Simulizi : Jini Zaituni
Sehemu Ya Nne (4)
Kioo kilishushwa nilipokaribia na nilipofika kabisa nilizidi kubaki mdomo wazi, lilikuwa ni tabasamu laini kutoka kwa Zai na macho ya kunihadaa
"Mbona unashangaa hivyo Zaka au huamini kama ni Mimi?"
"Siyo
kwamba hayawezi kuisha la hasha! Ila nahisi unayapenda haya Maisha au unataka
nikuache kwenye jumba lako hili la udongo etii?" Yaani sikuwahi kufikiria kwamba
siku moja nitakutana na mrembo mbishi namna hii loooh! Nilijuta kufahamiana nae
japo nilivumilia tu
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Sijui
nikuhakikishiaje kuwa nimeyachoka maisha haya lakini kuomba kwangu msaada ni
kithibitisho tosha kuwa sihitaji kuishi hivi kwahiyo usichukie kwasababu sisi
binadamu si wakamilifu katika kila jambo
tunalolifanya"
"Yameshaisha Zaka lakini usiwe
unanikasirisha hivyo ili uone sirika yangu huwa sirudi nyuma nikishatoa maamuzi
hivyo chunga" nilishusha pumzi kusikia yameisha lakini akili ikanituma niwe
mpole ili nifanikiwe la sivyo nitajutia milele nafasi adimu
niliyoipoteza
Siku hiyo nililala nikiwa na amani
tele nikiwa na hamu ya kutumia ile shilingi mia tano niliyopewa kama
kianzio.Asubuhi na mapema niliamka nikiwa peke yangu ndani kwa kuwa kulikuwa
bado hakujapambazuka vizuri nilitulia ndani nikiwa bado nina shauku ya kutaka
kujaribu ile hela.
Nilipiga hesabu ni wapi niende
kujaribia hela yangu baada ya kuitoa katika sanduku kama nilivyoelekezwa, wazo
langu likatua kwenye mikate ile mikubwa huwa naisikia tu kwa wateja wetu
wanaiita lesi lesi ambazo zitakuwa kitulizo cha njaa
niliyonayo.
Nilifanikiwa kufika katika duka moja
kubwa la mtaani kwetu nikaulizia mikate ile, Nilipopewa nikaanza kujishauri.
Nikastukia nimeropoka
"Samahani bosi unanidai
shillingi hapa"
"Jumla ya vitu vyote ni shillingi
elfu sita tu bosi wangu"
"Anhaaaa! Ok, aaaah!
Sawa, sasa kwani na hizo dawa za mbu bei
gani?"
"Shillingi elfu tano tu bosi wangu
nikupatie?"
"Hapana ila na viberiti bei gani
bwana?"
"Ni shillingi mia mia tu bosi ila dazani
utanipa mia tano tu."
"Sawa, alafu siku hizi
mnauza na redio humu etii?"
"Bosi wangu acha
masihala bhana wakati unaona kabisa hili duka ni la vyakula sasa iweje niuze
redio ama runinga?" Niliuliza maswali ambayo hata mtoto mdogo angeulizwa angetoa
majibu kwa kuliangalia tu hilo duka lenye bidhaa mbali mbali hasa vyakula hiyo
yote kwasababu ya kuogopa kutoa ile hela
yangu.
"Eeeeh! Aaah! Kweli nimejisahau tu bosi
wangu samahani kwa hilo" nilianza kuomba samahani nikiwa bado na maswali
kichwani nitaanzaje kumpa hii mia tano kwa vitu vyote
vile.
Nilibaki nimeduwaa wateja wakizidi kuja na
kutoka mpaka nikaulizwa tena
"Bosi bado hujalipia
unasubiri nini au kuna kitu kingine
nikuongeze?"
"Ha...pa...na, ila kuna kitu kimoja
nahisi nimesahau sasa najiuliza lakini sikumbuki" niliongea kwa kigugumizi uongo
unaofanana na ukweli
Nilijiwazia peke yangu sikuwa
na lakufanya nikaitoa ile mia tano nikamkabidhi muujazi, Alianza kutabasamu kwa
muda kisha akaangua kicheko huku akiangalia ile
hela.........
"Aaaah! bro unatisha siku hizi na
misimbazi yako yaani toka wiki iliyopita ulipovuna mapesa mpaka Leo hii bado
unatanua tu si mchezo aiseee!
"Kawaida mbona bosi sema tu najibana
sana ndo mana siishiwi mapema." Moyo wangu ulitulia baada ya muujazi kuniambia
ni elfu kumi hapo nikapata na amani kidogo
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nilipewa sarafu na
noti kama chenchi nilipotaka kuziweka mfukoni niliisikia sauti ikijirudia
kichwani nwangu ikisema"Zaka haupaswi kutumia hizo sarafu mpe huyo au fanya kama
umeangusha uziache."
Mmmmh! Niliguna peke yangu
mpaka muuzaji akaniangalia "vipi bosi mbona unaguna peke yako kulikoni au
nimekuzidishia chenchi?"
"Hapana ila mbona wewe
unawaza kuzidishia watu ila hauwazi kuwa labda umemuibia mteja chenchi
yake?"
"Si.. Si.. Kwa..mba....si..a..mi..ni..i..la....." Nilikatakata
maneno ni kama nina kigugumizi kwa mshangao ulionipata hadi nikashindwa
kuendelea kuongea
"Heheheeeeee!! Hilo lako babu weee kumbe ujanja wote
huo ila kitu kidogo kinakubabaisha hivyo" niliambulia kicheko cha Zai kama
unavyoelewa wanawake kwa utani wao. Ikabidi nijikakamue kuongea ili nisionekane
mwoga mbele yake japo ulikuwa ni udhaifu wangu kwake toka
mwanzo
"Aaaah! Mrembo ni mstuko tu sikutarajia kama utanifanyia
sapraiz kubwa kiasi hiki sikutegemea kiukweli" nilianza kutoa hotuba kwa Zai
kama mtu vile huku moyo ukijitahidi kutaka kutokea kwa nje
"Aiseee!
Lazima ustuke maana nimekuja kivingine kabisa tofauti na
ulivyodhania"
"Ni kama ulikuwepo maana Mimi nimezoea kuona umeshafika
kama si nyuma yangu basi ni karibu yangu"
"Ni kweli ila kwa sasa hivi
itabidi uzoee hali zote"
"Sawa lakini hii ya Leo ni mpya
kabisaaa"
"Usijali Zaka wangu huu ni nwanzo tu na kama ni mziki basi
ndiyo unatungwa hivi"
"Nashukuru kipenzi changu kwa kuniingiza katika
ulimwengu mpya"
"Aaaah! Zaka si wakati wake kwani bado mapema mno
kufanya hivyo hata hivyo nipo kwaajili yako tu"
"Mimi sina neno zaidi
ya kusikiliza na kufuata kile unachosema"
"Ooooh! Kama ni hivyo basi
tuanze safari au hujajikamilisha?"
"Nipo tayari toka jana wangu ni
wewe tu na amri yako jemedari wangu" niliongea kwa utani zaidi nikiongeza vionjo
kadhaa kwani mrembo yeyote au hata mpenzi wako kama hamna utani basi hilo penzi
litadumaa miaka yote haliwezi kukua na hiyo itasababisha kuchokana na mwisho wa
siku mtaachana kabisa.
"Zunguka mlango ule tuondoke" lakini sikufanya
hivyo bali nilisogea katika mlango wa dereva nikaufungua kisha nikamkaribisha
malkia wa moyo wangu aingie ndani na alipofanya hivyo nami bila ya kuchelewa
nilizunguka mlango unaofuata na safari ikaanzia hapo.
Gari yetu
ilisimama nje ya geti kubwa katika jumba moja la kifahari ambalo kwa kulitazama
tu utajua kuwa mmiliki ni mtu mwenye pesa sana. Zai alitoa kiongozi cha geti
hilo na kubofya na Mara moja nikaona geti lile likifunguka taratibu na kuacha
uwazi wa kutuwezesha kuingia ndani, Roho yangu ilitamani kujua vilivyomo humo
ndani pia nilitamani sana kujua tumefikia kwa nani?
Vinyweleo
vilinisimama baada ya gari kupaki nikaambiwa nishuke,nilipokanyaga chini
palipotengenezwa vizuri nikagundua kuwa sikuwa na hadhi ya kuwa humo ndani hali
iliyopelekea joto la mwili wangu kuanza kupanda.
Nilijiuliza mengi
hasa hili kwamba watu waliomo humo ndani watanionaje muonekano wangu maana
nilionekana wazi ni wa shambani huko kwani yeye Zai alikuwa amependeza kama
mwanamitindo fulani ambaye ni wa daraja la juu mno
Zai alikuja
kunishika mkononi akiwa mwingi wa tabasamu lililozidi kumpendezesha
haswa
"Zaka karibu na ujisikie upo nyumbani kwako"
"Mmmh!
Mbona unasema nijisikie nipo nyumbani kwangu kwani humo ndani hakuna watu?"
Nilimuuliza swali lililoutesa ubongo wangu kwa kitambo kifupi toka niingie humo
ndani
"Swali nzuri, hapa ni makazi yako mapya na ndiyo Maisha yako
mapya kwa ujumla pia humu ndani utaishi wewe na mimi tu hakuna mtu
mwingine"
"Unasema kweli Zai?" Niliuliza bila
kujiamini
"Hakika ni kweli ninayo yasema."
Moyo ulilipuka
kwa furaha iliyochanganyikana na machozi, sikuficha hisia zangu nilimkumbatia
Zai kwa nguvu huku kilio kikiongezeka Zai akawa ananipiga piga mgongoni
kunituliza, nilimuachia nikapiga magoti chini nikimshukuru hata muumba kwa
kunifikisha pale nikazidi kulia nikiwa nainuka nilipokuwa nikamkumbatia tena
Zai.
Tuliingia mpaka ndani nikaonyeshwa mazingira yalivyo nikiwa
natembezwa kila chumba na baada ya hapo niliruhusiwa kuoga japo siku hiyo
ilikuwa ya tofauti kwangu Zai alikuja bafuni kunisugua sugua kitu ambacho
sikuwahi kufanyiwa hapo kabla.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baada ya kuoga
nilikuta nguo nadhifu zilizoendana na watu wazito(wenye pesa zao) nikazivaa na
kuongozwa moja kwa moja na Zai sehemu ya kulia chakula. Nilishangazwa na vyakula
vile ambavyo sikujua vimepikwa saa ngapi na Zai na aliandaa saa ngapi maana
nilikuwa nae karibia mda wote.
Siku hiyo ilikuwa ya vichekesho na
vituko sana kwa Zai kila aliponiangalia kwani sikuwahi kutumia uma wala visu
kukata na kula sasa ikanibidi kutumia mikono na zile juisi zilipata kazi siku
hiyo maana nilimaliza jagi nzima hata vile vyakula nilikula karibia vyote mpaka
nikahisi kuvimbiwa.
Zai hakuwa na neno zaidi ya kucheka ninavyofanya
maajabu yangu.......
Nilipomaliza kula loooh!
Nilikuwa nimeongezeka uzito kwani sikuweza kuinuka kirahisi na hapo ndipo aibu
zilinishika baada ya kuangalia mezani palivyo chafuliwa kwa fujo
zangu.
Zai alikuwa ananiangalia tu hakuwa akishughulika na chochote
zaidi ya kucheka na kutabasamu kwa vitimbi nilivyoonyesha siku hiyo, aliamua
kuinuka akanifuata nilipo akaanza kuninawisha mikono japo mimi sikuwa na
muangalia kutokana na aibu kuu niliyoionesha kwake tena ingekuwa afadhali kama
ni mwanaume nwenzio lakini kwa mwanamke ni aibu
isiyoelezeka.
Tuliingia chumbani kupumzika Zai akiwa amevaa nguo laini
za kulalia ambazo zinaonyesha umbo lake halisi,nikawa na kazi ya kumtazama jinsi
alivyopendelewa katika uumbaji. Hakika nilitamani kuweka historia siku ile ya
kufungulia nyumba ya gharama namna ile na pamoja na kupata penzi la Zai kwa siku
moja.
Lakini haikuwezekana kutokana na umahiri niliouonesha mezani
mpaka nikawa najilaumu kwanini nilikula kwa papara vile bila kufikiria,sikuwa na
jinsi niliamua kuutafuta usingizi japo tumbo lilikuwa linauma kutokana na mzigo
mzito kulielemea.
Asubuhi ya siku hiyo niliamshwa na Zai jambo ambalo
sikulizoea hapo kabla,alinibusu katika paji la uso
"Umeamkaje mpenzi
wangu" alinisabahi baada ya kunibusu
"Salama tu mama watoto sijui wewe
u hali gani?"
"Mimi ni mzima wa afya kabisa pole na
uchovu"
"Mmmh! Uchovu upi tena mbona sikufanya kazi
yoyote"
"Aiseee! Kweli nimeamini wewe ni msahaulifu kwani ulivyolala
uliota nini?"
"Mmmm! Aaaah! Ni ndoto ya kawaida tu"
"Zaka
acha kudanganya,uliota nini Jana?" Aliweka mkazo lakini si kwamba nilishindwa
kumwambia ila aibu zilinitawala mno
"Ile ndoto Zai ni kama ndoto
nyingine tu hivyo usiwe na wasi wasi" nilizidi kujitetea
"Hivi Zaka
jamani usiponiambia mimi mkeo mtarajiwa utamwambia nani sasa kama hilo jambo
ndogo tu unashindwa kusema"
"Ni kweli ni jambo ndogo kwako lakini
kwangu ni kubwa"
"Basi na mimi siondoki mpaka uniambie uliota nini
mpendwa" nilikuwa nimekamatika kwasababu mimi naelewa kuwa waswahili wanasema
ndoto uliyoota usimuhadithie mwenzio ila Zai alikuwa ameniganda kama
nini?
"Zai sikiliza kwa makini Mimi niliota nipo katika kitanda kimoja
cha kifahari japo hata chumba kilikuwa cha ghali mno na sikuwa peke yangu bali
na wewe hapo,ila kilicho nishangaza tulikuwa katika mechi na nadhani ilikuwa
fainali maana mchuano ulikuwa si wa kitoto kama zilivyo mechi nyingine. Hiyo
ndoto ndiyo niliyoota"
"Ha! Ha! Ha! Ha!" Zai alikuwa
ananicheka
"Sasa unacheka nini? au ni mazuri hayo kwasababu ndoto hata
haichekeshi" nilianza kukasirika baada ya kuona Zai
ananicheka
"Haichekeshi ila umenifurahisha ulivyokuwa unaficha ficha
ni kama vitu vya ajabu"
"Ina maana Zai wewe unaona ni kitu cha kawaida
hicho tena unavyoniona hapa nina mchoko hata sijiwezi ni kama ile mechi ilikuwa
ya ukweli" nilizidi kumsisitiza Zai kuhusu hiyo ndoto kwani yeye aliichukulia ya
kawaida mno
"Pole kipenzi changu kwa ndoto uliyoota na ni kweli kabisa
siyo ya kawaida"
"Nimeshapoa japo bado nina mchoko"
"Sawa
lakini nilikuuliza nikiwa na kusudio langu maalumu"
"Lipi tena mbona
unaanza kunitisha" nilistuka kusikia alikuwa na lengo lake kuniuliza niliota
nini?
"Umeuliza vyema,ile ndoto uliyoiota haikuwa ndoto kama
ulivyofikiria wewe bali ni ukweli mtupu ila nilifanya vile kwasababu sikupenda
haya mazingira tufanyie kitu kama kile." Alijieleza kwa upana ili nimuelewe
lakini mimi niliona wazi kuwa anatania
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Zai acha utani
mbona mimi nilikuwa nimelala na kama ingekuwa tumefanya kweli si ningekuwa
katika ufahamu wa kawaida kuwa nilifanya hicho kitendo"
"Mimi naona
hatuaminiani ila vithibitisho ni viwili kwanza angalia kama umevaa chochote
mwilini mwako." Nilijichungulia haraka ili nihakikishe anachosema
"Ni
kweli sijavaa chochote" nilimjibu kwa wasi wasi nikimuangalia
usoni
"Je, unakumbuka kama jana ulilala na nguo au
mtupu?"
"Nililala na nguo" nilimjibu upesi
upesi
"Vizuri,kithibitisho cha pili ni huo mwili wako unajisikiaje
hapo ulipo?"
"Ni mchovu mno kama nilietoka kutumika mda si mrefu sana"
nilimjibu nikiwa nimeinamisha kichwa kwa aibu
"Safi,kwahiyo umeamini
nilichosema hapo mwanzo?"
"Ndiyo,nimeamini na sina kipingamizi
chochote" nilimjibu huku nikijaribu kumtazama usoni ambapo tulikutanisha macho
ana kwa ana ila yeye aliyashusha macho yake chini kwa haraka
"Zaka
nilikuahidi kuwa kama utatimiza masharti yote nitakupa zawadi ya mwili wangu
mara moja tu na ndivyo nilivyofanya ile jana na hutonigusa tena mpaka tuoane"
aliniambia akiwa ameinamisha kichwa vile vile safari hii akiwa ananionea aibu
mimi jambo lililofanya nitoe tabasamu la kuibia ibia
"Nimekuelewa Zai
sasa ni wewe tu kuniambia ni lini unaenda kunitambulisha ili nikuoe" niliongea
hivyo kwasababu ile mechi ya jana yake ilikuwa adimu sasa Mimi nilitaka walau
niirudie japo nilijiuliza kwa mfumo upi na jibu likawa ni kuoa
tu
"Zaka wangu kunioa si rahisi kama unavyofikiri kwani bado una
mitihani mingi mbele yako"
"Mmmh! Ina maana mitihani haijaisha tu!"
nilimuuliza kwa mshangao
"Ulifikiri umemaliza ile ilikuwa ya kwangu tu
sijajua kama nyumbani watakuachia au la"
Nilibakia mdomo wazi maana
Mimi nilijua kuwa nimeukata sasa kusikia mitihani bado akili ikaanza kuvurugika
kwasababu kama mitihani ya Zai ilinitoa jasho itakuwaje hiyo mitihani ya wazazi
wake.
"Zaka hayo mawazo yako yatakupa presha bure,si nimeshakwambia
kuna walakini kati ya kupewa au kutopewa mitihani kwahiyo kuwa mpole" alinipa
moyo kwasababu alijua ninachokiwaza
"Kama watasamehe kunipa mitihani
nitakuwa na amani tele"
"Nitajaribu kuwaambia
wakuache"
"Nitashukuru sana mpenzi"
"Zaka kifungua kinywa
kipo tayari mezani hivyo inatakiwa ukaoge kisha uungane nami kupata chai na
baada ya hapo nikakukabidhi ofisi yako na kukutambulisha kwa wafanyakazi wako
kama bosi mpya"
"Heeee! Ina maana kila kitu tayari imebaki ni mimi
tu?" Niliuliza kwa mshangao maana sikutarajia kama nitaanza kazi mapema kiasi
hicho
"Ndiyo nataka uwe mzoefu mapema na kazi yako ndiyo maana
nimewahi kukuandalia mapema hiyo kazi"
Nilimkimbilia pale alipo
nikamkumbatia huku nikitoa mabusu mfululizo mpaka Zai akanitoa kwa
nguvu
"Hebu wahi ukaoge bwana tunachelewa"
"Nitaenda ila
hautaki hata nikushukuru kidogo"
"Kwani wewe Zaka uliwahi kusikia wapi
kuna shukrani za aina hiyo"
"Niliwahi kushuhudia kwenye runninga
wapenzi wanavyopeana pongezi za kipekee kama nilivyofanya Mimi" nilimtania Zai
wangu kwa mbwembwe
"Mmmh! Aya baba watoto endelea kuiga siku moja
yatakutokea puani"
"Sawa nitakazana ili ufurahi mama
watoto"
Niliingia bafuni kuoga na baada ya dakika kadhaa nilikuwa
nimeungana na Zai mezani kupata kifungua kinywa cha siku hiyo,kiukweli yale
mapishi hayakuwa ya kawaida kwani ladha yake sikuwahi kuisikia na hata
kuisimulia sidhani kama itaeleweka kwasababu ile chai ilikuwa imepikwa ikapikika
ni kama sio ya dunia hii........
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nilijitahidi sana
nisifanye kituko kama cha jana hivyo nikawa nakula taratibu mno tena kwa umakini
wa hali ya juu,Nilimsifia sana Zai kutokana na ufundi wake wa kupika mapocho
pocho ambayo hata kama angekuwa ni mgonjwa asiye na hamu ya kula lazima angekula
chakula kile kwa jinsi kinavyovutia kwa nje.
Tulifika katika jengo
moja kubwa na kujitoma ndani ikiwa ni sehemu yenye mandhari nzuri kiofisi na
inayovutia kwa mteja yeyote anayetaka kuhudumiwa mahali hapo. Wafanyakazi
walikuwa wawili sehemu ya mapokezi wote wakiwa wa kike na wenye mvuto japo
hawakumfikia mrembo wangu Zai.
Kila mtu alikuwa bize na majukumu yake
ila walipotuona waliacha shughuli zao na kutukaribisha kwa nyuso za furaha
mno,Zai alinitambulisha kama bosi mpya kwao,wao hawaku shangazwa na ujio wangu
kwani taarifa walikuwa nayo na pia sikufanana na yule Zaka wa zamani maana
nilikuwa nanukia pesa kwa mavazi na hata mvuto niliokuwa
nao.
Nilipelekwa mpaka katika ofisi yangu na kukabidhiwa majukumu
yangu kama bosi wa kampuni ya usafirishaji wa bidhaa na vitu mbalimbali hasa nje
ya nchi. Nilianza kazi siku hiyo kupitia maelekezo kadhaa kutoka kwa Zai na
nilishangazwa na uwezo niliokuwa nao wa kutimiza majukumu yangu na kutambua
baadhi ya vitu ikiwa ni siku yangu ya kwanza kabisa kuanza kazi
hiyo.
Nilikuwa najiandaa kutoka ofisini kwaajili ya kwenda kupata
chakula cha mchana lakini kabla sijafanya hivyo nilipata mgeni,ni kawa sina budi
kumruhusu aonane na Mimi kwani huyo ndiye mteja wa kwanza kutaka kuonana na Mimi
tofauti na wengine waliomaliza shida zao mapokezi.
Aliingia msichana
mmoja mrembo mno mpaka mwili wangu ulisisimka,macho yakizidi kung'ang'ania
kumtazama,fikra nazo zikamsujudu kwa urembo aliokuwa nao,ni kama mioyo yetu
ilikuwa na uvutano au mawasiliano kwasababu Mimi nilivyokuwa namtazama yeye
ndiyo kwanza aliacha mdomo wazi kwa mshangao licha ya hivyo vyote lakini
hakuthubutu kuongea japo hatukufahamiana na ni Mara ya kwanza
kuonana.
Sikuwa na ujanja siku hiyo mbele ya mrembo kama yule hasa
pale ambapo macho yangu yalitua kifuani kwa binti yule na kukumbana na cheni
moja nzuri ya dhahabu iliyomkaa vyema,niliamua kuvunja ukimya kwa kumkaribisha
aketi nae bila kusita aliitikia wito huo na kuanza maongezi
"Habari
yako dada?" Nilianzisha maongezi hayo kwa salamu
"Safi,pole na
kazi"
"Sijapoa bado mpaka nitakapomaliza majukumu ya Leo" tulicheka
kwa pamoja ni kama marafiki wa mda mrefu
"Nafikiri wewe ndiye mhusika
mkuu katika hii kampuni ya usafirishaji"
"Haswaaa ndiyo Mimi sijui
nikusaidie nini mrembo" nilimuuliza nikiwa hata jina
sijamfahamu
"Sawa,kwa jina naitwa Silvana ni mmoja kati ya wahusika wa
kusambaza bidhaa mbalimbali nchini hivyo nimefika hapa kwaajili ya kuomba
kusaini mkataba wa kusafirishiwa bidhaa toka nje ya nchi kuja humu
nchini"
"Haina tatizo unaweza kufika pale mapokezi utapewa mkataba
uusome kama unakubaliana nao basi utakamilisha kila kitu
huko"
"Ahsante na nikutakie kazi njema" alinipa mkono kisha akaanza
kuondoka mimi nikiwa namsindikiza kwa macho lakini ghafla alisita kuendelea
akanigeukia
"Samahani kama nitakuudhi,ningependa kufahamu jina
lako"
"Bila samahani Silvana nilisahau hapo awali kujitambulisha,niite
Zaka itapendeza zaidi"
"Una jina nzuri,pia nina ombi lingine kama
hautojali"
"Bila shaka unaweza kuendelea" nilijua naumbuka kama
litakuwa swali kuhusu kampuni yetu hivyo nilajiandaa kuruka swali kama
litanishinda
"Naomba unipatie mawasiliano yako
tafadhali"
"Mmmh! Sawa" niliguna kwa mshangao maana isingekuwa rahisi
yeye kuchukua namba yangu badala ya namba ya kampuni kitu ambacho kiliniongezea
maswali lukuki kuhusu yeye.
Silvana aliniaga huku akilifinya jicho
moja kama wanavyosema wenzetu "kukonyeza" akizidi kutabasamu na Mimi nikafanya
vivyo hivyo japo sikuwa nawaza sana kuhusu yeye au urembo
wake.
Nilienda kupata chakula cha mchana kisha nikarudi ofisini mwangu
kuendelea na majukumu mpaka ilipohitimu saa kumi jioni ndipo nilifunga ofisi
yangu nikiwaacha wafanyakazi wa mapokezi
nilipofika nje nilishangaa
kumuona Zai akiwa ameegemea gari yake akinisubiri sikushangazwa sana na ujio
wake kwani nilifahamu wazi ni jinsi gani anavyonipenda lakini nilistaajabishwa
na uangaliaje wake ni kama mtu ambaye ndiyo Kwanzaa tumeonana siku
hiyo.
Nilianza kujistukia kuwa labda amenigundua nilichofanyiwa
ofisini Leo na Silvana nikazidi kusonga mbele kwa uoga na nilipomkaribia
alitabasamu
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Umebadilika sana
Zaka si yule aliyekuwa mvuvi kwa muonekano ulionao"
"Mmmh!!
Ninaonekanaje kwani mbona Mimi naona sina tofauti yoyote na hapo awali"
niliongea nikiwa najitazama vizuri huku nikijigeuza kama mgombea
umisi.
"Zaka sasa hivi wewe niwa tofauti kwanza una mvuto kwa kila mtu
anayekutazama na pili ni mtanashati wa nguvu ambaye mda si mrefu utaanza
kusifika kila kona"
"Inawezekana unayoyasema ila sina uhakika nayo"
niliongea nikionesha mashaka kuhusu suala hilo
"Zaka nikuambie mara
ngapi kuwa kwangu umefika hivyo amna linaloshindikana mpenzi wangu bado
hauniamini tu"
"Nakuamini kwa vyote hivyo huna budi kujiuliza kama
nakuamini kipenzi cha moyo wangu" niliongea kwa msisitizo baada ya kubaini kuwa
hajatambua chochote kuhusu Silvana.....
Tukutane tena Alhamisi pia
ahsanteni wote mlionipa pole kutokana na afya yangu kwa sasa Mungu awabariki kwa
mioyo mliyonayo.
"Nakuamini kwa vyote hivyo huna
budi kujiuliza kama nakuamini kipenzi cha moyo wangu" niliongea kwa msisitizo
baada ya kubaini kuwa hajatambua chochote kuhusu
Silvana.....
Tulipanda katika usafiri aliokuja nao
Zai,sikuwa najua kutumia vyombo vya moto kama gari na pikipiki hii ilinifanya
niwe mtazamaji kwa dereva wangu Zai jinsi anavyoumiliki usukani
vilivyo.
Zai alitambua umuhimu wa mimi kufahamu
kuendesha gari ili niendane na maisha hayo pia kupunguza ghasia za hapa na pale
endapo mpenzi wangu huyu atakuwa ametingwa kwa namna moja ama
nyingine.
Nilimshangaa Zai kwani hakupitia
nyumbani kama ilivyokuwa safari yetu baada ya kutoka kazini ila alienda moja kwa
moja katika uwanja wa mpira kwaajili ya kunielekeza jinsi ya kuendesha
gari.
Nilifurahi sana kwasababu sikuweza kumwambia
anifundishe kutokana na aibu niliyonayo pia nilikuwa ni mzito sana wa kusema
jambo na mara nyingi huwa nahangaika nianzie wapi kusema
kinachonisibu
Mazoezi yalianza nikiwa najifunza
taratibu na kwa vitendo zaidi na kwa bahati nzuri nilipata mwalimu muelewa sana
kwani alinifundisha kwa vigezo maalumu na wala hakuwa mwepesi wa hasira,hii
ilinifanya Mimi nielewe mapema mno kuliko hata
alivyotarajia.
Zilipita siku kadhaa Silvana akiwa
anawasiliana na Mimi Mara kwa Mara mpaka ikafikia wakati tunatoka nae kula
chakula cha mchana na mda mwingine huniomba nikapate kifungua kinywa nyumbani
kwake lakini nilimkatalia kata kata ijapokuwa sikumwambia kama tayari
nimeshaoa.
Utajiri wangu ulizidi maradufu huku
sifa na kufahamika vikiwa mbele kutokana na ukarimu,utanashati pia fedha
nilizokuwa nazimiliki kupitia kampuni yangu ambayo hakuna hata mmoja aliyejua ni
nani anayefanikisha hayo yote.
Waswahili walisema
pesa ni sabuni ya roho sio uongo kabisa kwani walitokea wadada warembo kupita
maelezo wakinitaka niwe nao kimapenzi lakini niligoma kabisa kwasababu sikuwahi
kuwaona kipindi cha nyuma ambacho nilikuwa hohehahe tena masikini wa
kutupwa.
Hata ofisini kwangu wafanyakazi niliokuwa
nao walithubutu hata kuvaa nusu utupu ilimradi bosi wao niwaone lakini hauwezi
kuamini machoni nilikuwa na pazia ambalo ni jeusi tii na nzito kiasi kwamba
sikuona hayo yote wanayoyafanya mbele yangu. Ndipo niliamini Kuwa Zai ameniteka
vilivyo na wala sikuwa na ujanja mbele
yake.
Nakumbuka siku moja nikiwa ofisini alikuja
msichana mmoja mzuri wa wastani akiwa amevalia koti moja refu na la
kisasa,nilimkaribisha kama mteja wangu lakini kadri sekunde zilivyozidi kuyoyoma
ndivyo alivyozidi kurembua macho yakiwa yamemregea,ghafla akainuka kwenye kiti
na kulitupa koti chini
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Yalabiii!!
Sikutegemea tukio kama hilo kutokea ofisini kwangu nikabaki nimekodoa macho bila
hata kupepesa kope zangu,Yule msichana hakuishia hapo alikuja kukaa mezani akiwa
na chupi tu na sindiria vilivyositiri nyeti zake hakika Mimi Zaka nilijuta
kufahamika.
Nikiwa katika sintofahamu ya nini
nifanye nilighutuka baada ya kumuona yule msichana akiwa ameshazunguka upande
ule nilipo lahaulaaa!! Kama ni upele ulikuwa umemfika mkunaji aliyebobea lakini
kwangu ilikuwa kama sinema lililopambwa vizuri mbele
yangu.
Katika Maisha niliyowahi kuishi hata haya
mapya ya kiutajiri sikuzoea starehe wala kuona vitu vya ovyo kama hiki
kilichonitokea,yule mdada alifika mpaka nilipokaa akageuza kiti na kunikalia
miguuni loooh!! Alipofanya vile nilijihisi kupaa kutokana na kutopata vitu hivyo
kwa siku nyingi,
Hali yangu ikiwa tete mda huo
yule mdada alitumia udhaifu huo kwa haraka akailegeza tai na kuanza kufungua
vifungo vyangu taratibu,nikiwa namtazama bila kufanya lolote la kunisaidia
katika sakata hilo.
Alifungua vifungo vyote
nakuanza kunishika shika kifua akaona bado haitoshi akahamia kwenye zipu ya
suruali yangu,baada ya kusikia zipu inafunguka ndipo akili ikanirudia sawia
nilipiga yowe la hatariii kumuita
Zai
"Zaiiiiiiiii....... Zaiiiiii......Zai......."
sikumalizia kuita radi ilipiga katika pembe moja wapo ndani ya ofisi yule mdada
akaniachia kutokana na kupagawa akiangalia kule ambako radi imetokea akiwa
anapumua kwa kasi
Moshi mzito ulitanda ofisini
kisha ukaanza kupungua hapo ndipo nilishuhudia Zai akiwa anatisha mno macho yake
yakiwa mekundu kama nyanya zilizoiva kupita kiasi,akiwa amekunja sura
akimuangalia yule mdada
Mimi nilikuwa natetemeka
mno ni kama nimewekewa mtetemo wa simu ya nokia,ganzi mwili mzima huku nikiwa
nashangaa Zai alivyokuwa kiumbe wa ajabu anaetisha mno ambaye sijapata kumuona
hapo
kabla.
"A...a...a..na..ta...ka...Ku..ni...ba....ka"
niliropoka bila kukusudia
Zai hakusema neno zaidi
ya kumkazia macho yule mdada,akatoka katika ile kona na kumfuata na kabla
hajamfikia nilisikia kelele za mjeredi zikitokea kule aliko yule mdada huku
akitoa kelele za maumivu makali na alama za mistari zikiwa zinapita kila sehemu
ni kama mtu anayechorwa chata.
Zai hakuwa na
huruma nae hata chembe alichokifanya ni kumsogelea yule mdada na fimbo zikakoma
hapo hapo,alimshika usoni kwa makucha yake akiwa anamfinya finya huku damu
nyingi zikiwa zinamwagika,yule mdada akiwa anapiga kelele za kuomba
msamaha.
Zilipita kama dakika mbili akiwa
anamfinya kisha akatumbukiza mkono mwingine kifuani na alipoutoa nilishuhudia
akiwa ameshika kitu kinadunda dunda kwa ufahamu wa kawaida niktambua ni moyo
ule.
Nikiwa katika tukio la kusikitisha kama lile
nikiwa naushuhudia ukatili wa Zai kwa macho yangu mawili kiukweli nilitokea
kumuogopa sana Zai huku nikijiapiza kutovunja masharti mpaka
kufa.
Zai hakujali kama nipo pale alikula ule moyo
mbele yangu kisha akatoweka na yule msichana,Nilikurupuka pale nilipo na
kukimbilia katika mlango,nilipotoka nikakutana na wafanyakazi wakinitazama kwa
hofu wakiniuliza kulikoni huko nilikotoka nakumbuka niliwajibu kuwa "hamjasikia
kelele yoyote ile" wao wakajibu hakuna
aliyesikia
"Msichana aliyetoka humu ofisini
kwangu amepita hapa?" Niliwauliza nikiwa bado na
kiwewe
"Hapana bosi hakuna msichana aliyepita
hapa,kwani ulikuwa na mtu ofisini?" Nilitupiwa swali lililozidi kuuchanganya
ubongo wangu
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/--
"Swali gani hilo
mnaloniuliza kwani nyie si mmemruhusu dada mmoja hivi anione ofisini?" Na Mimi
niliuliza swali ikawa ni swali kwa swali
"Hapana
bosi hatujaruhusu mdada yeyote yule kuingia ofisini kwako" jibu hilo lilinifanya
nichanganyikiwe zaidi
"Ooooh!! Sawa sawa Mimi
naenda kupumzika hivi sasa kwahiyo mambo yote simamieni sijisikii vizuri kabisa"
niliamua kuondoka kutokana na kuzidi kuvurugwa na majibu
yao............
Nilichukua usafiri wangu
nikielekea nyumbani kwangu nikiwa siamini kile kilichotokea ofisini muda mfupi
uliopita,nikiwa njiani nilikumbuka kelele za maumivu alizokuwa akipiga yule
msichana nilishindwa kuvumilia chozi likinidondoka taratibu kwani lile tukio
lilinitisha mno.
Nilifika nyumbani nikapaki gari
yangu na kuanza kuelekea ndani lakini kabla sijaufikia mlango ulifunguliwa na
Zai akiwa katika tabasamu pana hali iliyodhihirisha ni mwenye furaha isiyo na
kifani,nilisimama nikiwa namtazama usoni nakujiuliza maswali kuwa kwanini
anafurahi wakati tukio lililotokea ofisini ni kubwa kuliko matukio mengine
yaliyowahi kunitokea hapo nyuma.
Sikutabasamu wala
kuongea kutokana na msongo wa mawazo ulioletwa ghafla na matukio ya ajabu
ajabu,mpaka nafika nyumbani pale nilikuwa sijielewi kama ni Mimi ndiye niliyaona
Yale aliyofanya Zai au niliota na ukizingatia maelezo ya wafanyakazi wangu ndiyo
yalizidi kunichanganya zaidi.
Zai alikuwa ametanua
mikono anikumbatie lakini Mimi sikuliona hilo kutokana na kuchanganyikiwa
nilazidi kusimama nikimtazama lakini mawazo hayakuwa hapo nilipo nilikuwa mbali
mno
"Zaka mpenzi wangu ina maana hautaki
nikukumbatie jamani eeeeh!" Alikuwa ananisemesha lakini bado nilisikia huku
vikatokea kule
"Zaka...Zaka....Zaka....weee Zaka
si nina kuita Mimi" nilishtuka kusikia sauti ya ukali ya Zai nikama nimepigwa
shoti ya umeme
"Hivi Zaka una mawazo gani mpenzi
wangu mpaka unakuwa hivyo hata kunikumbatia hautaki au nimefanya vibaya kuja
kukupokea hapa nje?"
Aliniuliza maswali mfululizo
na halo ndipo akili yangu ikazinduka nikakumbuka alichokifanya looooh!!
Niliogopa hata kumsogelea pale alipo nikaanza kutetemeka upya nilipoikumbuka ile
sura yake ilivyokuwa inatisha
"Zaka tafadhali
njoo usiogope ni hasira ndiyo zilisababisha nikafanya vile njoo mpenzi wangu
njoo" alianza kuniita akiwa ananibembeleza lakini sikuthubutu kunyanyua kiatu
changu kusogea pale alipo
Aliniangalia kwa huruma
papo hapo nikaanza kumfuata na kumkumbatia sikutambua amenifanyia kitu gani
mpaka nikakubali kumsogelea kirahisi namna ile,Ilipita siku hiyo na asubuhi
iliyofuata sikutamani kwenda kazini tena hivyo nikaomba wafanyakazi wangu
wanisaidie shughuli mbali mbali mpaka pale nitakapojisikia
kwenda.
Nilikaa nyumbani siku mbili nikiwa na Zai
na uoga ule ulinitoka kabisa kwani sikukumbuka lile tukio mara kwa mara na kila
nilipolikumbuka na kutaka kumuuliza Zai nilisahau nakuanzisha mada nyingine
tofauti.
Ndani ya hizo siku mbili Silvana alikuwa
ananijulia hali kila mara jambo ambalo lilizidi kuniweka matatani hasa
nikimfikiria Zai japo yeye hakuonesha kujali hata kama nawasiliana nae nikiwa
nae pamoja tukifurahia penzi letu.
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Siku hiyo nilienda
ofisini kama kawaida na utendaji wangu wa kazi haukushuka kiwango ila ulizidi
kuwa bora zaidi,mchana nilitoka na Silvana kupata chakula cha mchana kisha kila
mtu anarudi kazini kwake kuendelea na majukumu,nilishangazwa sana na Zai kwani
alionekana kutokujua kabisa jambo hili na wala hakulitilia
shaka.
Siku zilizidi kusonga huku mahusiano kati
yangu na Silvana yakishamiri vilivyo ikafikia wakati hata chai ya Zai sikuinywa
nikiwa natoa sababu za kuwahi vikao na mengine mengi.Hakika niliona mabadiliko
yangu waziwazi na kila nilipojaribu kujirekebisha na kujizuia nisiwe na Silvana
haikuwezekana kabisa kumbe sikujua kilichopo mbele yangu mpaka nikawa
vile.
Zai hakuonesha tofauti siku zote hizo
nilizoanzisha visababu vya ovyo ovyo bali alizidisha upendo kuliko ule wa awali
mpaka nikawa najihisi vibaya lakini ningefanyaje wakati njia ya kujinasua
sikuiona ikanibidi niwe nalia kimoyo moyo kusogeza hukumu
yangu.
Asubuhi moja nikiwa ofisini kwangu alikuja
Silvana akiniomba niende nae mgahawani ili tupate chochote kuridhisha matumbo
yetu nilimkubalia huku nikiwa nimeacha kazi nyingi ambazo toka niwe karibu na
Silvana nilikuwa mvivu wa kupindukia katika utendaji wangu wa
kazi,
Tulifika mpaka mgahawani na kupata chakula
ambacho tulitumia muda mrefu kukimaliza,kwa muonekano tulifanana na wapenzi
walioshibana lakini haikuwa hivyo kwani hakuna aliyemtamkia mwenzie kuwa
anampenda.
CHANZO:
https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment