Search This Blog

KISIWA CHA HARISHI - 5

 







    Simulizi : Kisiwa Cha Harishi

    Sehemu Ya Tano (5)





    “Wewe kijana fungua kizibo hicho?’ Sauti ya Harishi ikanigeukia mimi.

    “Usifungue. Mwache atoke mwenyewe. Sisi tumeshajitolea, liwalo na liwe!” Yasmin akaniambia.

    Wakati wote nilikuwa najiuliza kama Harishi alikuwa hawezi kutoka mwenyewe kwenye ile chupa mpaka atuombe sisi tufungue kizibo. Nikataka kupata uhakika kama kweli Harishi alikuwa amenasa na asingeweza kutoka bila msaada wetu.





    Nikamwambia Yasmin “Tusifungue hii chupa tuone nini kitatokea”

    “Wewe achana naye, kama akitoka mwenyewe na atoke, potelea mbali!”

    Nilikuwa nimesimama kando ya lile kabati. Yasmin alisimama karibu na kitanda. Macho yetu sote yalikuwa kwenye ile chupa.

    Ingawa nilikuwa nimejikaza kiume, hofu ilikuwa ikitambaa kwenye mishipa yangu. Yasmin hakuonesha kuwa na hofu hata chembe. Nilishangaa kuona msichana ambaye siku zote nilimuona dhaifu, siku ile alikuwa amejaa ujasiri usio kifani. Hapo niliamini kweli kuwa Yasmin alikuwa amejitolea kufa kupona.

    Ile sauti ya Harishi iliyokuwa ikitoka kwenye chupa ilipotea lakini ule moshi uliendelea kuonekana. Kwanza ulionekana moshi wa rangi nyeusi kisha ukabadilika na kuwa wa rangi nyeupe. Baada ya muda kidogo ulibadilika tena na kuwa wa rangi nyeusi.

    Mawazo yangu yote yalikuwa kwenye kifo kibaya kilichokuwa kinatungoja.

    . Nilijua kuwa Harishi angekizibua mwenyewe kile kizibo na kutoka. Hapo hasira zake zisingekuwa na kifani. Nilipata wazo la kumwambia Yasmin tukimbie lakini nikajiuliza tutakimbilia wapi usiku ule? Na ni wapi ambapo Harishi hataweza kufika?

    Muda uliendelea kupita. Tuliona Harishi hatoki kwenye ile chupa kama ilivyo kawaida yake. Aliendelea kututaka tukifungue kizibo kwa sauti ya upole akiahidi kwamba hatamuua yeyote.

    Nikahisi inawezekana kwamba kitendo kile cha kuwahi kukifunga kile kizibo cha cha chupa wakati Harishi yumo ndani ya chupa ile akiwa katika umbile la moshi, kilikuwa kimemzuia kutoka na hakuwa na uwezo tena wa kutoka mwenyewe.

    Hapo hapo nikazikumbuka simulizi za wazee wa zamani ziizosema kwamba majini walikuwa wakifungiwa ndani ya chupa na kutoswa baharini pindi wanapofanya makosa.

    Kumbe ni kitu kinachowezekana kweli, nikajiambia.

    “Sisi tunaiondoa hii chupa!” nikasema kwa sauti ili kusikia Harishi atajibu nini.

    “Usiiondoe. Nataka mnifungulie niende zangu” Sauti ya Harishi ikasikika kutoka kwenye ile chupa.

    “Hakuna atakayekufungulia muuaji wewe”Yasmin akamwambia.

    “Nifungulie nitakurudisha kwenu”

    “Mbona siku zote hukunirudisha?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nakwambia kweli kabisa. Ukinifungulia nitakurudisha kwenu Comoro”

    “Kwenda zako, mimi si mjinga wa kukufungulia wewe.. Bora ubaki humo humo. Siku zako zimeshafika”

    Yasmin akanigeukia mimi na kuniambia.

    “Twende tukaizike hii chupa”

    “Hapana.. hapana. Msiizike!” Sauti ya Harishi ikalalamika.

    “Mimi naona tukaizike baharini” nikamwambia Yasmin.

    “Hapana…hapana. Msiitose baharini!” Ilikuwa sauti ya Harishi lakini hatukuipatiliza.

    “Niliwahi kusikiakule kwetu kwamba majini wanafungiwa kwenye chupa na kutoswa baharini” nikamwambia Yasmin.

    “Tukiitosa baharini itaelea na kisha itarudishwa ufukweni na mawimbi”

    “Labda tuifunge kamba na jiwe ili izame chini”

    “Nyinyi msifanye hivyo. Mimi nimeshwambia sitawaua. Nifungulieni niende zangu” Harishi akatuambia.

    “Basi tutaifunga na jiwe tizamishe” Yasmin akasema.

    “Hamsikii hivi ninavyowambia. Nyinyi mnataka mfe?” Sauti ya Harishi ikasikika kutoka kwenye chupa.

    “Utakufa wewe, mbona huwezi kutoka !” Yasmin akamwambia.

    “Tusubiri kuche” nilimwambia Yasmin.

    “Linaweza likatoka!”

    “Usiku huu hatutaweza kwenda baharini”

    “Basi tusubiri”

    Tukasubiri. Harishi sasa alikuwa amenyamaza. Sauti yake haikusikika tena. Lakini ule moshi uliendelea kuonekana ndani ya ile chupa. Ulikuwa unabadilika rangi kila mara.

    Nipoona kunaanza kupambazuka nilijaribu kuishika ile chupa. Ilikuwa nyepesi kama chupa tupu.

    Yasmin alileta kapu. Akaniambia tuitie kwenye kapu.

    “Tutapata wapi kamba?” nikamuuliza.

    “Twende nayo, tutapata kamba huko huko”

    Tukatoka nje ya lile jumba. Mimi ndiye niliyeshika lile kapu. Kulikuwa na baridi kali lakini tulijikaza hivyo hivyo. Wakati tunaelekea baharini tuliokota kipande cha kamba na jiwe tukavitia kwenye kapu.

    Tulipofika ufukweni mwa bahari tuliitoa ile kamba tukaifunga kamba kisha ile kamba tukaifunga na jiwe.

    Tulimsikia Harishi akisema maneno ndani ya ile chupa lakini sauti yake ilikuwa ya chini kiasi kwamba hatukuelewa anasema nini.

    Mimi na Yasmin tulijitosa kwenye maji. Tukatembea kwa miguu hadi tulipofika kwenye maji mengi tukaanza kuogelea kwenda mbali zaidi tukiwa na ile chupa tuliyoifunga jiwe.

    “Tuizamishe hapa hapa” Yasmin akaniambia.

    Nikaiachia ile chupa, ikazama ndani ya maji taratibu. Hatukuiona tena.

    “Sasa turudi. Zama za Harishi zimekwisha” Yasmin akaniambia.

    Tukaogelea kurudi ufukweni. Tulipofika ufukweni nilimwambia Yasmin.

    “Sidhani kama atatoka tena”

    “Hawezi kutoka. Labda atokee mtu aifungue ile chupa”

    “Na huyo mtu atatokea wapi?”

    “Labda wavuvi”

    “Wavuvi ni watu wanaojua. Wakiona chupa chini ya bahari hawaifungui. Na pia hakuna wavuvi wanaofika huku”

    “Lakini ni kitu cha ajabu. Ujanja wote ule alionao ameshindwa kujitoa kwenye chupa!”

    “Ndio maana tunaambiwa kiumbe hakukamilika kwa maumbile wala kwa ujuzi. Mkamilifu ni Mungu peke yake”

    “Tungejua mapema tungemfungia tangu tulipofika, tungesalimika sote”

    “Hatukujua. Hata mimi ningeweza kumfungia. Sasa nimeshajua sababu ya kunisisitiza kila siku kuwa niweke mbali kile kizibo na nisiifunge hata siku moja”



    “Yasmin tumeepuka kifo cha aina moja, sasa tunakabiliwa na kifo cha aina nyingine” nikamwambia Yasmin.

    “Kifo gani tena?”

    “Tutaondokaje kwenye kisiwa hiki?”

    “Usijali. Mungu mkubwa”

    Tukarudi katika lile jumba. Tulipofika tulioga maji baridi. Yasmin alinitolea “Ni kwa nguo za kiume alizokuwa akiletewa na Harishi, akaniambia nivae.

    Kwa vile kulikuwa kumeshakucha alipikauji aliouchanganya na asali, tukanywa. Kwa sababu moyo wangu ulikuwa umetulia nilikunywa vikombe vitatu.

    Wakati nakunywa kikombe cha tatu Yasmin akaniambia.

    “Leo umekunywa uji mwingi kuliko siku zote!”

    sababu nina njaa na roho yangu imetulia”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Yasmin akacheka.

    “Jana hukutaka kula kabisa!” akaniambia.

    “Ni kwa sababu ya yule mshenzi, alinisababishia hofu sana”

    “Sijui ulipata wapi akili ya kufunga kile kizibo?”

    “Niiona tu akili yangu ikinituma nikifunge nilipoona ule moshi”

    “Pengine ni kwa sababu ya zile dua ulizokuwa ukiomba tangu juzi”

    “Pengine”

    Wakati tunajadiliana na Yasmin tulishituka tulipoona wazungu wawili wanaume namtu mweusi mmoja wakiingia ndani ya ile nyumba.

    Nguo zao zilikuwa zimeroa maji. Walionekana walikuwa wamatoka baharini.

    Tukapatwa na uoga kwa vile hakukuwa na watu waliokuwa wakifika katika kisiwa kile.

    Tulikuwa tumekaa pale ukumbini Yasmin akanyanyuka na kuwauliza kwa Kiswahili.

    “Nyinyi ni kina nani”

    “Samahani jamani. Tumekuja kuomba msaada” Yule mtu mweusiakatuambia.

    “Mnatoka wapi?”

    “Tunatoka Zanzibar. Chombo chetu kilipigwa na dharuba kimepinduka. Tumeogelea hadi tumetokea katika kisiwa hiki”

    “Nyinyi ni kina nani” Yasmin akawauliza tena.

    “Hawa wenzangu ni watalii wanatoka Ufaransa. Mimi ni Mzanzibari. Nilikuwa nawatembeza kwa boti kwenye Bahari ya Hinndi ndio tukapatwa na ajali”

    “Mimi pia najua Kifaransa, ngoja niwaulize” Yasmin akasema na kuwageukia wale wazungu. Aliwauliza maswali kwa kutumia lugha ya Kifaransa. Wazungu hao walimjibu na kufurahi kuona Yasmin alikuwa akizungumza lugha yao.

    “Karibuni make” Yasmin akawambia kwa Kifaransa.

    Watu hao watatu wakakaa chini.

    “Kwanza tunawapa pole sana kutokana na mkasa uliowafika. Mmesema kuwa mnaomba msaada, mtufahamishe mnaomba msaada gani?” Yasmin aliwauliza.

    Msaada wowote tu unaostahili kwa binaadamu kwani tumezunguka sana katika kisiwa hiki hatukuona mtu yeyote. Tulichoona ni nyumba tupu na kwingine tulikuta mafuvu na mifupa ya bianaadamu” Mzanzibari alisema.

    “Ni kweli” Yasmin alimjibu.

    “Ni kwanini?”

    “Kwanza mlitakiwa mshukuru kuwa mmefika katika kisiwa hiki katika muda mzuri, vinginevyo na nyinyi mngekuwa kama yale mafuvu mliyoyaona”

    “Kwa niaba ya wenzangu nasema kuwa tumeshukuru lakini tuna shauku ya kutaka kujua kilichotokea mpaka mkabaki nyinyi peke yenu”

    “Nitawaeleza”

    Ndipo Yasmin alipoanza kuwaeleza kisa cha kisiwa hicho. Alianza kwa kujitambulisha kuwa yeye ni binti wa Rais wa Comoro na jina lake ni Yasmin. Akawambia kwamba alisoma elimu yake nchini Ufaransa na ndiyo sababu akawa anajua kuzungumza Kifaransa.

    Akaeleza alivyoposwa na mwana wa mkuu wa majeshi nchini mwao lakini siku ile ya harusi akakumbwa na jini anayeitwa Harishi ambaye alimpeleka katika kisiwa hicho na kumgeuza mke wake.

    “Sikujua nilivyofika katika kisiwa hiki. Nilijishitukia tu nikiwa ndani ya jumba hili nikiwa sijielewi” Akasema.

    Watu hao watatu, wazungu wawili na Mzanzibari mmoja walishikwa na mshangao mkubwa kusikia habari ile.

    Yasmin aliendelea kuwaeleza kuwa jini aliyemkumba ndiye aliyekuwa akiua watu katika kisiwa hicho kwa kuwafyonza damu na kula ubongo wao.

    “Aliwamaliza watu wote waliokuwa katika kisiwa hiki na kuacha majumba yakiwa matupu. Niliishi peke yangu kwa karibu mwaka mzima” Yasmin alieleza.

    Aliendelea kuwaeleza jinsi tulivyofika katika kisiwa hicho na kumkuta yeye ndani ya jumba hilo na jinsi tulivyoanza kuuawa na Harishi mmoja mmoja hadi nikabaki peke yangu.

    Ni dhahiri kuwa maelezo ya Yasmin yalikuwa yamewatia hofu watu hao kwani nyuso zao zilizidi kupata fadhaa.

    “Mungu ni mkubwa” Yasmin alisema kabla ya kueleza jinsi walivyofanikiwa kumfungia Harishi kwenye chupa na kwenda kuizamisha baharini asubuhi ile.

    “Hiki ni kisa cha ajabu kweli kweli. Je tunaweza kwenda kuiona hiyo chupa? mzungu mmoja akauliza.

    “Hatuwezi kujua tumeizamisha wapi lakini kwa sasa Harishi yuko chini ya Bahari”

    “Je hao watu waliouawa tunaweza kuwaona?”

    “Hao mnaweza kuwaona”

    “Tunaomba mtupeleke tukawaone kama hamtajali”

    Yasmin akanitazama.

    “Umeridhika twende tukawaoneshe hawa wageni miili ya ndugu zako?” akaniuliza.

    “Nimeridhika” nikamjibu.

    Yasmin akawambia wale watu “Twendeni”

    Tukaondoka sote watu wanne. Yasmin alianza kuwaonesha miili ya wenzetu waliouawa ambayo ilikuwa karibu na lile jumba. Walikuwa ni wale wenzangu waliouawa mwanzo mwanzo.

    Yasmin alikuwa akieleza jinsi watu hao walivyokuwa wakiuawa kila siku mmoja baada ya mwingine.

    Tukaenda mbali zaidi katika ile nyumba aliyouawa Haji. Wazungu hao pamoja na Mzanzibari waliyekuwa naye wakauona mwili wa Haji.

    Mimi nilitakiwa kueleza alivyouawa Haji. Nikaeleza kwa Kiswahili huku Yasmin akitafsiri kwa kKifaransa.

    Baada ya hapo tulikwenda katika nyumba aliyouawa Shazume.

    Tuliwaonesha mwili wa Shazume na nikawaeleza jinsi Shazume alivyouawa.

    “Hapa ndipo nilipokata tamaa kabisa. Nilijua na mimi ningeuawa leo” nilisema.

    Yasmin akaeleza kuwa nay eye alikuwa ameshajitolea kufa kwa ajili yangu.

    “Nilisema kama atauawa basi tuuawe sote” akasema na kuongeza.

    “Niliona Hakuna haja ya kuendelea kujificha. Nilimwambia mwenzangu twende kule ninakoishi. Harishi akija atukute sote”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wazungu hao walimsifu Yasmin kuwa alikuwa msichana jasiri na mwenye moyo.

    “Kumbe na sisi tungekuja kufa!” Mzanzibari naye aling’aka.

    “Ndiyo maana niliwambia mwanzo kuwa mshukuru kwa kufika katika kisiwa hiki katika kipindi cha usalama” Yasmin akawambia.

    “Sasa kule nyumbani Comoro wanajua uko wapi?” Yule Mzanzibari alendelea kumuuliza Yasmin.

    “Wao hawajui niko wapi na kwa sasa wanaamini kuwa nimeshakufa”

    “Je wakikuona tena itakuwaje?”

    “Itakuwa mshangao mkubwa. Wazazi wangu hawataamini”

    “Ni mkasa wa kutisha kweli na unastahili kuandikwa katika historia ya Comoro”

    “Hapo ni kama tutanusurika na nitarudi kwetu kwani kama niivyowambia mwanzo hapa hatutarajii kupata msaada wowote. Hatima yetu tumemwachia Mwenyezi Mungu”



    Wakati tunazungumza tulikuwa tumeshaondoka katika ile nyumba aliyouawa Shazume na tulikuwa tunaelekea ufukweni mwa bahari. Tulipofika ufukweni Yasmin akataka tukae kidogo tupumzike kwani tulikuwa tumetembea mwendo mrefu.

    “Tangu niletwe katika kisiwa hiki, nyinyi ni wageni wangu wa pili kufika hapa” Yasmin aliwambia wale watu wakati tumeketi.

    “Wa kwanza walikuwa kina nani” Mzanzibari akamuuliza.

    “Wa kwanza walikuwa ni hao watu saba ambao waliuawa na Harishi na kubaki mtu mmoja mliyenikuta naye”

    Yasmin alinionesha mimi.

    “Ulikuwa unakula nini?”

    “Harishi alikuwa akiniletea chakula”

    “yeye alikuwa anakipata wapi?”

    “Anaiba kwenye masoko. Harishi ni mwizi na anatembea sehemu nyingi kuanzia kwetu Comoro hadi Afrika Mashariki”

    Tulikaa pale ufukweni tukazungumza na wale wageni hadi Yasmin aliposema kuwa anhitaji kurudi nyumbani.

    Wakati tunarudi yule Mzanzibari aliyekuwa pamoja na wale wazungu alituambia kuwa boti waliyokuwa wakitalii nayo ilipopigwa na dharuba waliweza kupiga simu Zanzibar kuomba msaada lakini baadaye mawasiliano yalikatika.

    “Boti ya polisi wanamaji inaweza kuwa inatutafuta baharini” akatuambia.

    “Lakini haitawapata, mmeshafika huku” Yasmin akamwambia.

    “Ni vizuri kama tungeendelea kukaa ufukweni ili tuangalie vyombo vinavyopita. Tunaweza kuwaona”

    “Sawa. Mnaweza kwenda kukaa. Tutawafuata baadaye”

    Mzanzibari huyo alizungumza na wale wazungu na kukubaliana kuwa wabaki kule kule ufukweni. Tukawaacha na kurudi kwenye lile jumba.

    “Unajua ni kwanini nimetaka turudi?” Yasmin akaniuliza.

    “Sijui”

    “Ninataka kupika”

    “Ukipika tutawapelekea chakula na wale jamaa?”

    “Tutawapelekea. Wameshakuwa wageni wetu”

    “Nilitaka kujua hilo tu”

    “Jibu umeshalipata?”

    “Nimelipata”

    “Sawa” Yasmin akaanza kushughulika. Baada ya masaa mawili akawa ameshaivisha wali na mboga ya uyoga.

    “Unaonaje ukaenda kuwaita tuje tule nao hapa?” Yasmi akaniuliza.

    “Ni sawa. Ngoja nikawaite”

    Nikatoka. Wakati nachanganya mwendo kuelekea ufukweni nilisikia mlio wa helikopta. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kusikia mlio kama huo tangu tulipofika katika kisiwa hicho. Nikashituka na kutazama juu. Niliona helikopta ikipita chini chini. Ilinipita ikaendelea kwenda na kupote mbele yangu.

    Laiti ningekuwa na uwezo wa kuisimamisha, ningeisimamisha lakini sikujua ningeisimamishaje. Nikabaki kuikodolea macho huku nikisikitika.

    Mlio wa helikopta hiyo ulikuwa bado ukisikika masikioni mwangu. Ilikuwa kama inayozunguka kwenye hicho kisiwa. Ghafla nikausikia tena mlio huo ukitokea kwa nyuma yangu. Nikageuka na kuitazama. Ilinipita tena na kuendelea kuzunguka.

    Ghafla kwa mbele yangu nikasikia kelele za watu zikitokea kwenye miti. Baadaye kidogo nikawaona wale wazungu pamoja na yule mswahili wamevua mashati wakiifukuza ile helikopta huku wakiipungia mashati yao.

    Ile helikopta ilirudi tena upande niliokuwa mimi. Sasa mwendo wake ulikuwa wa taratibu na ilikuwa chini chini sana. Ilitafuta sehemu iliyokuwa wazi ikatua. Kitendo cha kutua kwa helikopta hiyo kilinipa furaha na kunirudishia matumaini. Nikajua msada umeshapatikana. Nilitaka nirudi mbio nikamchukue Yasmin lakini naye alishausikia mlio wa helikopta hiyo. Alitoka na kuja mbio.

    Ndani ya ile helikopta walishuka watu watatu. Moja alikuwa na mavazi ya kipolisi lakini sikuweza kujua alikuwa polisi wa wapi na pia sikuweza kujua ile helikopta ilitokea wapi na ilikuwa inatafuta nini kwenye kile kisiwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Watu hao waliposhuka walitutazama.Yule polisi akauliza.

    “Yinyi ndio ambao mliripoti kuwa chombo chenu kinazama?” Alikuwa akimtazama yule Mzanzibar aliyevua shati pamoja na wale wazungu.

    “Ndiyo sisi” Mzanzibari huyo akajibu haraka.

    “Na hao wataliiwa Kifaransa ndio hawa mabwana?”

    Aliwaonesha wale wazungu.

    “Ndio hawa niliokuwa nao kwenye boti. Tuliogelea hadi kwenye kisiwa hiki”

    “Tumezunguka sana baharini kuwatafuta bila mafanikio. Huku tulikuja kubahatisha tu, ndio tunaona watu wanatupungia. Poleni sana”

    “Tunashukurusana kwa msaada wenu”

    “Tuliambiwa mlikuwa watu watatu, na hawa watu wengine ni kina nani?”

    “Ndio wenyeji wetu tuliowakuta hapa kisiwani, hakuna watu wengine”

    “Ninachofahamu mimi ni kuwa hiki kisiwa kilihamwa na watu. Sasa hawa wametokea wapi?”

    “Wametueleza habari ya kusisimua sana. Huyu msichana ni binti wa Rais wa Comoro. Aliletwa katika kisiwa hiki katika mazingira ya kutatanisha,mwenyewe akiwa hajifahamu. Na ameishi hapa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake”

    Watu hao watatu waliotoka kwenye helikopta walipatwa na mshangao waliposikia habari ile.

    “Eti ni kweli?” Yule polisi akaniuliza.

    “Ni kweli” Yasmin akamjibu.

    “Wewe ni binti wa Rais wa Comoro?”

    “Ndiyo”

    “Ulifikaje katika kisiwa hiki kisichokuwa na watu na ulikuwa unaishije?”

    Yasmin akaeleza kisa chake kuanzia alivyokumbwa na Harishi katika siku ya harusi yake hadi kuletwa katika kisiwa kile.

    Akeleza jinsi alivyokuwa anaishi.

    “Wageni wangu wa kwanza kufika katika kisiwa hiki ni huyu kaka na wenzake”

    Alinionesha mimi.





    “Wametueleza habari ya kusisimua sana. Huyu msichana ni binti wa Rais wa Comoro. Aliletwa katika kisiwa hiki katika mazingira ya kutatanisha,mwenyewe akiwa hajifahamu. Na ameishi hapa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake”

    Watu hao watatu waliotoka kwenye helikopta walipatwa na mshangao waliposikia habari ile.

    “Eti ni kweli?” Yule polisi akaniuliza.

    “Ni kweli” Yasmin akamjibu.

    “Wewe ni binti wa Rais wa Comoro?”

    “Ndiyo”

    “Ulifikaje katika kisiwa hiki kisichokuwa na watu na ulikuwa unaishije?”

    Yasmin akaeleza kisa chake kuanzia alivyokumbwa na Harishi katika siku ya harusi yake hadi kuletwa katika kisiwa kile.

    Akeleza jinsi alivyokuwa anaishi.

    “Wageni wangu wa kwanza kufika katika kisiwa hiki ni huyu kaka na wenzake”

    Alinionesha mimi.



    “Wenzake wote waliuawa na Harishi na kubaki yeye peke yake. Siku yake ya kuuawa ilikuwa ni leo lakini Mungu mkubwa, amenusurika” Yasmin akaeleza.

    Alilieleza tukio zima la kumfungia Harishi kwenye chupa lililotokea usiku uliopita.

    “Hatukudhani kuwa ungekuwa mwisho wake. Sisi sote tulikuwa tumeshapanga kufa”

    “Sasa ikawaje?” Polisi aliendelea kumuuliza kwa shauku.

    “Harishi alishindwa kutoka ndani ya chupa na leo asubuhi tukaenda kuizamisha baharini”

    “Ni habari kubwa nay a kushangaza kwa kweli. Unaweza kwenda kutuonesha nyumba uliyokuwa unaishi?”

    “Ninaweza. Twendeni”

    Yasmin akaliongoza kundi hilo la watu kuelekea katika lile jumba alilokuwa anakaa.

    Watu hao waliingia ndani na kujionea jumba hilo lilivyokuwa. Yasmin aliwatembeza sehemu zote za jumba hilo hadi katika chumba alichokuwa analala.

    Watu hao walimpa pole na kumsifu kuwa alikuwa msichana jasiri aliyeweza kuishi katika mazingira kama yale.

    “Leo imekuwa ni siku yako ya uokozi, wewe na mwenzako” polisi aliyetoka kwenye helikopta alimwambia na kuongeza.

    “Washukuru hawa watalii ambao chombo chao kilizama kwani wao ndio sababu ya sisi kufika hapa na kuwagundua nyinyi”

    “Nawashukuru nyote kwa jumla, hawa watalii na nyinyi mliokuja kutuokoa” Yasmin akawambia watu hao huku akitabasamu.

    “Sasa twendeni tukajipakie tuondoke” Polisi huyo akatuambia.

    Yasmin akanitazama.

    “Hatutakula tena?” akaniuliza.

    “Hata njaa yenyewe siioni, kwaniwewe unahitaji tena kula?”

    ‘Basi ningojeni nibadili hizi nguo zangu”

    Yasmin akaingia chumbani kwake haraka. Yule polisi akawambia wenzake.

    “Unaona kama alikuwa anaishi maisha ya kawaida kumbe alikuwa katika mazingira magumu”

    “Ameyazoea” Yule Mzanzibari akasema.

    “Na pia ni jasiri sana” na mimi nikati akauli. “Mimi nimekaa hapa kwa siku chache tu lakini nimeshachoka. Inakuwaje kwa yeye aliyekaa kwa zaidi ya mwaka?”

    Wote wakatikisa vichwa.

    Baadaya robo saa hivi Yasmin alitoka. Alikuwa amebadili nguo na kuvaa vazi jingine lililokuwa limempendeza na kufanya aonekane kama malkia. Vazi hilo lilikuwa ni moja ya mavazi aliyokuwa akiletewa na Harishi. Alikuwa amejitia manukato yaliyokuwa yakinukia vizuri na nywele zake aliziweka katika mtindo wa Kikomoro.

    Alikuwa ameshika mkoba wa kike mkono mmoja na mkono mwingine alishika begi kama msafiri.

    “Hili vazi umelipata wapi?” Yule polisi akamuuliza.

    “Nililipata kutoka kwa huyo jini. Alikuwa akiniletea nguo”

    “Na hilo begi na huo mkoba?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Vyote”

    Watu wote wakatazamana kwa mshangao.

    Tulitoka katika lile jumba. Wakati tunatoka Yasmin aligeuka juma akalitazama jumba hilo kwa mara ya mwisho. Sikujua alikuwa akiwaza nini. Baada ya kulitazama kwa sekunde chache aligeuka mbele na kuendelea na safari.

    “Lete begi nikusaidie” nikamwambia.

    Nilimpokea begi. Lilikuwa zito kiasi.

    “Umetia nini?” nikamuuliza.

    “Mna vitu vyangu”

    “Umeamua kuondoka navyo”

    “Nataka wazazi wangu wakavione”

    “Naamini watafurahi kukuona”

    “Na mimi nitafurahi kuwaona”

    “Tulifika mahali ilipoachwa helikopta. Rubani akatufundisha jinsi ya kujipakia kwenye helikopta.

    “Mnapotaka kupanda helikopta mnainama namna hii ili kukwepa mapangaboi na hata wakati wa kushuka mnainama” akatuambia huku akituonesha jinsi ya kuinama.

    Yasmin ndiye aliyetakiwa ajipakie kwanza. Baada ya Yasmin kujipakia tulifuatia sisi.

    Sote tulipokuwa ndani ya helikopta, helikopta ikapaa juu na kuanza safari. Nilimuona Yasmin akitazama chini kupitia kwenye vioo. Bila shaka macho yake yalikuwa yanaagana na kisiwa hicho alichokikaa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake na asiye na matumaini ya kunusurika.

    Kwa upande wangu nilikuwa siamini kuwa tunaondoka. Niliona kama niko kwenye ndoto.

    Nasaha za Yasmin zilikuwa zimetimia siku ile. Nilikumbuka kuwa aliwahi kuniambia kuwa aliota ninamuua Harishi na kumuokoa yeye. Wakati huo niliona kama maneno ya mzaha lakini kweli yametimia. Bila kutegemea nimemzamisha Harishi chini ya bahari na hatukutegemea kama angeweza kutoka tena.

    Pia nilikumbuka jinsi Yasmin alivyokuwa akinipa moyo kuwa tutaokoka. Na siku ile tukaokoka kweli.

    Wakati helikopta ikizidi kuyoyoma na Yasminakiendelea kukiangalia kisiwa hicho, pengine akikumbuka enzi zake na Harishi, nilikumbuka jambo moja tena jambo muhimu.

    Niliikumbuka ahadi yetu ya kumuoa Yasmin pindi tutakaponusurika na kurudi makwetu.

    Sikudhani kuwa Yasmin alikuwa angali akiikumbuka ahadi ile japokuwa alinipa siku chache tu zilizopita

    Niliamini kuwa kwa vile tulikuwa tumeshaokolewa mawazo ya Yasmin yanaweza kuwa yamebadilika. Kule aliniona kama mwenza wake kwa vile tulikuwa kwenye kifungo. Sote tulikuwa sawa. Lakini tukifika huko tunakokwenda yeye atakuwa binti wa rais mwenye hadhi na heshima, na mimi nitakuwa mvuvi nisiye na thamani yoyote. Sikudhni kama nitakuwa na maana tena kwake.

    Helikopta sasa ilikuwa ikipita juu ya Bahari ya Hindi. Yasmin aliacha kutazama chini, sasa akawa anatazama mbele. Kwa vile viti vyetu vilikuwa vinapakana aligeuza uso akanitazama mimi. Nilidhani alitaka kuniambia kitu. Na mimi nikamtazama. Lakini hakuniambia kitu. Nikauona uso wake ukichanua tabasamu. Na mimi nikatabasamu. Baada ya hapo aliugeuza uso wake mbele.

    Sikuweza kujua alikuwa akiwaza nini au aliwazia nini aliponitazama na kutabasamu lakini vyovyote ambavyo aliwaza alikuwa ameniwazia vizuri.

    Wakati helikopta ikiendelea kupasua bahari niligeuka nyuma kuangalia kwenye vioo vilivyokuwa vimeizunguka helikopta nzima. Nilikuwa naangalia kile kisiwa tulichokuwa tumekiacha kwa mbali. Tuliendelea kukiacha kadiri helikopta ilivyozidi kusonga mbele.

    Hatimaye tulikuwa katikati ya bahari. Hatukuona nchi tena. Baadaye tuliona mitumbwi ya wavuvi wakivua samaki. Baada ya muda ambao sikuweza kuukadiria tuliona nchi kwa mbali. Ilianza kutokea mbele yetu kama chuguu ya rangi ya kijani iliyochukua eneo kubwa. Kadiri tulivyozidi kwenda chuguu hiyo ilizidi kuonekana kubwa.

    Sasa tuliweza kuona miti kwa mbali. Kijani tulichokuwa tunakiona ilikuwa miti iliyokuwa imeenea katika ardhi. Majumba ya ghorofa na barabara sasa vilionekana waziwazi. Nikajiambia kwamba tulikuwa tumekitokea kisiwa cha Unguja.

    Muda si muda tukawa tumeivuka bahari. Sasa tulikuwa tunapita juu ya kisiwa cha kwetu baada ya kukitoka kile kisiwa cha kifo. Nilishukuru sana.

    Tuliona vespa, bajaji na magari yanayokokotwa na punda yakipita chini yetu. Nikawa natabasamu peke yangu.

    “Yasmin unakuona kwetu?” nikamwambia Yasmin.

    “Ahaa ndio hapa!” Yasmin akaniuliza.

    “Hapa ni Zanzibar. Kisiwa hiki kinaitwa Unguja”

    “Uliniambia wewe unatoka Pemba”

    “Pemba ni kwetu na Unguja pia kwetu. Yote ni Zanzibar moja”

    Yasmin akatabasamu.

    “Nimefurahi kufika kwenu. Nitawaona wazazi wako na ndugu

    zako”



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati nazungumza na yasmin helikopta ilikuwa inatua kwenye kiwanja cha ndege. Tukaacha mazungumzo na kuchungulia kwenye madirisha. Tuliona jingo la kiwanja cha ndege kwa mbele. Pia tuliona ndege kadhaa zikiwa zimeegeshwa huku wafanyakazi wakienda huku na huko.

    Helikopta ilipotua tulishuka

    Kwa vile rubani alikuwa akifanya mawasiliano tangu tukiwa juu. Tulikuta maofisa wanne wa polisi wakitusubiri. Polisi tuliyekuwa naye aliwapa maelezo ya zoezi lililofanyika. Akawaeleza pia tulivyopatikana katika kile kisiwa.

    Polisi hao walituchukua katika chumba kimoja wakaanza kuwahoji wale wazungu pamoja na mwendesha boti waliyekuwa naye. Baada ya wao kutoa maelezo lilikuja gari likawachukua. Tukaanza kuhojiwa mimi na Yasmin. Maelezo yetu ndio yaliyowaacha hoi maofisa hao.

    “Unasema wewe ni bini wa rais wa Comoro na ulikumbwa na jinni aliyekupeleka katika hicho kisiwa mwaka mmoja uliopita?” Afisa mmoja akamuuliza Yasmin.

    “Ndiyo”

    Niliposema “ndiyo” maofisa hao walitazamana kwa mshangao.

    “Hebu tueleze ulivyofikishwa katika kisiwa hicho kutoka Comoro?” Afisa huyo akaendelea kumuuliza.

    “Sijui. Ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kwenye sherehe ya harusi yangu nikaanguka na kupoteza fahamu. Nilipozinduka nikajikuta niko katika kile kisiwa ndani ya lile jumba nililokuwa ninaishi” Yasmin aliendelea kueleza.

    “Ulijuaje kuwa ulikumbwa na jinni?’

    “Wakati nazinduka nilimuona jinni mwenyewe. Aliniambia anaitwa Harishi na kwamba yeye ndiye aliyenikumba na kunileta pale”

    “Alikuwa anataka nini kwako?”

    “Alikuwa anataka niishi naye kama mke wake”

    “Na ukawa unaishi naye?”

    “Sikuwa na la kufanya zaidi ya kukubali”

    “Ulikuwa unapata wapi chakula na mahitaji mengine?”

    “Alikuwa ananiletea yeye chakula na nguo”

    “Anavipata wapi?”

    “Aliniambia kuwa anaiba kwenye maduka”

    “Wapi?”

    “Alikuwa anazunguka sehemu nyingi za Afrika Mashariki pamoja na Comoro”

    Tumeambiwa kwamba kisiwa ulichokuwa unaishi wewe hakina watu isipokuwa nyumba tupu, ni kwanini?”

    “Harishi alinieleza kuwa watu waliokuwa wakiishi katika kisiwa kile aliwaua yeye kwa kuwafyonza damu na kula bongo zao. chakula chake kilikuwa damu na ubongo”

    Maafisa hao wakatazamana tena kwa mshangao.

    “Chakula chake kilikuwa damu na ubongo wa binaadamu?” Afisa huyo akamuuliza tena Yasmin.

    “Ndiyo” Yasmin alimjibu.

    “Kwanini wewe hakukula?”

    “Mimi alinichukulia kama mke wake”

    “Na tuliambiwa kwamba kuna watu saba ambao chombo chao kiliharibika baharini na walifikakatika kile kisiwa, ni kina nani?”

    “Mmojawapo ni huyu hapa” Yasmin alinionesha mimi na kuongeza.

    “Walifikapale wakiwa watu saba wakauawa na Harishi akabaki yeye peke yake”

    “Kwanini yeye hakuuawa?”

    “Kuna kisa kirefu kimepita”

    “Tunataka tukisikie”

    Yasmin akawaeleza yaliyotokea hadi tukaweza kumzamisha Harishi chini ya bahari akiwa ndani ya chupa.

    Baada ya Yasmin kuhojiwa nilihojiwa mimi. Nilijieleza kuwa nilikuwa Mzanzibari na kazi yangu ilikuwa uvuvi. Nikaeleza jinsi nilivyofika katika kisiwa kile na kumkuta Yasmin ndani ya lile jumba.

    Nilipomaliza maelezo yangu simu zilipigwa sehemu mbalimbali. Haukupita muda mrefu maofisa usalama wa ikulu pamoja na waziri wa nchi ofisi ya raisi walifika kiwanja cha ndege.

    Baada ya kupata maelezo yetu, waziri wan chi alimuuliza Yasmin kama kweli alikuwa binti wa rais wa Comoro.

    Yasmin akasisitiza kuwa alikuwa binti wa rais huyo na akaomba aunganishwe naye kwenye simu.

    Taarifa za Yasmin zilipofika ikulu, Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi iliwasiliana na Wizara ya mambo ya nje ya Comoro.

    Mpaka inafika saa kumi na moja jioni ndege ya serikali iliyotoka Comoro ikiwa imempakia kaka wa Yasmin ambaye alikuwa kanali wa jeshi pamoja na maofisa usalama wa ikulu ya Comoro ilitua kiwanja cha ndege cha Unguja.

    Watu hao walipokewa na mkurugenzi wa usalama na kupelekwa kukutanishwa na Yasmin ambaye mpaka wakati huo nilikuwa pamoja naye.

    Kaka wa Yasmin Kanali Umar Sharif Abdilatif alipomuona Yasmin alishituka. Na Yasmin naye alishituka. Walitazamana kwa sekunde kadhaa kabla ya kukimbiliana na kukumbatiana kwa furaha na majonzi.

    Maofisa usalama waliotoka ikulu ya Comoro ambao walikuwa wakimfahamu Yasmin nao walishangaa walipomuona kwani taarifa zilizokuwa nchini mwao zilionesha kuwa Yasmin alipotea katika mazingira ya kutatanisha wakati wa harusi yake zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

    Baada ya maofisa hao kumsalimia Yasmin walithibitisha kwamba alikuwa binti wa Rais Sharif Abdulatif aliyepotea nchini mwao katika mazingira ya kutatanisha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati huo Yasmin alikuwa akitiriikwa na machozi kwa kumuona kaka yake.

    Yasmin aliwaeleza masahibu yaliyokuwa yamemtokea, maelezo ambayo yalimshitua kaka yake pamoja na maofisa hao.

    Baada ya kuthibitishwa kwamba Yasmin alikuwa binti wa Rais wa Comoro aliitwa ikulu pamoja na kaka yake. Yasmin aliomba na mimi niwemo kwenye msafara huo. Ombi lake lilikubaliwa. Nilipatiwa mavazi mengine tukapakiwa kwenye gari kupelekwa ikulu ambako tulikutana na rais wa Zanzibar.

    Rais wa Zanzibar alimsikiliza Yasmin na kushangazwa na maelezo ya binti huyo wakati akimsimulia masahibu aliyokutana nayo.

    “Hata hivyo wewe ni shujaa kwa sababu hukukata tama” Rais alimwambia Yasmin. Pia alinipongeza mimi kwa kunusurika kufa.

    “Mkasa uliowakuta ni historia kubwa ya visiwa vyetu” Rais aliendelea kutuambia.



    Rais wa Zanzibar akawasiliana na Rais mwenzake wa Comoro na kuzungumza naye.

    “Binti yako Yasmin ninaye hapa” Rais wa Zanzibar alimwambia Rais wa Comoro.

    “Nimepata habari zake na nimeshukuru sana kusikia kwamba mwanangu bado yuko hai. Sisi tulidhani ameshakufa” Rais wa Comoro alisema kwenye simu.

    “Ni kweli kwamba alipotea siku ya harusi yake mwaka mmoja uliopita?”

    “Nikweli. Lilikuwa tukio la kushangaza sana!”

    “Ameniambia alikuwa akiishi katika kisiwa kimoja kisicho na watu na hajui alifikaje katika kisiwa hicho”

    “Binti yangu alipata masahibu makubwa lakini nashukuru kuwa amenusurika”

    “Huyu hapa, ongea naye”

    Rais alimpa Yasmin mkono wa simu ili azungumze na baba yake.

    “Asalam alaykum baba!” Yasmin alimwamkia baba yake.

    “Wa alaykum salam warahmatulahi wabarakat. Hujambo mwanangu?”

    “Sijambo baba. Matatizo yaliyonitokea ni kama ulivyoyasikia”

    “Nimeyasikia na nimemtuma kaka yako Umar na maofisa wangu kuja kukuona. Nimeambiwa kuwa mmeshakutana”

    “Tumekutana na kaka ninaye hapa”

    “Nimefurahi kwamba uko naye kwa rais mwenzangu. Je wewe afya yako ikoje?”

    “Afya yangu si nzuri lakini pia si mbaya sana. Nikija huko mtaniona”

    “Ulikuwa unaishi vipi huko kisiwani ulikokuwa?”

    “Nimeishi kwa taabu tu baba. Nikija nitawaeleza vizuri”

    “Ningependa uzungumze na mama yako ili umtoe wasiwasi lakini hatapatikana kwa sasa kwa sababu mimi bado niko ikulu”

    “Hakuna wasiwasi baba. Mwambie mama mimi ni mzima. Ni masahibu tu yamenikuta na ishallah nitakutana naye”

    ”Si mtakuja hii leo?”

    “”Kama tutaruhisiwa kuondoka tutakuja leo”

    “Sawa. Sasa mpe simu mheshimiwa rais”

    Yasmin akampa samu rais wa Zanzibar.

    “Umeshazungumza na mwanao?” Rais wa Zanzibara akamuuliza rais wa Comoro kimzaha.

    “Tumezungumza kidogo. Unatarajia wataweza kuondoka leo hii kurudi Comoro”

    “Kwa vile ndege iko tayari sioni cha kuwazuia kuondoka leo”

    “Basi ningependa uwaruhusu kuondoka na mtupatie taarifa muda ambao wanaondoka”

    Baada ya maraisi hao kumaliza kuzungumza, rais wa Zanzibar alizungumza na maofisa wake.

    “Nataka mhakikishe kuwa ugeni huu unaondoka leo kurudi Comoro. Na kwa upande wa huyu binti apatiwe mahitaji yote ya kibinaadamu kwa gharama ya serikali wakati akiwa hapa nchini kwetu bila kumsahau kijana Zahrani aliyekuwa naye kule kisiwani”

    Baada ya rais kutoa agizo hilo aliagana na sisi na kuwatakia safari njema akina Yasmin.

    Yasmin alimuahidi rais wa Zanzibar kuwa hataisahau Zanzibar na atarudi kuitembelea tena atakapojaliwa.

    Tulipotoka ikulu tulipelekwa katika hoteli ya Bwawani ambako tulipatiwa huduma mbalimbali kama vile chakula, nguo na mahali pa kupumzika. Hapo tulikutana na watu mbali mbali waliopata habari zetu na kututembelea. Walikuja maofisa wa serikali na pia mawaziri.

    Kusema kweli nilipata umaarufu mkubwa kutokana na Yasmin. Kwa vile mwenzangu alikuwa binti wa rais na alikuwa akieleza mara kwa mara kuwa kama si mimi na yeye angeangamia, watu waliotutembelea walikuwa wakitupa pole pamoja na kunipongeza.

    Maelezo yetu yalionekana kama kioja kikubwa kwa vile yalimuhusisha jini anayeitwa Harishi ambaye alimteka Yasmin nchini Comoro na kumpeleka katika kile kisiwa cha mauti.

    Taarifa zilipowafikia waandishi nao walianza kumiminika katika hoteli ya Bwawani kutuhoji na kutupiga picha.

    Baadhi ya waandishi hao baada ya kupata maelezo kutoka kwangu na kwa Yasmin, walimuhoji Yasmin kutaka kujua jinsi tulivyoishi katika kisiwa hicho tukiwa peke yetu.

    Mwandishi: “Mliishije na Zaharani mkiwa watu wawili wa jinsia tofauti katika kisiwa hicho?”

    Yasmin: “Tuliishi kama marafiki”

    Mwandishi: “Mlitarajia kuwa mngeokoka?”

    Yasmin: “Kusema kweli hatukutarajia ingawa tulikuwa tunaomba sana”

    Mwandishi: “Mlikuwa mnalalaje usiku?”

    Yasmin: “Usiku wa jana ndio tulilala pamoja lakini pia hatukulala usingizi kwa sababu tulijua kuwa tungeuawa”

    Mwandishi: “Sasa umeshaokoka. Unadhani utaendelea kuwa karibu na Zahrani?”

    Yasmin: “Bila shaka. Tulipokuwa kule kisiwani nilimpa ahadi Zahrani kuwa kama tutasalimika atanioa”

    Mwandishi: “Una maana kwamba umempenda Zahrani?”

    Yasmin akacheka kabla ya kujibu. “Nimempenda sana”

    Mwandishi: Je sasa unadhani utatimiza ahadi uliyomuahidi?”

    Yasmin: “Ndiyo nitaitimiza”

    Mwandishi: “Kwa hiyo una mpango wa kuoana na Zahrani?”

    Yasmin: “Mpango bado, ni mawazo tu ambayo naamini hayatabadilika”

    Mwandishi: “Umetuambia kuwa kabla ya kupotelea katika kisiwa mlichokua mnaishi ulikuwa unaolewa na mwana wa mkuu wa jeshi la ulinzi la Comoro, je kijana huyo akitaka muoane tena itakuwaje wakati umeshamuahidi Zahrani kuwa mtaoana?”

    Yasmin: “Nadhani atakuwa ameshaoa”

    Kaka wa Yasmin Umar Sharif Abdulatif ambaye alikuwepo wakati Yasmin anahojiwa alithibitisha kuwa aliyekuwa anamuoa Yasmin kabla ya Yasmin kupotea Comoro alishaoa mke mwingine na walikuwa wanaishi Ufaransa. Visiwa vya Comoro vilikuwa koloni la Ufaransa.

    Mwandishi: “Kwa hiyo unatarajia kwenda Comoro na Zaharani?”

    Yasmin: “Natarajia hivyo”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mwandishi: “Ndoa yenu itafanyika lini?’

    Yasmin: “Siku yoyote wazazi wetu watakaponiidhinisha kuolewa na Zaharani”

    Mwandishi aliyekuwa akimuhoji Yasmin alinigeukia mimi.

    Mwandishi: “Je umeyachukuliaje maelezo ya Yasmin?”

    Zahrani: “Yamenifurahisha sana”

    Mwandishi: “Uko tayari kuoana na msichana ambaye baba yake ni rais wa nchi?”

    “Zahrani: “Kama wazazi wake watakubali niko tayari”

    Mwandishi: “Mtakuwa mnaishi wapi

    mtakapooana, Zanzibar au Comoro?’

    Zahrani : “Popote tu tutakapokubaliana”

    Mara tu baada ya waandishi wa habari kuondoka maofisa usalama kutoka ikulu ya Zanzibar walinitambulisha kwamba umefika wakati ambapo nitaachana na Yasmin kwa vile muda wa safari yao ya kurudi Comoro ulikuwa umefika.

    Kauli ile ilinivunja moyo hasa kwa vile nilitegemea kuondoka na Yasmin. Yasmin akawaomba maofisa hao waniache niende naye Comoro.

    “Hatumzuii mtu yeyote kwenda mahali popote anapotaka ila Zahrani hana hati ya kusafiria” Afisa mmoja alimwambia Yasmin.



    Mwandishi: “Mtakuwa mnaishi wapi

    mtakapooana, Zanzibar au Comoro?’

    Zahrani : “Popote tu tutakapokubaliana”

    Mara tu baada ya waandishi wa habari kuondoka maofisa usalama kutoka ikulu ya Zanzibar walinitambulisha kwamba umefika wakati ambapo nitaachana na Yasmin kwa vile muda wa safari yao ya kurudi Comoro ulikuwa umefika.

    Kauli ile ilinivunja moyo hasa kwa vile nilitegemea kuondoka na Yasmin. Yasmin akawaomba maofisa hao waniache niende naye Comoro.

    “Hatumzuii mtu yeyote kwenda mahali popote anapotaka ila Zahrani hana hati ya kusafiria” Afisa mmoja alimwambia Yasmin.

    sasa endelea...

    Ilikuwa kweli sikuwa na hati ya kusafiria na hata Yasmin hakuwa nayo lakini kwa vile aliingia Zanzibar kidharura alilazimika pia kuondoka kidharura.

    Yasmin akanitazama kwa butwaa.

    “Hivi huna hati ya kusafiria?” akaniuliza.

    “Sina” nikamjibu huku nikitikisa kichwa.

    “Kuna kipindi ulikuja Comoro, ulifikaje bila ya hati?”

    “Sina maana kwamba sina kabisa. Hati yangu ya kusafiria iko pemba”

    “Kumbe unayo. Sasa tutafanyaje?”

    “Amua wewe”

    “Sasa sikiliza” Yasmin alitaka kusema kitu lakini akasita na kumtazama kaka yake. “Kaka kama una dola mia tano mpatie Zahrani zimuwezeshe kuja Comoro”

    Umar alitoa dola mia tano hapo hapo na kunipa.

    “Hizo zitakuwezesha kwenda Pemba kuonana na ndugu zako na kujiandaa kwa safari ya kuja Comoro siku yoyote utakayopenda” Yasmin akaniambia.

    Umar akanipa namba za simu za kuwatambulisha wakati nitakapokwenda Comoro.

    Nilikubaliana na Yasmin kwa shingo upande. Mwenyewe alijua kuwa sikuridhika kuniacha Zanzibar ingawa nilipatiwa nauli ya kwenda Comoro siku nitakayopenda kuondoka.

    Baada ya Yasmin kuniambia hivyo aliishia kunitolea tabasamu lenye mchanganyiko wa furaha na majonzi.

    Mimi sikuweza kutabasamu. Kwa siku chache nilizokuwanaye nilikuwa nimeshamzoea Yasmin. Kitu muhimu ambacho nitakikosa kwake ni ile hewa ya mwili wake. Alikuwa na hewa tamu nay a kusisimua ambayo huisikia kila ninapokuwa karibu naye.

    Hewa ile ilikuwa inaniliwaza kuliko manukato ambayo hujitia mwilini mwake.

    “Nitasubiri. Sina la kufanya” nikamwambia kwa sauti nzito ya huzuni.

    “Tutakutana mahabuba wangu. Sitakuacha” Yasmin akaniambia kwa sauti ya chini. Hakutaka isikiwe na wengine.

    Sasa msafara ulikuwa unakwenda kiwanja cha ndege. Na mimi nililazimika kuwasindikiza nikiwa pamoja na maofisa usalama.

    Giza lilikuwa limeshaanza kuingia na taa za mji wa Unguja zilikuwa zimewashwa. Tulikuwa katika basi dogo ambalo liliweza kutupakia sote. Gari la maofisa usalama lilikuwa limetutangulia.

    Tilipofika kiwanja cha ndege niliagana na kaka wa Yasmin kisha nikaagana na Yasmin mwenyewe. Kwa mara ya kwanza Yasmin hakuona aibu kunikumbatia mbele ya macho ya kaka yake.

    Kwa mujibu wa tamaduni za Wangazija wa Comoro, kitendo hicho kwa watu wa jinsia tofauti ambao si ndugu kilikuwa ni cha faragha sana. Lakini Yasmin alikifanya kuonesha mapenzi yake kwangu.

    Wakati ananiachia aliupeleka haraka mkono wake kwenye macho yake kufuta machozi yaliyoanza kumtiririka.

    Kwaheri, tutaonana” akaniambia na kunisisitizia “Nitakusubiri Comoro. Usichelewa kuja. Usiwe na majonzi, tutaonana”

    Yasmin alijaribu kutabasamu licha ya uso wake kujaa huzuni. Tabasamu lake lilinifariji sana.

    Maofisa usalama walikuwa wakimtazama Yasmin alivyokuwa ananiaga kabla ya kugeuka na kuungana na wenzake’

    Sikuondoka hapo kiwanjani hadi ndege waliyosafiri kina Yasmin iliporuka na kuanza safari.

    Nilijisikia mwenye majonzi sana lakini nilijikaza.

    “Wewe hujui kama yule ni binti wa rais?” Afisa usalama mmoja aliniuliza wakati tunaondoka kiwanjani hapo.

    “Ninajua” nikamjibu.

    “Sasa mbona unataka kututia aibu. Unataka kwenda naye wapi?”

    Swali hilo lilinikera sana. Nikamtazama yule afisa usalama aliyetaka kunishushua.

    “Yeye ndiye aliyeomba aondoke na mimi” nikamwambia.

    “Wewe pia si ulikuwa unataka kwenda?”

    Nilijua kuwa yule afisa alikua ameona donge. Nilitaka kumuuliza “Sasa kinakuuma nini?” lakini nilimstahi. Nikamwambia. “Ni baada ya yeye kutaka aondoke na mimi”

    “Sasa yule ni binti wa rais, wewe huwezi kufuatana naye. Ukifika huko utasema nini?”

    Niliona nisijibizane naye. Nikaamua kubaki kimya.

    Maofisa hao walinipakia kwenye gari na kunirudisha kule hoteli. Wakaniambia nitalala pale na asubuhi nirudi Pemba.

    “Tutakufuata asubuhi tukupeleke bandarini” Afisa mmoja akaniambia.

    Nikamjibu “Sawa”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nililala pale hoteli. Usiku kucha nilikuwa namuwaza Yasmin. Asubuhi simu iliyokuwa mle chumbani ikaita. Nilipoipokea niliambiwa nipokee simu yangu kutoka Comoro.

    Hapo hapo nilisikia sauti niliyoitambua kuwa ni Yasmin ikinisalimia.

    “Subalheri muadhamu (asubuhi njema mpendwa)”

    “Subalnuur azizi (asubuhi yenye nuru mremo)” Kwa kutaka kuhakikisha kuwa alikuwa Yasmin nikamuuliza “Wewe ni Yasmin?”

    “Naam, ndiye mimi. Nilitaka kukujulia hali”

    “Nashukuru, mie sijambo. Je mlifika salama?”

    “Alhamdulilahi. Tulifika salama. Nimekutana na wazazi wangu na ndugu zangu na pia wananchi wenzangu. Wamefurahi kuniona na mimi nimefurahi kuwaona. Kumbe bado uko hapo hoteli?”

    “Ninaondoka hii asubuhi kwenda Pemba na mimi nikaonane na wazazi wangu pamoja na ndugu zangu. Najua wameshanikatia tama”

    “Ni kweli. Basi ukifika unaweza kunipigia kwa kutumia zile namba ulizopewa na kaka”

    “Sawa, nitakupigia”

    “Ongea na mama yangu”

    Mara nikasikia sauti nyingine ikiniuliza. “Hujambo mwanangu?”

    “Sijambo mama. Habari za huko?’

    “Huku ni salama. Unajisikiaje hali yako?”

    “Hali yangu ni nzuri. Nashukuru”

    “Pole sana kwa masahibu yaliyowafiaka”

    “Tumeshapoa mama”

    “Tunakusubiri kwa hamu huku. Utakuja lini?”

    “Siku ya kuja nitawambia. Kwanza nataka nifike Pemba nikawaone wazazi na ndugu”

    “Basi utatujulisha siku utakayokuja tukupokee”

    “Asante mama. Nitawajulisha”

    “Nampa simu Yasmin”

    “Haya mpe”

    “Hallo Zahran!” Sauti ya Yasmin ikasikika.

    “Ndiyo Yasmin”

    “Usijali kuwa mbali nami, ishallah tutakuwa pamoja. Nimeshamueleza mama yangu kilicho ndani ya moyo wangu kuhusu wewe”

    Aliponiambia hivyo, mwili wangu ulisisimka.

    “Hakuna tatizo Yasmin. Wewe pia usijali”

    “I miss you” Yasmin akaniambia kwa kingreza.

    “Sikujua jinsi ya kujibu, nikabaki kucheka. Yasmin naye akacheka.

    “Bye bye (baibai): akaniaga.

    “Bye…”

    Simu ikakatwa.

    Je Zahrani ambaye ni mvuvi na masikini asiye na elimu atamuoa Yasmin binti wa rais? Usikose toleo lijalo.



    MWISHO





    KISIWA CHA HARISHI

    Napenda kuwaarifu wasomaji wangu kuwa muhusika mkuu katika hdithi yetu ya Kisiwa cha Harishi alifanikiwa kuoana na Yasmin huko Morani Comoro. Hadithi kamili inatikana kwenye kitabu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

0 comments:

Post a Comment

Blog