Search This Blog

KABURI LA KAZULA - 1

 





    IMEANDIKWA NA : ALEXIS WAMILLAZO



    *********************************************************************************



    Simulizi : Kaburi La Kazula

    Sehemu Ya Kwanza (1)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Licha ya umasikini aliokuwa nao kijana Kazula,lakini ndoa yake bado ilionekana kukumbwa na misuko suko ya hapa na pale,kwani kila kikicha mama yake alidai mtoto,hata mke wake nae ambae aliitwa mele,alikuwa akimlaum saaana mumewe kwa kushindwa kumpa ujauzito..kitu ambacho kilimnyima furaha kazula,akajiona hana bahati..hata ham ya kufanya tendo la ndoa lilipotea kabisa..kwani aliona haina maana yeye kujamiana na mke wake pasipo mafanikio ya kumpatia mimba.

    Siku zilizonga miezi nayo ikasogea,kazula akizidi kukosa amani..hatimae miaka ipatayo miwili ikapita,ambapo ilikuwa asubuhi moja siku ya juma tatu,,kimvua cha vuli kilipokuwa kinanyesha..kwenye ukungu mwepesi alionekana mama yake kazula ambae alionekana kula chumvi nyingi..alikuwa akizipiga hatua kuelekea kwenye nyumba ya mwanae huku moyoni mwake akionekana kuwa mtu mwenye neno la kutaka kumwambia mwanae.

    Mama Kazula baada kuisogelea nyumba ya mwanae,ghafla alisimama baada kusikia Mele mke wa kazula akizozana na mume wake..huku maneno machafu yakiwa ndio yametawala,mele akimtukana Kazula huku akitishia kurudi nyumbani kwao.

    Hakika yale ya Mele yalimsikitisha sana mama kazula,ambapo aliweza kusema na moyo wake.."Ee mungu msaidie mwanangu apate hata mtoto mmoja ili alinde heshima yake ya ndoa.." alijisemea hivyo mama kazula,wakati huo mlango wa nyumba ya kazula ulifunguliwa,ambapo alionekana mele mke wa kazula akiwa na Begi lake akirudi nyumbani kwao..,Kazula nae hakuta mke wake aondoke,kitendo ambacho aliweza kumpigia magoti ili mêle abadili maamuzi yake ya kumwacha solemba.

    Lakin mele licha ya kupigiwa magoti na kazula,bado alionyesha msimamo wake wa kurudi nyumbani kwao,huku akidai hawezi kuishi na mwanaume asie weza kumpatia ujauzito.

    Mele akaondoka zake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Machozi ya masikitiko aliyadondosha kazula huku magoti yake yakiwa chini,,na hapo hapo mama yake alimsogelea kisha akamwinua..akamwambia. "Yote mtihani mwanangu,natumaini mungu atakufuta machozi yako..nyamanza acha kulia chukulia majaribu haya kama mtaji kwako.." Kazula akitokw na kwikwi,alijifuta machozi yake kisha akaketi sebleni na mama yake..ambapo waliweza kuzungumza Mambo mbalimbali ya kuhusu maisha yao,,yote hayo mama kazula alitaka mwanae asahau kile kilichotokea muda mfupi uliopita.

    Wakati hayo yakiendelea..upande mwingine nako alionekana Mele akiwasili nyumbani kwao.Hivyo mama Mele alishtuka baada kumwona mwanae akiwa na begi,,kwa mshangao mkubwa,mama mele alihoji "Kuliokoni mwanangu mbona asubuhi yote hii na vifurushi??.." Mela akajibu "Njoo ndani mama Nikuulize kila kitu.." Alijibu Mele,ambapo mama Mele aiachia fagio lake kisha akaingia ndani na mwanae.

    Na mala baada wote kukaa sawa..wa kwanza kuongea alikuwa mele ambapo alianza kwa kumsalimia mama yake.."Malakhaba mwanangu..haya niambie kitu kilichokufanya asubuhi yote hii kudamkia nyumbani kwenu badala kulala na mume wake.." Aliongea hivyo mama mele baada ya salam akiyopewa na mwanae.

    Hivyo mele baada kusikia..nae akionekana kukunja uso wake alijibu.."Mama mume wangu hana uwezo wa kunipatia mtoto..kwa hiyo mimi nimeamua bora niachane nae tu.." Alisema Mele.

    "Hapana mwanangu mimi kama mzazi wako sikubaliani na uamuzi wako kwa sababu bado hujajua tatizo lipo kwake mumewe au kwako wewe.."

    "Kwangu?? ." Alishtuka mele

    "Ndio kwani wewe huwezi kuwa na tatizo la uzazi??.."

    "Hapana mama mimi ninauhakika kabisa sinaaa tatizo hilo.."

    "kweli unauhakika mwangu??.."

    "Ndio mama uhakika ninao"

    "Sawa kama unauhakika huna tatizo,,basi tatizo lipo kwa mume wako..lakini tatizo hilo isiwe sababu ya wewe kumkimbia kwa sababu linaweza kutatuliwa na furaha ya ndoa yenu ikarejea.."

    "Kweli mama!

    "Amini mwangu cha muhimu kisho twende kwa Mzee baluguza anaweza kututatulia tatizo hilo.."

    Mama na mtoto walikubaliana hivyo,,ili waende kwa Mzee baluguza,,Mzee ambae ni mganga wa kienyeji.

    Kweli asubuhi ilipofika Mama Mele na Mele walielekea kwa mganga Baluguza,,ambapo walipewa dawa huku mganga Baluguza akiaminisha kabisa kuwa Kijana kazula ndio mwenye tatizo la uzazi.

    "Chukua dawa hii..muwekee mumewe kwenye chakula,pia hii nyingine utauweke upande anao lala yeye kitandani..Na hakikisha asikuone pindi utakapokuwa ukifanya haya...Ivo mnaweza kuondoka.." Alisema mganga Baluguza huku akiwakabidhi dawa mbali mbali za kienyeji.

    Hivyo baada mama Mele kufika nyumbani na mwanae,,hatimae alimwambia arudi kwa mumewe huku akimtaka asisahau kufanya yale aliyoambiwa na mganga Baluguza.

    Kweli Mele nae akirudi akionekana mnyenyekevu,,aliweza kumwomba msamaha Kazula kuhusu yale aliyomfanyia..Kazula nae kwa moyo mkunjufu akimpokea mke wake kwa mikono miwili.

    Na usiku ulipoingia,chakula kiliandaliwa..M

    ele akafanya kama alivyo ambiwa na mganga Baluguza..huku yeye ili asile kile chakula aliamua kujifanya mgonjwa wa tumbo kuhara..Hivyo alimwambia mume wake ale yeye atakula mpaka pale tumbo litakapo tulia.

    Kazula alikula kile chakula..Na baada kumaliza walienda kulala..lakini kesho yake asubuhi Mele alishtuka baada kumgusa mume wake na kukuta mwili ukiwa wa baridi huku ukiwa umekakamaa...Mele alipagawa haraka sana alimfunua shuka ili amtazame vizuri mume wake..Mungu wangu,mele hakuamini kile alichokiona..Kazula alikuwa amefariki..kumbe Mele hakupewa dawa bali alipewa sumu ya kumwondoa mume wake duniani.

    "Nitasema nini mimi kwa mama kazula?..Hali ya kuwa kazula ndio mtoto pekee kwa mama kazula? .." Alisema Mele huku akiupapasa mwili wa kazula ili ahakikishe kama kweli kazula kapoteza maisha.



    "Nitasema nini kwa mama kazula? Hali ya kuwa kazula ndio mtoto pekee kwa mama kazula?.." Hayo ndio yalikuwa maneno ya Mele baada kugundua kuwa dawa aliyopewa na mganga Baluguza imemuua mume wake.

    Hivyo Mele akionekana kuchanganyikiwa

    ,akatoka ndani.akazipiga hatua kuelekea nyumbani kwa mama yake,kwenda kumwambia juu ya kile kilichotokea kwa mumewe ambae ni kazula,,hali ya kuwa upande mwingine nako,mama kazula alionekana akitembea kuelekea nyumbani kwa mtoto wake ili kumjulia hali kama alivyo kuwa amejiwekea utaratibu huo.

    Wakati huo huo Mele akafika nyumbani kwao huku akilia kwa uchungu,na mama Mele ambae aliitwa Bi kibwana baada kusikia sauti ya mwanae akilia,haraka sana alitoka ndani na kisha kwenda kumsikiliza.

    Hakika Bi kibwana alitaharuki baada kumwona mwanae akilia huku akimtaja mganga alie mpa dawa,kitu ambacho kilizidi kumshtua Bi kibwana ambapo alimwambia mwanae wakae kitako ili amweleze kitu kinacho mliza.

    Lakini kutokana na uchungu aliokuwa nao Mele,kwa Hakika alishindwa kusimulia kitu kilichomkuta mume wake,,hivyo alizidi kulia kwa uchungu.Bi kibwana akamshika bega kisha akamfuta machozi yaliyokuwa yakimtililika mashavuni.Ambapo baada kufanya kitendo kile,Bi kibwana alimtaka Mele anyamanze ili amsimulie mkasa ambao unamfanya atokwe na machozi.

    Na hatimae Mele akanyamanza,akayafuta machozi kwenye mboni zake kwa kutumia kiganja chake. kisha kwa huzuni kubwa Mele akamwambia ukweli mama yake kuwa mganga Baluguza hakuwapa dawa ya kumtibu Kazula tatizo la uzazi,bali aliwapa sumu ya kumuuwa.

    Lakini cha kushangaza,baada Mele kumwambia hivyo mama yake..Ajabu Bi kibwana alicheka sana huku akipiga vigelele,,na mwishowe akasikika akisema hivi. "Mele mwanangu..kifo cha yule kijana ambae ndio alikuwa mkwe wangu,,wala kisikupe shida..bali we furahia maisha sasa..." Alisema Bi kibwana mama yake Mele.Wakati huo Mele akiwa ameduwaa,akishindwa kumuelewa mama yake kuhusu kile alichokizungumza mama yake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hivyo Moyo wa Mele ulizidi kutandwa na giza nene,akijutia uamuzi alio ufanya..uamuzi wa kwenda kwa mganga wa kienyeji akiamini kuwa mganga ataweza kumpatia dawa ya kumtibu mume wake ambae ni kazula ili aweze kumpatia mimba.

    Lakini yote kwa yote Mele akajikuta akimkosa mume wake pia hata ile ndoto ya yeye kuzaa na kazula nayo iliyeyuka.. Kwa Hakika Mele alilia sana huku akijiuliza kuwa ataificha wapi sura yake kijijini kwao endapo kama atagundulika juu ya kifo cha kazula?

    Na kabla hajapata jibu,ghafla Mama yake aliingia ndani na kutoka,kisha akafungua fundo iliyokuwa imefungwa kwenye khanga yake..ambapo Bi kibwana alipo fungua ile fundo,alitoa kiasi cha fedha shilling elfu sita..fedha ambayo moja kwa moja alimkabidhi mwanae..baada ya hapo akasema "Mwanangu Mele..usilie sana hadi ukamkufuru mungu..kazula tayali kafa hata ukulia Sawa na bure tu,,hatorudi...kilichobaki ni kumsahau kwa maana wewe bado mschana mdogo tu hivyo umri wa kuolewa na mwanaume mwingine bado unao..tena mwanaume mwenye uwezo wa kukujaza mimba,na sio huyo aliekufa...Hivyo hela hiyo mwanangu shilling elfu sita,nakuomba nenda kijiweni kawachukue vijana wawili ongea nao vizuri waufukie mwili wa marehem mume wako,,la sivyo jela litakuhusu na kama sio jela basi utapigwa hadi ufe.."Bi kibwana alisema.Mele akashtuka kusikia suala hilo,,papo hapo akawaza na kuwazua na mwishowe akaona hakuna namna zaidi ya kumzika kazula kimya kimya bila mwanakijiji yeyote kujuwa akiwemo na mama kazula mwenye.

    Na wakati Mele alipokuwa akifikilia suala hilo,upande mwingine nyumbani kwa kazula,mama kazula alipiga hodi huku akimwita mwanae ili amsabahi,,lakini kazula hakuitikia kwani alikuwa tayali amesha fariki,,hivyo mama kazula aliamua kurudi nyumbani kwake ingawa nafsi yake ikimsuta kuwa aende tena nyumbani kwa mwanae ili ajue kwanini hajaitikia baada kumwita ili amsabahi.

    Vilevile,Mele nae baada kuwaza na kuwazua.hatimae akaona wazo alilompa mama yake,ni wazo nzuri ingawa roho ilikuwa ikimuuma ila ilimlazimu afanye vile..

    Baada Mele kuliafiki wazo la mama yake,Mele alizipiga hatua kuelekea kijiweni kwenda kuwatafuta vijana ambao watamzika kazula kimya kimya saa za usiku,na kwa bahati nzuri aliwakuta vijana wawili wakicheza mchezo wa bao la kete..vijana hao mmoja anaitwa Solomon na mwingine anaitwa Marongo.

    Hivyo Mele alipowakalibia Vijana wale,aliwaza atanzaje anzaje kuwaambia kuhusu habali ya kumzika mtu kimya kimya?

    "Ee mungu nisaidie"Alijisemea Mele huku akionekana mtu mwenye hofu kubwa kama mtu aliefumwa ugoni.

    Lakini yote kwa yote,Mele akapiga moyo konde kisha akamwita Marongo faragha..ambapo Marongo nae kabla ya kusimama kumfuata Mele,alizitazama kete zake jinsi zilivyo.akasema."Ole wako Solomon uvuruge bao,kete zote nimesha zikariri.." Solomon akacheka...wakati huo Marongo nae alikuwa ameshamfikia Mele.

    Kwa Hakika kwa masikitiko na hofu kubwa Mele alimuelezea Marongo kila kitu kuhusu msiba alio upata,na kwa kuwa kwa kipindi kirefu sana Marongo alikuwa akiwaza jinsi ya kumpata Mele,,hivyo kupitia kifo cha kazula,Marongo aliona hiyo ndio itakuwa nafasi ya yeye kuishi na Mele.

    "Sawa wewe usijali,tena kazi hiyo nitaifanya mimi peke yangu..Na sitohitaji malipo kutoka kwako" Alisema Marongo kwa tabasam pana..Baada Marongo kujibu hivyo,Mele alimsihi aje usiku nyumbani kwake kazula,kisha Mele akaondoka zake.

    "Eeh je,umefanikiwa kuwakuta vijana watakao mzika marehem mumeo?..Alihoji mama Mele Ambae ni Bi kibwana.

    "Ndio!.." Akajibu Mele.

    "Nani sasa kwa maana vijana wa kijiji hiki si wote waaminifu.."

    "nimeongea na Marongo.."

    "Saaafi sana mwanangu..Eeh yule ndio mwanaume bwanaa sio hao wengine vikaragosi tu....Sasa niambie,Marongo amesema ataifanya kazi hiyo kwa bei gani?.."Hakika akionekana kuwa na furaha,mama Mele alihoji hivyo..

    "Kasema bure!..

    "Buree???...Eeh ha! ha! ha! ha!..kweli yule Marongo na huyo anakufaa awe mume wako kwa maana kitendo hicho anachotarajia kukifanya ni Mzigo mkubwa mno,lakini kijana wa watu kaamua kujitolea kukusaidia..".Mele hakujibu kitu akakaw kimya.

    Na usiku ulipo ingia,kijana Marongo aliandaa mapema vifaa vya kuchimbia kaburi,ambapo alichukua sululu,chepeo pamoja vifaa vingine mbali mbali..kisha akazipiga hatua kuelekea nyumbani kwa kazula..wakati huo Mele kitambo alikuwa ameshafika,,ila alikuwa amekaa kitako na mama yake mkwe akijaribu kumdanganya kuwa,kazula alikwenda kuwinda tangu alfajiri.Hivyo hata yeye anashangaa hadi muda huu usiku bado hajafika...Kwa Hakika ulikua ni uongo ambao pia Marongo aliu-support,nia n'a mazumuni kumdanya mama kazula ambae nae alijawa na tumbo joto,ingawa nafsi yake ikawa inamsuta asikubaliene na maelezo ya Mele kwa maana haikuwa kawaida kwa mtoto wake kuondoka mahala bila kumpa taarifa mama yake.

    Lakini wakati mama kazula alipokuwa katika sinzofaham kuhusu mwanae,,hali ya kuwa Marongo nae akisubili muda ufike ili amzike kazula..ndani ya nyumba ya kazula alitokea mganga Baluguza...!





    Mganga baluguza alionekana chumbani kwa kazula,lakini punde si punde akawa amepotea..wakati huo maongezi mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea Kati ya mama kazula,Marongo pamoja na Mele..yalikatis

    hwa baada mama kazula kuhisi usingizi,kitu ambacho kilimfurahisha sana Mele..zaidi alisubili mama yake mkwe anyanyuke aingie ndani ili na wao wakafanye shunghuli nzima ya kumzika kazula kimya kimya pasipo kujuwa mtu yeyote.

    Kweli ni jambo walilofanikiwa,kwani baada mama kazula kuzama ndani,Mele pamoja na Marongo walizipiga hatua kwenda kuchimba kaburi nyuma ya nyumba na kisha kumzika kazula.

    Hivyo baada suala hilo kufanikiwa..usiku ule ule kijana Marongo aliweza kuzungumza na Mele kuhusu hisia zake..Na kwakua Mele aliona msaada alioufanya Marongo..hatimae alimkubalia,ila alimtaka akatafute mahali na ndipo waoane.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kweli ndani ya siku kadhaa,Marongo alifanikiwa kupata mahali aliyoambiwa ambapo aliuza mbuzi watatu na kondoo mmoja..kwa maana Marongo alikuwa mfugaji.Hivyo taratibu za wao kuona zilifuata,ambapo Bi kibwana ambae ni mama Mele alifurahi sana siku hiyo,alialika ndugu na jamaa zake kutoka vijiji jirani na wengine kutoka mjini,wote kwa pamoja waliungana kwenda kusheherekea sherehe ile ya Mele kuolewa.

    Lakini wakati sherehe ile ilipokuwa ikiendelea,upande wa pili kule nyumbani kwa kazula,nyuma ya nyumba ambako lipo kaburi la kazula.kaburi lilofukiwa na kisha kufunikwa na majani ili lisionekane,ghafla juu ya kaburi alionekana paka mweusi paka ambae alilia kwa sauti Kali kisha punde akawa amepotea..ambapo baada paka yule kupotea,kando kidogo ya kaburi ambako kulikuwa na kichaka,alionekana nyoka mkubwa kiasi,nyoka aina ya cobra alijiburuza hadi kwenye kaburi la kazula,,ambapo aliingia ndani.bila shaka katika kaburi lile lilikuwepo shimo.

    Wamati nyoka yule alipokuwa akiingia ndani ya kaburi la kazula,kwingineko mama kazula alianguka chini kwa mshtuko baada kusikia kuwa Mele anaolewa na mtu mwingine,,hivyo hapo mama kazula akawa amehisi ya kuwa Mele atakuwa kampoteza mtoto wake ili aolewe na mwanaume mwingine...Hakika hali hiyo ya mshtuko iliweza kumpeleka umauti mama kazula kwa maana miaka dahari alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifafa...Na baada mama kazula kufariki alizikwa na wanakijiji,ila sehem aliyokuwa akiishi ilipigwa bei na mdogo wake ambae aliitwa Mzee makumbuko kwani baada mama kazula kufariki,mrithi wa mali hakuonekana zaidi ya huyo Mzee makumbuko ambae nae kwakua alikuwa mlevi,aliona heri auze mashamba na kiwanja ili pesa akanywee pombe.

    Hivyo kwa kuwa Marongo lasmi alianza majukum,hatimae aliamua kununua yale mashamba na uwanja ambao tayali ulikua na nyumba mbili..nyumba ya marehem mama kazula na nyumba ya kazula..

    BAADA YA MWAKA MMOJA.

    Maisha ya Mele pamoja na mume wake Marongo yalikuwa mazuri ya furaha na amani,lakini furaha hiyo ilitoweka baada siku moja saa sita usiku wakati Marongo anaelekea chooni kujisaidia,ghafla alishtuka baada kumwona mtu alievaa nguo nyeupe mbele yake,na punde si punde yule mtu akawa amepotea.

    Marongo kwa woga,alizipiga hatua za haraka haraka kuelekea chooni,akajisaidia haja yake kisha akarudi ndani hima.

    Na wakati akiwa kitandani na mke wake Mele,ghafla upepo mkali ulivuma ukipitia dirishani,,kiasi kwamba upepo ule uliweza kudondosha baadhi ya vitu vyepesi vya mle ndani.."Mele mele mele..! Marongo alimwamsha mke wake ambapo Mele nae baada kusikia sauti ya mume wake ikimwita,alishtuka kutoka usingizi.."Amka mke wangu..!! tutoke humu ndani,kwa maana upepo huu unaweza kuangusha nyumba..!

    Wakionekana kuwa na hofu juu ya ule upepo,Mele pamoja na mume wake Marongo walitoka nje usiku ule ule,,ambapo baada kufika nje,cha ajabu upepo ule ulitulia kisha sauti ya ngoma na nyimbo za asiri zilisikika kutoka nyuma ya nyumba kule lilipo kaburi la kazula....Na mtu wa kwanza kuisikia ile sauti alikuwa ni Marongo,ambapo aliduwaa kwa muda wa dakika kadhaa kisha akamuuliza mke wake "Mele unasikia nini! "Sisikii kitu chochote,Kwani wewe unasikia nini?

    Alihoji Mele kwa mshangao lakini Marongo hakutaka kumwambia,zaidi alimtaka mke wake warudi ndani kulala.Ila licha ya Marongo kurudi ndani na mke wake Mele,bado suala la kupata usingizi lilikuwa gum kwa upande wao,Kwan ilifikia hatua Mele nae akawa anaisikia ile sauti ya ngoma na nyimbo za asiri zilizokuwa zikiimbwa kutoka nyuma ya nyumba mahali alipozikwa kazula.

    Kwa Hakika usiku ulionekana mrefu kwa wapenzi hao,kwani baada sauti ile kudumu kwa muda wa nusu saa,hatimae ilipotea kisha wakasikia sauti ya kazula ikimwita Mele kwa hisia na Kali,sauti hiyo Mele aliisikia aliogopa sana kiukweli..Marongo akahoji kwa kunong'ona "Hiyo sauti ni yakuzula?.."

    "Ndio yenyewe.."Akajibu hivyo Mele,ambapo baada Marongo kujibiwa hivyo na mke wake,haraka asana alinyanyuka kutoka kitandani..kisha akazipiga hatua kulisogelea dirisha,ambapo baada kulifikia,aliifunua pazia ya dirisha kisha akatazama kule ilipo kaburi la kazula,,,kwa Hakika Marongo alistaajabu baada kuona kaburi la kazula likiwa limejengewa,wakati walipo mzika walilifunika kwa kutumia majani ili pasijulikane kama mahala pale kuna kaburi..."Mungu wangu,tume kwisha! Alisema Marongo ndani ya nafsi yake huku akitetemeka mwili mzima,,wakati huo kule kwenye kaburi,ulionekana mwanga wa touch,mwanga huo ulionekana kuusogelea nyumba ya Marongo..Marongo kwa woga alifunika dirisha kwa pazia kisha akarejea kitandani lakini kabla hajaulaza mwili wake,ghafla kibatari kilizima na punde si punde akasikia mlango wa nyumba yake ukigongwa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Bwana marongo akiwa na mke wake mele,walisikia mlango ukigongwa nje.Wakati huo zile sauti za nyimbo na ngoma za asiri iliyokuwa ikitokea kule kwenye kaburi la kazula,ilikata.Ambapo Marogo baada kusikia mlango wa nyumba yake ukigongwa,ghafla akajawa na hofu kubwa moyoni mwake.Marongo akasimama kutoka kitandani,kisha akawasha kibatari chake,moja kwa moja akausogelea mkoba wake ambao ulikuwa na dawa mbali mbali za asiri,dawa ambazo bwana Marongo alipewa na marehem baba yake kwa niaba ya kulinda mifugo yake.Hivyo marongo akaona ajaribu kujipaka ile dawa ambayo ni maalumu kwa kuwapaka ng'onbe,kondoo au mbuzi ili pindi ambapo mnyama mkali atakapo vamia zizi,asiweze kuona mfugo wowote.

    "Lazima nijaribu kujipaka hii dawa,na ndipo niende kumwona huyo mtu anae nigongea mlango usiku huu wote"Alisema Marongo huku akimalizia kujipaka ile dawa kwenye paji la uso wake.Na mala baada kumaliza,bwana marongo alizipiga hatua kuelekea mlangoni kwenda kufungua mlango.Lakini kabla hajafungu mlango! Ghafla marongo alishtuka baada kusikia sauti ya kicheko cha kazula kikitokea nyuma ya nyumba yake ambako ndiko lilipo kaburi la kazula..Bwana marongo aliisikilizia kwa umakini saana ile sauti,na wakati marongo alipo kuwa akitega sikio lake kuisikiliza ile sauti ya kicheko iliyokuwa ikitokea nyuma ya nyumba yake? Pale mlangoni alipokuwa amesimama akitaka kutoka nje,napo mlango uligongwa.Hivyo marongo kwa kujiamini kwa kuwa kajipa ile dawa,hatimae alifungua mlango kwa nguvu.Lakini hakuona mtu yoyote.

    Hakika marongo alistaajabu sana,akatazama mbele kulia na kushoto,ila hakufanikiwa kumwona mtu yoyote.Ambapo Marongo akaona haitoshi,bora akachungulie kwenye kaburi la kazula ili aone kinachoendelea kwenye hilo kaburi.

    Hivyo Marongo akiamini dawa imemfanya asionekane,alizipiga hatua za kunyata akilisogelea kaburi..na mala baada kuliona,kwa hakika marongo alipigwa na butwaa kwani hakuamini kama angelimwona kazula..kwamaana alijuwa kuwa vile alivyomzika,ndio misho wake..Kiukweli Bwana marongo aliogopa sana,haraka sana alirudi ndani,wakati huo kwenye kaburi la kazula..alionekana kwa mala nyingine tena Mganga Baluguza,ambapo mganga huyo alichukuwa kitu frani ambacho kinafanana na mkia wa ng'onbe,kisha akachovya kwenye kibuyu chake na moja kwa moja akamnyunyuzia kazula..kitendo ambacho hakikuchuwa muda..kazula kupotea pele juu ya kaburi..Baluguza akacheka kisha nae punde si punde akapotea pale kaburini.

    Kesho yake asubuhi,mtu wa kwanza kuamka alikuwa ni mele,ambae yeye kama mama wa nyumbani ilimlazim awahi kuamka ili akamue maziwa kabla mume wake hajazipeleka ng'ombe porini kuchunga.Lakini baada Mele kumaliza shughuli zake zote,ghafla akaingiwa na hofu kubwa baada kuona mume wake hatoki ndani japo kunawa uso.Ambapo Mele alingia ndani kwenda kumwamsha mume wake..punde si punde Mele akajikuta akilia baada kumwona mume wake kavimba mwili mzima..Marongo ile dawa aliyojipakaa usiku ili weza kumuathiri ngozi yake,,

    Hivyo mele akianguwa kilio,alizipiga hatia za haraka haraka kuelekea nyumbani kwao kwenda kumpasha habari mama yake juu ya kile kilichomkuta Marongo,lakini kabla Mele hajafika kwao,alisimama akakumbuka ushauri wa mama yake jinsi ulivyo yanghalim maisha ya mume wake wa zamani ambae anaitwa Kazula. "Hapana siwezi kurudia kosa" Alisema Mele kisha akageuka kuelekea kwa Bibi wa rafiki yake ambae nae alijihusisha na mambo ya kutibu magonjwa mbali mbali kwa kutumia miti shamba.

    Na wakati mele alipokuwa akihaha kutafuta dawa ya kumtibu mume wake,nyuma ya nyumba mahali ambapo lipo kaburi la kazula..ghafla udongo tifu tifu kwenye kaburi ulicheza,na punde si punde kiganja kilionekana ikafuata goti..na mwishowe kabisa mwili wote wa kazula ulionekana juu ya kaburi,hakika kazula alitisha sana kwani mwili wake wote ulikuwa ukitoa wadudu mbalimbali,lakini punde si punde kazula alionekana akiwa katika mavazi yake yaleyale aliyozikwa nayo.

    Kazula akatazama huku na kule,hakuona mtu,ambapo alizipiga hatua kuingia ndani ya nyumba,na moja kwa mojs alimkuta Marongo akiwa hoi kitandani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Marongo! Marongo! Marongo!.." Aliita kazula kwa ssuti ya huzuni kabisa..Marongo alikiwa ameyafumba macho yake,lakini aliyafumbua baada kusikia sauti ikimuita.na baada kufumbua hakumeona mtu yoyote.Madongo alichoka kukweli akatamani kuikkmbia nyumba...lakini uwezo huo hakuwa nao.

    Na wakati huo mele alirejea na dawa ya kumtibu. Mume wake,lakini alipoingia chumbani dawa akaiweka juu ya meza kwanza ...na punde si punde ile dawa ikapotea kimazingara..kitu ambacho kilimsthua mele akajikuta akistaajsbu huku kijasho kikimtoka mwili mzima.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog