisha akafungua geti Mr Aloyce akatoka na kuelekea kule alikopotelea mkewe.



    Eddy alibaki na mlinzi wao pale nje, alikuwa na mawazo mengi sana kichwani hivyo alikuwa amejiinamia kimya tu bila kuzungumza chochote.



    "Eddy mbona unawaza sana?" Aliuliza mlinzi. Lakini Eddy hakujibu kitu akabaki kimya amejiinamia.

    "Eddy si naongea na wewe husikii au?" Aliuliza tena kwa sauti ya ukali kidogo. Safari hii Eddy aliinua kichwa na kumtazama.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Demu wako amekutosa nini? Maana sielewi elewi humu ndani.. Mara mtoke mara muingie kimaajabu ajabu siwaelewi kabisa.!"



    "Yanakuhusu?"

    "Yanaweza kunihusu kwa sehemu.. !" Alisema mlinzi yule kwa masikhara.

    "Sitaki kelele.." Alisema Eddy na kujiinamia.

    "Sikia Eddy... Mnanionaga chizi chizi sana ila nina akili zangu... Tatizo lako nalijua na ninaweza kukusaidia.... Sasa endelea hivohivo... Ila jua mficha uchi hazai..!" Alisema mlinzi kisha akasogea pembeni na kuchukua shuka lake ili ajifunike.

    "Anko! Umesemaje?"

    "Sijasema chochote ..!"

    "Anko nisamehe.. Umesema unaweza kunisaidia tatizo langu?"

    "Ndio na ni kazi ndogo... Ila endelea kunifanya mwehu kila siku....!"

    Eddy alimtazama mlinzi wao kwa mshangao wa hali ya juu.



    ********

    Bi Carolina hakuwa tayari kumuacha Doreen abaki peke yake kwenye kituo cha mabasi ilhali alimuahidi kumsaidia. Hakujali kabisa maneno ya mume wake kwani alijua tu kuwa mumewe hapendi wageni nyumbani kwake.

    Bila kuchelewa wakabeba mizigo na kufuata taxi iliyokuwa mbele yao kisha wakapanda.

    "Mnaelekea wapi?"

    "Forest Mpya.."



    Dereva aliondoa gari haraka kuelekea Forest Mpya. Doreen alikuwa amekaa karibu kabisa na dereva wa taxi. Macho ya dereva yalikuwa hayakauki usoni kwa Doreen kwani kila mara alimtazama kiwizi binti yule.

    "Mama! Hivi huyu ni mwanao!?" Aliuliza Dereva taxi.

    "Ndio! Kwani vipi?"



    "Daaah Mama umezaa mtoto mzuri kuzidi malaika.. Kha! Kuna wazuri ila huyu mwanao kazidi!" Alisema dereva taxi na kumfanya Doreen atabasamu huku akiinamisha kichwa chini kwa aibu.

    "We dereva bwana.." Alisema Bi Carolina na kucheka.

    "Ningekuwa sijaoa ningekuja kuchumbia huyu mtoto..!" Alizidi kutania dereva yule ingawa utani wake ulikuwa na ukweli ndani yake.

    "Oa mke wa pili!" Alitania Bi Carolina.

    "Mke wangu atajinyonga.. Maana ana wivu sana, tena akigundua Bi mdogo kamzidi uzuri ndo basi tena"



    Wakati wakiendelea kuzungumza hayo walikuwa tayari wamefika eneo la Mbeya Carnival na muda mfupi baadae walifika kwenye jumba moja la kifahari, lililovutia sana.

    "Tumefika dereva!"alisema Bi Carolina dereva akapaki gari wakashusha mizigo. Kisha Bi Carolina akatoa pesa na kumpa dereva.

    "Asante mama.. Ila nitunzie huyo bibie..!"

    Wote wakacheka kisha wakaingia ndani na kuiacha taxi ile ikiondoka kwa fujo.



    "Karibu Doreen hapa ndo nyumbani jisikie uko nyumbani... Sawa mama?" Alisema Bi Carolina huku wakiingia ndani.

    "Asante mama kwa ukarimu wako"



    "Wala usijali.." Bi Carolina alimkaribisha vizuri sana Doreen bila kujua kuwa alikuwa akimkaribisha shetani mbaya mwenye kila sifa ya kuitwa katili. Alikuwa kama fisi anayekaribishwa buchani kwa ukarimu sana wakati nyama ikiwa imejaa. Doreen alifurahi sana moyoni mwake alijua ushindi wake upo karibu.



    Waliingia ndani na kumkuta baba Pamela akiwa ameketi kwenye sofa akitazama televisheni huku akiwa ameshika rimoti na kubadili Chanel.

    "Za kutangulia mume wangu.." Alisema Bi Carolina.

    "Mama Pamela!"

    "Abee!"

    "Hakuna heshima tens katika ndoa yetu sio?"

    "Ipo mume wangu..!"

    "Nimekuambia usije na huyo binti hujanisikia... Bila haya unaniambia eti 'habari za kutangulia?' Hivi una akili kweli?" Alifoka baba Pamela.

    "Nisamehe mume wangu ila inabidi utumie utu sio kila wakati unakuwa na roho mbaya!"



    "Ok sawa.. Naheshimu maamuzi yako ila ipo siku utanikumbuka..!" Alisema Baba Pamela mbele ya Doreen kisha akaondoka zake na kwenda chumbani.

    Bi Carolina hakuzielewa kauli za mumewe aliona kama ana roho mbaya isiyojali wageni wala kuwathamini wanyonge. Aliamua kuachana na maneno ya mumewe badala take akamkaribisha kiti Doreen na baada ya kupumzika kwa muda akampeleka kwenye chumba kimoja ndani ya nyumba yao na kumkabidhi Doreen.

    "Utalala humu.. Na hiki kitakuwa chumba chako.." Alisema Bi Carolina akitabasamu.

    "Ahsante.. Mama naomba niulize kidogo..!"

    "Uliza tu usijali.."

    "Dada Pamela yuko wapi?"

    "Pamela yupo kwa shangazi yake.. Atarudi kesho kutwa mtakuwa pamoja!"

    "Asante"



    Bi Carolina aliingia jikoni na kuandaa chakula kizuri. Wakala kisha wakaenda kulala.

    Wakiwa chumbani baba Pamela hakutaka kuzungumza lolote na mkewe mpaka usingizi ulipowachukua wote wawili.

    Majira ya SAA kumi alfajiri Baba Pamela aliishtuka usingizini na kumshtua mkewe kwa nguvu.

    "Vipi?"aliuliza Mama Pamela kwa sauti ya nyono kwani bado alikuwa na usingizi.

    "Amka nataka nikuambie jambo..!" Alisema baba Pamela.



    ********

    Baada ya ndoa ya Mansoor na Dorice, maisha mapya ya ndoa yalianza. Penzi zito la Mansoor kwa Dorice lilijidhihirisha rasmi na alimpenda kwa dhati mkewe. Furaha take aliyoitafuta kwa muda mrefu sasa ilitawala moyoni mwa Mansoor kwani tayari alishampata ampendae. Dorice hakuwa na furaha sana na ndoa yake kwani mawazo yake yote yalikuwa juu ya uhai wa mpenzi wake wa Moyo Eddy Alloyce. Kila mara alimfikiria Eddy, na aliona amefanya kosa kubwa sana kufunga ndoa na jini.

    Wakiwa wametulia tuli katika pozi la mahaba, Dorice na Mansoor. Dorice alifungua kinywa na kuyasema Yale yanayomsibu, masuala yanayousumbua moyo wake kwa kipindi kirefu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mansoor..!"

    "Niite Mume wangu.." Alisema Mansoor, Dorice akacheka kidogo.

    "Mume wangu!"

    "Naam! Hapo sawa mke wangu.!"

    "Nataka nikukumbushe kitu."

    "Sema tu mpenzi wa roho yangu!"

    "Vipi kuhusu ahadi yako ya kunipeleka duniani na kumwokoa Eddy?"

    Maneno hayo yaliupasua moyo wa Mansoor na kuiyeyusha ghafla furaha yake. Hakutamani wala hakuwa tayari kuwa mbali na mkewe, alimpenda sana na alitamani awe wake daima milele. Kwake, Doreen alikuwa kama chanda ambayo bila hiyo Pete haina uthamanu wowote, machozi yalimlenga machoni mwake.



    "Unataka kuondoka?"

    "Ikumbuke ahadi yako..."

    "Mke wangu unataka kunitenga? Unadhani ukienda duniani utakuwa wangu tena????"alisema Mansoor. Dorice akamtazama kwa mshangao.



    ..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.

    "Vipi mke wangu?"

    "Najuta Mansoor.. Najuta sana kukukubalia, sikujua kama hautakuwa mwaminifu kwa ahadi zako!" Alisema Dorice kwa hasira.



    "Sina maana mbaya mke wangu mpenzi.. Usinielewe vibaya tafadhali...Nakupenda sana!"

    "Unanipenda? Unanipenda nini uongo mtupu..!" Alisema Dorice kwa hasira huku machozi yakimshuka mashavuni mwake. Alijikuta anamchukia Mansoor kupita kiasi. Hakutaka hata kumsogelea karibu.

    "Baby! Nimekuelewa basi naomba uwe na amani moyoni mwako" alisema Mansoor huku akimsogelea Dorice na kutaka kumkumbatia lakini Dorice alimsukumia kando Mansoor na kuongeza kilio chake.

    "Sitaki uniguse mpaka utakaponiambia ni lini utatimiza ahadi yako"



    "Baada ya wiki moja nitaitimiza ahadi yako..!" Alisema Mansoor kwa huzuni kwani alijua ni kiasi gani Dorice alimpenda Eddy na alijua kwamba endapo angemrudisha Dorice duniani basi angemsahau Yeye na kuponda raha na Eddy. Kila alipofikiria hilo Mansoor aliumia sana moyoni mwake. Hakutamani kumkosa Dorice lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutunza uaminifu wa kutimiza ahadi yake.

    "Una uhakika utanipeleka baada ya wiki moja?" Aliuliza Dorice akimtazama Mansoor.



    "Ndio.. Usijali!" Mansoor alijibu kwa unyonge sana.

    "Hapo umenifurahisha!" Alisema Dorice na kumkumbatia Mansoor.

    "Lakini kabla haujaenda huko kuna kitu muhimu unatakiwa ufanye!" Alisema Mansoor akiwa bado amemkumbatia Doreen.

    "Kitu gani?" Aliuliza Dorice.

    Mansoor alimuachia Dorice kisha akanyoosha mkono wake na kumuonesha Dorice kiganja cha mkono wake. Kwa mshangao kidogo, Dorice akatazama kiganja cha Mansoor.

    "Unaona nini hapa?"

    "Sioni kitu.."

    "Huoni kitu? Hebu tazama vizuri"

    "Naona Pete" alijibu Dorice kwa mshangao.



    *********

    Eddy alimtazama kwa mshangao mlinzi wao. Alimkazia macho huku akimwomba msamaha kwa kumjibu vibaya hapo mwanzo.

    "Usijali.. Najua matatizo yako yanakufanya uwe hivyo" alisema mlinzi.

    "Sasa utanisaidiaje? Maana nateseka sana!"

    "Nitakusaidia tu wala usiwe na haraka... "

    "Lazima niwe na haraka Anko maana mpaka sasa hivi sijawahi hata kukojoa!"



    "Mmh! Haraka zilimponza chura zikafanya awe na mabaka. Vuta subira tu maana umefanyiwa mchezo mbaya sana." Alisema mlinzi yule huku akijifunika vyema shuka lake na kujigesha ukutani ili amalizie usingizi wake. Lakini ghafla akapigwa Kofi zito shavuni, aliruka kama kuku aliyeona hatari. Kabla hajakaa sawa Kofi lingine zito lilitua shavuni kwake, akajishika shavu na kutazama kama alikuwa amechanika lakini haikuwa hivyo kwani hakukuwa na damu yoyote ile.



    Mlinzi yule akatazama huku na kule lakini hakuona Mtu aliyempiga makofi Yale mazito yaliyotua shavuni kama radi wakati wa mvya Kali.

    "Vipi Anko?"

    "Ah.. Hanna kitu.. Niko sawa tu.."

    "Mbona umeruka sana?"

    "Usijali Eddy.. Mimi nimeaga kwetu Musoma.. Niliwaaga wajita wenzangu..!" Alisema Mlinzi huku akisikilizia maumivu makali ya vibao alivyopigwa.

    "Sikuelewi Anko ."

    "Nimeaga.. Hakuna wa kunichezea!" Alizidi kuropoka mlinzi yule kisha akatulia kimya. Mawazo tele yakamjaa kuhusu vibao vile alivyopigwa kiuchawi. Aliwaza sana kwani alikuwa ana zindiko kubwa sana, sasa kwanini apigwe vile wakati ana kings anayoiamini? Alijiuliza sana bila kupata jibu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kulipambazuka kabisa, kimwanga kidogo cha jua kilianza kuchomoza kwa mbali. Wakati huo Mr Alloyce alikuwa kwenye gari take kuelekea msituni alikopotelea Mama Eddy.

    Kichwani mwake alifikiria sana jinsi ya kutatua matatizo yanayoikumba familia yake. Hakupata njia kamili ya kuweza kutatua matatizo yake.



    Aliendesha gari kwa mwendo wa SAA moja na nusu hatimaye akawasili kwenye eneo alilotakiwa kufika, akashuka kwenye gari na kuangaza macho yake huku na kule kuona kama atamwona mkewe.



    ******



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog