Simulizi : Jini Husnat
Sehemu Ya Tano (5)
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
MAKUBWA! tafakuru la mawazo ya mshangao yakajijenga katika pande la uso wake! wasanii wakubwa karibia wote alowajua walikwemo kule kumbe awakufa kwa mapenzi ya MUNGU? ALLAH! okoa kizazi chako.
wakapiga hatua watu walikuwa uchi wazee vikongwe kwa vijana
"kah na hawa? fido"
tayari vergan alishamzoea kiumbe yule fidodido
"hawa ni wanga wamezoea kula nyama za wenzao wachawi wenzao zamu yao imefika awana cha kutoa wengine asahasa vile vibibi vimetoa watoto wao wote muda wao nao ukafika! wengine ndo walotolewa kafara ndo kana ivyo dogo"
sasa VERGAN alikuwa kachoka mwili na roho aliitaji kupumzika.fidodido akalitambua hilo.tutazunguka tena badaye saivi ukaoge upate mlo upumzike..umechoka sasa
"naam swadakta"
akajibu vergan kwa tabasamu pana.Itaendelea usiku.....
******
wakajongea kwa mwendo wa taratibu kuondoka katika eneo lile,eneo la mateso kwa viumbe jamii yake viumbe vilivyosadikika vimekufa kwa mapenz ya MUNGU!
Wakaelekea katika lango kuu la chuma lililonakshiwa kwa dhahabu tupu walipolifikia lango lile likajifungua lenyewe wakapita likajifunga ndani walikutana na mazingira tofauti na walipotokea! kwanzia khali ya hewa,mandhari,
"bado tupo kuzimu kweli?"
swali likamponyoka kuuliza,swali ambalo akuliandaa kabisa katika serikali ya kichwa chake! fido akatabasamu akujibu swali ilo wakaelekea katika nyumba moja ya ghorofa isiyo na mwisho kuelekea juu wakaingia katika lifti fido akabonyeza namba kadhaa za kirumi lifti ikaanza kupanda juu dakika chache ikafika ilipoitajika mlango ukafunguka! MAAJABU! wakatokea katika ukumbi mkubwa ulotawala watu wa asili tofauti tofauti waarabu,wazungu,wataliano wakicheza miziki ipigwao duniani,miziki ya watu maharufu ambao baadh yao walikuwa wakichomeka! kitendo cha kuingia tu msichana mrembo alovaa kimini,matiti yote yalikuwa nje akamfata vergan!
"nipo kwa ajili yako je unani itaji?"
vergan akamtupia jicho fido! fido yeye alitabasamu tu!
"chukua mzigo huo"
nafsi ilimsihi.macho yake yakadondokea kidoleni! PETE,
JINI HUSNAT,kwa mara ya kwanza toka amezwe na OBISHI na kusafirishwa kuletwa katika ulimwengu wa maaswi KUZIMU akamkumbuka jini yule! faraja ikatoweka moyoni mwake,mshangao ukageuka na kuwa simanzi! dada yule akamlalia kifuani mkono wake akiuingiza katika sehemu nyeti zilizokwisha simama.mazingira ya ndani mule ayakuvutia kabisa ilikuwa baadh wanacheza mziki,wengine wanafanya mapenz adharani akuna alokuwa na habari na mwenzake!
"samahani dada naomba niache!"
dada yule akapigwa na butwaa akamuacha,
"tuondoke maeneo haya fido."
fido akatii wakaifata ngazi na kupanda kuelekea juu katika ukumbi ambao watu walikuwa wamepumzika.wakatafuta sehemu wakakaa
"najua kinachokuumiza best! ni juu ya jini wako siyo?"
VERGAN akapigwa na butwaa.
"pEndo la moyo wako! ila pole vergan HUSNAT sasa ni mke wa mtu?"
"what? hapana fidodido unataka kunambia nin? siyo husnat wangu! aiwezekani! haiwezekani aiwezekan fido husnat akubali kuolewa! vip kiapo tulichokula wakati tukiwa dunian kabla ajanipa hii pete? eti leo aolewe kama uwez kaa na mim katika ukanda huu wa kuzimu ruksa kuondoka na kuniacha mwenyew..."
"common vergan listen my frandy sit down kwanza punguza munkari nipe maskio yako upasw kuamaki mpak watu wanatwangalia? unageuka burudani kwa wapumzikao!"
"aijalishi fido! ila ukwel uwez nambia husnat...yah kipenz changu jini husnat kaolewa"
"VERGAN!..." fido akaita! vergan akamtumbulia macho ishara ya kumsikiliza!
"uwezi pindisha ukweli kuwa uwongo nevar happen! pokea ukwel japo mchungu! husnat ajakusaliti kaolewa kwa sababu maalumu!"
"sababu maalumu? ipi hiyo?"
"ni juu ya kisas kwa OBISHI! yule nyoka alokumeza!" kwa mara ya kwanza kumbukumbu za vergan zikaanza kutiririka kama maji yatiririkayo kutoka bombani.akakumbuka akiwa kakamatwa kisawasawa na nyoka yule mpaka akapoteza fahamu! baada ya hapo ikawaje? akukumbuka! naam fido akayasoma mawazo yale akamjibu!
"akakumeza na kukusafirisha mpaka huku kuzimu akakutema nje ya lango la ujinini ukapokelewa na toxic walojua tayar u maiti ulokufa duniani wakawa tayar kukuwaisha katika moto ndipo father mkuu alipokuokoa"
vergan akawa kashaelewa kila kitu! ila fido akazidi kumwelewesha! "ujinini kule majini wanajua ukimezwa na nyoka yule ni lazima uwe umekufa! hivyo hata husnat wako anajua obishi kausika na mauaji yako na obishi aonekani kwa nguv za kawaida! lengo la husnat kuolewa ni aongezewe nguvu kama malkia wa zuluwalad nguv zitakazo mwezesha kukutana na obishi ana kwa ana na kumwangamiza papo hapo"
"ooohpsss!!!"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
vergan akaachia mwayo mkubwa! alichoka!
"naitaji kuongea na husna kumtaarifu kuwa bado nipo hai!"
"wazo zuri JOHN but utamchanganya hali ya ujinini bado si shwari yupo katika uangalizi wa babu yake muu ajuaye kila awazacho take time".....
******
MAUMIVU ya kusalitiwa tena mshtuko wa kushtukiziwa unauma inakuwa ni sawa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali katikati ya moyo! moyo wa VERGAN uliraruliwa na fido! akutaka kusikia la muwadhin wala la mnadi swala! yeye alichoitaji ni kuwasiliana na HUSNAT tu! alishindwa kabisa kuyazuia maji mepesi yalotoka katika kingo za macho yake na kulowanisha mashavu yake.vergan alilia.alililia penzi la jini! akaukumbuka utamu aloupata! wakati wakiwa pamoja,utani walofanyiana! kilio kile kikabadilika na kuzaa kwikwi! ghafla akanyanyuka fido akajaribu kumzuia lakini alishachelewa akauendea mlango ulokuwa mbele ya macho yake mlango ukafunguka JOHN akapita mlango ukajifunga.ndani akapokelewa na chumba kipana chenye kila aina ya uzuri ndan yake! akaenda kujibwaga katika kitanda.akaiangalia ile pete kwa hasira akaivua! pete ikagoma "HUSNA, HUSNA!,HUSNAT nakuita ewe kiumbe msaliti amka kwa nin umenfanyia hivyo nimekukosea nini? umeolewa etieee! na jini mwenzako si ndiyo? nakuitaji mbele ya macho yangu husna njoooo njoooo njoooo nakusubir HUSNA"
GHAFLA mtetemeko ukaanza,ulianza taratibu ukamtupa huku na kule ukampigiza katika ukuta
"HUSNAAAAAAAA"
Akapiga ukelele,akijaribu kuzuia kupandishwa juu akujua anapopelekwa! mikono akainyanyua juu,sauti ya vicheko vikimkejeli katika masikio yake.akujua tayari MUU alishafanya yake.yeye ndo alikuwa kikwazo.aliitaji amuondoe haraka kuzimu kuiokoa ndoa ya mjukuu wake HUSNAT na sasa alikuwa angani akisafiri kwa spidi kali kuelekea katika sayari ya marz.
HIMAYA YA JINI ZULUWALAD
Ulikuwa ndo usiku wa kwanza, kwa wachumba hawa kuwa pamoja,husnat alikuwa mwingi wa furaha alimwangalia mume wake kwa jicho lililolegea ashki za kufanya tendo la ndoa likampanda ZULU akamvamia husna,naye bibie akampa ushirikiano wakawa wamekumbatiana kabla awajandondoshana katika kitanda kipana."HUSNA kwa nini umensaliti!? kosa gani hasa nlokufanyia vipi ahadi tuloahidiana HUSNA HUSNA HUSNAAAAA"
Ghafla sauti ya vergan ikayavamia masikio yake.
*********
Sauti ile ya malalamiko iliingia mpaka katikat ya moyo wake!,kwa kasi ya ajabu akajirusha kutoka kitandani mpaka katikati ya pembe,alishaiona hatari ilokuwa mbele ya mpz wake! jini zulu akiwa na mshangao akajiandaa kumfata HUSNAT,kumzuia,jini yule akamwona mumewe kama kikwazo kwake! akamwangalia kwa macho ya hasira na kumnyooshea mkono wake! shoti kali za umeme zikamtoka na kumvamia ZULU akadondoka na kutulia tuli
"HUSNAT umeua?"
aliisikia sauti ya babu yake muu! akaipuuza! muu kosa alilofanya nikuelekezea nguvu zake zote kwa VERGAN bila kukumbuka hatari ilokuwepo pale HUSNAT atakaposikia sauti ya kipenz chake na hata pale alipokumbuka alikuwa tayari kashachelewa.zuu aligeuka maiti! KIZAAZAA,....
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
JINI HUSNAT akiwa juu ya farasi wake aendaye kwa kasi! aelea hewani mkononi kashika upanga unaomeremeta bado ghadhabu zilimuandama,hasira hizo zilimkosesha umakini na kujikuta akiwa katikati ya walinzi wa himaya yao.vita vikali vikatokea! jini husnat mbele ya majemedari makamanda watano akashindwa kujitetea nguvu zikamwisha.atimaye akasamli amri! akaweka katika nyavu tayari alikuwa ni muuaji akuthaminika tena katika himaya ya ujinini tena
vivyo hivyo hata kwa JOHN VERGAN babu muu baada ya kuona mjukuu wake tayar kakamatwa akuwa na sababu tena ya kumshikilia binadamu yule! majemedari wale wakamtia mkonon vergan na kumuambatanisha na jini husnat kuwarudisha ujinini kwa HUKUMU
Hakika taharifa aloipata jini mkuu MUKRAIYAH juu ya kuuwawa kwa mwanaye kikatili na JINI HUSNAT kilimfadhaisha sana
"naitaji wawe mbele yangu hapa sasa ivi?"
MUKRAIYAH akatoa amri,makamanda wale wakatoweka! malkia sumaiya kila mara alipoteza fahamu kwa mfadhaiko aloupata,wanajamii wa himaya ya ZULUWALADI na MUKRAHIYA wote walisikitika,zulu alikuwa ni jini mpole,msheshi mwenye kusaidia wenye matatizo mbalimbali,kila mtu alikuwa na hasira na JINI HUSNAT na VERGAN.ni wazi wangetafunwa wazimawazima.amani katika himaya ya zulu ilitoweka.majini waso na subira waliwavamia wazazi wa HUSNA
*****
Majini wale wenye wahka uvumilivu uliwashinda! wakawateka wazazi wa HUSNAT na kuwaweka pamoja wakawafunga na minyororo! katikati ya tanuri la moto! awakuwa na kosa nani alilitambua ilo? walizomewa wakapigwa mawe! majini walikuwa ni wengi katika uwanja mkubwa wakishuhudia kusambaratishwa kwa familia ya jini HUSNAT.
dakika chache badae jini HUSNAT na VERGAN waliwasilishwa wakiwa katika nyavu zenye matundu madogo madogo,kelele,na hasira zikazuka! uwanja ule mkubwa ulozungukwa na viumbe vilivyotisha,vikatili,vilianza kwa kuwanyanganya nguvu zote za asili! kwa wausika wote isipokuwa vergan yeye akuwa na nguvu za kijini.sasa awakuwa na uwezo wowote wa kujikinga na dhahama ilokuwa ikiwanyemelea kwa kasi ya ajabu WALIKUWA HATARINI.
Alikuwa ni jini mwenye sura mbaya pengine kuliko kiumbe chochote katika asili ile ya ujinini pembe mbili zenye ncha kali,mweusi tii zaidi ya mkaa macho yake yalowaka zaidi ya tochi,maskio kama ya ngurue kitovu kilichochongoka meno marefu kucha zake ndefu na miguuni alikuwa na kwato alikuwa na manyoya mengi katika mwili wake mkononi alishika upanga mkali ulowakawaka,alikuwa ni JINI MAUTI jini mwenye idhini ya kutoa uhai wa kiumbe chenye asili kama yake,jini asiye na huruma mkorofi na mwenye uchu katika kuuondoa uhai wa kiumbe hai chenye asili kama yake.yeye ndo alokabidhiwa rungu la kuwatoa uhai familia hiyo na kuifuta katika ramani ya ujinini akasimama na kuusogelea mwili wa baba yake HUSNAT na kunyanyua panga lake majini wote wakapiga kelele kushangilia.husnat na wenzake wakafunga macho walipofumbua waliachia kilio kikali cha uchungu!
mwili wa baba yake ulikuwa chini huku mkononi jini mtoa roho yule akiwa kashikilia kichwa cha baba yake akikitafuna kwa uchu! moyo ulimuuma akashindwa kuyazuia machozi kumdondoka.hata vergan huruma ilimjaa katikati ya kifua chake.wote walilia.ilikuwa ni furaha kwa majini wote walojaa katika kiwanja kile.baada ya kumaliza kuutafuna mwili ule jini maiti akausogelea mwili wa mama yake kipenzi....
Jini mauti yule akiwa kaushikilia upanga wake akaendelea kujongea taratibu mahali alipofumbwa mama yake HUSNA,uchu wa kula nyama za mama yule ukiwa umemvaa akaunyanyua upanga juu tayari kuushusha katikati ya shingo ya mama yule.
wakati jini maiti akijongea viumbe vyote vilikuwa makini kushughudia kinachoenda kutokea! ghafla jemedari wa ulinzi akaenda kumnongoneza kitu mfalme MUKRAHIYA,mfalme akashtuka akanyoosha mkono juu kuzuia kuuwawa kwa mama yule "kuna jambo la dharura limetokea ulinz uimarishwe tunavamia walinzi kaeni tayari kwa chochote!" mfalme alitoa taharifa ulinzi ukaimarishwa eneo lile ghafla mvua ya moto ikaanza kunyesha! watu wakatupwa huku na huko ardhi ikamomonyoka na kuwabeba baadh ya viumbe waloathiriwa na tetemeko lile! mvua ile ya moto yenye damu ndani yake ikazidi maradufu!...ghafla ikagoma,hali ya utulivu ikarejea.mvua ile waloweza kuizuia baada ya kuacha iliacha maafa makubwa ya raia.chanzo chake akikujulikana.wakati utafiti wa maafa yake ukiendelea ghafla kikazuka kimbuka kikali! kimbunga kilicho kuwa na nguvu ambayo si ya kawaida,jini mukraiyah akakinyooshea kimbunga kile fimbo yake huku akizungumza lugha asiyoielewa kimbunga kile kikajiunda umbo la kiumbe! mbabu mwenye ndevu nyeupe.babu muu.mwokozi alobakia katika familia ya jini HUSNAT!
"Amuwezi teketeza kizazi changu nami nkakaa kmya MUKRAHIYA!"
"ha! ha! ha! we shetwan mwenye nguvu za kuiba ulokimbia kujificha marz! leo umerudi nakwangamiza kwa mikono yangu!"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"uwezi ibilisi! nakwangamiza kwa mateso makali!"
alijitapa muu! na hapo hapo akaachia kombora la ghafla,Mukrahiya aliyoliona vyema akalikwepa na kuachia lake ambalo lilimpata vyema MUU! akapepesuka,kitendo kilichopelekea mukrahiya kutabasamu kwa dharau.muu akatema moto ulomezwa na mukrahiya mukrahiya akaivuta fimbo yake na kumchapa nayo muu.muu akaachia yowe la uchungu,nguvu zake zilikuwa ni ndogo sana kulinganishwa na MUKRAHIYA. akamchapa alivyotaka.muu akalegea mukrahiya akamsogelea tayari kwa kummaliza.............
*********
Akiwa kashika fimbo yake ya kifalme ambayo sasa iligeuka na kuwa upanga kwa mwendo wa taratibu bila haraka akajongea kusogea eneo alilokuwepo MUU.Mdomoni akiachia tabasamu la dharau.MUU alimwangalia kwa macho ya huruma yamkini akiwasilisha ujumbe aurumiwe! ila MUKRAHIYA alipuuza! watu walipiga kelele ishara ya kushangilia! jini mukrahiya alimfikia muu na kunyanyua upanga wake juu alipoushusha uliondoka na uhai wa jini yule alobaki tumaini! katika kizazi kile kidogo! akainyonya damu yake kwa kuifyonza! huku akiungamua utamu kwa kukitingisha kichwa chake taratibu!
"hudumu utawala wa mukrahiya"
"hudumu,udumu,udumu milele na milele!"
"sasa wakati naendelea kula nyama tamu ya huyu swaiba wangu MUU sasa ni mrudishie uwanja jini maiti aendelee kunyofoa uwah wa viumbe hawa! jini HUSNAT awe wa mwisho akishuhudia vifo vya vipenz vyake."
JINI mukrahiya alitoa maelezo yakinifu yalopokewa kwa vifijo.jini maiti akajongea eneo la tukio na kuondoka na uhai wa mama yake HUSNAT mwili wake akaukata kata mapanga na kuupiga shoti kwa nia ya kuugeuza mlo mara eneo lile likatawaliwa na harufu ya nyama ya kuchoma akawa anakata mapande ya minofu na kuwatupia walokuwa wanashughudia tukio lile nao wakawa wakiigombania nyama ile! huku kinywaji ikiwa ni damu mbichi ya maiti zile.Sasa HUSNAT akulia tena,machozi yalikata,uchungu uliushambulia moyo wake mdogo! babu yake MUU,baba yake,mama yake wote walikuwa maiti kwa ajili yake! kwa ajili ya penzi la binadamu ambaye naye anaelekea kufa! akamwangalia VERGAN ambaye aliona mtetemeko wa wazi.alikuwa akitetemeka huku akiwa kaachia haja zote kubwa na ndogo.kilio cha kwikwi kikisikika kwake.
"chanzo cha matatizo yote ni huyo binadamu atauwawa kwa kukatwa kiungo kimoja kimoja! yeye ndo kaja kuuchafua mji huu.kama si yeye HUSNAT asingemuua mwanangu nawachukia binadamu jini maiti anza kukata kidole kimoja kimoja ukimaliza vyote kata mguu paja kiuno na kichwa."
JINI MUKRAHIYA akiwa anamwangalia VERGAN kwa jicho kali akatoa maelekezo.....
*********
Majini wale wenye hasira! bado waliendelea kupaza sauti! kuarakishwa kwa hukumu ya kifo kwa wapenzi wale wawili! JINI HUSNAT na JOHN VERGAN!,wahka!,jazba vilimpanda jini maiti yule alihisi kitendo cha kumkata kiungo kimoja kimoja binadamu yule angechelewa kuitafuna nyama yake ilokuwa ikipendwa sana na viumbe wale.akaunyanyua upanga wake na kumsogelea VERGA,muda wote husna alikuwa akilia huku akiomba msamaha akijutia kwa alichokitenda.alijiesabia tayari yeye ni mfu mwenye mda mchache wa maumivu! alifumba macho pindi jini maiti aliponyanyua upanga juu ili asishughudie kichwa cha mpenzi wake kikitenganishwa na kiwiliwili.
JINI MAITI kwa nguvu zake zote akaushusha upanga kuelekea shingoni kwa vergan....ghafla akalakiwa na sura yake mwenyewe! yani sura ya vergan ilitoweka na sura ya jini maiti ikaonekana.yani akawa anajiona.HATARI! akaisi kitendo cha kujikata angejiua mwenyewe AKASITISHA ZOEZI LILE huku akiwa kahamaki kwa mshangao wa alichokiona,bumbuwazi likauvaa uso wake macho yake akayapeleka kwa jini HUSNAT alokuwa kaiweka mikono yake miwili usoni kutokushughudia tendo lile.liumizalo moyo.shingo yake akairudisha kwa VERGAN alikuwa ni vergan naye akishangaa kutokujua kulikoni! jini maiti akazidi kupigwa na butwaa! jini HUSNAT alifumbua macho akitegemea kuiona maiti ya mpz wake naye akapigwa na butwaa baada ya kumuona jini maiti akiwa kamtumbulia vergan macho ya mshangao! si jini husnat pekee alokumbwa na mfadhaiko ule hata umati ule ulibaki ukimshangaa jini yule mwenye roho mbaya kwa kitendo cha kusitisha zoezi lile,minongono ya chini kwa chini ikaanza! jini maiti kwa mara nyingine akaunyanyua upanga wake alipotaka kuushusha hali ikawa ni ileile....VERGAN alibadilika na kuivaa sura yake
"ni ni ni kinachoendelea hapa?" jini maiti akajiuliza akakata shauri liwalo na liwe kama ni kujiuwa na iwe.akafumba macho yake makali kama taa na kuushusha kwa nguvu upanga ule kuelekea kichwani kwa VERGAN...,.kwa nia dhabiti ya kuuondoa uhai wake bila kujali maajab
*******
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
JINI maiti akakata shauri liwalo na liwe! akayafumba macho yake makali na kuushusha kwa nguvu upanga ule...akakata hewani.wakati kabla ajafumba macho alilenga sawia shingo ya kijana yule akafumbua macho yake! asalaleee! watuhumiwa wake awakwepo! mashuhuda wote midomo wazi,tayari jini HUSNAT na VERGAN walishatoweka katika mazingira ya kutatanisha!!!
NGUVU gani zinazotumika hapa? zilizojuu ya nguvu zao? akuna alojua! kimuyemuye kikazuka! tafakuru makelele yakazuka! yamkini akuna aliyetambua nani yupo nyuma ya mchezo ule! walipoangalia kuzimu apakuusika,sasa tatizo? mganga mkuu wa himaya ile akaitwa akapanda kilingeni kwa mbwembwe alikuwa ni jitu nene jeupe lenye kichwa cha ngurue tumbo kubwa manyoya ya kutosha kucha ndefu na meno yalochongoka nje! baada ya kufanya vimbwanga akatoka na jibu lililo waacha hoi majini wote
"WAPO DUNIANI! BINADAMU WABAYA WAMENUNUA VITA!"
"tutapambana nao kufa na kupona hawana nguvu kutushinda sisi"
"hidumu himaya hii"
"hidumu! hidumu! hidumuuu!"
vijakazi walinzi watatu wakatumwa duniani.mchezo ndo ulikuwa unaanza.....
-....-....-....-
NDANI YA ULIMWENGU WA DUNIA
Ilikuwa ni nyumba moja ya kifahari sebuleni mwa nyumba hiyo waliketi watu watatu! mzee wa makamo ambaye kichwa chake kilitawaliwa na mvi zilizo meremeta,usoni alivaa miwani na mwilini alivaa nguo za gharama,huyu aliitwa MZEE VERGAN CHILO maarafu kama mzee CHILO baba yake VERGAN,pembeni yake aliketi mwanamama wa makamo alovaa gauni la kitenge lililonakshiwa na mapambo ya kuvutia alikuwa ni mama alojaliwa macho mazuri na unene ulopitiliza huyu alikuwa ni MAMA VERGAN,na watatu alikuwa ni msichana mrembo mwenye umbo namba nane macho malegevu,dimpoz katika mashavu yake huyu alikuwa ni JASMINI mfanyakazi wa ndani nyumbani kwa JOHN VERGAN.Wazazi hao walikuwa wakimsikiliza kwa makini binti yule mzee CHILO akauliza swali kwa mshtuko
"umesema wiki nzima VERGAN ajaja nyumbani?"
JASMIN huku akiwa anatetemeka akatingishwa kichwa ishara ya kukubali...
********
Mzee CHILO na mke wake wakatazamana kwa mshangao!!
"mke wangu ulishaongea na huyo mtoto siku za karibuni?"
mama VERGAN akatingisha kichwa ishara ya kutokubaliana na jambo ilo,chilo akachukua simu yake na kuitafuta namba ya VERGAN akaipiga lakini namba ile aikuwa ikipatikana!
"rudi nyumbani mamaa ntalifatilia hilo!" mzee yule akamweleza mfanyakazi aliyejinyanyua kwa uchovu na kuaga! akiacha hali ya sintofahamu katika familia ile yenye uwezo kiuchumi
"au atakuwa kasafiri?"
Mzee CHILO alitoa sauti ndogo kama anaongea mwenyewe lakini ukweli alikuwa anaongea na mke wake
"sidhani mme wangu! asafiri bila taarifa?"
"itabidi niende kazini kwake ntajua pa kuanzia kumtafuta huyu mtoto kabla atujatoa taharifa polisi"
mzee CHILO akaitimisha kwa kujinyanyua katika sofa lile alilokuwa kakalia mke wake akaachia muayo mkubwa ambao aukujulikana kama ni wa uchovu,usingizi,ama mashaka....
.......................
kwa jina alitambulika kama ALEX ila wengi walimtambua kama MWANDISHI,kutokana na tabia yake ya umbea,unoko,unafki na uchunguzi akiwa ni mmoja wapo wa wafanyakazi walotegemewa katika kampuni alomiliki VERGAN,akipendwa na viongozi wa juu kutokana na kuwasilisha umbeya alougundua chini kwa wafanyakazi wenzake!,na pia alipendwa na wafanyakazi wenzake kwa kuwaletea umbea utokao juu.huyu ndo alikuwa mwandishi kijana mrefu kiasi,maji ya kunde mwenye tabasamu la ucheshi muda wote!
mwandishi Alikuwa ndo wakwanza kuwa na wasiwasi juu ya upoteaji wa VERGAN lakini ilibaki siri ya moyo wake! ALISHUGHUDIA kila kitu akiwa katika uchunguzi wake! jicho lake likiwa katika tundu la funguo mlangoni aliuona ugomvi wa JINI HUSNAT,VERGAN,na MOURINE mpaka MOURINE aliposhambuliwa shoti na WAKATOWEKA.hakika kitendo cha kuona kilimchanganya sana.maajabu ni kwamba akuweza kufungua mdomo wake kusema.japo hamu ya kutoa habari ile ambayo ingempa uma harufu alikuwa nayo lakini alishindwa kusema.alikuwa kama kagandishiwa gundi mdomoni KWA NINI? sababu aikujulikana mwandishi akakosa amani..
Ilikuwa ni kampuni kubwa katikati ya jiji ilomilikiwa na kijana mdogo JOHN VERGAN,jengo ilo lilikuwa ni kivutio kwa wapita njia,jengo ilo la kisasa lilibeba ghorofa nne za vioo kwenda juu lilikuwa ni moja wapo ya majengo maarufu jijini pale
mzee wa makamo alishuka ndani ya gari yake ya kisasa aina ya TOYOTA VEROSA,alikuwa ni mzee chilo,baba yake vergan akachepuka kwa mchepuko wa hatua zake fupi fupi ila za haraka haraka kuelekea ndani ya jengo lile "RECEPTION" ulisomeka mlango ulokuwa mbele ya macho yake ambao palikuwa na uwazi pasina mlango wa kuingilia akazama ndani alipopokelewa na wafanyakazi nadhifu ambao kila mmoja wao alikuwa bize katika kompyuta yake na ma faili katika meza zao
"shikamoo mzee!"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
mwandishi akatoa salamu huku akiamisha macho yake toka katika kompyuta kujua kulikoni? alihisi kitu
"si kawaida huyu mzee aje kututembelea! kuna kitu lazima niwe makini nisipitwe!" aliji tahadharifa
"marhaba! JANETH naweza nikamuona meneja?" baba yake VERGAN akajibu salamu wakati huo huo akimfata msichana ambaye alionekana ndo secretari.msichana yule akatabasamu akaukwapua mkonga wa simu na kuuweka masikioni akabonyeza tarakimu kadhaa MWANDISHI alikuwa makini asipitwe.kwake lilikuwa ni kosa kubwa
"haloow bosi! mzee anaitaji kukuona!....sawa mzee ingia!"
mzee CHILO akaiparamia ngazi kuelekea juu! mwandishi naye akajinyanyua na kumfata kinyume nyume wafanyakazi wala hawakumshangaa walishamzoea walisubiri habari mpya mzee chilo akafika katika mlango uloandikwa maneno "mkurugenzi" akabisha hodi mara moja kabla ajakitekenyua kitasa cha mlango ule kikamtii akazama ndani.mwandishi akaishia mlangoni akapiga chabo kujua kinachoendelea ndani! ndani mzee CHILO alimkuta mzee wa makamo kidogo JENGUA wakakumbatiana kwa furaha! huyu alikuwa ndo msaidizi wa VERGAN baada ya makaribishano CHILO akaeleza shida,dhumuni la kwenda pale ni juu ya kupotea kwa mwanaye mmiliki wa kampuni ile JOHN VERGAN
mwandishi akashtuka pale mlangoni na kuweka mkono..
********
mwandishi akashtuka!,akaweka mkono mdomoni kwa mshtuko aloupata kumbukumbu zikarejea wakati JINI HUSNAT na MOURINE(JINI ZAYDATU) wakirushiana shoti na wote watatu wakatoweka sasa ni wiki mbili zimekatika bila kuonekana kwa bosi wao VERGAN! kwa unyonge mikono kaiweka nyuma akarudi eneo alipotokea "mapokezi!" akapokewa kwa bashasha na wafanyakazi wenzake!
"mwandishi baba kaja na shida gani?" mfanyakaz mmoja alimchokonoa akikaa kiumbea
"sijui sijawa kivuli chake" mwandishi alijibu kwa mkato na kuendelea na kazi! umbea ulimwisha.ilimlazimu afunge domo lake akujua kwa nin
kule ndani mzee jengua alishangaa kupotea kwa mkurugenz wake VERGAN katika mazingira ya kutatanisha! akukuwa na habari ambayo ingewafumbua macho.ikabidi mzee CHILO aage kwa minajili ya kwenda kituoni.akaruhusiwa bila kipingamizi.akatoka,akawaaga mapokezi! muda wote mwandishi alitaka kufumbua mdomo wake lakini alijikuta akishindwa mpaka mzee CHILO akaondoka katika eneo lile.
............
alishangaa siku iyo mawazo kumtawala na kuyakosea majibu! ili kuyapoteza mawazo hayo ni lazima akapate bia mbili tatu! mwandishi SIRI ilimtesa aliitaji kuwa huru mwingi wa furaha kwa kuitoa siri hiyo! ila kwa nini kila nikitaka kusema nashindwa? akawaza akigubia bia ile kwa fujo! ghafla pombe zikamkaa kichwani wazo ambalo alikuwa mwanzo likajijenga! akatabasamu ni wazo ambalo lingemwingizia hela! wazo hilo lililomtesa kwa muda mrefu tangu alipolishughudia kwa macho yake mawili likageuka dili.dili ambalo kama angelicheza vizuri angekula ela nyingi,..akili ya pombe sasa zilimletea faida.akashika simu yake na kupiga namba kadhaa
"naongea na mama VERGAN?"
"ndiyo mimi ni mwandishi ALEX....ndiyo baba alikuja kazini nkashindwa kumwambia kutokana na itikadi zake za kidini ila naitaji tuonane uwe peke yako nikueleze mahali mwanao alipo! kweli mama sikutanii ila uniandalie ela kidogo! nyumbani? amna mtu? poa naja saivi mama"
baada ya kumaliza kuongea na simu akaikata na kujinyanyua kiuchov huku akiwa anapepesuk
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
******
Akiwa anapepesuka MWANDISHI alianza kujongea kutoka eneo lile la club muda mwingi akikosa muhimili na kudondokea meza na viti maeneo yale! akujali alinyanyuka na kuliendea gari lake.akaingia ndani na kuliondoa.....
maajabu!! usingeweza kuamini yule mlevi ambaye dakika chache alikuwa akipamiana na viti ndo aliyomo ndani ya gari ilo.mwandishi alikuwa makini barabarani japo aliwaza kilevi!
"ili ni dili la fedha! kwa kuwa ni swala nyeti...ni dili ambalo ntashrikiana na familia hii mpaka nijue mwisho alafu habar hii sitomuadithia mtu ntaipeleka kwenye magazeti ambapo ntalpwa kiwango kikubwa cha ela! aya macho yanaenda kuntajirisha." aliwaza huku akiingia mtaa walokuwa wakiishi wazazi wa bosi wao.akaelekea mpaka kwenye nyumba ya kifahari mlinzi akafungua geti mwandishi akaingiza gari lake mpaka ndani.akashuka huku akipepesuka akaelekea sehemu alimostaili kuelekea.....
...........
alipigwa na butwaa alomkuta ndani akutegemea kumkuta.moyo ukaanza kumwenda mbio na pombe taratibu zikaanza kuyeyuka.ni baada ya kumkuta mzee chilo baba yake VERGAN ambaye kiukweli alimuogopa
"karibu sana mwandishi sijui uletewe kinywaji gani?"
"maji tu yanatosha" alijibu ki khofu huku mwili wote ukimloa jasho kwa anguko la tetemeko.mwandish Alex alitetemeka hadi meno mama VERGAN akaliona ilo ili kumtoa khofu akamwambia
"mwandishi usijali kama ni pesa utapata na usimwogope mzee naye yupo pamoja nami tueleze mwanetu yupo wapi au katekwa na nani na wanaitaji nini?" moyo wa Mwandishi kidogo ukaridhika baada ya kutolewa khofu akaanza kuongea kwa kujiamini
"wazee wangu hii ni siri nyeti siri ambayo baada ya kuitoa yaweza chukua uhai wangu je ntaiachaje familia yangu? bila milioni 50 kuingizwa kwenye akaunti yangu sifumbui mdomo"
"unasema?" mzee CHILO akauliza kwa hasira
"milioni 50 nieleze ninachojua juu ya bosi hata nikifa familia yangu isipate tabu"
"milioni 50 eeh subiria nkakuletee....." mzee chilo akaingia ndani na kuchukua simu na kupiga kituo cha polisi
aliyepokea simu kituoni akaidi robo saa kuwa maeneo yale.
............
afande au waweza kumwita SAJENTI KIKOTI akiwa kituoni,alikuwa kavaa nguo za kiraia,wakati akiwa kituoni hapo mara simu yake ya mkononi ikaita akaangalia mpigaji akaachia tabasamu dogo na kuaidi kufika eneo la tukio robo saa.akainuka na kuchukua maafande wawili na kuingia katika difenda!
........
wakati mwandishi akiwa anasubiria milioni 50 zake aliamua kukunja nne kabisa,mawazo yake yalikuwa mbali sana kifikra! maendeleo aliyoyawaza yalikuwa ni zaidi ya fedha alizoitaji! aliwaza kutengeneza bonge la nyumba maeneo ya wanaoishi matajiri ufukweni mwa bahari!,magari ya kisasa,ajenge maoteli ya nyota kah! kwa milioni 50? na vimilioni 5 vyake benki! akaachia tabasamu afifu alilolizima ghafla baada ya kuingia maaskari moyo wake ukapasuka paaaaa! tayari hatari ilishawaka katika fikra zake.
"afande huyu kijana anajua kila kitu anaitaji milioni 50 eti ndo atueleze"
"what?"
kikoti alistaajabu akaendelea
"afande marwa piga pingu ilo likaeleze kila kitu kituoni sijapata kuona jambaz jinga namna hii"
machozi yakatiririka katika mashavu yake! akajiona mjinga kuwaza ujinga.akabebwa mzobe zobe mpaka kituoni aliposhushwa na kuanziwa mahojiano muda huo huo
"unaitwa nani"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"alex"
"majina yako matatu" kikoti alizidi kumuoji
"ALEX BANDAMA KINAINAI"
"kah" afande alistaajabu!
"unafanya kazi wapi?"
"vergan compuny!" kah kwa hiyo ndo umeshiriki kumteka bosi wenu? (hapana afande mi sijashiriki!) haya tueleze waloshiriki upate kuwa huru! (siwajui) alijibu MWANDISHI huku akilia...afande kikoti akusema kitu akaondoka aliporudi alikuwa na mkebe akaufungua kulikuwa na plaizi mikasi spoku na vifaa ambavyo akuweza kuvitambua kwa haraka! (ntaanza kwa kukuchomoa kucha moja moja mpaka utakapoeleza wanaousika kwa kupotea kwa vergan) MWANDISHI mdogo ulimtetemeka akutaka kuwa katika maumivu akaamua kuueleza ukweli! ukweli ambao katu aukuwaingia maafande akilini! (anayeusika katika upotevu wa vergan jini)
***********
Mwandishi hakuwa tayari kungofolewa kucha zake akaamua kusema ukweli! ukweli ambao aukuwaingia akilini kabisa polisi wale!
"vergan kachukuliwa na jini?"
"what?" kikoti na maafande wengine wakatazamana.kilichofatia ni kumvurumishia kipigo mangumi mateke,bila kujali damu ilokuwa ikimtoka! ila msimamo wake ukabaki palepale....serikali haikuamini mambo hayo ivyo kulionekana kuna kitu anaficha!
............
"nimeshakwambia mme wangu! yule si mtoto mdogo kusema maneno yale lazima twende kwa mganga tuka angalie huku polisi wakiendelea na msako"
MAMA VERGAN alikuwa ni miongoni mwa wazazi waliosikilizwa na wanaume zao,yani wao ndo walikuwa kichwa cha nyumba.mzee CHILO kila alichoambiwa na mke wake akuweza kuweka mkatao ilikuwa lazima akubali leo hii alimfikishia habari mke wake juu ya yanayoendelea kituoni kule,mke wake akamjia juu na kumlazimisha waende kwa mganga.chilo akukataa wakafunga safari na kuelekea kwa mganga maarufu sana kwa majini
................
KWA MGANGA
Ilikuwa ni nyumba nzuri ambayo usingeweza kuamini kama kuna mganga wa asili ndani ya nyumba hiyo ilikuwa ni nyumba ya kisasa yenye bati la vigae geti nje na hata mlinzi alikwepo.walipaki gari lao sehemu palipostaili wakatoka walipokelewa na watu wengi walokuwa wakisubiria huduma.walienda kizamu zamu mpaka zamu yao ikafika wakaingia: ilikuwa ni chumba kidogo ambacho mlangoni kwa ndani kilichomekwa fuvu la kichwa.aijulikani ni la kiumbe gani chini kulitundikwa jamvi na mganga yule aliketi akiwa kavaa nguo nyekundu pia chumba kile kilipigwa rangi nyekundu mpaka mapazia yalikuwa mekundu! "ibana iyanyeeee,ivyuna kyaleeee aaaah haaaaa haaaaa"
"ndiwaona mwaja(nawaona mnakuja)"
"ivua rwandu(vueni viatu)"
Mkalimani akawa anafanya kazi ya kuwatafsiria! mganga akachukua mbegu flani akazinuizia akazipiga chini mbegu zile zikatoweka akatoa kicheko na kuanza kuimba
rudi inyumenyume:(rudini kinyume nyume)" wakatii wakaketi chini mganga akapandisha maruani akaongea vitu visivyoeleweka mkalimani akatafsiri
********
Mganga akaachia cheko tena! na kuongea lugha isiyoeleweka!
"babu tumekuja na sh..."
mama VERGAN kabla ajamalizia tumekuja na shida akakatizwa."najua! najua! hahahaaaa najua kilichowaleta! ni vita kali binadamu mna roho mbaya sana!" wote wakashtuka!
"mimi ndo mganga NDUMBWENDUMBWELE najua mmekuja kwa shida ya kupotea kwa mwanenu VERGAN"
Mzee chilo na mke wake wakaangaliana kwa mustaajabu mkuu
"ndiy,..o....ba.bu"
"sema tawile!" mkalimani akamsahihisha
"tawile" wote wakajibu
"mumefanya vibaya sana! mwandishi kawaokoa kwa kuwaeleza ukweli mahali alipo mtoto wenu maisha yake yalikuwa hatarini kama jini yule angekuwa huru ivyo yapaswa mumuachie huru kwa kuwa kama si yeye msingepata akili ya kuja huku mumpe hela anayotaka kama mnayo...."
"tawile babu" wakaitika pamoja huku mzee chilo akiwaza yake kichwani.
"huyu mzee nuksi ndo maana mi siwaaminigi milioni 50..."
"usiniwazie vibaya mzee leo utatuamini tazama tv asilia tazama uone mahali alipo mwanenu tazamaaaaaaa"
Mzee CHILO alista ajabu kwa mawili kwanza uwezo wa yule mzee kusoma mawazo.akakaza macho yake katika kitambaa cheupe kutazama.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ghafla kama sinema katika kitambaa kile kukatokea picha.picha ilo onekana MKUTANO ULE wa hukumu ya jini HUSNAT na VERGAN
"mnaona? ila mmewai mimi ni mganga ndumbwendumbwele na uwezo wa kuwazuia na kuwaleta duniani hahahahaha ndumbwendumbwele! ashindw na kitu ni Uwezo MUNGU alonipa"
wakati kule jini maiti akinyanyua upanga wake huku NDUMBWENDUMBWELE alifanya mazingaumbwe sura ya jini maiti ikaivaa sura ya VERGAN.jini maiti akajiona na kusitisha zoezi lake
"ha ha ha ha ha mmewah mwanenu mngempoteza."
wazazi wale wawili walichoka.mganga akaanza kuimba akamchukua paka mweusi aloletewa na mfanyakaz wake akamchinja akamfyonza damu.ghafla akatoweka.alipo rudi wakarudi watatu JINI HUSNAT,VERGAN na NDUMBWE NDUMBWELE.PATASHIKA
"hawa wanapendana yapaswa waishi pamoja humu duniani kwa sababu huyu msichana atakiwi kwao tena.hahahaha" mganga yule aliongea huku akijitaidi kuwapatia ufa
********
Mganga alokuwa kiboko ya majini ukanda wote wa africa mashariki NDUMBWENDUMBWELE aliendelea na jitihada za kujaribu kurudisha fahamu za wateja wake ambao ni JINI HUSNAT na VERGAN kwa kuwamwagia maji ya bahari! ila hakukuwa na mabadiliko yeyote akagundua kitu ambacho akupenda akigundue lakini ndo ivyo alishakigundua KAZI ILIKUWA NI NGUMU ZAIDI YA ALIVYOTEGEMEA ilibidi/ilimlazimu hatumie "plan b" plani ambayo ilikuwa ni hatari kwa maisha yao kiujumla! njia ya kwenda kuwazamisha kabisa baharini! njia ambayo pia ingezirudisha nguvu za HUSNAT ambazo zingekuwa ni hatari! baada ya kuwaeleza hivyo wazazi wa VERGAN wakakubali waungane pamoja usiku huo kwenda baharini walimpenda sana mtoto wao WANGEJUA?!
.............
KATIKATI YA USIKU
UFUKWENI MWA BAHARI:
Hali ya hewa ilikuwa niya utulivu!,upepo mwanana ulipepea na kuleta ka upepo ka tamu kwa kubarizi!,mawimbi ya maji yalipiga taratibu na kuongeza ualisia wa ufukwe huo.eneo ilo la ufukwe katika usiku huo mnene lilitawaliwa na giza,giza ilo lilifanya kutisha kwa mandhari ya eneo hilo ila mtisho huo aukuwatisha viumbe saba walokuwa pembezoni mwa bahari wakifanya kilichowaleta.katika eneo hilo akukuwa na kiumbe kingine zaidi yao si wavuvi wala wanyama!,si ndege wala wadudu viumbe wale wote walijifunga kaniki nyeusi tiii! na walijichora usoni na mikaa walikuwa ni mganga
ndumbwendumbwele,alokuwa na hirizi kubwa ilokuwa ikipumua kifuani kwake akiivaa kama cheni shingoni,kichwani alijifunga kitambaa chekundu mkononi alishika usinga,pembeni yake walikwepo vijana wawili ambao mmoja alimshika njiwa mweusi tiii asiye na doa,mwingine alimshika paka mweusi mwenye macho ya njano alokuwa akilia muda wote.mama VERGAN alikuwa kashika kibuyu na kisu kikali na panga,mume wake alikuwa kashika nazi!,na mayai jini HUSNAT na VERGAN wenyewe awakushika kitu walibaki wamenata vilevile kama masanamu wakishangaa eneo moja palepale ufukweni vijana wale wakamchinja yule paka na damu yake wakaimimina katika kile kibuyu alichokishika mam
*********
Wakamchinja paka yule ambapo damu yake waliimimina katika kile kibuyu alichoshika mama vergan.walipomaliza wakamchinja na yule njiwa damu yake wakaichanganya na ya paka katika kile kibuyu wote wakachovya kidogo na kujipaka usoni,wakanywa na nyingine wakamwaga eneo la ardhi,baada ya kumaliza mganga NDUMBWENDUMBWELE akachukua maziwa na kufanya vilevile! wakanywa machache mengine akayamwaga palepale alipoimwaga damu.akachukua kisu na kujikata damu akaimiminia sehemu moja wote wakafatisha kwa zamu baada ya kumaliza kila mmoja kutoa damu yake kila mmoja akaonja ilobakia wakaimwaga palepale kama una moyo mwepesi usingeweza kunywa vile! ila wote walikuwa tayari! tayari kwa chochote MAAJABU!
cha ajabu zaidi pale walipojikata awakusikia maumivu yoyote wala jeraha! kaaah! huyo ndo alikuwa NDUMBWENDUMBWELE kiboko ya majini! baada ya kumwaga damu ile chini palepale alipomwaga damu,maziwa ghafla vikatoweka FADHAIKO
mganga akaachia cheko moja ishara ya ushindi
"ha! ha! ha! mizimu imekubali sadaka yetu sasa ni zamu ya kuwazamisha majini yani kama kuwabatiza jini HUSNAT akigusa maji ya kwao tu atarudiwa na fahamu! zake pamoja na nguvu zake alizonyanganywa na mfalme wake MUKRAHIYA ila VERGAN mpaka azamishwe kabisa katikati ya kina kirefu ivyo tutaanza na HUSNAT kama likitokea la kutokea awe msaada kwetu!"
"tawile babu" wote wakaitikia.
"mtanifata nyumanyuma"
aliongea mganga NDUMBWE akimvuta jini husnat!,jini yule akagoma! KIZAAZAA!
akamlazimisha lakini husnat hakuwa tayari! ni ishara mbaya,ni ishara ambayo kama angeijua asingemlazimisha ila usilolijua ni sawa na usiku wa giza.machoni mwa jini yule machozi yakaanza kumtiririka! machozi ya damu MAAJABU!CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Tayari alishaiona hatari ilokuwa mbele yao.laiti kama wangegusa maji yale.mganga akujua yeye baada ya kuona husna anakataa! akachukua dawa flani na kumwagia husna KOSA!
husna akawa kama tahira akamtii mganga akamfata nyuma wakayasogelea maji katu mganga akujua hatari ilokuwa mbele yake na laiti kama angeijua!
********
Katu mganga akujua hatari ilokuwa mbele yao na laiti kama angelijua! wangelifata kile HUSNAT alichotaka lakini kila kiumbe MUNGU alikibarikia uwezo wake binafsi! wakasogea taratibu eneo lile la maji ile wanataka kuyakanyaga maji ukatokea mlipuko ulowarusha wote nyuma kwa ghafla muda huo huo hali ya hewa ikaanza kubadilika! ghafla! viumbe viwili virefu visivyo onekana mwisho wao miguuni wakiwa na kwato vikatoke KIMBEMBE!
Mganga ndumbwendumbwele akasimama akiwa tayari kwa lolote! viumbe vile taratibu vikaanza kufupika! vilikuwa ni viumbe vilivyotisha kichwani walikuwa na pembe mbili zilizochongoka!,kila kiumbe kilijaliwa jicho moja kubwa katikati ya paji la uso,jicho jekunduuu,lililowakawaka na lililotisha kwa aliangaliaye! walikuwa na meno mawili marefu yalochomoza nje ya kingo ya midomo yao,katika paji la uso juu ya jicho walikuwa na herufi 666,mikononi walikuwa na kucha ndefu zilizochongoka!,walicheka! kicheko icho kikawa ni maumivu kwa binadamu wale kasoro mganga na HUSNAT kwa sauti ya kukwaruza na yenye kitetemeshi wakasema:
"binadamu! mumeingia katika vita binadamu!!!" kila walipo ongea sauti ilijirudia mara mbili kama mwangwi.
"nyinyi ni nani na mnataka nini kwangu?" mganga NDUMBWE aliuliza kwa ukali!.upande wa kwa wazazi wa VERGAN walikuwa wakitetemeka kwa moyo wa kibinadamu awakupaswa wakione walichokiona!,walilala palepale chini waliporushwa bila kujitingisha wakitetemeka! ilikuwa ni kama wameambiwa walale vile.jini husnat alibaki ameduwaa!!! akujua kilichokuwa kinaendelea na mwenzake VERGAN wenyewe walikuwa nje ya ufahamu!,watumishi wawili walibaki wakitetemeka wakimwangalia kwa huruma bosi wao mganga NDUMBWE
"upaswi kutujua tunaitaji viumbe vyetu!" viumbe wale walizidi kuongea kwa sauti ya kitetemeshi!,sauti yenye mkwaruzo kama wa radi!.mganga NDUMBWE akaachia cheko! cheko la dharau! cheko la majidahi,cheko la kiburi na akafatiwa na maneno ambayo yaliwatiya hasira wale viumbe!
"nyie viumbe mlolaanika,viumbe wachafu...."
*******
"Nyie viumbe wachafu! mlolaaniwa mkalaanika naomba mfutike katika mbon4 ya macho yangu kabla sijawaangamiza!"
Viumbe vile vikazidi kukasirika midomo yao kwenye mashavu kukajaa! yamkini kulikuwa na kitu WAKAKITEMA kwa pamoja! lilikuwa ni kombora la moto ambalo liliungana pamoja na kumwendea kwa kasi mganga yule mganga akaliangalia kombora lile kwa dharau na kulionyeshea usinga wake! kombora lile likatoweka!...naye akaunyoosha mkono wake ukaanza kutema cheche mfululizo kama risasi zichomokapo katika bomba la bastola lenye bomba tatu! ukienda kwa kasi upande waliopo viumbe wale! lilikuwa ni tukio la ghafla! kimuyemuye kikazuka! madubwasha yale walijitaidi kujikinga bila mafanikio hatimaye wakatoweka! wakimwacha mganga akiwa kachoka kwa ile vita kali
"mumeona mimi hawaniwezi! mumeona mimi ni kiboko yao! mizimu ya kusini mashariki,kaskazini,magharibi yote ipo upande wangu hawaniwezi...."
mganga akaendelea kujisifu
"muchanganyiko wa damu mulokunywa imewasaidia!....mizimu imetulinda sasa tunaweza kuendelea kuwarudishia ufahamu...." aliongea mganga huku akimwangalia jini HUSNAT
"mamaa twende mama hatari ulokuwa unaiogopa imepita mamaa...."
HUSNA akamtupia tabasamu!,mwanya wake mdogo ukaonekana katika meno yake meupe! tabasamu lile ilikuwa ni tafsiri nzuri kwa mganga NDUMBWE NDUMBWELE,sasa Vergan na wazazi wake walibaki nchi kavu,woga mkuu ukiwatawala,kimbelembele cha kumfata mganga nyuma nyuma kilifutika kwenye maji waliigia wa nne mganga,JINI HUSNAT,na wasaidizi wake wawili!
kitendo cha jini yule kukanyaga maji yale ya bahari macho yake aliya angaza angani shoti zikitoka! NGUVU ZAKE ZILIKUWA ZINARUDI,nguvu zake za kijini bado mganga na wafuasi wake waliendelea kuimba,ghafla JINI HUSNAT machozi mfululizo yakaanza kumtoka machozi ya damu!!!
ilikuwa ni ishara ya maumivu tele katika moyo wake mdomo ukaanza kumtetemeka kwa hasira! mabega yakaanza kupanda juu,kilio hafifu kikasikika jini husnat alikuwa akilia,akiwalilia ndugu zake....kisasii
*******
Ilikuwa ni furaha kwa mganga NDUMBWENDUMBWELE
kufanikisha kwa kazi yake!,sasa kazi ilobakia ilikuwa ni ndogo tu kumrudishia ufahamu VERGAN,na kumtuliza husnat hasira zake,asilolijua mganga yule ni kwamba hasira za vergan haziwezi kuzuiliwa pasina kulipiza kisasi,kisasi kwa himaya yake ilousika na mauaji ya wazazi wake.kisasi kilichokuwa katikati ya moyo wake,mganga akambembeleza sana jini husnat watoke baada ya kumbembeleza sana jini husnat akatii!,wazazi wa VERGAN walimshangaa husnat baada ya kupata nguvu zake....
"asalam aleykum warahmatulah taghala wa barakat"CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
jini husnat aliamkia kwa kirefu huku macho yake yakiwa kwa VERGAN
"walekumussalam" wakaitika! jini husnat alikuwa ni binti mwenye heshima wazazi wa vergan walivutiwa na binti huyu! baada ya salamu mganga aliitaji kumchukua Vergan na kwenda kumzamisha baharini! lakini husnat alimkataza akamwaidi kumponya yeye mwenyewe akamwekea mkono kichwani na kumsomea baadhi ya aya za QURUAN kitabu kitakatifu! vergan akarudiwa na fahamu zake! WAKAKUMBATIANA kwa furaha!!!
wote kwa pamoja wakiwa na furaha katikati ya usiku huo wakarudi nyumbani kwa mganga wakiwa wamepona!!!
...............
MASAA MAWILI MBELE KATIKA USIKU HUO HUWO
Nyumba ya kifahari ya mganga ilikuwa ni kubwa ivyo VERGAN na mpenzi wake walipewa chumba chao na chilo na mke wake naye walipewa chumba chao,ilikuwa ni wakati wa wapenzi hawa kukumbushana enzi zao kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake,wakazama katika mahaba mazito...,mahaba yalopelekea kutungwa kwa mimba bila wenyewe kwa muda huo kuelewa.mwisho wa mahaba yale kutokana na uchovu VERGAN alilala usingizi mzito,hali ilikuwa ni tofauti kwa JINI HUSNAT,usingizi aukutaka kumchukua mawazo ya hasira,chuki na kisasi vikimtawala akaamka kwa lengo kuu.....
lengo la kurudi kwao ujinini usiku huo huo kwa kazi moja tu ya KULIPIZA KISASI!
hasira zake kwa sasa azikuzuilika! wakati akijiandaa kutoweka ghafla likatokea asilotegemea,lililovunja mawazo yake yote na kumuweka katika
**********
Wakati jini HUSNAT akijiandaa kwa tendo lile la kutoweka! ghafla akatokea mvulana mzuri,mvulana wa kiarabu alovaa kanzu nzuri ambayo hata HUSNA mwenyewe alibaki akiikodolea macho kwa uzuri wake,kichwani alijifunga kilemba.alipendeza aswaaa!,mkononi,mkono wa kushoto alishka tasbih,na wakulia alishka ule msahafu mdogo(quran tukufu) wenye zipu,usoni alikuwa akiwakawaka katika paji la uso wake katika (singda) nuru.
"asalam aleykum warhamattulah taghala wa barakatu!"
"waleykumussalam warhamattulah taghala wa barakat"
alisalimia kijana yule alozuka ghafla maeneo yale.naye jini HUSNAT akaitikia huku akijistiri unywele wake ulofika mgongoni kwa kujifunga ushungi.yule mkaka akatabasamu kidogo meno yake ya dhahabu yalopangwa vyema katika mdogo wake na kumuongezea uzuri yakaonekana!
"mimi ni malaika!,mjumbe wa ALLAH!,nimetumwa kwako iwe kiumbe wake,mateso makali umepata!,umepoteza wazazi wako!,na unaitaji kulipiza,mwenye kutoa HUKUMU ni ALLAH pekee na si binadamu wala nyinyi majini!....samehe ndo NUSRAT kwako jini kuolewa/kumuoa binadamu MUNGU amekataza ila amenituma kwa kuwa mmependana muda mrefu...ruksa kuoana na sasa tumboni mna kiumbe....msilimishe kijana mfunge ndoa japo itabaki kuwa siri kwa baadhi ya watu kuwa wewe si binadamu ila wengi wao watawatambua kama nyote ni binadamu na utaishi kama binadamu japo utakuwa ng nguvu zako mengine ALLAH YAGHALAM,MUNGU mjuvi wa mengi muwe na maisha mema."
malaika yule akatoweka!
hasira ya jini HUSNAT kama barafu ikatoweka ghafla vergan akashtuka kumbe ndotoni alimwona malaika yule na ujumbe ule alipotoweka naye ndo akazinduka.wakaangaliana kwa tabasamu
"nimefrah umenibebea kiumbe!"
"mmh umejuaje?!" HUSNAT kwa sauti ya kimahaba akamuoji
"nisha anza kuwa na uwezo kama wako!" Vergan alitania
"maishaaa!!!" JINI HUSNAT alimdhihaki
"uamini sasa?"
"nnachotaka usilimu!"
"ungependa niitwe jina gani?"
"ningependa uitwe OMARI"
"mh kwa nini?"
"ni jina la baba yangu"
"sawa kipenz cha moyo mama NUSRAT....."
********
"Waooh umejuaje mama yangu anaitwa NUSRAT?!"
"ni malaika alokutokea kakwambia uwasamehe viumbe wenzako ndo NUSRAT kwako basi kama mwanangu akizaliwa wa kike aitwe NUSRAT!"
"waoooh! na pia nusrat ndo jina la mama yangu! ila je akizaliwa wa kiume aitwe nani?"
"ataitwa ZULUWALAD ili tuwapunguzishe hasira majini wenzako kwa kutambua bado tunawajali"
"mh! basi sawa mume wangu tulale sasa...." wakalala wakiwa wamekumbatiana.
............
Asubuhi walipewa ruksa na mganga ndumbwendumbwele ambapo kabla awajaelekea nyumbani walielekea msikitini! ambapo JOHN VERGAN alisilimu na kuitwa OMARY,siku chache badaye kharusi kubwa ilifungwa,OMARY na HUSNAT wakaishi kwa amani,kharusi iloacha gumzo nchini TANZANIA na hata chini ya bahari ujinini wakarudi kwenye nyumba yao ya kifahari wakimsubiria kijacho......
...........CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Jini mkuu MUKRAHIYA baba yake ZULUWALAD hasira zilimpanda sana aliamua sasa kwenda duniani na walinzi wake kwa lengo moja tu! kumuangamiza OMARY na JINI HUSNAT cha ajabu walipoifikia nyumba ya JINI HUSNAT walikuta bahari nyumba awakuiona walipojaribu kuisogelea waligundua maji yake yalikuwa yakichemka! wakahamua vitavyao waviamishie kazini.nako mambo yalikuwa hivyo vivyo! walipowatafuta wabaya wao katika salelaiti zao awakuona kitu zaidi ya moto! ambayo kwao ni ishara mbaya,wakaleta waganga na waganguzi hali ikawa ile ile MUNGU ni mweza wa kila kitu aliwalinda Kina omary na husnat bila wao wenyewe kujijua.majini wabaya wakaachana nao.....wakakubali kushindwa.
MWISHO ............ TOA MAONI
0 comments:
Post a Comment