Search This Blog

THE NIGHTMARE - 3

 







    Simulizi : The Nightmare

    Sehemu Ya Tatu (3)





    ***********************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Maisha ya upweke bila ya kuwa na wazazi wala walezi wa kuwasimamia yalianza muda mfupi tu baada ya mazishi ya wazazi wao. Karim alipewa majukumu yote ya kusimamia mali za wazazi wao kwakua Sharji alikua bado mwanafunzi.



    Kampuni moja iliuzwa kutokana na kuwa na mnadeni mengi waliyokuwa wanadaiwa baada ya Karim kushindwa kuiendesha.



    Sharji alipohitimu kidato cha nne, alinunuliwa gari na kaka yake kama zawadi ya kuondokana na maisha ya kuwa mtoto wa serikali na kuwa raia rasmi. Alipenda mdogo wake awe kijana anayeenda na wakati kama yeye. Hivyo alimpeleka club na sehemu mbalimbali za starehe kwakua alimuhesabia kuwa ameshakua



    Mapenzi ya ghafla kati Karim na mdogo wake yalishika kasi kiasi cha kwamba walikua kama marafiki walioshibana. Hawakuwahi kugombana na kila mmoja alimfanya mwenzake kuwa msiri wake. Hata baada ya matokeo kutoka na Sharji kufanya vizuri kwa kupata Division II, lakini kaka yake alimkatalia swala la kuendelea na shule kwakua walikua na hela za kutosha za kutumia mpaka uzeeni.



    Ta masha kubwa la mwanamuziki wa marekani Chris brown na Rihanna, ndilo liliwakosesha usingizi. Hawakutaka kulikosa hata kidogo.



    Tarehe ya tamasha ilipokaribia. Walipanda ndege wawili hao na kwenda kwenye tamasha hilo lililomeza mashabiki wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani.



    Starehe juu ya starehe ndio zilikua ndoto zao kila walalapo. Hakuna walichokiwaza kwakua walitumiwa hela mara kwa mara na babu yao aliyekuwa makazi yake ni nchini Uingereza.

    Pia kampuni yao ilikua inakua kutokana na misingi mizuri iliyowekwa na wazazi wao ambao kwa sasa walikua wameshatangulia mbele za haki.



    Mahudhurio ya kazini kama Managing Director yalikua hafifu sana. Hata alipokua akionekana ofisini basi haikuchukua hata masaa mawili. Tayari alishaondoka. Hali hiyo ilifanya kampuni yao kupoteza sifa kama mwanzoni. Lkini hayo yote Karim hakujali kwakua alikua na wateja wengi ambao kuna wengine wanategea mikopo kutoka kwake.



    Msemo wa tunakula ujana uliwakaa mdomoni kila watokeapo watu na kuwapa ushauri juu ya matumizi mabaya ya fedha waliyonayo..



    Kila siku walibadilisha wasichana kama wabadilishavyo nguo. Hawakutongoza, ila pesa iliongea.



    Hakika walikua zaidi ya masharobaro kutokana na kutopitwa na Fashion yoyote iingiayo mjini na wao kuwa watu wa mwanzoni kuzivaa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ukilinganisha na asili ya kishombe waliyorithi kutoka kwa mama yao ndio kabisa, walikua kivutio mpaka kwa watoto wa kizungu waliokutana nao katika hotel mbalimbali walizokuwa wanaenda.



    “mdogo wangu nina bonge la Surprise.” Aliongea Karim baada ya kurudi tu kutoka ofisi kwake.

    “ipi hiyo kaka.” Aliongea kwa shauku kubwa Sharji baada kusikia hayo. Maana alimjua kaka yake akiongea hayo ni lazima kuwe na kitu cha kumshangaza.

    “najua kuwa hujawahi kusafiri kupitia majini, sasa wiki ijayo tutaenda visiwa vya Comoro kama picnic fulani hivi na washikaji kibao kupitia boti ya kukodi. Unaiyonaje hii?”

    Aliongea Karim na kumuangalia Sharji ambaye muda huo tayari alijawa na furaha.

    “ndio maana huwa sikupingi brother, napenda unavyonipenda na kila siku unavyonidhihirishia upendo wako juu yangu.”aliongea Sharji na kumfata kaka yake na kumkumbatia kwa furaha.

    “usijali, we ungependelea tuondoke jumamosi au jumapili?” aliongea Karim na kumtazama mdogo wake kusubiri maamuzi atakayoyachukua.

    “jumamosi itakuwa poa zidi.” Aliongea Sharji na kaka yake akatingisha kichwa chake kama ishara ya kukubaliana nae.

    Baada ya hapo kila mmoja aliingia chumbani kwake na kujipumzisha. Kwani tayari ilishagota saa nne usiku.



    Asubuhi kulipokucha, Karim alimuachia hela mdogo wake za kutosha kula hotelini cha na chakula cha mchana. Swala la kupika kwao lilikua swala gumu sana.

    Karimu alifika ofisini kwake na kupokea nyaraka mbali mbali kutoka kwa secretary wake ambaye alikua kama msimamizi wa ile ofisi. Maana mambo mengi aliambiwa ayamalize yeye na kusababisha kupendwa sana na Karimu kwakua bosi wake alikua mvivu sana.



    Siku zilisogea taratibu sana kwa Sharji kwa kua alikua na hamu sana ya kusafiri na boti kwakua ndio chombo pekee ambacho hajawahi kukipanda toka azaliwe.



    Maandalizi yalizidi kupamba moto juu ya safari hiyo ya kwenda kustarehe kama camp kwenye visiwa hivyo vya Comoro. Kila kilichohitajika kilipatikana mapema. Walitenga bajeti kubwa itakayowawezesha kununua vitu watakavyotamani kununua wakiwa huko.



    Waliingia dukani na kununua nguo mpya kadhaa kama kawaida yao na kuzipaki kwenye mabegi yao.

    Pia hawakusahau kununua camera kwa ajili ya kurecord matukio mbali mbali watakayo yaona huko.



    Mpaka kufikia siku ya alhamisi, tayari walishatimiza kila kitu. Kilichobaki ni siku husika kufika tayari kwa safari hiyo adhimu kwao.



    Asubuhi ya siku ya ijumaa, Karim aliamka kama kawaida yake na kumuamsha mdogo wake na kumuachia kiasi cha fedha na yeye kuelekea kazini.

    Sharji aliamka kivivu na kuchukua taulo lake na kuelekea bafuni. Alipomaliza kuoga na kupiga mswaki, alilipigilia pamba zake kati ya pamba anazozikubali zaidi na kuliendea geti la kutokea nje baada ya kujitazama kwenye kioo na kuridhika na alivyotokelezea.



    Alipanda kwenye gari lake na safari ya kuelekea kwenye restaurant kwa ajili ya kupata kifungua kinywa ikaanza.

    Akiwa njiani alianza kusikia harufu nzuri ya perfume ikitokea nyuma ya gari yake. Alipogeuka hakuona mtu yeyote aliyekuwa ndani ya gari zaidi ya yeye mwenyewe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alijinusa ili aangalie kwamba ni yeye ndiye anayenukia vile, lakini aliona ni kitu kisichowezekana maana harufu ya perfume yake anaijua.



    Alichukua perfume ya kwenye gari lake na kujipulizia mkononi, aliponusa bado harufu hiyo ilikuwwa tofauti na anayoisikia. Alichoamua ni kufungua vioo na kuendelea na safari bila kujali chochote.



    Alipofika maeneo ya best bite, alipaki gari yake na kuingia ndani. Aliagiza chakula na kutengenezewa oda yake, kisha akawasha mchuma na kurudi nyumbani.



    Alipofika aliliendea friji na kuchukua kinyaji baridi akipendacho na kurudi sebuleni na kuanza kucheza game kwenye PS 3.



    Kutokana na kupenda kucheza game, muda ulisogea mpaka kufikia saa tisa mchana. Njaa ilimuuma tena na kuamua kurudi tena best bite kupata chakula cha mchana.



    Wakati oda yake ikiwa inatengenezwa, kwa mbaali akaanza kuisikia tena ile harufu ya perfume ikipuliza kutokea nyuma yake. Harufu hiyo ikamshawishi Sharji kugeuza shingo yake kutazama nyuma.

    “waoooooh!”



    Alijikuta outomatic akijisemea kwa mshangao baada ya kumuona dada mmoja mrembo mwenye asili ya kiarabu akiingia mule ndani. Hakuvaa ushungi kama alivyowazoea kuwaona waarabu wengi ambao alikutana nao. Huyu alivaa suruali ya jeanz nyeusi na juu akiwa na kikoti chake cheusi. Kati kati kulikua na nguo Fulani nyeupe iliyonakshiwa vizuri kwa mtindo wa V.



    Nakishi hiyo ndio iliwachengua wanaume wote waliobahatika kugeuza shingo zao na kumuangalia mtoto huyo wa kiarabu mwenye uzuri wa ajabu.

    Kwani aliacha sehemu kubwa ya kifua chake wazi na kuziruhusu baadhi ya sehemu ya maziwa yake kuonekana. Kifua cha binti huyo kilibeba maziwa makubwa kiasi lakini yaliyosimama bila kupigwa jeki. Pia chuchu zake zilichongoka utafikiri zilikua zinataka kutoboa nguo aliyovaa.



    Mate ya uchu yaliwajaa wanaume karibu wote na kuwafanya wengine kusogeza viti vyao kama ishara ya kumwambia akae nae siti moja.



    Catework za yule binti zilifanana na mabinti wanaoshandania urembo wa dunia. Alitembea huku anazihesabu hatua zake taratibu huku macho yake yakiwa hayaonekani kwa sababu ya miwani nyeusi aliyovaa.



    Wakati sharji na yeye akiungana na wanaume wengine kumshangaa mrembo huyo. Alishangaa zaidi baada ya mrembo huyo kusimama mbele yake na kuvuta kiti na kukaa naye meza moja.



    Alipomuangalia tu usoni yule binti, alipokelewa na tabasamu pana lililosimamisha mpaka vinyweleo vya mikono yake.



    “mambo”

    alisalimia yule dada na kuvua miwani aliyo vaa. Hapo Sharji alizidi kudata. Kwani uzuri wa yule binti ulipunguzwa kidogo na ile miwani. Maana alipovua alikua amefanana kabisa na migizaji wa filamu za kihindi Deepika Padukone.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini alipotabasamu alifanana na Manduri Dixit na alipocheka ndio kabisaa. Dimpose zilisababisha Sharji ajione yupo meza moja na Prity Zinta.



    “karibu” aliongea muhudumu baada ya kupeleka oda ya Sharji.

    “na mimi nitengeneezee kama hivi.” Aliongea yule dada baada ya kuona chakula alichokiagiza Sharji.

    “uko poa” alisalimia tena yule dada baada ya kuona salamu yake ya kwanza imemezwa baada ya muhudumu kuingilia kati.

    “niko poa sana,” alijibu Sharji huku akizidi kumuangalia yule dada ambaye kiumri alionekana ni mkubwa kidogo kwake.

    “huwa unapendelea sana kula chakula hicho?” aliuliza yule dada kama njia ya kufungua tena mjadala, maana baada ya salamu kimya kilipita kama dakika tatu nzima.

    “ ndio, japokuwa kuna vyakula vingine vipo ninavyovihusudu.” Alijibu Sharji.

    “mimi si mpenzi kabisa wa chipsi kuku, nimeagiza tu kwakua nimekuona unakula.” Aliongea yule binti na kumshangaza kidogo Sharji, maana alijua kuwa madada wengi wa mjini ndio chakula chao wakipendacho zaidi.

    “ kwa hiyo unataka kuniambia unapendelea sana ugali eeh?” aliuliza Sharji kwa kudhihaki.

    “umejuaje?..ukiwekea chipsi kuku hapa na ukaleta ugali samaki, mimi nachagua ugali samaki. Tena kukiwa na mlenda pembeni ndio hunitoi kabisaa. Yaani kama wewe ndio ungelikua unakula hicho chakula, nisingesubiri oda yangu. Tungekula pamoja halafu oda yangu ndio ungekula wewe.” Aliongea yule dada na kumfanya Sharji atabasamu.



    “karibuni sana, mjisikie mpo nyumbani.” Hiyo ilikua kauli ya muhudumu baada ya kumletea yule binti oda yake.



    Dakika moja baadae yule binti alinyanyuka na kumuaga Sharji na kwenda kulipa oda yake. Sharji alibaki kumshangaa sana yule binti kwakua hakula kabisa kile chakula. Zaidi alionja chipsi moja na kunyanyuka kama vile hakupendezwa na ladha ya kile chakula.



    Wakati akiwa amepigwa na butwaa, alishuhudia yule binti akipanda pikipiki kubwa aina ya baja yenye bomba mbili na kuondoka zake.



    Baada ya kumaliza kula chakula chake, Sharji alimchukua kuku aliyemuacha yule binti bila ya kumgusa na kuanza kumla. Alipomaliza alinyanyuka na kwenda kulipia oda yake.



    “ushalipiwa kaka na yule dada uliye kaa nae, pia kuna mzigo katukabidhi tukupe.” Aliongea cashier na kumkabidhi bahasha ndogo ya khaki.

    Alivuta taswira toka yule dada anaingia pale hakua amebeba mzigo wowote, hata hiyo Sharji alipuuzia na kuichukua ile bahasha na kuondoka nayo.



    Safari ilimpeleka mpaka nyumbani ambapo alimkuta kaka yake amesharudi toka kazini. Alishangaa kidogo uwepo wa kaka yake pale nyumbani mapema kiasi kile.



    Alijua si kawaida yake, maana hata kama akitoka mapema. Basi lazima ampigie mmoja kati ya mademu zake na kwenda kutanua nao. Hiyo ndio ilikuwa starehe kubwa ya kaka yake ambaye alikua hachagui week end wala jumatatu. Kwake ni bata kila siku.



    “vipi brother, mbona mida hii home?” aliuliza Sharji huku akiliendea friji na kuchukua kinywaji alichokua anakipenda na kurudi sebuleni ambapo kaka yake alikua anacheza game.

    “ nimeamua tu, si unajua kesho safari, xo part itakuwa humuhumu ndani mpaka mida mibovu. Muda si mrefu wataingia washikaji kwa ajili ya mkesha wa safari.” Aliongea Karimu huku akiwa bize na Game.



    “achana na game bro, kuna bonge la ishu nataka kukupa.” Aliongea Sharji na kumfanya Karim aachie padi na kusikiliza.

    “unajua brother kuna mademu halafu kuna wanawake ambao ukiweka ndani basi huhitaji pambo lingine maana anatosha kuwa pambo la nyumba?” aliongea Sharji na kumfanya kaka yake kuwa makini. Maana alikua mgonjwa wa wanawake wazuri. Akitajiwa tu warembo basi zipu humtaka kufunguka kwa umelu wa wasichana wazuri.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “bila shaka umekutana na kifaa cha ajabu sana. Nipe sifa zake nimpe maksi.” Aliongea Karimu na kumuangalia Sharji ili avute taswira ya picha halisi kwa kile atakachokiongea mdogo wake.

    “punguza mchecheto bro, unajua mazali mengine yanatuangukiaga vijukuu vya mitume kama sisi. Maana wakati nimeenda best bite kupata makulaji. Ndipo alipoingia demu mmoja mwarabu mrefu. Ananukia hatari. Hizo nguo alizo vaa basi, katokelezea mbaya.

    Hakuna mwanaume rijali aliyekua hajageuza shingo yake kumuangalia. Basi mtoto kama kafumba macho vile. Kawapita watu wote na kukaa na mimi. Hapo ndipo nilipohisi kuwa pritty zinta yupo mbele yangu. Demu akaagiza chakula nilichoagiza mimi kisha tukaanza kupiga story mbili tatu. Sema nilivyomcheki alikua mkubwa kwangu. Basi demu alipoletewa oda yake, kala kidogo tu kisha akanyanyuka na kwenda kulipia bili yake. Mwanao nilipomaliza kula, nikagonga na kuku wake aliyemuacha kisha nikaenda kulipa. Nilistaajabu kukuta yule demu kanilipia na kuacha zawadi kwa ajili yangu..”



    Aliongea sharji huku akionyesha baadhi ya vitendo alivyoweza kuviigizia. Wakati wato huo Karim alikua makini kusikiliza huku akitabasamu.

    “amekupa zawadi gani?” aliongea Karim kwa shauku kubwa ya kutaka kujua zawadi aliyopewa mdogo wake.

    “lakini napata wasi wasi kidogo, maana yule dada hakuingia na kitu chochote. Hata hakuwa na mkoba useme aliutumia kuweka hiyo zawadi. Sasa amewapa wale wahudumu saa ngapi?” aliongea Sharji na kutaka ushauri kutoka kwa kaka yake.

    “kwa hiyo haujaifungua?” aliuliza Karim na kumuangalia mdogo wake.

    “ndio.” Alijibu Shari na kumuangalia kaka yake aliyekuwa bize kuyasoma na kuyatafsiri maelezo yake.

    “kailete hiyo zawadi.”

    Aliongea Karim na Sharji akatii amri na kwenda kwenye gari yake alipoiweka. Alirudi na ile bahasha na kumkabidhi kaka yake.



    Uzito wa ile bahasha walishindwa kutabiri kitu kilichokuwa mule ndani. Kwa utaratibu mkubwa, Karimu alianza kuichana ile bahasha na kukuta karatasi lililoviringishwa mafungu mawili yenye ukubwa unaofanana. Walitazamana kwa sekunde kadhaa kisha wakashauriana waendelee kufungua ili wajue kilichopo ndani.

    “Damn..woooooh!”



    Huo ulikua ukulele wa Karimu baada ya kukuta maburungutu makubwa ya hela za kimarekani. Yalikua mabunda mawili yaliofungwa vizuri yakiwa na noti za dola mia mia.



    Thamani ya maburungutu yale walipoyalinganisha na thamani ya hela za kitanzania. Walijikuta wamepata zaidi milioni 300 za kitanzania.



    Huku Shariji na kaka yake wakiwa hawaamini kile walichokiona, kwa mbali walikiona kikaratasi kikipepea. Walijua moja kwa moja kilikua kimetoka mule ndani ya ile bahasha. Wakakifuata na kukisoma. Hicho kikaratasi kilikua na namba ya simu na jina la kike lililosomeka BARQIS.



    “Barqis, kweli atakua mwarabu. Maana hili jina limekaa kiarabu arabu sana.” Aliongea Karim huku akiziandika zile namba kwenye simu yake.

    “vipi, nimpigie?” aliuliza Karim baada ya kumaliza kuinakili ile namba.

    “hamna shida, we twanga tumsikie.” Aliruhusu Sharji na kaka yake akabofya kitufe cha kupigia simu na kuanza kusikiliza sikioni kwake.

    “inaita” aliongea Karimu kwa sauti ya chini baada ya kusikia muito wa qaswida ya kiarabu.

    “haloo”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilisikika sauti nyororo masikioni mwa Karimu. Aliweka koo lake vizuri tayari kwa kujibu.

    “haloo, mambo.” Aliongea Karim na kumfanya mdogo wake kumsogelea karibu ili asikie sauti ya upande wa pili.

    “safi, samahani naomba niongee na mdogo wako” iliongea sauti ya upande wa pili na kumfanya Karimu ashangae.

    “hayuipo hapa, ameenda kuoga.” Alidanganya Karim.

    “basi akirudi mwambie anipigie kupitia simu yake.” Aliongea yule dada na kukata simu.



    Karimu alijaribu mara kadhaa kupiga simu, lakini haikupatikana. Alimuangalia mdogo wake ambaye naye alikua haelewi chochote.

    “kwani wewe umeshawahi kuonana nae kabla au ulimpa information kuhusu mimi?” hatimaye Karim alijikuta anamuuliza mdogo wake swali lile.

    “yaani leo ndio siku ya kwanza kumtia machoni.” Aliongea Sharji.



    Wakati wapo katika mjadala juu ya yule msichana kuwafahamu wao vizuri, Simu ya Sharji ilianza kuita na kwenye kioo cha simu hiyo ilitokea namba ngeni. Walipoiangalia ilikua inafanana kabisa na ile ya Balqis. Waliangaliana na kutafakari kwa kile kilichotokea. Hata Shariji mwenyewe hakujua kua yule binti ameitoa wapi nama yake kwakua hawajapeana namba za simu kule mgahawani.



    Simu iliita mpaka ikakatika. Ilipoita tena kwa mara ya pili, Sharji alikata shauri na kuipokea bila kuongea chochote.

    “mambo SHARJI”



    Salamu hiyo ilimfanya sharji atoe macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.



    “Safi, tu.” Alijibu Sharji kiuoga.

    “nimefurahi sana kuisikia sauti yako Sharji.” Aliongea Balqis.

    “ha..hata mimi, sema umelijuaje jina langu?.” Aliuliza Sharji huku akijaribu kupeleleza maelezo ya Balqis.



    “wewe hunifahamu mimi, ila mimi nawafahamu kuanzia nyinyi hadi wazazi wenu. Mama yangu na mama yenu wamesoma chuo kimoja” aliongea Balqis na kushusha preasure aliyokuwa nayo Sharji.

    “weka loud speaker!”

    Aliongea Karim kwa sauti ndogo ambayo ilisikika vizuri na Sharji.

    “toa loud speaker bwana.”

    Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.

    “kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.

    “kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.

    “hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya upole.

    “sasa?” aliongeza Balqis

    “najisikia vibaya mnavyonitenga.” Aliongea Karimu kinyonge.

    “basi poa, unakaribishwa kwenye maongezi yetu.” Aliongea Balqis na kuachia kicheko kidogo.

    “hivi utakua na nafasi wiki hii?” aliuliza Karimu baada ya kupata nafasi ya kuongea na Balqis.

    “yap… kwanini umeniuliza hivyo?” aliongea Balqis na kumpa nafasi Karimu ya kuongea dhumuni lake.

    “tuna safari kesho ya kuelekea kwenye visiwa vya Comoro, tutakaa wiki nzima tukila raha huko. So kama una muda ni vizuri ukajiunga na sisi hiyo kesho.” Aliongea Karimu huku akionyesha msisitizo wa kile alichokiongea.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “ Sharji atakuwepo?” aliuliza Balqis na kumfanya Sharji aliyekuwa kimya wakati wote kushtuka na kujibu haraka.

    “mimi ndio kinara wa hiyo safari.” Aliongea Sharji na kufanya wote watatu kucheka.

    “kwakua Sharji atakuwepo basi nitakuja, mchango ni kiasi gani.” Aliongea Balqis na kuwafanya Karimu na Sharji kuangaliana.

    “hakuna mchango mama, tunaenda kama camp kula bata maeneo hayo waki nzima.”

    Aliongea Karimu na kumfanya Balqis kucheka.

    “poa, tutaonana kesho asubuhi.” Aliongea Balqis na kukata Simu.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog