Simulizi : Vampire Nusraty
Sehemu Ya Nne (4)
Tulipoishia
“Eti Hafidhi mimi nishike nini,,,,leo hii mie navuta bange sio?....kwa hasira Baba akanipiga zinga la kofi ajabu sikuweza kusikia maumivu yeyote Yale zaidi ya Baba kuanza kulia huku akiwa kaushikilia ule mkono alionipiga kofi,CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Hii mkono wangu,,,,,ayaaa,,,uwiiiiiiiiii
....Baba akadondoka chini huku akitapatapa nikaita kwa sauti huku nikimshika
“Baba!!!baba,,,,,,"
Nikamuona Dada na ndugu wengine ambao walikuja kwenye msiba wa Mama walikuwa bado hawajaondoka wakaja mbiombio na kuuliza
Kunanini kimetokea kumbe nyumbani alikuja mganga maana nae akatoka ndani ajabu
Aliponiona mimi tu akatoka mbio ajabu huku tunguri zake akizitupa ndugu baada kuona vile nao
Wakanihofia.
Songa nayo
Sasa
Nikabaki nikijiuliza maswali mazito pasipo kupata jibu hata moja.
Kwanini Baba amenipiga kofi kisha sikusikia maumivu yeyote,,,,"kwanini yule Mganga amenikimbia Mimi
Huku ndugu nao wakianza kunihofia, maana wakambeba Baba
na kuingia nae ndani kisha wakafunga milango. Nisiweze kuingia ndani, nilibisha hodi sana huku nikiita na kuwaomba wanifungulie,
“Shangazi tafadhali njoo unifungulie mlango please nawaomba jamani kwanini mnanifanyia kitendo kama hiki jamani",,,,,,usiku wote huu nitalala wapi mie!!!,,,,Dada Fatuma
Kwanini nawewe unanitendea hivi kumbuka sisi ni damu moja njoo unifungulie usiniache hapa nnje peke yangu",,,,Baba mdogo unaniachaje mwanao!!!,,,,
Niliongea huku nikilia ajabu hakuna hata mmoja aliyekuja kufungua mlango basi nikaenda kibarazani kujilaza
Nikaomba duwa Allah (s.w.t) anilinde usiku ule
Nikiwa najilaza ghafla akaja
Nusraty huku akiwa anatabasamu na kuniita
“whao Mume wangu mtarajiwa huyoo vipi mbona mpaka saa hizi hujaenda ndani kulala?"
Nilimkata jicho la gadhabu nikamtusi kwa kumsonya
Huku nikimwambia kitu kimoja
“Nyoo***mshenzi mkubwa wewe nani Mumeo hivi unadhani Mimi naweza kuowa zombie?,,,,,,arafu vitu vingine sio vya kuuliza wakati unajuwa kila kitu kwanini nipo nnje kwa wakati huu, kwa taarifa yako nilikuwa nakungojea wewe nikuuwe,,,,,"
Akaniambia
“Hafidhi tambua kitu kimoja tu binafsi nakupenda sana tena sana tu siwezi kukuacha ukiteseka kwa jambo.lolote lile!"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nyamaza Mwanamke usiekuwa na haya kabisa ungekuwa unanipenda ungemuuwa Mama yangu mpendwa hivi unaijuwa thamani ya Mama wewe?",,,,,,,
Akaniangalia kama dakika mbili hivi kwa sauti ya upole akatamka
“Kwanza nisamehe Mume wangu maana inaonekana umekasirika vibaya mno nimefanya yote haya kuhitaji wewe uniowe Mama yako sijamuuwa nipo nae ukikubali kufunga ndoa nami
Nitamrudisha Mama yako!"
Nikawa kama siamini hivi, maana kwa macho yangu Mama tulimzika tena nilikuwa mmoja kati ya watu wanne tulioingia kaburini kuupokea mwili wa Mama. Iweje huyu aseme eti
Mama bado yupo hai, nikamuuliza
“je nitakuamini vipi kama Mama yangu bado ni Mzima?"
Akageuza shingo yake na kuita
“Mama mkwe"....mama mkwe!!!
Sauti ya Mama ikasikika akiitika
Abee mkwe wangu!"
“Embu njoo Mara moja,"
Unajuwa nikatoa macho pima kama mjusi vile kabanwa na mlango maana dahaa,,,,,,ni kweli alikuwa ni Mama mbele ya upeo wa macho yangu akasimama kwa heshima na taadhima akaniuliza
“Hafidhi mwanangu kwanini unamtesa mwenzio kila siku akulazimishe wewe tu tena kitu kimoja tu!"
“hapana Mama sio hivyo binafsi siko tayari kufunga ndoa na Nusraty kumbuka yeye sio binaadamu
Kuonyesha kuwa sitaki nitamuowa mdogo wake,"
Nusraty akasema
“Whaoo unamaanisha utamuowa Hasina sio?"
Nikamuitikia
“ndio maana yake",
Akakunja ndita kwa hasira akapotea na Mama ajabu Mama kuna kikaratasi alikiacha pale aliposimama
Basi nikaenda kukiokota
Nikakitupia macho niweze kukisoma nikashindwa,
Kwa mara ya kwanza sikuweza kwenda kuswali swalati subuhi mpaka kunakucha,,,,nikaja kuamshwa na
Baba ndipo nikastuka kutoka usingizini
Nikamsalimia
“Assalamu alaykum warahatullah wabarakatur yaa Abii?,,,,,,
Baba akaitikia kwa sauti ya unyonge sana akaniambia
“Hafidhi mwanangu kwanza pole sana kisha naomba unisamehe mimi kwa kile nilichokufanyia jana usiku
Hukustahili kulala nnje mwanangu
hakika Mama yako kanijia ndotoni kanisema sana mimi
Baba akaanza kulia
Ghafla tukasikia sauti ikitusalimia
“Assalamu alaykum jamani"
Hakuwa mwingine kumbe ni Shekhe milongo imamu wetu mpya baada Shekhe Yusuf kufariki
Basi tukaitikia akauliza
“vipi mbona kama mnalia kwema lakini?"
Nikamjibu,
“ewe Shekhe wetu nahofia kukwambia hili nikijuwa ya kwamba na wewe nitakupoteza!"
Akastaajabu pia na kuniuliza ni jambo gani hilo kijana wangu huku akikaa pale kwenye kabaraza
Sikuwa na jinsi zaidi ya kuanza kumpa full.story
Baada kumaliza akajifuta jasho yani story mpaka watu wakatokwa na vijasho kisha akasema
“Binafsi sikuwai kufikilia kama waumini kama nyie mnaishi na matatizo makubwa kama haya yani mnakuja msikitini kila kipindi kumuomba Allah kumbe kwenye vichwa vyenu mmebeba gunia lenye misumari
Sasa basi baada swalati dhuhur
Huyo jini nitamwita mbele yenu nitampa onyo aache ujinga
tena nitamwita akiwa na wenzake wawe mashahidi
Asipo sikia atakiona cha mtema kuni
Jini kwa binaadamu kama sisimizi tu utakiwi kuwa na hofu kabisa subirini muone.
Hakika kauli ya Shekhe mirongo kusema ya kwamba ataweza kumwita Nusraty na kumpa onyo kilinifurahisha sana, nikatamani hiyo saa
Saba iweze kufika haraka maana nilikuwa na kimuhemuhe ajabu. Niliweza kuongea mambo mengi sana nikiwa na Baba, hatimae Adhana ikasikika nikasema
“ehee ule muda ndio huu"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Tukatoka kwenda msikitini kuswali
Alhamdulillahi Shekhe milongo alikuwepo..."
Baada kuswali ndipo akasimama na kutoa mawaidha kidogo kwa kusema
“Assalam alaykum warahamatullah wabarakatur",,,,,
Waumini wote tukaitikia
Kisha akaendelea.
“Watukufu Waislamu ningependa kuzungumza japo kwa uchache tu kuhusu Asiri ya viumbe wanaoitwa Majinni kwanza kabisa Jinni ameumbwa kutokana na ndimi ya moto katika karne hizo, hakika ya majinni walikuwa na mji wao basi wakawa wanafanya mambo mabaya tena machafu kabisa ya kumkufuru Allah (s.w.t) ndipo Allah akamtuma Malaika kwenda kuuwangamiza mji ule,
Malaika akaenda na kuuchota ule mji kama wewe unavyoweza kuichota chapati kisha ukaigeuza ndivyo ilivyokuwa
Malaika yule akaupindua mji ule kichwa chini miguu juu,
Mji wote ukaangamia isipokuwa akabaki mtoto mdogo tu wa Kijinni
Basi akachukuliwa mpaka mbinguni huko akalelewa na kuisoma Qur'an
yote,
Baada kupita karne kazaa ndipo Mwenyezi Mungu akawageukia Malaika na kuwaambia anataka kuongeza kiumbe kingine ambaye ni Adam,
Malaika wakapinga na kukataa kwa kusema
“hakika unataka kumuumba mwanaadamu atakuja kufanya mambo mabaya machafu watamwagana damu.
Bora usimuumbe tu sisi tunatosha maana tunakusabihi na kukutukuza.
Allah akasema hakika ya yeye anajuwa yaliyo jificha na kufichikana.
Ndipo akaumbwa Adam na kufundishwa majina ya vitu vyoote kisha
Mwenyezi Mungu akawageukia Malaika na kuwaambia wamtajie majina ya vitu vile,
Malaika wakashindwa kwa kusema
“ewe Mola wetu hakika sisi hatuna elimu yeyote ile isipokuwa ile uliyotufundisha"
Mwenyezi Mungu akamwambia Adam ataje akataja ndipo
Malaika wakaambiwa wamsujudie Adam wote wakakubali isipokuwa yule Jini akakataa kwa kusema
“hakika Mimi ni bora kuliko huyu Adam kwanza Mimi nimeumbwa kwa moto yeye kaumbwa kwa udongo
Kingine yeye ni mdogo kwangu.
Allah (s.w.t)
Akampa laana yule Jini ndipo likapatikana jina la Shaitwani ibirisi
Na kuambiwa hakika milango saba ya moto ni yakwake yeye na vizazi vyake vyote,
Jini yule akaomba kitu kwa kusema
“najuwa nimepewa laana kubwa sana ila naomba usiniuwe wala usinipotezee uwezo wangu mpaka nitimize kiapo changu hiki
Nitawateka watoto wa Adam ili milango saba ya moto niingie nao
Allah (s.w.t) akamkubalia ombi lake kisha akatupwa kutoka kule mbingu ya saba mpaka huku Ardhini
Je unajuwa kilichotokea baada kutupwa huku Ardhini tukutane baada swalat Ishai....."
Hakika mawaidha yalinigusa sana
Basi ikapigwa duwa kisha tukatoka msikitini tukiwa na Shekhe milongo mpaka nyumbani kwake.
Tukala chakula cha mchana kisha tukatia hudhu tena na kuswali rakaa mbili hivi,
Shekhe akachukuwa kichanja akaweka moto akawasha Udi kisha akasema
“jamani ndugu zanguni hili jambo tunaro taka kulifanya hapa sio jambo dogo kabisa kwanza msiwe na uwoga wa aina yeyote ile pindi watakapo kuja hapa"
Tukaitikia kwa pamoja
“sawa Shekhe"
Akauliza,
“ehee huyo binti anaitwa nani yani jina lake kamili?"
Nikamtaja japokuwa la babu yake silifahamu,
“Anaitwa Nusraty Nassoro"
Shekhe akasema
“sawa Hafidhi embu chukuwa ubani kisha taja ilo jina kimoyomoyo Mara tatu!"
Nikafanya kama Shekhe alivyo niagiza kisomo kikaanza
Hakika kilikuwa kisomo kweli
Alisoma Surat Mulk tena harakaharaka akaongea maneno flani hivi kwa kiarabu kisha akaita
“Binti makata,,,binti Nusraty Nassoro,,,,binti Kidawa Maimuna
Nawaita haraka sana mje hapa,,,,CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Moshi ukaanza kufuka ndani ya chumba kile kupitia pembe ya Chumba viumbe vya ajabu vikaingia huku wakiwa wameinamisha sura zao chini kwa heshima na taadhima wakapanga mistari
Mpaka hapo nilihisi haja ndogo na kubwa vikitaka kunitoka kwa pamoja
Nusraty akainua Uso wake akanitizama kwa gadhabu sana.
Mpaka nikaona Aibu
Shekhe kwa ujasiri mkubwa kabisa akasema
“kwanza kabisa samahanini kwa kuwaita hapa najuwa mnamajukumu kibao tu ya kufanya,
Nilichowaitia hapa ni kuweza kuwapa mashitaka kuhusu Binti yenu kumsumbua kijana wangu nikaona si vyema kujichukulia hatua mikononi mwangu. Pasipo kuonana na nyinyi wakubwa zake.
Kwanza kabisa naomba amuachie Mama wa huyu kijana yani Mke wa huyu Baba kingine aache kumfatilia huyu kijana, kuanzia muda huu,
Asipofanya hivyo
Tusije tukatafutana, wote kwa pamoja wakatikisa vichwa ishara ya kwamba wamekubaliana na
Shekhe milongo kisha wakapotea
Baada vile viumbe kupotea kimiujiza mule ndani,
Shekhe milongo akaongea maneno flani kisha akasema
“binafsi naweza kusema kazi imekwisha japokuwa siwezi kusema yule Binti ametii hii kauli moja kwa moja au laa,
Cha umuhimu ni kumuomba Allah hakika yeye ndio mjuzi wa kila kitu,
Baada kusema vile tukasoma kisomo cha kuagana
Kisha tukarudi nyumbani,
Fatuma alifurahi sana kutuona nikajuwa furaha yake labda kamuona Mama karudi nikaingia ndani kwa shahuku kubwa sana,
Nikaambulia patupu hakuna cha Mama wala nini, kama kawaida saa mbili Usiku ikatimu nikaenda msikitini kuswali
Nikiwa nimepiga hatua kazaa kuupita ule mbuyu nikasikia kicheko kikitokea nyuma yangu sikuogopa wala nini nikageuka na kumuona
Nusraty akiwa na Shekhe milongo nilistuka sana na kutamani kukimbia,
Kwa sauti ya unyonge yenye kukata tamaa
Shekhe milongo akaongea
“Tafadhali kijana nisaidie please usinikimbie ukaniacha hapa peke yangu nisaidie!"
Nikabaki kumtizama tu nikaitaji kwenda kumshika ghafla nikajikuta napigwa na kitu kizito sana tumboni mpaka nikarushwa na kwenda kutua chini nilihisi kama mguu wangu umeteguka hivi, nikawa naugulia maumivu pale chini nikatapika nyongo
Dahaa
Nusraty kwa mwendo wa speed akanifata pale nilipolala kisha akaninyanyua kwa kunikaba yani akanining'iniza utasema kuku kishingo vile
Nusraty macho yake yakabadirika na kufumbua mdomo wake Minjino yake miwili ikachomoza
Na kuwa kama vampire. Nikahisi haja ndogo ikinidondoka,
Akiwa kanikazia macho.
Hafidhi sikuwa na jinsi zaidi ya kufumba macho tu kama kufa wacha nife wamekufa Mitume sembuse mie kapuku tu,
Ajabu akaniachia na kujirudi katika umbile lake la kuwa binti mrembo
Akanishika na kusema
“Hafidhi pole sana mpenzi hivi kwanini unataka haya yote yatokee kipenzi changu, tambua sitaki uumie sitaki upotee please nielewe Hafidhi nakupenda,
Akanishika kichwani kisha akapotea huku yale maumivu yakiniisha
Nikatoka mbio mpaka msikitini nikakuta watu washaswali wanamalizia sunna tu,
Nikatawadha
Na kuingia kuswali ajabu
Shekhe milongo alikuwepo msikitini nikabaki kushangaa pasipo kufunga Sala,
Sijui alifahamu au vipi maana akasimama na kuja pale nilipo simama akasema kwa sauti ya kuninong'oneza
“kijana usiogope fanya ibada kwanza!"
Kisha akarudi sehemu ile ya aliyokaa na kuendelea kusoma Qur'an
Siwezi kujuwa wala kufahamu kama swala yangu iliweza kupokelewa au vipi.
Maana niliswali pasipo kujuwa idadi za rakaa, baada kuona nimemaliza nikatoka nnje
Binafsi nilikuwa na uwoga sana,CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Shakhe milongo akanikimbilia huku akiniita
“Hafidhi kijana wangu embu njoo usikimbie Shekhe wangu,,,," unaogopa nini kwani?"
Nikasimama na kugeuka, kwakuwa alikuwa tayari ameshanifikia
Akanishika mkono
Na kuniuliza,
“embu niambie nini tatizo Shekhe wangu?
Sikuwa na jinsi zaidi ya kumwambia ukweli wote,
Shekhe milongo mpaka ikapelekea Mimi kuchelewa kuswali!"
Akatamka shahada kwa kusema
“Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwa hakika Muhammad ni mjumbe wake!"
Kijana huyo jini katangaza vita embu twende nyumbani kwangu haraka sana
Maana tukisema tulale usiku wa leo utakuwa mgumu sana kwetu"
Tukaongozana kufika tu pale
Mbuyuni nikaona wenge baada
Nusraty kututokea akiwa na wenzake nikataka kukimbia Shekhe milongo akanishika mkono
huku akisema
“tulia kijana unaogopa kuku tu hawa!"
Nusraty akacheka kicheko cha kifedhur
huku akisema
“Shekhe au panya leo ndio mwisho wenu akapiga kombora kumuelekezea Shekhe ajabu
Shekhe akatoa kitabu na kufanya kama ngao yake vile kombora likamrudia
Nusraty mwenyewe
Akarushwa hewani huku wenzake wakitoka mbio nae akapotea,
Nilifurahi balaa huku nikikenua meno 32 yote nnje kumbe Shekhe milongo balaa hakika
Nusraty leo kajamba
Ha!ha!ha!ha!
Shekhe milongo nae akacheka na kuniuliza
“ha!ha!ha!....vipi kijana mbona wacheka sana mpaka umeniambukiza namie nicheke?"
Nikamjibu huku nikiunyanyua mkono wake juu yani kama bondia au mcheza mieleka kashinda
“hakika Shekhe milongo wewe ni mshindi,
“Hapana Shekhe wangu Mimi sio mshindi kama vita ndio vimeanza cha umuhimu tumtegemee Allah (s.w.t)
Hakika yeye ndie muweza wa kila kitu!"
Nikamuuliza,
“hivi Shekhe kwanini namimi unaniita Shekhe haliyakuwa bado sijafikia hata cheo cha kuwa Hustadhi?"
Akatabasamu na kunijibu,"
“Napenda nikuite Shekhe kutokana na ucha Mungu wako,
Kwani natarajia Allah akijaalia utakuja kuwa Shekhe mkubwa sana kwahiyo mpaka sasa wewe ni Shekhe!"
Nikamuuliza swali lingine
“hivi Shekhe mbona Shekhe Yusuf alishindwa kupambana na Nusraty?"
Akaniambia,
“Kuhusu swala la Shekhe Yusuf tuseme alijisahau hakika Shetani ana vitimbi vya kila aina,
Kwahiyo yule Jinni akaona njia pekee ya kumteka Shekhe Yusuf ni kupitia mkewe
Akaenda kumuingia mwilini
Usiku Shekhe akafanya tendo la ndoa na mkewe akajisahau au kusahaulishwa kwenda kuoga kwa ajili ya kuondoa Janaba,
Akalala ndipo yule Jinni akatumia nafasi hiyo kumdhuru.
Kumbuka unapokuwa huna
Hudhu Qur'an inakuwa mbali nawe
unakuwa hauna ulinzi wowote,
Cha umuhimu tudumishe kuwa na hudhu kila sekunde kila dakika na masaa yaendayo kwa
Allah (s.w.t)!"
Baada kuniambia vile tukawa tayari tushafika nyumbani kwake
Akasema kazi ianze,"
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment