Search This Blog

KITABU - 2

 





    Simulizi : Kitabu

    Sehemu Ya Pili (2)



    kilionekana kichwa cha benjamini kikiruka kutoka shingoni na kudondoka kando....damu nyingi ziliruka benjamini akadondoka chini na kupoteza maisha.

    kisha akaonekana yule kiumbe wa kutisha akiwa ametapakaa damu kwenye mkono wake wa kulia kisha akaivuruta maiti ya benjamini na kuilaza kando kando ya maiti ya baba na mama yake..kisha akatoka akalifuata gari la benjamini akaingia upande wa ndani....aliiona simu ikiita akaipokea lakini hakuongea kitu akaikata simu hiyo.. na kuvunjavunja kisha akacheka kwa sauti ya ajabu yenye mngurumo wa kutisha akatoka ndani ya gari hilo na kuzipiga hatua kurudi upande wa ndani alikichukua kichwa cha benjamini pamoja na vile vichwa vya wazazi wa benjamini..........akatoweka kimiujiza..



    *****************



    Upande mwingine Latifa alionekana kupagawa akazipiga hatua kuelekea upande wa nje....akaanza kutimua mbio mpaka barabara kuu...akasimamisha bodaboda kisha akasema ""nini ni ni nipileke haraka ubungo

    river side.....dereva bodaboda aliendesha pikipiki kwa kasi..baada ya dakika kadhaa walifika.....latiffa akashuka haraka kutoka kwenye bodaboda akatimua mbio kuelekea upande wa ndani ya nyumba huku akimuita benjamini.....alipoingia ndani aliogopa kukuta damu nyingi zimetapakaa kuanzia mlangini.....alipoangaza angaza macho alipiga kelele baada ya kuona maiti ya benjamini ikiwa imelazwa kado ya maiti za wazaizi wake....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    latifa alitimua mbio kurudi upande wa nje...ghafla aliteleza na kudondoka chini baada ya kukanyaga damu ilioyokuwa imetapakaa kwenye sakafu...akanyanyuka haraka akatimua mbio mpaka nje ya geti akamwambia dereva bodaboda""tuondoke......dereva aliwasha pikipiki wakaondoka.....akiwa njia simu yake ikaita alipoitazama alikuwa anapigiwa simu na mama yake kuwa Meinda ameuwawa namaiti yake kuning'inizwa juu ya nguzo ya umeme....

    Meinda alikuwa ni rafiki yake kipenzi aliyekuwa anafanya nae kazi katika kituo cha radio....meinda alikuwa na likizo kwa ajili ya kujifungua....hivyo hakuja kazini kwa kipindi cha miezi mitatu..alikuwa na mimba ya kukaribia kujifungua.....

    latifa alizidi kuchanganyikiwa aliogopa sana.....baada ya dakika 40 walifika nyumbani kwa latifa kisha akatoa nyingi alizokuwa ameziweka kwenye sidiria aliyokuwa ameivaa...kutokana alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa hakuzihesabu pesa hizo akampa zote dereva bodaboda....kisha akatimua mbio kuingia ndani kwake.....akachukua kitabu cha chery akakifunua kurasa mpaka sehemu ya nne akasoma muendelezo wa hadithi...aliona mchoro wa mwanamke aliyeuwawa kikatili na kutundikwa juu ya nguzo ya umeme....macho yalimtoka akaendelea kuisoma hadithi.......alistuka kuona kunatukio la mauwaji ya watu wengi wakiwa kwenye basi la kusafirisha abiria......simu yake ikaita alipoitazama alikuwa ni binamu yake wa kike anampigia simu hiyo.......



    ******************



    Latifa akaipokea....waliposalimiana binamu yake alisema""nipo safarini nakuja dar es salaam naomba uje unipokee ubungo ghafl mtandao ukakata kwa sababu walikiwa porini....latifa akapiga ile namba ya binamu yake simu ilimjibu

    samahani mteja unayempigia hapatikani...latifa akaangua kiliona kusema""ee Mungu wy me??

    akakifunika kitabu na kukirudisha kabatini haraka akajitupa kitandani huku akilia kwa uchungu wa kuwapoteza marafiki wawili kwa wakati mmoja...mbaya zaidi tukio linalofuata ni mauwaji yatakayofanyika ndani ya basi la abiria...latifa alizidi kulia kwa sauti alijua binamu yake arauwawa muda mchache ujao....ghafla SMS iliingia kwenye simu yake upande wa WhatsApp akapuuzia kuifungua baada ya kuona ni SMS za kwenye magroup ya WhatsApp...akanyanyuka akaingia bafuni kuoga alipotoka bafuni aliweka neti kisha akapanda kitandani baada ya dakika kadhaa alijikuta machozi yakimtoka akashindwa kujizuia akaanza kulia kwa sauti ya chini. akanyanyuka na kwenda sebuleni akawasha Runinga(Tv)na kuanza kuangalia....lakini fikra na mawazo yake yalikuwa hayapo kwenye Runinga(Tv) akaamua kuizima na kurudi chumbani...



    *********



    akafanya maombi kwa kumuabudu mungu amlinde usiku wa leo..alipomaliza alijilaza na kuanza kuutafuta usingizi lakini alishindwa kulala alikuwa akitafakari juu ua mauwaji ya mfululizo yanayojitokeza...alibaki macho kwa masaa machache kisha akachukua simu yake ili atazame picha za benjamini na Mainda enzi za uhai wao....baada ya kumaliza kutazama picha hizo walizopiga pamoja akaingia upande wa whatsApp na kufungua SMS za kwenye Group.....



    Latifa aliangua kilio baada ya kusoma SMS ile...kisha aliona picha za mauwaji ya kutisha katika basi hilo lililopata ajali.....inasemeka kuna kiumbe wa ajabu alijitokeza katikati ya barabara na kusababisha ajali hiyo mbaya kisha akalifuata gari na kuanza kumtoa nje abiria mmoja moja na kuwanyofua vichwa ka kuvivuta kwa kutumia mikono yake yenye nguvu za ajabu....kisha akatoweka....

    latifa hakuweza kupata usingizi alilia sana mpaka pakakucha....akanyanyuka kitandani na kuelekea bafuni kuoga....



    ***********

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    upande mwingine alionekana mwana dada mmoja akiwa amefungiwa katika chumba chenye mwanga hafifu wenye rangi nyekundu huku mikino na miguu yake imefungwa kwa minyororo....mwanadada hiyo alionekana kudhohofika sana...ngozi yake ilionekana kuwa na vidonda kwenye sehemu alizokuwa amefungwa minyororo......macho yake yalionekana kuregea kama mtu mwenye njaa kali sana......alipojaribu kunyanyuka alionekena kutokuwa na nguvu za kisimama....akajivuruta mpaka kwenye kona ya chumba hicho akajilaza sakafuni....kumbukumbu ilianza kumjia alikumbuka tukio lililomtokea miaka kumi na mbili iliyopita.....ilikuwa hivi...

    siku hiyo chery alionekana akimuaga Latifa latifa baada ya kuhitimu masomo ya elimu ya juu kwenye chuo alichokuwa akisoma.....alikumbuka alimuachia kitabu lafiki yake kipenzi aitwae latifa...kisha wakakumnatiana na kuagana....

    kumbe mwanadada huyo ndiye yule chery aliyepotea miaka kumi na mbili iliyopita...pia alikumbuka baada ya kuagana na Latiffa alielekea kwenye kituo cha mabasi.....alipodika aliingia kwenye sehemu ya mapumziko akaketi na kuagiza matunda.....akanza kula matunda huku akilisubiri basi lifike kituoni hapo...

    wakati chery anakula alikuwa anawaza juu ya hadithi ya kitabu alichokitunga...huku akijisemea moyoni lazima nikichapishe kitabu hiki...naamini nitapasa pesa nyingi kupitia kitabu hiki.....wakati chery anawaza matukio na michoro ya kwenye kitabu chake...kumbe pembeni yake alikuwepo mwanke mwenye asili ya wingereza...mwanamke huyo alikuwa na uwezo wa ajabu!!! aliweza kuyatambua mawazo nafikra za chery....alivitiwa sana na hadithi hiyo aliweza kuisoma kupitia fikra za chery....kisha akafungua mkoba wake na kutoa biskuti kisha akaanza kula.......baada ya sekunde kadhaa alitoa kipande kimoja cha biskuti na kumpa chery huku akimsihi chery kwa maneno ya ukarimu ale biskuti hiyo....chery aliipokea na kuanza kula....baada ya sekumde kadhaa chery alihisi kizunguzungu huku nguvu zikimuishia......akapoteza fahamu....

    mwanamke yule mwenye asili ya wingereza aliita taxi na kumchukua chery akamuingiza ndani ya taxii kisha wakatokomea kusikojulikana......na baada ya miaka kumi na mbili kupita mwanamke huyo alianza kufanya mauwaji ya kikatiri na uenye kutisha kwa kufuata mtiririko wa hadithi ya kitabu cha chery....kumbe muuwaji sio chery ni yule mwanamke mwenye asili ya wingereza



    *************



    upande mwingine alionekana latiffa akitoka bafuni kisha akanza kuvaa nguo ili aende kazini...alipomaliza alitoka uoande wa nje ma kufunga mlango wa nyumba yake....akazipiga hatua kuelekea kazini.....akiwa njiani kabla hajafika mbali wazo lilimjia kuwa arudi nyumbani akachukue kile kitabu akipeleke polisi akatoe taarifa kuhusu matukio yanayojitokeza yanafanana na matukio pamoja na michoro iliyopo kwenye kitabu hicho....latifa aliamua kurudi akafungua mlango na kuingia moja kwa moja mpaka chumbani kwake akafungua kabati na kukitoa kitabu cha chary....akakiweka ndani ya mkoba wake..lakini alisita akakitoa ili asome tukio linalofuta kwenye sehemu ya tano..akafunua kurasa haraka haraka mpaka sehemu ya tano kisha akaanza kusoma.......ghafla mapigo yake ya moyo yakaanza kwenda mbio...macho yalimtoka akaingiwa na uwoga wa hali ya juu akatimua mbio na kutoka nje huku akikiacha kitabu juu ya kitanda chake...



    latifa alitimua mbio huku anapiga simu kule kazini kwake....simu ilipokelewa. latifa akasema"Kimbieni tokeni hapo mtakufa muda si mrefu....

    yile mtu aliyepokea simu hiyo alistahajabu akauliza ""latifa umepatwa na nini?? mbona sikuelewi???

    ""jamani nasema hivi ondokeni hapo haraka mtakufa wote..

    mtu yule alikata simu ya latifa akaendelea na shughuri zake....lakini akili yake ilikiwa ikitafakari maneno ya Latiffa..akajisemea moyoni"au latifa kachanganyikiwa!!! aliamua kunyanyuka na kuwafuata watangazaji wenzake akaanza kueleza kile alichoambiwa na Latiffa wafanyakazi wenzake walipuuza wakaanza kucheka...mmoja akaropoka ""kwani nini ni wageni kwa Latiffa huwa anapenda sana utani...yele mtu aliyeeleza taarifa hiyo akaamua kuondoka akaingia kwenye ngazi ya kutumia umeme(lift) na kubonyeza kitufe ili lift ishuke upande wa chini...alipofika chini kabisa alitoka kwenye lift na kuondoka zake.....



    kumbe latifa aliposoma kile kitabu cha chery kilionesha jengo kubwa lililokuwa na kuituo cha radio ghorofa ya tano....jengo lile lilifanan na mchoro wa kwenye hadithi ya kitabu cha chery...hadithi ilieleza kuwa kuna kiumbe wa ajabu alivamia jengo hilo na kuuwa watangazaji wote isipo kuwa watangazaji wawili...mtangazaji wakiume na mtangazaji wa kike.....



    **************



    yule mtu aliyeshuka kutoka kwenye lift kabla hajafika mbali alisikia vioo vikipasuka alipogeuka nyuma aliona vioo vya madirisha ya ghorofa ya tano ndivyo vinavyopasuka kisha akaona watu wanatupwa nje kupitia madirisha hayo....watu hao walidondoka chini na kupasuka vichwa.....mtu yule alikimbia haraka kuelekea kwenye tukio....alipofika aliogopa kuona watangazaji wenzake wote wameuwawa na kupasuka vichwa vyao....watu walikusanyika kushuhudia tukio hilo lakini haikufahamika ni nani aliyefanya tukio hilo.....



    ************



    upande mwingine kule juu ya ghorofaya tano..alionekana yule kiumbe akiwa bado yumo ndani ya kituo hicho cha radio..akaharibu mitambo yote inayohusika kurusha mawimbi ya radio hewani..kisha akatoweka kimiujiza.....CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    muda mchache polisi walifika eneo la tukio..wakaelekea juu kwenye kituo hicho cha radio...waliweka siraha zao tayari kwa kupambana kisha wakaingia mpaka ndani ya kituo hicho(UCCTV)...walistahakabu kukuta kila kitu kimeharibiwa isipokuwa kamera za ulinzi zilizokuwa zimetegeshwa ndani ya kituo hicho...

    polisi mmoja aliifuata kompyuta iliyokuwa inahusika kurekodi mambo yanayoendelea ndani ya kituo hicho......alipotazama matukio yaliyorekodiwa masaa machache yaliyopita..matukio yote yalionekana isipokuwa tangu kiumbe yule alipojitokeza kamera hazikuwa na uwezo wa kurekodi tukio lolote......kipande hicho kilionesha giza..... na baada ya kumaliza kufanya mauwaji pamoja na uharibifu wa vitu vilivyokuwemo humo ndaani..akatoweka na kamera zikaendelea kurekodi kama kawaida hakuonekama muuwaji katika kamera hizo..

    yule askari alistahajabu sana akajisemea moyoni""

    bila shaka kunajambo lilitokea ambalo sio la kawaida...kisha wakapiga picha kwa ajili ya upelelezi wakaondoka zao..



    ************



    upande mwingine alionekana yule mtangazaji alinusurika kifo...akizipiga hatua za haraka haraka bila kujua ni wapi anakoelekea.....akachukua simu yake na kumpigia Latiffa....

    latiffa aliipokea simu hiyo haraka""mtu yule akasema ""umejuaje kuhusu hili jambo kama litatokea???

    latifa alidakia na kusema""jamani nakusihi waambie watu wote mtoke humo mdani mkimbiesipofanya hivyo mtakufa....

    yule mtu alijibu""muda mchache uliopita wafanyakazi wenzetu wote wameuwawa na kutupwa kutoka ghofani mpaka chini.....kabla hajamaliza kuongea latifa alikata simu......macho ualimtoka jasho likaanza kumtiririka huku ikiambatana na vijampo vya uwoga(bhu bhu)

    akatimua mbio kurudi ndani kwake akafunua kitabu cha chery akaendelea kusoma sehemu ya tano ili aone tukio linalofuata........latifa alistahajabu kuona tukio la mauwaji ya kutisha katika shule ya watoto(chekechea) aliogopa sana alipoutazama mchoro uliokuwa umechorwa kwenye hadithi ya kitabu cha chery sehemu ya 5

    hakuelewa mchoro ule ulikuwa unafanana na sehemu gani alijaribu kuvuta kumbukumbu huenda alishawahi kuona shule hiyo....Latifa alistuka akazipiga hatua kurudi nyuma kwa uwoga huku amebaki mdomo wazi......



    Latiffa akachukua simu yake haraka na kupiga namba za vyombo vya dora....akasita akaacha kupiga simu hiyo akajiuliza moyoni""mmh!! naweza kutoa taarifa hii nikawa matatizoni mungu nisaidie......akakifunika kitabu kile akakirudisha ndani ya kabati.. akatoka nje...akiwa anatembea wazo likamjia kuwa arudi chumbani achukue kitabu kile akipeleke kwenye vyombo vya dora

    "" aagh liwalo na liwe....akazipiga hatua akaingia chumbani kwake akafungua kabati akakitoa kile kitabu......akakiweka ndani ya mkoba kisha akatoka upande wa nje.....akazipiga hatua mpaka kwenye barabara kuu...akakodi bodaboda akaenda mpaka kituo cha polisi Ostabey...alipofika alianza kutoa maelezo......maaskari walistahajabu sana....kisha akakitoa kitabu kile na kuwaonesha maaskari hao waliokuwa zamu.....walimcheka kisha wakasema wanakazi nyingi za kufanya hawana muda wa kufatilia jambo la kufikirika ... latiffa alishangazwa na majibu ya maaskari hao....akachukua kitabu na kuondoka zake.......akaenda kwenye mgahawa akaagiza chakula.....wakati anakula alisikia watu waliokuwa wamekaa nyuma yake wakionge jambo lililomfanya ageuze shingo yake awatazame watu wale..... walikuwa wanaonyeshana picha katika simu huku wakionekana kusikitika.....mmoja wapo akasema """sijui ni nani aliyefanya mauwaji haya ya kikatiri...yani hana hata chembe ya huruma... watoto hawa wadogo wanakosa gani!!!! mwingine akadakia ""mmh inasikitisha wameuwawa watoto wote......latiffa aliposikia hivyo alijua wazi kuwa tukio hilo ndio tukii aliloliona kwenye kitabu cha chery.....alisikitika sana machozi yakaanza kumlenga.....akaacha kuendelea kula akaondoka zake......akaenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwake.....alipofika akaingia chumbani kwake akakitoa kile kitabu akafunua kusarasa mpaka sehemu ya sita...akaanza kusoma huku uwoga umetanda juu yake....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***********************



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog